Kwa muda mrefu Tanzania tumekuwa na tatizo la kukosa waandishi wa vitabu. Waliotakiwa kuandika wamekuwa wakilalama kwamba hata wakiandika hakuna wasomaji achilia mbali wanunuaji wa vitabu. Bila shaka aliyetoa “utani wa ukweli” kwamba ukitaka kuficha kitu na mtu mweusi asikione,basi kifiche kwenye kitabu,alikuwa ameiangalia Tanzania pia.
Tatizo hilo linaelekea kupata ufumbuzi. Pengine inatokana na mabadiliko ya kidunia ya sayansi,tekinolojia na mawasiliano au ni wakati tu umefika wa Tanzania nayo kuzinduka na kuamua kuingia kwenye ramani ya watunzi na wasomaji wa vitabu.
Hivi karibuni,aliyewahi kuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu nchini Tanzania,Edwin Mtei, ameandika kitabu. Kitabu kinaitwa From Goatherd to Governor ambacho kwa tafsiri ya moja kwa moja ya Kiswahili ni Kutoka Mchunga Mbuzi mpaka kuwa Gavana. Ni kitabu kuhusu maisha yake kikiwa na mengi kuhusu uhusiano wake na Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye kama wengi tunavyojua,hawakuelewana katika mambo mbalimbali ya sera za kiuchumi.Ukitaka kukinunua kitabu cha Edwin Mtei bonyeza hapa.

Mbali ya Edwin Mtei, aliyewahi kuwa Miss Tanzania 1999,Hoyce Temu naye ametoa kitabu chake.Kinaitwa Nayakumbuka Yote.Mbali ya kuongelea kuhusu maisha yake,kitabu cha Hoyce ni muongozo mzuri kwa wasichana ambao wanataka kuingia au tayari wamo katika sanaa ya mitindo na urembo.Kinacho kipengele cha “Maswali na Majibu” kuhusu sanaa ya urembo.Kukipata kitabu hiki bonyeza hapa.
Hoyce Temu wakati wa uzinduzi wa “Nayakumbuka Yote”
Huu ni mfano na muelekeo mzuri kwa nchi yetu na kwa wapenzi wa kujisomea. Bila shaka hatutaishia kwa Mtei na Temu bali katika siku za karibuni tutaona wengine wakijitokeza na kuandika. Utamaduni huu ni miongoni mwa tamaduni ambazo mimi binafsi naona zinafaa kuiga.Wenzetu ni mabingwa wa kuandika na kujisomea.Hongera Mtei.Hongera Hoyce.
Vitabu vyote vimetolewa chini ya usimamizi wa kampuni ya Mkuki na Nyota.
Feedback / Comments
16 Responses to “UMEWASOMA EDWIN MTEI NA HOYCE TEMU?”
Leave a Reply


sending...
wachaga bwana!
i think it is high time we get to know autobiographies of some tanzanians
Haki ya nani Kikwete umenichekesha mno. Umewaza nini mpaka kuwaza kabila? Katu sikuliona hilo hapo mwanzoni. Ila inapendeza kuwaona mamiss wa Tz wanaonekana kwa mazuri kwenye media kuliko wengine waliojaa makashfa mpaka wanatia kizunguzungu.
ningenda nikipate hicho kitabu cha Mr. Mtei halafu niapply hizo maprincipal zake, nikitegemea kutoka kimtindo
Papo hapo hivi karibuni kilitoka kitabu cha Simba wa Vita, Mzee Kawawa.
Papo hapo, hivi karibuni kilitoka kitabu cha Simba wa Vita, Mzee Kawawa.
Mzee Mtei safi sana kwa kuandika kitabu hiki na kwa kweli sisi vijana ni wakati wa kujua kutunza kumbukumbu zetu na, inapendeza mno.
Let me say this – “Well done BRAIN HERO”
Big up siz!!
looong tym gal!!qyt duu lol…so creative..sio kuwa na makashfa ya ajabu ambayo hayana faida sijui wanaona sifaa!!!keep it up mumyy
congrats you all, Mtei and Hoyce. What you did others may copy for their life. its good men!! Big up!
wachaga wako juu sana hongereni
hakuna haja ya kutaja ukabila kwa waTanzania. Kwani mnataka kutambika. Iwe kwa mazuri au mabaya ukabila tusiutaje. Tutukuze utanzania wetu
keep on moving never com back
SAFI SANA HUO NDO UJASILIAMALI.VERYGOOD.
ILIKE CREATIVE PEOPLE LIKE U.VERYGOOD,KEEP IT UP.
pale mwanzo kabisa sikumuelewe Kikwete alichomaanisha lakini Wachagga bwana wacha waitwe wachagga BIG UP