“PAMBAZUKO”-SHAA Ft.AY

shaa2bc

Kama unafuatilia Bongo Fleva kwa makini bila shaka hivi sasa umeshalisikia jina la Sarah Kaisi au Shaa (pichani) kama ambavyo anajulikana kwa mashabiki na wapenzi wa B Fleva.

Shaa ameingia kwenye game kwa kishindo.Uwezo wake wa kumiliki jukwaa,kuimba na kwa ujumla kukidhi haja ya mashabiki wa muziki huo wa kizazi kipya,ndivyo vitu ambavyo vinamfanya azidi kupanda chati na hivyo kuungana na wasanii wengine wa kike ambao wanafanya vizuri.

Hivi sasa anatamba na nyimbo zake Zamu Yangu na Pambazuko huku akiwa anapika kitu kingine studio ambacho mwenyewe anasema ni zawadi aliyopewa na Judith Wambura aka Lady Jaydee.Tunasubiri.

Leo tunao wimbo wake Pambazuko. Katika wimbo huu amemshirikisha msanii maarufu wa B Fleva,Ambwene Yessayah au AY. Usikilize. Kama kawaida maoni yanakaribishwa(ila jitahidi kutoa maoni yanayojenga badala ya kubomoa au kuonyesha chuki na dharau).Umeupenda wimbo? Unasemaje.Shaa atazidi kushika chati?Karibu.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

shaa1bc

Shaa on stage!

Page 1 of 3 | Next page