MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

china

Viongozi wengi wa Africa wapo jijini Cairo nchini Misri kuhudhuria kongamano kuhusu ushirikiano baina ya nchi zao na China.Rais wetu,Jakaya Kikwete,ni miongoni mwa viongozi wanaohudhuria kongamano hilo.

Sasa kama unavyojua,uhusiano wa China na nchi za Africa ikiwemo yetu ya Tanzania una historia ndefu.Kuna ambao wanasema China ndio nchi pekee duniani ambayo imekuwa “true darling” wa bara la Africa.Wanaosema hivyo wanaangalia vitu kama misaada kutoka China,unafuu wa kufanya biashara na China,masharti nafuu ya misaada na mambo kama hayo.

Lakini katika siku za karibuni,uhusiano baina ya nchi za Africa na China umekuwa ukiongelewa katika namna tofauti.Masuala ya biashara,masoko,misaada nk ndio yameshika hatamu badala ya habari za udugu na ujamaa zilizokuwepo enzi zile kina Nyerere na Mao walipokuwa wakipanda mbegu za ushirikiano wa China na Tanzania.Hapo ndipo suala la kujadili au kufanya tathmini za uhusiano au ushirikiano huu linapokuwa na umuhimu wa aina yake.

Mijadala mbalimbali inazuka kila kukicha.Swali lililopo katika kichwa cha habari hapo juu ndilo linasumbua.Nani anafaidika zaidi na mahusiano haya? Je China wanafaidika zaidi au Africa ikiwemo nchi yetu ya Tanzania ndio inafaidika? Na bila kuficha wala kukwepesha macho,mtanzania wa kawaida ndiye anayefaidika au zaidi na uhusiano huo au ni viongozi wetu?Naomba kufungua mjadala.

Pichani ni Rais Jakaya Kikwete akiwa na Rais wa Misri,Hosni Mubarak huko Misri ambapo Rais Kikwete yupo kuhudhuria Kongamano la Ushirikiano baina ya China na Africa.Picha na Freddy Maro-Ikulu)

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

5 Responses to “AFRICA NA CHINA:NANI ANAFAIDIKA?”

  1. Comment by Jeston JM Mwkabuje on November 11th, 2009 5:00 am

    ki ukweli afrika tunafaidika hasa tz kaka yaan hawa jamaa hata kama kuna kitu wanatafuta kweli wamejipanga yani huwezi kuwashitukia kirahisi nilibahatika kuona walipokuwa wanajenga reli ya tazara sio siri jamaa wachapa kazi nawapa big up kwa mtizamo wangu afrika tunafaidika na uhusiano huu

  2. Comment by Sylva on November 12th, 2009 1:13 am

    Naungana na mdau hapo juu.Kiujumla kwa sasa jamaa wana nia ya dhati na bara letu (ukilinganisha na Marekani au nchi za Ulaya),cha msingi tuanze kuona mbele kabla ya kutokea hayajatokea.

  3. Comment by Lynn on November 12th, 2009 1:34 am

    Ama kwa hakika China ndio inafaidika saaana na Tanzani kiduuuuchuuuu.

    Lol!!!!

  4. Comment by Flora on November 12th, 2009 3:10 am

    From my point of view I see that China benefits more from African countries compare to what we receive from them if I look at the issue into details I see we only get nothing from China. We call as a country that work hand by hand with Africa but there support its irrelevant there so many companies in Africa occupied by Chinese e.g. construction where the majority top positions employees are Chinese few indigenous who work for them are treated like animals into their own country, they do hard/small job and get little wages the huge amount of money still go back to the Chinese. When I take a closer look the work done by these people doesn’t take even five years to prove that the job were done by expertise, so many fake materials are brought into Africa were we keep on wasting money to repair same thing within year and years. Bursaries released by Chinese to support Africa end up to be given to top official children’s.

    Medicine/products exported from China sold in African, those products have a lot of side effects the Chinese does not use the product, but are brought into Africa. One should have a question in mind women give birth let say 3 children and expect to use Chinese product to change their nature body want to make the sag breast into same shape as they were before giving birth or make their face to look younger, increase hips etc how does that work and what benefits do we receive from it? If not cancer, kidney failure, brain damage, not be able to conceive are those benefits we real want from China, milk for the Babies produced by Chinese killed a lot of innocent children luckily there were no one died in Africa unless if I did not get the news.

    African government are quite over the issues and letting Chinese to import the killing products into our country and kill our beloved fellow country mate who have no one to educate them. There so many issues uncovered between Africa and China and if we are not carefully we will be colonized by Chinese in the coming few years.

    Good day

  5. Comment by KICHEFUCHEFU on November 12th, 2009 2:41 pm

    ……@#@$$%%%^%^^^^^@#@####!……ngoja nikae chonjo…nisikilize…..na kutazama…..!….mmmmh……kiukweli…..nilazima tukubali kuwa shule ni muhimu…..ndio..maana…tunakaliwa…..na mataifa yote ulimwenguni…..hii inatokana na elimu finyu…na upeo….mdogo……ambao…..hutusukuma…..na kutupa kiburi…..na tabia….sizizo na manufaa……!

Leave a Reply