
Obama aliposhinda katika uchaguzi wa Marekani na hivyo kuwa Rais wa kwanza mweusi,wapo waliotabiri kwamba ushindi huo ni mwanzo mpya wa watu weusi duniani.Ni tumaini jipya.
Kama wewe ni miongoni mwa waliotabiri hivyo,bado unazo sababu za kuamini kwamba ulichokitabiri ni cha kweli.Hivi majuzi,huko Uingereza,kwa mara ya kwanza katika historia ya mashindano ya urembo ya nchi hiyo,taji limekwenda kwa binti mweusi aitwaye Rachel Christie(20) kama anavyoonekana hapo pichani.
Je unakubaliana kwamba huu ni mwanzo mpya wa watu weusi duniani? Well..hata kama Rachel hasomi hizi blogs zetu za lugha ya Kiswahili,sisi tunampongeza kwa hisani ya weusi wote wanaoishi huko Uingereza.Najua ndugu zetu wabongo mpo kwa wingi tu…Reading,London,Manchester,Milton Keynes na kwingineko.Yes You Can.
Page 1 of 3 | Next page