HIVI UMEMUELEWA MREMA?

Mrema

Zimebaki siku chache tuumalize mwaka 2009 na kuingia mwaka 2010 ambao kwa mujibu wa katiba ya nchi yetu,ni mwaka wa kupiga kura ili kumchagua tena mtu atayeongoza jahazi la nchi yetu kwa miaka mingine mitano.Tunauita mchakato huo “demokrasia”.

Tunapoelekea kwenye mwaka wa uchaguzi,tayari vibweka vya wanasiasa vimeshaanza kujitokeza.Nimesahau sio wanasiasa tu,hata wanajimu kama kina Sheikh Yahya.Wanasiasa wameanza kujitokeza na kumkingia kifua Rais aliyepo madarakani,Jakaya Mrisho Kikwete. Hawataki aguswe.Hawataki kusikia mtu anasema Kikwete alitoa “ahadi hewa” aliponadi sera ya maisha bora kwa kila mtanzania. Alijua haiwezekani lakini hakujali.Akajivika ngozi ya ukweli ya uanasiasa.Longolongo.Mageuzi huhitaji muda ati!

Miongoni mwa wanasiasa waliojitokeza ni Augustine Lyatonga Mrema. Anasema kama watu wanataka kumpinga JK basi waanzishe vyama vya siasa ili wawe wapinzani.Huna haki ya kumpinga Rais kama hujavaa kofia ya upinzani! Kuwa mwananchi,mzalendo,msema kweli na mpenda maendeleo haitoshi.Anzisha chama.

Mrema anatumia mbinu ya utaratibu.Anasema kama upo ndani ya CCM na unataka kumkosoa Rais,basi fuata utaratibu wa vikao vya chama na sio hadharani.Vikao vya chama huwa vinafanyika in closed doors! Kwa Mrema,hiyo ndio demokrasia ya kweli.Hajali kitu kinachoitwa Uhuru wa Habari na Uhuru wa Kujielezea.

Huyu ndie mpinzani ambaye huenda akawania Urais hapo mwakani!Ni Mwenyekiti wa chama cha upinzani cha Tanzania Labor Party(TLP).Watabiri wa masuala ya siasa wanasema Mrema keshakwisha kisiasa.Sasa anatapatapa.Ujumbe wangu kwa Mrema ni kwamba Mzee hatuendi hivyo.Wacha watu waseme,wajielezee.Kama JK kakosea,lazima aambiwe.

Page 1 of 3 | Next page