MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Mara ya kwanza tuliwasiliana mwaka jana.Akanieleza mipango yake,ndoto zake na mikakati aliyonayo katika kutimiza ndoto zake.Kama ilivyokuwa kwa mamilioni ya watu ulimwenguni, Babu Sinare ambaye kisanii anajulikana kwa jina la Albino Fulani, alikerwa na kuhuzunishwa na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi(albino) kwa imani za kishirikina. Kwake yeye,ilikuwa ni kama vile wametonesha kidonda ambacho alidhani kilishapona kwani Babu Sikare ni albino pia.

Miongoni mwa mipango yake ilikuwa ni pamoja na kuanzisha NGO yake ambayo italenga kusaidia albino wengine.Kupitia muziki wake,aliahidi kwamba atazidi kukemea mauaji ya albino.Hakuwa anatania.Alianzisha shirika lisilo la kiserikali na kuliita Afro-Bino. Matunda ya shirika hilo yameanza kuonekana.

Pichani juu ni Babu Sikare(kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa Huduma za Hospitali kutoka Wizara ya Afya, Dr. Magreth Mhando (kulia) karatasi yenye maelekezo ya msaada wa mafuta ya kuzuia ngozi isiharibike na jua kwa ajili ya watoto wenye ulemavu wa ngozi Tanzania (Albino) yenye thamani ya dolla 1,500. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ustawi wa Jamii Bi. Magreth Njimba.

Kutoka moyoni,naomba kumpongeza Babu Sinare na shirika zima la Afro-Bino.We salute you and we support you.

Albino Fulani anatamba pia na wimbo wake Barua Kwa Mama.Bonyeza hapa kuusikia.


Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

3 Responses to “WELL DONE BABU SIKARE”

  1. Comment by Kijazi on February 8th, 2010 3:42 am

    Safi sana kaka….. Una muelekeo mzuri..Iwe fundisho kwetu sote kuwa na moyo wa kujitolea

  2. Comment by Kakalao on February 9th, 2010 2:02 am

    Nimevutwa sana na huu moyo!!!! Vry Nice!

  3. Comment by bob on February 9th, 2010 9:32 pm

    Safi sana Albino fulani!!People say dont forget where u com from!!!!

Leave a Reply