
Mkurugenzi Mtendaji wa Global Publishers & General Enterprises Ltd na mjasiriamali, Bw. Eric Shigongo(pichani), anatarajiwa kuhutubia nchini Marekani katika Mkutano maalum ulioandaliwa na Watanzania waishio nchini humo (Diaspora Council of Tanzanians in America – DICOTA).
Katika mkutano huo unaotarajiwa kufanyika kwa muda wa siku nne kuanzia Julai 1, mwaka huu katika jiji la Minneapolis, Marriott Hotel, Minnesota, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mh. Aman Abeid Karume, amealikwa kuwa mgeni rasmi. Viongozi wengine watakaohudhuria mkutano huo ni pamoja na maofisa waandamizi na wafanyabishara wakubwa kutoka Serikali ya Tanzania na Marekani.
Aidha, Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni ya IPP, Bw. Reginald Abraham Mengi, naye ni miongoni mwa wageni waalikwa wa mkutano huo ambao unafanyika kwa mara ya pili nchini humo ukiwakutanisha Watanzania waishio ughaibuni. Mada mbalimbali zitatolewa na Watanzania waishio ndani na nje ya Marekani.
Katika mkutano huo, Bw. Shigongo anatarajiwa kutoa mada itakayoelezea jinsi ya kufanikiwa kiuchumi katika mazingira ya Tanzania na anatarajiwa kuwahamasisha Watanzania waishio ughaibuni kuwekeza nyumbani Tanzania.
Katika siku za hivi karibuni, Bw. Shigongo amejipatia umaarufu kwa kutoa elimu, ushauri kwa vijana na wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo vikuu nchini kupitia mikutano na hafla mbalimbali anazoandaa au kualikwa kwa lengo la kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vijana wa kitanzania.
Kwa taarifa zaidi juu ya mkutano huo tafadhali tembelea ukurasa wa Diaspora Council of Tanzanians in America-DICOTA)
Feedback / Comments
4 Responses to “SHIGONGO KUHUTUBIA NCHINI MAREKANI MWEZI UJAO!”
Leave a Reply


sending...
BC –
Ratiba ya conference haioneshi kwamba Eric atahutubia, bali atakuwa panelist kwenye mada mojawapo – ” Unleashing the Diaspora Potential”. Kiongozi wa panel hiyo ni Dr. Lemmy Meekisho.
Kwa mantiki hiyo, habari uliyoiweka hapa inapotosha.
Mbona hii kitu haikutangazwa vizuri huku US?Nyie waandaji vipi?
BC,
Mimi napingana na jazzie hapo juu,kuhutubia mtu anaweza kuhutubia hata kwenye panel.Kwa hiyo sioni kosa.Panelists wote wanaweza kuhutubia kwa zamu halafu ndipo mada zingine zikaendelea.Chanzo cha neno ni “Hotuba”.tujifunze kiswahili jamani.
Eric you are the man, big up mchuchu.I am so proud of you.