MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Warembo wanaoshiriki katika mashindano ya kimataifa ya urembo ya Miss East Africa 2009 wataanza kuwasili nchini wiki hii(au wameshaanza kuwasili) tayari kwa mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika tarehe 18 mwezi wa 12 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.

Aidha, warembo watakaoiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo wanatarajiwa kutangazwa kesho kutwa baada ya kamati maalumu iliyopewa jukumu la kuratibu zoezi hilo kukamilisha kazi yake.

Mashindano ya Miss East Africa mwaka huu yanatarajiwa kuwa na mvuto wa aina yake kutokana na Nchi zinazoshiriki mashindano hayo kuchagua warembo wenye viwango vya hali ya juu ili kuziwakilisha katika mashindano ya mwaka huu

Miss East Africa 2009 itashirikisha warembo kutoka katika Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Eritrea, Somalia, Djibouti, na Mauritius ambazo zote zimeshathibitisha ushiriki wao.

Mashindano hayo makubwa ya urembo kwa ukanda huu wa Africa yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Limited ya jijini Dar es salaam.

Miongoni mwa makampuni yanayodhamini mashindano hayo kwa mwaka huu ni pamoja na Kunduchi Beach Hotel & Resort, EATV, Kings & Queens Worldwide, CMC Automobiles Limited na AKO Catering Services Ltd.

Hizi hapa chini ni picha,majina na umri wa baadhi ya washiriki wa mashindano hayo.

East1

Rebecca Getachew (23) Ethiopia,

East3

Asli Osman Mahamud(20)-Somalia

East4

Fatma Abdilahi (18)-Somalia

East5

Dalysha Nirena Doorga (21)-Mauritius

East7

Tabitha(20)-Kenya

East8

Queen Belle Monique (23)-Burundi


Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

5 Responses to “HERE COMES MISS EAST AFRICA!”

  1. Comment by Del on December 1st, 2009 4:56 am

    the chicks wako hot ila mbona sioni m-tz?

  2. Comment by khalfan on December 1st, 2009 8:59 am

    Jamani huku si kuoneyana sasa yupo wapi Miss TANGANYIAKA wetu nasi tujivunie??

  3. Comment by DEOS on December 1st, 2009 9:53 am

    this will be fantastic context better

  4. Comment by siba on December 3rd, 2009 6:01 pm

    ina maana nchi ya ethiopia, mauritius na somalia na zenyewe ni east africa? mbona mnataka kuvuruga watu vichwa…..

  5. Comment by Stella Njovu on December 11th, 2009 10:43 am

    Hmm inaonekana kuna “samsin”behind..where is awa Tz malkia..im sure kawafunika wote…!!walioko wako fine,hawatishi kiviiile…ha ha haa

Leave a Reply