
Kama mimi na wewe tunashabihiana kifikra, basi ulikuwa unatamani siku hii ifike.Siku ambayo angalau kwa muda mfupi,utapumzika kusikia kwamba kila production mpya ya Bongo Fleva, inakuwa imeelemea kwenye hadithi na visa kuhusu mapenzi.Sio kusema kwamba hadithi na visa vya mapenzi havina nafasi yake katika sanaa,La.Ni kuonyesha tu kwamba jamii ni pana na kuna mengi zaidi ambayo sanaa inaweza kuyagusia.
Aliyesikia kilio hicho ni Heavy-weight MC,Prof.Jay.Wimbo unaitwa Msilie akiwa amemshirikisha mkali mwingine wa hip hop nchini Tanzania,Chid Benz.Wimbo umetengenezwa na producer ambaye amekuja juu kwa sana.Ni Lamar kutoka Fish Crab Records.
Mambo kadhaa yamenifanya niusikilize wimbo huu siku nzima.Kikubwa ni ujumbe uliomo ndani yake.Kama ambavyo ungetarajia kutoka kwa Prof.kwa kina anaangalia yale yanayojiri katika jamii.Anatoa hoja,anafafanua,anaelekeza.Msikilize;
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Feedback / Comments
37 Responses to ““MSILIE”-PROF.JAY Ft.CHID BENZ”
Leave a Reply


Prof, nimekuaminia mkuu, hiki kipande cha muziki kimetulia sana! excellent rhymes, terrific verses, outstanding vocals! Dude you rock!
safi sana cna mjadala na ww uko juu,endelea kukaza kaka
Nakubali Jay, wewe mwisho.
Nimekupata mdogo wangu Prof.Jay.
…mabilioni ya BOT yanakuuma…yep weye ni mwananchi nchi inakuuma….nakupa tano kaka…
Muziki umetulia saana, ujumbe ni mzito…sauti ni nzuuuri saaana…keep it up.
ukisikia mambo tunayoyataka ndio haya,.safi sana prof yaani nakuaminia,kiswahili safi,mashairi yaliyopangika.Hadithi zenye sehemu ya maisha tunayo ishi nayo, safi sana.wewe mghani makini.
Naamini kwamba hakuna kijiji kisicho na mzee anayetegemewa kwa mawazo.
Na hata kama wasanii watakuwa wanapotea na kusahau vitu muhimu vya kuimba Prof. Jay ataibuka tu na kuwakumbusha kama ambavyo tumekuwa tukiona.
So guyz, huyu ndiye mzee wa kijiji cha “Bongo fleva”. Big up men. Nakuaminia as always.
HANDS DOWN!!!!!!!!!!! u gt it son!!!!!!!
Nimekupata mdogo wangu Prof.Jay.
…mabilioni ya BOT yanakuuka…yep weye nj mwananchi nchi inakuuma….nakupa tano kaka…
Muziki umetulia saana, ujumbe ni maito…sauti ni nzuuuri saaana…keep it up.;
Kaza kaka kazi unaweza we ni zaidi ya kichwa
Huyu Dogo anafanya kweli haigizi.Tatizo la wasanii wengi wanaigiza Lakini huyu tangu nianze kumsikia kwenye chemsha bongo hadi leo sichoki.Hongera zake mpeni.
Kila nikisikia vibao vyenye maudhui kama hiki, natamani kupiga marufuku bongofleva zingine zinazorudia rudia nyimbo za kupendana pendana. Nani kasema unaweza kupenda na njaa tumboni. JIZE lete mambo. HAPO VIPI? Nasema hapo sawa mtu wangu!!!
vocals are okey, good truck generally!
But sauti ya Shawn carter mwanzoni..mhh!
Mengi wamezungumza wadau kweli kaka hupo juu kama povu labia aminia.
I always liked Professor Jay and i always anticipate on what new he’s got cooking.Well done bro….
MKUU B.C. mbona kimya bwana unatunyima uhondo bwana,.Sisi wengine kwa sasa tupo mbali na bongo na haya ndio majanvi yetu, tunakutegemea wewe,naomba tuwekee post mpya basi mkuu.
The message is loud and clear. Big up Prof J.
big up sana proffesa.nilitamani sana kama chid angepata nafasi japo nusu verse apandishe mashetani kwenye goma hili.ebwana upo juu sana.
Kudos Prof. J
mara nyingi hhuna mpinzani kijana.kipu iti apu.
Liking the track, overall great track. The beat is smooth great production. On a criticism note, prof is contradicting himself on couple of bars, “mbona mnanunua silaha baada yakuwalipa walimu” and he goes on says “majambazi wanasilaha kuliko polisi”, never the less, i’m a fan…
Nianze kuungana na waliotangulia katika kusifia maudhui yako Kaka Joseph. Ni kweli kuwa wewe ni kati ya waimbaji wachache wenye kuimba mashairi ya maana katika sanaa hiyo. Unaigusa jamii halisi ya chini na kuwa “msemaji wa wanyonge” ukiuliza maswali mengi ambayo watu wa kima cha chini tunawaza.
Ni kazu nzuri saana na NAKUPONGEZA NA KUKUHESHIMU KWA HILI
Na sasa nirejee kwenye upande wa pili ambao naona una mapungufu. Na haya ni mapungufu ya ki-Utawala zaidi. Kwa Joseph kama msanii mwenye washabiki / mashabiki wengi, heshima kutokana na tungo zako na hata kukubalika kwa kazi zako, unastahili kuwa makini na mahala unapotengeneza nyimbo zako. Ninaloweza kusema ni kuwa MASHAIRI NI MAZURI SAANA ila midundo imepea na ina mapungufu makubwa katika kukusaidia kukua kimuziki. Kwa mashairi haya na aina ya muziki uutengenezao na ambao unaonekana kugusa matatizo halisi ya mTanzania, unastahili kuangalia namna ya kuingia katika midundo yenye uTanzania zaidi.
Ninaloamini mimi ni kuwa kama kuna watu wanaweza kupata midundo halisi na ya kiwango cha juu kutoka kwa wasanii wa nje, siamini kama ataona haja ya kumualika mtu ambaye anaigiza kuwa na midundo hiyo na hajaifikia.
Watayarishaji wa MUZIKI WA NYUMBANI ni lazima waheshimu na kutambua umuhimuwa kutumia zana asili katika kunogesha muziki wao.
Kwa hakika wanawaharibia wasanii kazi kwa kuwa wakati mwingine ni “beats” zinazoweza kumkosesha msanii “deal” la kutumbuiza mahala hata kama UJUMBE alionao unafaa na kujitosheleza kwenda kutumbuiza.
Na huu ni mtazamo wangu na natunza haki ya kukosea na kukosolewa.
Blessings
Thanks Prof… you remind me of my nigga 2 Pac. You are still the best rapper in East Africa and still at the peak of your skills which consist of much more than a great voice!!! like song writing, composing, message and you still have a voice. My kudos man…
wana comment huyu msani . ukisikia kibao chake kiko taiti sana . bingup sana mtuwa .hizi ndio nyimbo sio mapenziki kila siku watu tunataka ujumbe .mwana uko juu sanaaaaaaaaaaaaaaaaa. kaza
lakini sikuhizi bongocelebrity mnatuangusha kweli,yaani post moja inakaa mpaka inapata wajukuu bila kuona nyingine.kulikoni?sasa tuna-miss utamu,hii siyo bongocelebrity tuliyoizoea
Hi 2all friends here on BC! Prof Jay ni wa ukweli toka nimfahamu Jay mjukuu wa mzee Haule! Sijawahi kukosa hamu ya kusikiliza kazi zake! hii ni kali sana naikubali sana!
JAMANI HUKO BONGO CELEBRITY KULIKONI HAKUNA UPDATES NEWS KILA NIKIFUNGUA BLOG NAONA HABARI NI ZILE ZILE ZINA KAMA MWEZI MZIMA HIVI MBONA MNATUANGUSHA WADAU WENU,KWANI HUKO MTAANI HAKUNA UPDATES NEWS KULIKO KUTUWEKEA HIZI AMBAZO ZIMEEXPIRE
wewe Jay ni mkali baba’ake.
Wewe Prof. Jay ni mkali baba’ake.Pia Blog ya michuzi ni bab kubwa,inayoelimisha kutambulisha na kutoa changamoto mbalimbali kwa jamii.Justkeep it up.
keep it up mr. prof unatisha ile mbaya!!!!!! even zis blog of michuzi!! mzuka sana!!!!!!!!!!!!!1
jay upo juu sana ,tungo zako unaziandika vizuri sana na kuziwakilisha ipasavyo kadhalika.naipenda sana nyimbo yako ya Nisamehe uliyoimba na banana,vile vina umepangilia mzee.Ok big up kwa sana bro
prof unatisha ile kinoma na hilo songi lako lamsilie so keep it up men!!!!
nakukubali sana ackari wangu ni noma
kip it real kip it still jay lyk rocafellas jc let em know and no one 2 dis dat roger dat………….kip stunting bro’da 4rm anther boda! am gona bounc!
jay upo ju sana kazana
upo juu sn brooooooo!!!!!!mpango mzima
yooooooh prof! uko juu kinowma js wonnna hollla yu so kip it up men. jully from A twn
kwa kweli na ungana na wengine katika watu ninaowazimia wewe mmojawapo upo juuu kudadadeki