<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
		>
<channel>
	<title>Comments on: “NENDA KWA AMANI SIMBA WA VITA”-ZITTO KABWE</title>
	<atom:link href="http://www.bongocelebrity.com/2009/12/31/%e2%80%9cnenda-kwa-amani-simba-wa-vita%e2%80%9d-zitto-kabwe/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://www.bongocelebrity.com/2009/12/31/%e2%80%9cnenda-kwa-amani-simba-wa-vita%e2%80%9d-zitto-kabwe/</link>
	<description></description>
	<lastBuildDate>Sat, 11 Feb 2012 15:21:30 +0000</lastBuildDate>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
	<generator>http://wordpress.org/?v=3.3.1</generator>
	<item>
		<title>By: Mwanamke wa Shoka (UK)</title>
		<link>http://www.bongocelebrity.com/2009/12/31/%e2%80%9cnenda-kwa-amani-simba-wa-vita%e2%80%9d-zitto-kabwe/comment-page-1/#comment-33252</link>
		<dc:creator>Mwanamke wa Shoka (UK)</dc:creator>
		<pubDate>Sun, 03 Jan 2010 02:07:25 +0000</pubDate>
		<guid isPermaLink="false">http://www.bongocelebrity.com/2009/12/31/%e2%80%9cnenda-kwa-amani-simba-wa-vita%e2%80%9d-zitto-kabwe/#comment-33252</guid>
		<description>Oh what a touching obituary to Our very own Mzee Kawawa....We are already missing you!!

Kimito keep it up...you are really a proud Tanzanian....nchi inakuuma...but what can we do...hao wanaoajiriwa bOT eti wanajuwa kiingereza,...kiingereza chenyewe cha upupu mtupu...ni sawa na wanaoiuza Bongo kwa Wakenya eti kwa kuwa wanajuwa kiingereza....I am pissed off....

R. I. P. Mzee Kawawa...you were among the very few ones....and I can see no more...you all have departed now....We miss you.</description>
		<content:encoded><![CDATA[<p>Oh what a touching obituary to Our very own Mzee Kawawa&#8230;.We are already missing you!!</p>
<p>Kimito keep it up&#8230;you are really a proud Tanzanian&#8230;.nchi inakuuma&#8230;but what can we do&#8230;hao wanaoajiriwa bOT eti wanajuwa kiingereza,&#8230;kiingereza chenyewe cha upupu mtupu&#8230;ni sawa na wanaoiuza Bongo kwa Wakenya eti kwa kuwa wanajuwa kiingereza&#8230;.I am pissed off&#8230;.</p>
<p>R. I. P. Mzee Kawawa&#8230;you were among the very few ones&#8230;.and I can see no more&#8230;you all have departed now&#8230;.We miss you.</p>
]]></content:encoded>
	</item>
	<item>
		<title>By: kimito</title>
		<link>http://www.bongocelebrity.com/2009/12/31/%e2%80%9cnenda-kwa-amani-simba-wa-vita%e2%80%9d-zitto-kabwe/comment-page-1/#comment-33213</link>
		<dc:creator>kimito</dc:creator>
		<pubDate>Fri, 01 Jan 2010 05:51:29 +0000</pubDate>
		<guid isPermaLink="false">http://www.bongocelebrity.com/2009/12/31/%e2%80%9cnenda-kwa-amani-simba-wa-vita%e2%80%9d-zitto-kabwe/#comment-33213</guid>
		<description>Nimekuwa nikisema haya maneno kila siku hata kabla muumba hajamchukua simba wa vita.
Leo nayaandika tena. Laiti kama Nyerere na Kawawa wangekuwa ni hawa viongozi wa sasa basi tusingekuwa na mkoa wala wilaya. Nyerere na Kawawa wangeweza kugawana mikoa na kuiuza bila ya sisi kujua. Wakati wao nani alijua hata kitu kinaitwa hazina.
Wangechimba madini na leo tungekuwa na mabwawa yenye kina kirefu katika kila mgodi.
Wasingetuachia mashirika 450 na leo hatuna zaidi ya 10.
Kawawa hatujasikia hata siku moja mtu akidai wewe uliiba au ulifisadi hata senti moja.
Hatujasikia mtu akisema wewe umenyang&#039;anya wananchi Mashamba na unamiliki ekari 400 au 600 songea,Lushoto au Morogoro.
Umeishi maisha ya kawaida na hata ulinzi ulipewa tu kwa heshima kwasababu ungeweza kuishi mtaa wowote bila shida.
Watoto wako wamecheza chandimu na Nage. Hawa wa sikuhizi wanazaliwa Agakhan hatuwaoni tena wakirudi wanaajiriwa BoT kwasababu wanajua kiingereza zaidi kuliko kiswahili.
Tukiuliza tunaaambiwa uchunguzi unaendelea.
Kawawa wewe uliheshimu nafasi ya kazi na sio cheo,umefanyakazi na hata &#039;&#039;watoto&#039;&#039; wako kisiasa wakawa mabosi wako. Hukujali bali uvumilivu wa kisiasa ndio msimamo wako.
Wewe na Nyerere mkaunganisha makabila 120 na sasa tuna taifa. Eti wasomi sikuhizi wanatumia kitu kinaitwa BLOG kuchunguza waziri ni dini gani na kabila gani,mngekuwa wajinga kama hawa wasomi wa blog za jamii zetu siku hizi msingefanikiwa kumuondoa mwingereza. Kawawa tulidhani elimu ni ukombozi lakini ukisoma maoni ya wehu ndani ya blog kuhusu udini na ukabila utajua mumeacha kizazi cha mafisadi na wasomi wasiojua usomi zaidi ya kompyuta na key board. Wewe na wenzako hamkumjua mtu kwa dini wala kabila,la siku hizi ndio mada kwenye hivi vitu vinaitwa blog.
Kawawa msalimie swahiba wako Mwalimu na mwambie watoto wake kisiasa hawatakiwi kusema eti wakisema wanahatarisha usalama. Hata ile taasisi yake sasa inasakamwa na wenye nazo. Wananunua kila kitu na kifuatacho ni roho zetu.
Mwambie mwalimu watoto wake wawili kisiasa wameasi,baada ya yeye kuondoka wamegawana migodi na vituo vya maegesho,wakafungua kale kabenki kako kakubwa wakakomba wao na mafisadi. Mhakikishie mwalimu kuwa hawajakamatwa na tumekubaliana tuwaache wapunzike baada ya kazi nzuri ya kuuza kila kitu na kujigawia kilichobaki.
Mwambie mwalimu bado watoto wake wa kisiasa wachache wapo na ndio tunawategemea.
Kawawa mwambie mwalimu Uadilifu ni ujinga siku hizi. cheo si dhamana ni mtaji.
Tumepiga hatua hadi gavana anaishi kwenye jumba la bilioni na nusu, na kule kigoma na singida watoto wanasoma chini ya mti.
Naibu gavana ana nyumba ya bilioni moja na jirani tu hapa Dar kuna kituo cha afya hakina solar system mwaka sasa kwasababu matengenezo yake ni sh lakini tano na serikali haina fedha.
Mwambie mwalimu nchi imeendelea viongozi kama hawana VX hawana heshima,wewe na swahiba wako mlitumia Landrover eti wanasema ni ujima.
Jumamosi watakuja kukuaga watanzania,lakini pia mafisadi watakuja kushuhudia kwisha kwa enzi za Tanganyika huru. Huenda wakafanya tafrija!!!.

Msalimie Mwalimu, chediel mgonja,Amir Jamal,Dr Sterling,Kinjekitile,Mshume kiyante, Azizi Dosa,Dr Kleruu,mzee Mwapachu, Mzee Rupia, mzee Max Mbwana, Bibi TITI, Mzee Karume,mzee kombo jecha,Mzee Takadir,mzee Tambaza,akina Sewa haji,akina Abdulwahid,Mzee Bomani na wote mliomenyeka kwa ajili yetu.
TANGULIA SIMBA WA VITA NA UAMINIFU. TANGULIA UKAPUNZIKE KWA AMANI.BURIANI KAWAWA.</description>
		<content:encoded><![CDATA[<p>Nimekuwa nikisema haya maneno kila siku hata kabla muumba hajamchukua simba wa vita.<br />
Leo nayaandika tena. Laiti kama Nyerere na Kawawa wangekuwa ni hawa viongozi wa sasa basi tusingekuwa na mkoa wala wilaya. Nyerere na Kawawa wangeweza kugawana mikoa na kuiuza bila ya sisi kujua. Wakati wao nani alijua hata kitu kinaitwa hazina.<br />
Wangechimba madini na leo tungekuwa na mabwawa yenye kina kirefu katika kila mgodi.<br />
Wasingetuachia mashirika 450 na leo hatuna zaidi ya 10.<br />
Kawawa hatujasikia hata siku moja mtu akidai wewe uliiba au ulifisadi hata senti moja.<br />
Hatujasikia mtu akisema wewe umenyang&#8217;anya wananchi Mashamba na unamiliki ekari 400 au 600 songea,Lushoto au Morogoro.<br />
Umeishi maisha ya kawaida na hata ulinzi ulipewa tu kwa heshima kwasababu ungeweza kuishi mtaa wowote bila shida.<br />
Watoto wako wamecheza chandimu na Nage. Hawa wa sikuhizi wanazaliwa Agakhan hatuwaoni tena wakirudi wanaajiriwa BoT kwasababu wanajua kiingereza zaidi kuliko kiswahili.<br />
Tukiuliza tunaaambiwa uchunguzi unaendelea.<br />
Kawawa wewe uliheshimu nafasi ya kazi na sio cheo,umefanyakazi na hata &#8221;watoto&#8221; wako kisiasa wakawa mabosi wako. Hukujali bali uvumilivu wa kisiasa ndio msimamo wako.<br />
Wewe na Nyerere mkaunganisha makabila 120 na sasa tuna taifa. Eti wasomi sikuhizi wanatumia kitu kinaitwa BLOG kuchunguza waziri ni dini gani na kabila gani,mngekuwa wajinga kama hawa wasomi wa blog za jamii zetu siku hizi msingefanikiwa kumuondoa mwingereza. Kawawa tulidhani elimu ni ukombozi lakini ukisoma maoni ya wehu ndani ya blog kuhusu udini na ukabila utajua mumeacha kizazi cha mafisadi na wasomi wasiojua usomi zaidi ya kompyuta na key board. Wewe na wenzako hamkumjua mtu kwa dini wala kabila,la siku hizi ndio mada kwenye hivi vitu vinaitwa blog.<br />
Kawawa msalimie swahiba wako Mwalimu na mwambie watoto wake kisiasa hawatakiwi kusema eti wakisema wanahatarisha usalama. Hata ile taasisi yake sasa inasakamwa na wenye nazo. Wananunua kila kitu na kifuatacho ni roho zetu.<br />
Mwambie mwalimu watoto wake wawili kisiasa wameasi,baada ya yeye kuondoka wamegawana migodi na vituo vya maegesho,wakafungua kale kabenki kako kakubwa wakakomba wao na mafisadi. Mhakikishie mwalimu kuwa hawajakamatwa na tumekubaliana tuwaache wapunzike baada ya kazi nzuri ya kuuza kila kitu na kujigawia kilichobaki.<br />
Mwambie mwalimu bado watoto wake wa kisiasa wachache wapo na ndio tunawategemea.<br />
Kawawa mwambie mwalimu Uadilifu ni ujinga siku hizi. cheo si dhamana ni mtaji.<br />
Tumepiga hatua hadi gavana anaishi kwenye jumba la bilioni na nusu, na kule kigoma na singida watoto wanasoma chini ya mti.<br />
Naibu gavana ana nyumba ya bilioni moja na jirani tu hapa Dar kuna kituo cha afya hakina solar system mwaka sasa kwasababu matengenezo yake ni sh lakini tano na serikali haina fedha.<br />
Mwambie mwalimu nchi imeendelea viongozi kama hawana VX hawana heshima,wewe na swahiba wako mlitumia Landrover eti wanasema ni ujima.<br />
Jumamosi watakuja kukuaga watanzania,lakini pia mafisadi watakuja kushuhudia kwisha kwa enzi za Tanganyika huru. Huenda wakafanya tafrija!!!.</p>
<p>Msalimie Mwalimu, chediel mgonja,Amir Jamal,Dr Sterling,Kinjekitile,Mshume kiyante, Azizi Dosa,Dr Kleruu,mzee Mwapachu, Mzee Rupia, mzee Max Mbwana, Bibi TITI, Mzee Karume,mzee kombo jecha,Mzee Takadir,mzee Tambaza,akina Sewa haji,akina Abdulwahid,Mzee Bomani na wote mliomenyeka kwa ajili yetu.<br />
TANGULIA SIMBA WA VITA NA UAMINIFU. TANGULIA UKAPUNZIKE KWA AMANI.BURIANI KAWAWA.</p>
]]></content:encoded>
	</item>
</channel>
</rss>

<!-- Performance optimized by W3 Total Cache. Learn more: http://www.w3-edge.com/wordpress-plugins/

Page Caching using disk: enhanced

Served from: www.bongocelebrity.com @ 2012-02-12 05:53:52 -->
