Umewahi kusoma makala zake,vitabu vyake na pia kusikiliza muziki wake.Jina lake sio geni.Nimeshawahi kufanya naye mahojiano. Anaitwa Freddy Macha,mtanzania mwandishi,mwanamuziki mwenye makazi jijini London nchini Uingereza.
Mwezi wa Mei mwaka huu,Freddy aliitikia wito wa kurudi nyumbani Tanzania na kugawana na wengine ujuzi mbalimbali alionao katika masuala ya uandishi,fasihi, muziki, maisha ya ughaibuni, mazoezi,afya na chakula bora. Alifanya hivyo kupitia semina mbalimbali alizoziendesha pale British Council,Soma Cafe(Mikocheni), Shule ya Sekondari Mwandege na Nyumba ya Sanaa.
Semina alizozifanya Macha ziliandaliwa na Jarida jipya la Lucky-Ideas For Living.Freddy anatarajiwa kurudi tena Tanzania mwezi Septemba mwaka huu ili kuendesha semina zingine.Usikose

Freddy Macha akiongelea uandishi wa vitabu na makala.Hapa ilikuwa Nyumba ya Sanaa jijini Dar-es-salaam.

Freddy akimuelekeza mmoja miongoni mwa waliohudhuria semina jinsi ya kufanya mazoezi ya tumbo.
Page 1 of 3 | Next page