Nimewahi kusema siku za nyuma kwamba mojawapo ya mambo ambayo nayapenda hapa BC ni kupata nafasi ya kumtambulisha msanii katika jamii ya watembeleaji,wachangiaji na washirika wa BC.
Leo ninayo furaha kumtambulisha Patrick Newman,mtanzania, msanii wa muziki wa Gospel ambaye makazi yake ni pale Seattle,Washington nchini Marekani.
Kimsingi Patrick sio mgeni katika anga za muziki.Kwa muda sasa amekuwa akifanya kazi zake nchini Marekani.Amewahi pia kufanya maonyesho kadhaa nchini Tanzania na hivi sasa anajiandaa kufyatua album yake.
Huu hapa ni wimbo wake unaoitwa Siku ya Kifo.Bila kujali dini yako wala kabila,ni wimbo wenye ujumbe mzuri sana.Je ukifa hivi leo marafiki zako watasemaje? Watasema mazuri yepi na mabaya yepi?Usikilize.Well done Patrick.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Zaidi unaweza kutembelea blog ya Patrick kwa kubonyeza hapa.
Page 1 of 3 | Next page