
Miongoni mwa mahojiano ambayo yamewahi kutia fora hapa BC ni pamoja na yale niliyowahi kuyafanya na Miss Tanzania 2007,Richa Adhia(pichani). Kama hukuwahi kuyasoma,unaweza kufanya hivyo sasa.
Sasa jana kuna msomaji mmoja kaniuliza;yuko wapi hivi sasa Richa? Kwa faida yake na ya wengine ambao wanaweza kuwa na swali hilo mioyoni mwao,jibu ni kwamba sina uhakika sana.Juhudi zangu za kutaka kufanya naye mahojiano mengine kuhusu anachotarajia kufanya baada ya kuvua taji la Miss Tanzania,ziligonga ukuta.
Ila kwa mujibu wa tovuti ya Miss Tanzania, Richa hivi sasa yupo jijini Dar-es-salaam akiwa amefungua clinic yake ya masuala ya urembo inayoitwa Beauty Clinic maeneo ya Mikocheni.Bado ana ndoto za kufungua chuo au shule ya masuala ya urembo.
Feedback / Comments
Leave a Reply


sending...