MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

ijumaa-front-pgbc

Kwa undani wa vichwa hivyo vya habari, bonyeza hapa au jipatie nakala yako mitaani.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

7 Responses to “IJUMAA LA LEO”

  1. Comment by Gervas on July 3rd, 2009 8:48 am

    Yaani huwa napenda tu kusoma vichwa vya habari ktk magazeti haya ya udaku, hadi raha hasa kwa watu kama sisi kule uswazi maana ni burudani inayopunguza hasira na pressure za maisha uswazi. Hivo yana nafasi yake ktk jamii japo wengi uyalalamikia kwa uwazi yanayoutoa.

  2. Comment by BLACKMANNEN on July 4th, 2009 4:50 pm

    BC tunawajua ni watu waadilifu, na mnapotoa habari zenu, mara nyingi zinakuwa ni za uhakika. Mnapotuletea mambo ya watu wasiowaadilifu kama hizi, kutoka Global Publishers. Kwa maoni yangu mimi naona sio vizuri.

    GPL wana bifu kubwa sana na Ray C, kila mara, GPL wanamwandama Ray C, kwa kumwandika na kumtungia habari za uwongo, ilimradi tu kuharibu jina lake mbele ya jamii.

    Miugomvi kati ya mtu binafsi na wana habari wa magazeti mengine, nawaomba BC mwepukane nao, maana, mnaweza kujikuta mkiingia kichwakichwa na hata kujikuta mkijivunjia heshima, imani na kuthaminiwa na jamii, na hasa wasomaji na wapenzi wa BC, kutokana na kuchukua mambo ya watu wasiofuata maadili ya uandishi wa habari kama GPL.

    Hayo ni maoni yangu tu. Hayawakilishi mawazo ya mtu mwingine wala kikundi chochote, wala Ray C mwenyewe simjui na yeye hanijui.

    This Is Black=Blackmannen

  3. Comment by chogo on July 4th, 2009 9:48 pm

    yote tisa kumi ni habari ya marehemu AMINA CHIFUPA,jamani mnao ujua ukweli tuelezeni maana hata mie nimesikia eti toka marehemu alipokufa alikuwa anatokea na watu wanamuona ni kweli?maana nilivyosikia nikasema ntauliza wenyekujua habari hiyo,embu tupeni habari wenzenu jamani tafadhali

  4. Comment by mtimkavubongo on July 5th, 2009 5:16 am

    Kwa kweli ninamuunga mkono rafiki yangu Blackmannen hawa jamaa wa global publisher wakiongozwa na Eric anayesema kaokoka hawa jamaa wanatabia ambayo sio nzuri, wanatabia ya kumwandama mtu,kwa hata vitu ambavyo ni too personal, ambavyo havisaidii jamii, biblia inasema husihukumu ukaja kuhukumiwa, hawa jamaa global publisher hakuna Mtanzania asiyejua kuwa walichangia kumuharibia sifa dada wa watu Amina Chifupa,huu ni uuaji, wazungu wanasema character assisination-lakini huu ni uchawi sio uandishi wa habari-wewe unataka upate pesa kwa kuchafua majina ya watu eti unataka kurekebisha tabia huu ni uongo, sasa NATOA ONYO, PLEASE GLOBAL PUBLISHER STAY AWAY FROM OUR BONGO CELEBRITY-RC,I AM A HUGE FAN OF HER MUSIC-hakuna dunia asiyejua kuwa maisha ya mastaa wale wa muziki au sinema au chochote yanakuwa na mambo ya vituko, mfano mzuri michael Jacksoni, lakini sio busara chombo fulani kuonyesha mtizamo wa kibifu-hii tabia sio nzuri, historia ya global publishers iko wazi ni watu wa kugombana na watu kwa kuingilia maisha binafsi kupita mipaka acheni hiyo tabiaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
    RC uko juu, keep it up mama!

  5. Comment by Gervas on July 5th, 2009 12:30 pm

    Kuna tabia watu wanaziiga kutoka kwenye movies za ulaya ambayo hayakubaliki ktk jamii zetu za kiafrika kama kissing on public (denda, kuvaa nusu uchi? ambapo nani atashika kipenga kuwalekebisha hawa? watu wanaogopa siku izi kufanya mambo ya ajabu ajabu kwenye public na hasa hao ma-celebrity mnaowasema ndo wa kwanza sababu wanaogopa kuuza magazeti kesho yake. Kama mtu anaonewa sheria ya magazeti na mahakama zipo, mbona hatuwaoni wanashitaki ili walipwe na haya magazeti? Gazeti la The East African walishawahi mlipa Dr. Salim A.Salim Bilion moja na ushehe kwa kuandika porojo juu yake. Nayaunga mkono haya magazeti 100%

  6. Comment by KILO on July 9th, 2009 4:29 am

    Weee!! unayejiita Blackman.. acha ushamba magazeti kama hayo yapo dunia nzima .. wewe kwa ushamba wako unaona vitu vya ajabu .. inaelekea wewe ni wale wazee wenye siasa kali maana naona comments zako unajifanya unajua kila kitu

  7. Comment by BLACKMANNEN on July 10th, 2009 7:40 pm

    Mkuu “KILO”,

    Ahsante sana kwa kuzifuatilia na kuzisoma comments zangu. Ushamba ni sifa kubwa sana kwangu uliyonipa hapa, maana kila binadamu katika dunia hii, ana kula chakula kitokacho shambani ambako mimi ndiko kwangu kama ulivyosema wewe hapo juu kuwa mimi ni “mshamba”.

    Lakini pia nimefurahi kuona kuwa maoni yangu, unayasoma na yanakugusa sana, na pia kukusaidia kuwaza zaidi ya hayo niyasemayo katika comments.

    Ndiyo maana ukaniita kuwa mimi najifanya ninajua kila kitu, kwa jinsi nilivyokuchambulia mambo kitaalamu, mambo ambayo kwako yalikuwa magumu.

    Lakini katika kutaka na wewe uonekane, unajifanya kuyaona maoni yangu hayo kuwa, yapo chini ya kiwango, unachokiwaza wewe kichwani mwako.

    Ama kwa kiswahili fasaha tunasema, comments zangu “unazibeza”. Sio mbaya, tuwemo katika kutoa maoni, wasomaji watapata majibu sahihi. Nani anayejua asemacho, na nani asiyekijua apayukacho ilimradi na yeye anataka naye asikike.

    It’s Great To Be Black=Blackmannen

Leave a Reply