
Binti au mrembo unayemuona pichani anaitwa Lilian Mduda(21). Huyu ndiye mwakilishi wetu katika fainali za shindano la kumsaka Kisura wa Afrika kupitia Mnet(Mnet Face of Africa) zinatarajiwa kufanyikia jijini Lagos nchini Nigeria tarehe 6 Februari/2010. Jumla ya warembo 10 kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika ndio waliofanikiwa kuingia katika fainali hizo na kwa maana hiyo ndio wataochuana.
Warembo wengine waliofanikiwa kufikia fainali wanatoka katika nchi za Angola,Ethiopia,Ghana,Kenya,Mozambique,Nigeria,South Africa,Zambia na Zimbabwe.
Lilian Mduda ambaye ni mwanfunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam akisomea Biashara(B.Comm), amesema amejiandaa vyema kwa ajili ya shindano hilo na haoni mshiriki yeyote anayemtisha isipokuwa ni yeye mwenyewe anayeweza kujiwekea mazingira ya kushinda kwa kuzingatia yale yote atakayoelekezwa na kuyafanya kwa ufanisi ili aweze kufikia malengo yake katika fainali hizo.
Lilian anapenda kusoma novels zenye hadithi za kimapenzi na chakula akipendacho ni wali na maharage.Ndoto zake ni pamoja na kuweza kutembelea jiji la Paris siku moja.Pia anapenda mpira wa kikapu(basketball) na hupenda kusikiliza mziki na kujisomea.Kila la kheri Lilian.
Ukitaka kujua zaidi kuhusu Mnet Face of Africa na warembo wengine wanaoshiriki,bonyeza hapa.
Feedback / Comments
23 Responses to “HUYU NDIYE MWAKILISHI WETU MNET FACE OF AFRICA”
Leave a Reply


no comment
Duh!!! Katika ukweli hubaki ukweli. Kwa jinsi nimwonavyo mimi huyu binti, kwa kutumia ujuzi wangu mwenyewe wa kumjua mwanamke. Watanzania tumechemsha tayari.
Hapo ni hamna kitu kabisa (kwa upande wa sura). Labda kama kutakuwa na miujiza ya aina fulani Lilian anaweza kushinda.
Tegemeo ambalo Watanzania tulisubiri kwa Lilian, ni jinsi atakavyokuwa akijibu maswali ya “Waamuzi”, kwa vile Lilian ni “Msomi”. Anaweza kutuondolea aibu ya kushindwa kwetu kwa kujibu kwa ufasaha maswali atakayokuwa akiulizwa na kujieleza.
Siku zote nitaendelea kuwatetea wanawake wote wa Kitanzania, na ninawapenda sana. Lakini panapo na ukweli ni muhimu niseme pia.
Lilian, kutoka moyoni mwangu. Nakutakia kila la kheri na Baraka nyingi katika mashindano ya “Face Of Africa”, na urudi na ushindi mnono. Usife moyo kwa maoni yangu hapo juu. Sura sio kila kitu dadaangu.
It’s Great To Be Black=Blackmannen
aaaiii y7a kweli hayo? mimi sikai paris ilaa najua kwamba ni romantic city in da world mimi hua kila december nitie maguu huko.so ww tuwakilishe vizuri mrembo wetu afu mimi ntakupa ofa ya kwenda paris 8 hotelini mimi
mdau araound
Nampa 3/10
NATURAL BLACK BEAUTY SIMPLY THE BEST
Wadau kama kutuwakilisha katika MNET FACE OF AFRICA chaguo letu ni la matumaini ya kuwepo katika kumi bora.
Wachagiaji kama mmojawapo wa wataalamu wetu BLACHMANNEN kimtazamo kunawezekana kuwepo na
mawazo tofauti tuyaheshimu yatachangia katika matayarisho ya DA`LILIAN kabla ya mashindano.
Ningewaombeni kurudia kuianglia tena kwa makini hali halisi ya maumbile na sura ya mwafrika katika maisha yetu ya kila siku anayotutangazia chaguo letu DA`LILIAN,bila ya kuwepo na aina fulani ya mchanganyo kuongezea kivutio cha kutuwakilisha katika FACE OF AFRICA.
Kimtazamo upande wangu chaguo letu limetupa hali halisi ya asilimia kubwa kimaumbile na sura zidi ya maisha magumu ya mtanzania, kuna siri ya uzuri wa kuzaliwa uliyojificha kwa wasichana wetu.
DENMARK
HE huyu sio NELLY LEMA ?kutoka moshi?/bukoba hongera sana dada usituangushe katika kinyanganyiro hicho muhimu tunakutegemea sana,..huku china
Sasa ndugu yangu BLACKMANNEN wewe unaona fahari kuwa mwafrika,lakini unaona sura ya mwenzio haifai kwenye haya mashindano,sasa naomba utuelezee sura ipi inafaaa ambayo hao majaji hawakuiona.
Uzuri wa sura ya mtu ni mtazamo wa mwonaji au muangaliaji mwenyewe na hayo ni maamuzi yatokayo katika halmashauri ya kichwa chake [Mpoki .et al January 20, 2010.BongoCelebrity],.ambapo kwa nje huonekana kama mtazamo wake binafsi na kama ni hivyo basi tunaomba ubakishe kwako huo mtazamo wako.
Huna haki ya kumwambia mwenzio kuwa sura yake haifai kwa sababu kuna wanaoina inafaa,nzuri,au ya kawaida,.sababu kila mmoja ana mtazamo wake ambao umetawaliwa na fikra zake binafsi.
Na pia Ukumbuke kuwa huna hisa katika uumbaji wewe,au tuseme wewe ndie umeteuliwa kuwa msemaji wake MUUMBA?Heshima haiuzwi bwana.Unachofanya wewe kufastrate wenzako wakati wewe mwenyewe hujijui wengine wanakuonaje na wanajiheshimu ndio maana hawajakwambia.
jamani face of africa sio kuwa na sura nzuri kama miss world!! wewe unayejiita blackmamen sijui mannen acha kumvunja moyo binti wa watu..wewe tundika picha yako tukuone kama ungepita first round had if there was a male version of face of africa!!!
She’s got killer looks and she is sexy too but she is too tiny and skinny…so much for perception!!!
She looks like a ten year old girl with an eating disorder!!!!
So far so good,
Afterall vigezo vya ushindi ni vingi so hope she will make to her best kuhakikisha anashinda.
All the best lady!
hapo mie simo….
tanzania kuna warembo kushinda huyu.ni kama hajakula wiki nzima.hao majaji naona wlikula rushwa.huyu hafiki hata robo fainali
Mdau Bingo,
I might miss your point when you say “she`s got killer looks,sexy but too tiny and skinny.
Let me remind you,in every International competitions of “MODEL & BEUTY” that kind of tinny & skinny looks always counts and in many cases makes a difference.
I dont take your comment as one of critics but I`ll consider it as stepping stone to the preparations for our promising lady Lilian for the succes
Denmark
She is simply ordinary normal african girl with not a single uniqueness! Face of Africa wala hawatahangaika just one round she is gone! She is invisible!
You are beautifuly Lilian no matter what they say? Go girl and try your luck you rock.
Happy 2010!
MSICHANA KABAMBE.mrembo si kiwete,kipofu,si mwenye nunge,atembea kwa miguu.pongezi kwa wazazi wake.mema namuombea.mark salamba.sydney australia.
wapeni nafasi watoto wetu wajidai na kufanya wayapendao.dalili za maisha.kama wakiwa wizi bahati mbaya.maisha TAMBALA BOVU.mark salamba sydney austalia
hakuna ubaya kama wakitaka kuwa jesus.mohamad(swa).injinia,daktari na kazalika.waishi sasa.baadae nani ajua?mark salamba sydney australia
If she is tall as in over 5″9 or 10 with a good make over, hair, outfit and proper make up she defenately has a chance, if she is shorter than that then she might as well pack her bags and head home, no offence!
Mmh! ni ‘kimbau mbau’ mno lakini huwezi jua anaweza akaibuka mshindi.
Acheni kumponda kiasi hicho majaji walio mchagua sio wajinga
Hongera Lilian,
Umepita kumi bora, kumbe unaweza kuleta matumaini ya Tanzania. Majaji wetu kumbe wanazijua sura zetu.
Wengi tuliona kuwa, majaji itakuwa kwao rahisi kukuondoa katika hatua za mwanzo, maana hata sisi tunakuona kuwa hufai, kumbe unafaa kwa maoni ya majaji hao.
Kama nilivyokwambia huko mwanzo, nakutakia kila kheri , sura sio kama ni kila kitu dadaangu, japo kwa kukuangalia mimi nakuona huna sura nzuri!!! Hasa hayo mabega yako!
This Is Black=Blackmannen
wapeni nafasi wanene,wapeni nafasi wembamba,wapeni nafasi wenye madowido ya ambi na cheupe dawa,wapeni nafasi wana mama wote,dada zetu,binti wetu,wake wetu.UZURI WA WAKINA MAMA NI KAMA MAUA,rangi kila rangi,harufu kila harufu.mbona ni siri,mchaguwaje ndio ajuae.mark nigggga salamba sydney australia.