MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

jose_juma_naturebc

Mojawapo ya mambo ambayo yanaweza kukufurahisha kama unapenda muziki kutoka Afrika Mashariki ni pale wasanii kutoka nchi zinazounda Afrika Mashariki wanapoamua kushirikiana katika kazi zao. Mifano ipo mingi kuonyesha jinsi gani mipaka iliyowekwa na mtawala wa enzi hizo inaweza kuvukwa japo kwa kutumia muziki.

Nimewahi kuandika siku za nyuma kwamba wakati viongozi wetu wanasuasua katika kukamilisha muundo wa jumuiya ya Afrika Mashariki(ukiniuliza mimi nitakwambia ni kwa sababu kila mmoja anaweka mbele maslahi binafsi badala ya faida nyingi za muungano makini) wasanii wao wameshavuka kizingiti hicho.Wanashirikiana.

Miongoni mwa mifano ya ushirikiano huo ni huu wa Juma Nature akimshirikisha Jose Chameleon(Uganda) katika wimbo unaokwenda kwa jina Mikiki Mikiki. Kama ujuavyo hawa wote ni ‘majina makubwa” katika muziki wa ukanda wetu. Wanaposhirikiana tunategemea kitoke kitu makini.Nakuomba uwe muamuzi.Sikiliza Mikiki Mikiki hapo chini.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Picha na Muziki kwa niaba ya GetMziki.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

7 Responses to ““MIKIKI MIKIKI”-JUMA NATURE FT CHAMELEON”

  1. Comment by Vyne on June 30th, 2009 11:01 pm

    wanna boooooo.Hijanikiki kusema kweli

  2. Comment by BLACKMANNEN on June 30th, 2009 11:32 pm

    Ushirikiano ni kitu kizuri na muhimu sana katika kufanya jambo fulani. Lakini ushirikiano mwingine unapokuwa kwa manufaa ya upande mmoja, sio ushirikiano, bali ni kulaliana.

    Ushirikiano wa Kijumuia ya Afrika ya Mashariki, utakuwa mzuri na wa manufaa, iwapo washiriki wenzetu (nchi jirani) watakuwa na nia ya ushirikiano wa kikweli, badala ya kuimezea mate ardhi yetu ya Tanzania ilivyo kubwa na tajiri wa kila kitu.

    Jose Chameleon na Juma Nature, ushirikiano wao ni kwa manufaa yao kimuziki.

    Idadi ya wapenzi wa muziki wa Chameleon ni kubwa zaidi Tanzania, ukilinganisha na huko kwao Uganda.

    Vivyo hivyo, Juma Nature, ana wapenzi wengi sana Tanzania, na akiongeza na wapenzi wengine kutoka Uganda, ananufaika zaidi, kwa kupata wapenzi lukuki.

    Hapo, hakuna mtu anayemlalia mwenzake. Kila mtu anafaidika kwa kile alichokipanda na watakachokipanda pamoja kimuziki.

    Chameleon, ili kuhakikisha anapata wapenzi wa Kitanzania, amejikita zaidi kuitumia lugha ya kiswahili katika miziki yake mingi, ili kuwapata wapenzi wake wa Kitanzania.

    Ushirikiano wa Juma Nature na Chameleon, mimi ninaupalilia sana, maana unatuweka jirani zaidi na ndugu zetu Waganda.

    Kwa miaka mingi sasa, Waganda wamekuwa mbali na Watanzania kimahusiano kirafiki, na mambo mengine mbalimbali ya kijamii na hasa watu waishio nchi za nje ya Afrika.

    Hayafanani, ukilinganisha mahusiano ya karibu kati ya Wakenya na Watanzania. Wakenya na Watanzania, tupo karibu zaidi.

    Lakini hata hivyo, siku hizi, ninaweza kukaa na Mganda tukasikiliza pamoja miziki kwa usalama, bila ya kukumbushana mambo ya Idi Amin, Obote, Kabaka Mutesa na wengine.

    Ila kulonga kwetu na Waganda, bado ni kwa Kiingereza tu. Hapo sasa! Bado tuna safari ndefu.

    This Is Black=Blackmannen

  3. Comment by Mickey Jones - Denmark on July 1st, 2009 8:21 am

    USHIRIKIANO NI MAENDELEO KWA MZIKI WA KISASA

    Nakubaliana kabisa na mdau BLACHMANNEN ni muhimu saana kwa sasa kurudisha umoja wa bara la Afrika mashariki si kwa viongozi tuu bali kuwepo na mabadilishano ya kuvumiliana kimila na utamaduni haswa katika usanii wa mziki na michezo.

    Kiswahili kitumike katika kutuunganisha ingawaje kuna asilimia kubwa ya waganda hawakitambui wala kukikubali ukulinganisha na wakenya na hili litakuwa tatizo kubwa saana katika jumuia ya Africa Mashariki maana kuna wengi watanzania hawakitambui wala kukikubali kiingereza.

    Ukiunganika katika sherehe za waganda watakupa jina lingine la mwimbaji wa Uganda,wakisema “Chameleone” hawezi kuimba kwa kiingereza vizuri na ukiunganika na wakenya watakupa jina lingine zaidi ya “Juma Nature” kwa Tanzania watakwambia hawezi kuimba vizuri kwa kiingereza.

    Hili ni tatizo la asilimia kubwa ya jirani zetu kutokifahamu na kutokikubali kiswahili kama ufunguo wa milango yote katika muungano wetu bila ya hivyo muungano utabakia kama ndoto za usingizini.

    Juma Nature na Chameleone watufungulie njia ya umoja wa vijana kwa burudani za mziki wa kizazi kipya katika bara la Afrika mashairi kwa kiswahili ni lugha inayoeleweka na kukubaliwa na wengi,waliyobakia wachache itawabidi wajifunze kiswahili kama wanataka kuwa katika jumuia ya muungano.

    MJ

  4. Comment by marknigga salamba on July 1st, 2009 12:23 pm

    ushirikiano ndio maana ya ushrikiano,kuna wangine watapata kidogo,wangine watapata zaidi.ushirikiano kwa kusema kweli hakuna hisa,kumbukeni katika wale walioaamua ushirikiano,kila mtu.ananufaikasio kwa waganda,watanzania,mtu yeyote aneweza kuiimba kwa lugha yeyote,mradi waweke TAFSIRI(subtittle).mie muislam,nilikuwa nazikiri kwa maneno ya kiarabu,lakini utamu niliuuona,kwa kucheza,cheza.mwimbo ni sauti au musik,raha ile ile.hta kama wakutana na mtu akukumbusha ya idd amin,au kabaka,hayo ni maisha,maana maisha ni VITU.vingi,kumbukumbu,kuteta,kusengenyana,kuchekwa,kukosolewa,kukosa,kupata,kufiwa,kuzaa,basi mradi maisha ni maisha,ushrikiano ni nguzo za maisha,ki mpila,kuimba,kucheza,mpaka kutombana(natukana),mark salamba australia

  5. Comment by halima on July 2nd, 2009 4:40 am

    Safi sana nimependa hiyo

  6. Comment by Hombiz on July 2nd, 2009 3:33 pm

    Juma nature na Chameleon sio wasanii wakwanza kufanya hivyo. Hata Profesar Jay na Chameleon walishawahi kuimba pamoja. Jay pia amewahi kushirikiana na wasanii wengine toka Kenya. Vilevile, msanii maarufu wa hiphop toka Ghana aitwaye Kwae Kese, amemshirikisha prof Jay ktk kibao chake kiitwacho “who be you!” Pia wasanii wengine kadha wa kadha Tanzania wameshawahi kushirikiana na wenzao watokao sehemu mbali mbali barani Afrika ktk sanaa zao. Hivyo basi, hili sio jambo jipya kwetu. Na pia hii sio sababu ya kuwafanya viongozi wa nchi za Afrika mashariki wakurupukie muungano wa nchi zao.

    Nionavyo mimi, wasanii hawa wameshirikiana tu kisanii na si kuungana pamoja kama kuanzisha kundi jipya la muziki ambalo litakuwa ni kitu himoja. Wengekuwa wamefanya hivyo na kufanikiwa kusonga mbele, hapo kweli ningeita hiyo ni changamoto kwa viongozi wan chi zao.

    Nikirudi kwenye swala la muungano wa nchi za Afrika Mashariki, mimi naona hili sio swala la kukurupuka. Ni jambo nyeti na linalohitaji upembuzi yakinifu katika swala zima la manufaa yake kiuchumi, kisiasa, kijamii, kielimu, kiusalama n.k, kwa nchi hizo husika.
    Tusisahau kuwa jumuiya ya Afrika mashariki iliwahi kuundwa na kuvunjika miaka ya nyuma kutokana na sababu mbali mbali. Moja ya sababu kubwa ni tofauti za kiitikadi kati ya nchi husika. Kwa mfano, wakati Marehemu mwalimu J.K. Nyerere alikuwa na itikadi za kijamaa kwa Tanzania, Hayati Iddi Amini yeye alikuwa na itikadi za kidikteta kwa Uganda. Kwa upande mwingine, Kenyata yeye alipendelea itikadi za kibepari kwa Kenya. Hivyo basi, itikadi hizo tatu zinatofautiana saaana na zisingeweza kuunganishwa pamoja. Kuunganisha itikadi hizi pamoja ni sawa na kuzima moto kwa kutumia petroli.
    Pia hata hii leo, mimi bado naamini kuwa viongozi wa sasa wa nchi za afrika mashariki (Kikwete, Museveni na Kibaki) wana mitazamo tofauti, kiitikadi.

    Hivyo basi muungamo ukifanywa haraka haratu tu, bila utafiti na uchambuzi wa kutosha , utabaki kuwa ni muungano ule wa simba kucheza lumba na swala au chui kuimba na nyani.

  7. Comment by Mickey Jones - Denmark on July 3rd, 2009 5:57 am

    Mchangiaji Hombiz tunaheshimu maoni yako kufuatana na mtazamo wako kuhusu muungano
    wa bara la Afrika mashariki kama nyumba iliyobomoka miaka rudi,wengine mtazamo wetu
    tunaweza kufanya marekebisho ya nyumba iliyobomoka na kuisimamisha upya lakini kunatakiwa kuwepo na mwanzo wa misingi ya ujenzi.

    Nafikiri swala hili la mitazamo tofauti ningemwachia “BLACKMANNEN” mtaalamu wetu
    mchambuzi wa mjadala wa malengo ya umoja wa bara la Afrika mashariki utaleta mafanikio gani kufuatana na mtazamo kiuchumi,kielimu nk.

    kunaweza kuwepo mitazamo tofauti hatimaye tutafika katika makubaliano malengo gani bora kwa watanzania na jirani zake.
    MJ

Leave a Reply