Kama nilivyokuahidi wiki kama mbili zilizopita,huu hapa ni wimbo,re-make ya We Are The World ambayo imefanywa na artists wanaotamba hivi sasa ikiwa ni miaka 25 baada ya We Are The World ya kwanza.
Kwa mtazamo wangu,pamoja na kwamba najumuika na walimwengu wote katika kuunga mkono juhudi kama hizi za wanadamu kusaidiana na pia ukweli kwamba wimbo huu haukutengenezwa kwa minajili ya kushindana bali kusaidia wenzetu wa Haiti,nadhani bado We Are The World original ilikuwa ni bomba zaidi! Naona kama vile zamani kulikuwa na waimbaji kuliko sasa.Kwa mtazamo wangu,auto-tune inapunguza vipaji.Wasanii wengi wa sasa wanajenga tabia ya kuwa tegemezi na vifaa vya studio kiasi kwamba linapokuja suala la kuimba bila vifaa hivyo,panakuwa na utata kidogo.Wewe unasemaje?
Itazame We Are The World original kwa kubonyeza hapa na kisha We Are The World-remake hapo chini
You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video
Page 1 of 3 | Next page