Sijui kama nitakuwa nimekosea nikisema kwamba pengine AY na MwanaFA mpaka hivi sasa wanaweza kuwa wanashikilia rekodi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao wameshirikiana zaidi katika kazi zao.Kumbuka hawa wametoka mbali tangu enzi zao wakiwa East Coast Team iliyokuwa ikiongozwa na King Crazy GK ambaye sina uhakika yuko wapi siku hizi na anafanya shughuli gani.

Kuthibitisha kuzidi kukomaa kwa ushirikiano wao,AY na MwanaFA wakimshirikisha Hard Mad,wameachia single inayokwenda kwa jina Dakika Moja. Hii ni production kutoka B’Hitz Production iliyo chini ya Hermy B.

Sikiliza hapo chini;Ujumbe ni kwamba anaomba dakika moja tu aseme yaliyopo moyoni.Mmh,inawezekana kweli ndani ya dakika moja kikaeleweka?Sijui.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Feedback / Comments

Leave a Reply