BONDIA Mtanzania anayeishi nchini Marekani Rogers Mtagwa anatarajia kupanda ulingoni Januari 23 mwakani kupambana na Yuriorkis Gamboa, pambano la raundi 12 litakalofanyika jijini New York.
Pambano hilo la ubingwa linalotambuliwa na HBO litakuwa la uzito wa Feather, ambako mabondia hao wanaendelea kujifua kwa ajili ya shughuli hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Marekani zinaleza kuwa Mtagwa ana rekodi ya kushiriki mapambano 26 na kushinda 13 kwa pointi, kupoteza mawili na kushinda kwa KO 18.
Mpinzani wake Gamboa amecheza mapambano 16 na kushinda kwa KO 14, mawili kwa pointi na hajapoteza hata pambano moja.
Aidha, mbali ya pambano hilo pia kutakuwa na pambano la uzito kama huo ambalo litamshirikisha Juan Manuel Lopez atakayezichapa na Steven Luevano.
Pambano jingine linalotarajiwa kufanyika siku hiyo jijini Pasay nchini Philippines, Donnie Nietes atazipiga na Ivan Meneses.
Source:Tanzania Daima
Feedback / Comments
4 Responses to “ROGERS MTAGWA ULINGONI TENA MWEZI UJAO”
Leave a Reply



Correction:
Mtagwa ameshinda mapambano 26, ameshindwa 13, amedraw mapambano mawili na kushinda kwa ko mapambano 18
hana rekodi ya kuvutia!
Hellow… yes jamaa yupo vizuri mmno ila anakosa support yawatanzania, Nitafute tufanye kitu flani coz huwa nawasiliana nae mpaka sasa ni my hommy kabisa kutoka mtaani Kekomwanga…
Ideeply agree with fightfan,Mtagwa won that battle!My opinion,now it’s only (mine)Mtagwa had won fight.