Bila shaka utakubaliana na mimi nikisema kwamba ni vigumu kuongelea wachora katuni maarufu katika Afrika ya Mashariki bila kumtaja Godfrey “Gado” Mwampembwa.Katuni za Gado sio tu ni maarufu bali pia zimewahi kuamsha hisia kali za wahusika. Si unakumbuka jinsi ilivyokuwa Gado alipowachora waandishi wa habari wa kwetu kwamba wanalamba viatu vya mheshimiwa? Unakumbuka jinsi mjadala ule ulivyokuwa?

Godfrey” Gado” Mwampembwa,mzaliwa wa Tanzania ambaye pia ndugu wa kuzaliwa wa Robert Mwampembwa(yule mchoraji wa katuni maarufu ya Bi.Mkora) hufanyia kazi zake nchini Kenya. Yeye ni Political Cartoonist wa magazeti ya Nation ya nchini humo.

Hivi karibuni aliongea na CNN kuhusu kazi zake na hususani kazi zake wakati “watani zetu wa jadi” walipoamua kuangushiana dhahma kufuatia uchaguzi mkuu wa nchini kwao miaka michache iliyopita.Hayo hapo mahojiano yake.

Feedback / Comments

Leave a Reply