MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

q

Success belongs to risk takers.Wanaosema hivyo wanajua kwanini wanasema hivyo. Kwa Q-Chillah ambaye hapo zamani tulimuita Q-Chief, inaonekana ukweli huo unakwenda sambamba na mienendo yake kwa sasa.

Hivi majuzi alibadilisha muonekano. Kutoka Q-Chillah mwenye rasta(rasta za fasheni lakini na sio zile za imani) mpaka Q-Chillah unayemuona kwenyepicha hapo juu.Kutegemea na utashi binafsi wa mtu wapo wanaosema kapendeza kwa sababu sura imeonekana vyema nk na kuna wanaosema hapana…bora alipokuwa na rasta. Maneno ya mtaani pia yapo kama kawaida; Q-Chillah “kafulia” na hivyo faranga za kutunzia rasta zimeingia mitini.Yote hayo ni maneno tu au vijimambo.Muhimu ni jinsi yeye mwenyewe anavyojisikia.Uhuru binafsi alionao mtu inabidi upewe nafasi jamani.

Yote tisa,kumi katika kuthubutu kwa Q-Chillah ni kubadilika katika aina ya muziki anaopiga.Mwenyewe anasema anabadilika kama utabiri wa hali ya hewa. Q-Chillah sasa ameingia kwenye mnanda au mchiriku kama unavyojulikana kwa wengine. Miziki ya Pwani hii.Kumbuka Q ameshajaribu pia taarab katika siku za hivi karibuni. Sikiliza kitu alichokuja nacho Q-Chillah hivi karibuni hapo chini.Wimbo unaitwa Zaka Zaka.Je huku ni kuonyesha kipaji alichonacho,kubahatisha au kuthubutu kupita kiasi? Can we still call this “Bongo Fleva”?

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

20 Responses to “TAKING SOME RISKS”

  1. Comment by mr degree on July 16th, 2009 2:58 am

    kipindi cha nyuma alikua kila nyombo aanayotunga lazima amsakame baba yake wa kumzaa! yule mzee hakuwahi ku react na hivyo kumpa nafasi mwanawe kuendelea kuuza nyimbo za kumtusi na mbaya zaidi hela alizokua anapata kwa kumsanifu baba yake alizitumia kwa kuchukua machangu na pombe! sasa laana ndio hiyo inayomkumba sasa hivi kila anachofanya hakiendi sawa,ataimba kila style, ataishi mombasa, atanyoa rasta nk.lakini bado mambo yake yataenda kombo tuu.binafsi simtabilii mwisho mzuri huyo kijana soon atachanganyikiwa kabisa! kumtusi mzee sio kitu kizuri hata kidogo

  2. Comment by Gervas on July 16th, 2009 6:38 am

    Haya watani zangu Wazaramo na wakwele kazi kwenu nampa shavu Q kwa kukumbuka asili. Maana kuna hatari hii miziki ikapotea huko mbeleni na itaitwa ya kishenzi kama tamaduni zinginezo za kitanzania zinavoitwa tayari. Na ili uucheze vizuri mziki kama huu inabidi unywe kwanza Mnazi au ulanzi na sio bia.

  3. Comment by marknigga salamba on July 16th, 2009 12:00 pm

    usanii au art ni kubadilikabadilika kama hewa au kinyonga.mark salamba oz land

  4. Comment by kweliman on July 16th, 2009 1:38 pm

    Let me begin with Mr Degree. I certainly do respect your comment,don get me wrong.However,as appropriate as it might sound to you,brother,wouldn’t it be fair to respect Q chila’s privacy?In my opinion i would only describe your comment as TMI-too much information, That would be a very personal issue,if he has issue with his father.I dont ,under any circumstatnces,appreciate you ripping sombody’s privacy,just like that.Q Chillar has got to have his privacy respected just like yours too!.How does this sound? hes got issues with his father,so who cares! ,that is too personal,and i strong believe it would serve nothing good to BC members any way.But with all this,i do recognise and respect your freedom of expression .I dont mean to be nasty unnecessarily ,I dont wanna shut the heck out of you either .Sorry for any mis understanding on this one brother

    Q CHILLAR
    Now ,check this out Q-Chillar,your song is absolutely amazing. A music geneous!i can certainly call you just that .If you talk about crossovers and experimentals,personally i think you are way over the top!.It’s your ability to crossover into other genres.That,alone has got me on the hook.Sereously.Am not a big fan of Bongo flava or any kind of synthetically produced music.But the sounding of your song is way too unique.It has got me listening over and over.Categorically i would not say exactly what gives this song that edge.But there is something in it,definately, artistically.
    One good thing however, i noticed ,The sounding of every part of it is virtually original.Listen to the sounds of horns,strings,bass,and the singing itself,
    They don sound like congolese at all or even anything like Zouk,Kwaito and all that.Personally i found it unique,original and most of it soungds absolutely Tanzanian.Oh my God!if all other artist could learn this.I believe this is the way to go,in my oipinion,even though still everything is relatively produced syntheticlly and the music itself sounds just that.Q Chillar,i loved your song ,lots of potentials in it .This kind of attempts/risks are worthy if some artist could.We wanna hear that great TANZANIC SOUNDS LIKE THIS ONE.Anything and TANZANICALLY good music is all what we want.Folks you have our support, These kind of genre would definately pave way for some great Tanzanian music, bearing exclusively nothing but our own identities,regardlessly
    Great job Q Chillar .My complements

    PLAY ARTISTCALLY,ORIGINALLY.ACOUTICALLY AND MOST IMPORTANT TANZANICALLY
    Kweliman

  5. Comment by chapombe on July 17th, 2009 7:34 am

    mi sifikiri ni vizuri kama kila artist kutoka nyumbani akifanya kitu watu waongee tofauti naye.ok.mi nipenda hii nyimbo lakini sikulazimishi na wewe uipende.kuhusu yeye,huyu kijana mi nilikutana naye miaka ya nyuma kidogo,wakati ule ana-hang sana kati ya jiji,nafikiri ndio ilikuwa anajaribu kutoka.hapa naweza kumwelezea kama ni mtu wa kawaida,mpole au tuseme hana makuu au dharau,ni wakawaida tu.sema kila mtu ana mawazo yake,na hapa BC naweza kusoma tabia za watu kwa maoni yao tu…baadae

  6. Comment by Mickey Jones - Denmark on July 17th, 2009 7:49 am

    “COMMENT HIS PIECE OF ART NOT PERSONAL LIFE”

    Mchangiaji wa kwanza anayejiita Mr Degree kufuatana na mtazamo wake wa kibinafsi ingawaje tunauheshimu,lakini ingekuwa vizuri kwanza kuelewa pande zote mbili za matatizo kati ya msanii na wazee wake kabla hajatupa mtazamo wake.

    Msanii huyu Q-Chillah anayefanya mabadiliko ya mziki kufuatana na mabadaliko ya masoko ya utangazaji na uuzaji ulimwenguni,wasanii wa mziki wa kizazi kipya wapo wengi kwa sasa,mabadilisho ya mziki kila wakati kwa msanii ni kuonyesha kipaji cha msanii.

    Mchanganyiko wa mziki wa kisasa na zilipendwa “pwani na rumba” kufuatana na utaalamu wa studio za kisasa,tunaweza kuita “Bongo Fleva” kufuatana na soko la utangazaji na mauzo,linalopigana na “pirates” wezi wa mtandao wa “down loading” bila ya kibali cha makubaliano.

  7. Comment by mkaku on July 17th, 2009 10:34 am

    mr degree umefulia maneno kweli hapa si mahala pake ungesikiliza mnanda useme umeupenda au huupendi, qchilla anasauti ya pekee ananimaliza anavyoishusha, kuipandisha na kuitetemesha sio wengine kushuka na kupanda hawawezi kazi kubana pua

  8. Comment by Nancy on July 17th, 2009 12:01 pm

    Q chilla!! good job.. watu bwaaana, what is exactly bongo flavour? Hapa Q chilla amefanya kitu muhimu saana. amechukua utamaduni wa Tanzania na ku create a good song, with tremendous sound. This is what I call Bongo flavour, ina flavour ya bongo yenyewe. Badala ya kusapoti utamaduni wetu, tunaanza kumponda. wakiimba kama kina 50 cents tunasema oooh, wanasahau utamaduni. Watanzania inabidi tukae na tujiangalie tunataka nini..
    This is perfect song Q. Keep it up.

  9. Comment by SaLaMa on July 18th, 2009 2:13 am

    QCHILLA YANI WEWE KWELI MSANII NAPENDA SANA UBUNIFU WAKO YANI HUO MNANDA NI BABU KUBWA ACHANA NAO WASUUZA VINYWA NDIO ZAO KUBWABWAJA

  10. Comment by Mattylda on July 18th, 2009 2:44 am

    Mr Degree hujaacha tu kuingilia personal decisional za watu???nakupa 5 kweliman well said!!!!!!!QCHILLAH U LOOK GUD & THE SONG IS SO LOVED!

  11. Comment by NAIRA on July 18th, 2009 5:38 am

    DUH YANI MZUKA UMENIPANDA MIE UNANIKUMBUSHA MBALI SANA WE MWANA QCHILLA KWELI HAWAKUWEZI UPO KILA SEHEMU KAMA KITUNGUU SASA UJE UTOE NA MDUARA MWANA WANE VIPI NILISIKIA UMEIMBA NA TAARABU MBONA SIJAONA JAMENI SAUTI MASHALLAH.

  12. Comment by pk on July 19th, 2009 4:19 am

    huyu degre ana yake kasisa!!!!!!!!!!!!hizo tabia za uswahilini kama magazeti ya GPL ya kufuatana na watu kutaka kujua matatizo binafsi sio nzuri kabisa.sisi kwa msanii tunataka burudani ituliwaze na kutukumbusha home kiaina.maswala ya bibi sijui babu ,mjomba,sijui laana ya baba hatuna time nayo.hivi nani kati yetu hana matatizo katika familia yake?tukuwe wabongo achana na tabia za kishamba kama kina mark mushi.

  13. Comment by Dinah on July 19th, 2009 4:50 am

    Mafanikio ya “kazi yangu ya Dukani” by Dogo Mfaume ndio imesababisha Chillah kutoka na Mnanda?

    Kweli Para limekutoa vema sana.

  14. Comment by zaina on July 19th, 2009 10:51 am

    Hongdera Q Chillah!

    Nimeupenda huo mchiriku sanaaa, wow! kaka yangu unakipaji sana . songa mbele waache waziba riski kama degree waendelee kuziba, ila hiyo ni riski yako tangu ungali tumboni [kuimba]. kuhusu kunyowa u stil looking goooood bro! Big up Q

    Wewe degree wewe! hivi unajuwa nikiasi gani inauma kwa mzazi wako kutokuwepo katika maisha yako!? mimi mwenyewe nikipata nafasi ya kuwaonyesha wazazi wangu uchungu nilionao kwa wao kutonijali ama kuwepo kwenye maisha yangu nitashukuru. iwe kwa nyimbo ama kwa kitabu ama kwa movie!
    kuna wazazi wengine wanastahili kuambiwa ukweli , sio unakaa kimya kwa ajili ya heshima ya uoga lkn moyoni unauchungu kwa yale mzazi wako aliyo kufanyi! inauma wewe, hongera Q kwa kumwambia mzee wako ukweli.
    Kama ha kukufa ototoni wakati ulikuwa ukihitaji msada wake , wanini tena ukubwani! u know? inauma saaana jamani kama hayajawahi kukuta huwezi juwa uchungu wake dergee ! so, fikiri kabla hujasema ndio ubinadam.

  15. Comment by Mickey Jones - Denmark on July 20th, 2009 9:05 am

    “Q-CHILLAH AMEIBUKA NA-FUTURE-BONGO FLAVA”

    Kufuatana na mtazamo wa wengi katika kuutenganisha mtazamo wa MR Degree inatupa
    imani kama kweli Q-Chillah na wote wanaohusika katika mpangilio wa “ZAKA ZAKA”
    utungaji wa shairi,upangaji wa vinanda na sauti ya kupanda na kushuka yenye uzito mkubwa wa kipaji cha mwanamziki anayestahili
    kupata nafasi ya kutuwakilisha kimataifa kama watajitokeza wadhamini kuendeleza vipaji vya ” new bongo flava” tofauti.

  16. Comment by ZEINA on July 21st, 2009 1:49 am

    BC TAFADHALI HEBU TURUDISHENI NYUMA YA HUU WIMBO WA QCHILLA MTUWEKEENI HAPA ILI MR DEGREE AONE MANENO YALIYOPO HUMU.MIE JAMANI UNANILIZAGA SANA WIMBO HUU.

    INAUMA SANA UNAJUA INAKERA SANA UNAJUWA ETI BABA YAKO YUPO ILA HAKUJALI ANA TAIMU NA WEWE MOYO WANGU MOYO WANGU UMESHINDWA KUMSAMEHEEEEEEEEEEEEEE
    KAONA MTOTO KAIBUKA NA KIPAJI CHAKE CHA KUIMBA ANAJIDAI KUJILETA LETA NI KUMTIMUA TU.

    QCHILLA WEWE SONGA MBELE WATU WAKUOMBEA DUA LA KUKU HUMU ILA WAJUWE HALIMKUTI MWEWE HONGERA SANA UKO JUU MIE NASUBIRI KWA HAMU VIDEO YA HUO MCHIRIKU WAKO.NAJUA ITAKUWA BOMBA.

  17. Comment by Jamaa fulani hivi on July 22nd, 2009 11:20 am

    Si mchezo Qchilla ameibuka na mchiriku tena……inanikumbusha mbali sana hii kitu

  18. Comment by marknigga salamba on July 22nd, 2009 12:50 pm

    KUIMBA,KUCHEZA,KUPIGA VYOMBO.vyote hivi ni USANIFU.watekeleshaji,wana nafasi kufanya au kugeuza,kuongeza,kuuiga.maana vyote ni UTENZI.Q-Chillah.hivi leo akiimba kiarabu,kizungu,kindengeleko,kirusi au luga yeyeto.mie ntamuunga mkono,na sio yeye tuu,wasanii WOTE.duniani.hta kama sielewe luga mradi wakichanganyisha,mzik murua.je wewe,unayowakashifu,au kuwazarau,WAWEZA NINI .waweza kuimba tukupe mike,waweza kupiga tukupe gitaa,waweza kucheza tukuuimbie,wewe nini.sio utu TOA SIFA.ni huu ndio uhai.mark salamba australia.

  19. Comment by Alexander Ntonge on July 29th, 2009 2:22 am

    duuuuh! kumbe dogo ni bonge la handsome yaan angenyoa b4 ya lile shindano la sexiest man in dar, angeshinda. Thats goog guy, I blv in Bible that for Men to hav a long hair is not Good so kijana we do watever u like bcse no body feeding u…………

  20. Comment by maggie on October 7th, 2009 2:14 pm

    hahaha umefuliaaaaa

Leave a Reply