
Naamini umeshasikia kuhusu sakata linalomhusu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,David Jairo.Hivi sasa swali ambalo sote tunajiuliza au twapaswa kujiuliza ni je,nani zaidi kati ya Bunge,Serikali Kuu au pengine hata mahakama?Sakata hili linatufundisha au kutupa picha gani?Tujisikie vipi kuona mhimili mmoja wa dola unaonekana kuuletea “dharau” mwingine?Isitoshe,bado tatizo la msingi(ukosefu wa umeme) bado lipo pale pale.Kuna dalili za kutatua tatizo hili la msingi kwa mwendo huu?
Photo credit:Greyson Mwase-Ofisa Habari,Wizara ya Nishati na Madini

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal leo Jumatatu Agosti 22, 2011 amekutana na Balozi wa Misri nchini Tanzania Wael Adel Nasr ambaye amefika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam kumuaga kufuatia kupangiwa kazi nyingine, ikiwa ni baada ya kukaa nchini kwa miaka minne.
Balozi Nasr ambaye sasa anahamia kitengo cha nchi za Afrika Mashariki na Kati kama mwakilishi wa Misri alimwambia Makamu wa Rais Dkt. Bilal kuwa kuwepo kwake Tanzania kumemfunza mengi na kubwa ni kuwa Tanzania ni nchi ya amani na upendo hali iliyomfanya kuishi bila kujiona mgeni katika kipindi chote alichokuwepo nchini.
Balozi huyo aliongeza kuwa, hali inayoshabihiana katika utamaduni na maisha sambamba na mahusiano ya kihistoria baina ya nchi hizi mbili ni miongoni mwa sifa nyingine ambazo zimeyafanya maisha yake nchini Tanzania kuwa mazuri, hali inayomlazimu kutamka kuwa anaondoka Tanzania kimwili lakini moyo wake upo hapa Tanzania.
Akizungumzia mapinduzi yaliyofanyika nchini mwake, Balozi Nasr amefafanua kuwa, mapinduzi hayo yatabadili kwa kiasi kikubwa sera ya Mambo ya nchi za Nje ya Misri ambapo sasa nchi hiyo itarejesha sera inayotazama mahusiano ya karibu katika kuleta ukombozi na utanuzi wa demokrasia katika Afrika, kama ilivyokuwa wakati wa harakati za kupigania uhuru wa nchi za Afrika.
“Kama unakumbuka ndege ya kwanza kutua Tanganyika ilitoka Misri tena ilitua saa mbili baada ya Tanganyika kutangazwa huru. Hii inaonyesha kuwa ndege ile ilianza safari ya kuja Dar es Salaam saa kama nne kabla ya kutangazwa uhuru wa Tanganyika na hili ni moja ya mambo tunayoyakumbuka sana katika mahusiano yetu na Tanzania,” alisema Balozi Nasr.
Kwa upande wake Makamu wa Rais Dkt. Bilal alimwambia Balozi Nasr kuwa anashukuru kwa maelezo mazuri aliyoyatoa juu ya Tanzania na kwamba anatambua mchango wa Misri katika maendeleo ya Afrika na akasisitiza kuwa ni wakati sasa Afrika kujitegemea kwa kuongeza mashirikiano katika kukuza uchumi wa wananchi wa bara hili.

T.I is about to be released from prison. Here is the letter to the world and especially his fans.
- KING


Ukirudisha kalenda yako(japo katika mawazo tu) miaka kadhaa nyuma, katika uwanja mpana wa Bongo Fleva utamkuta Mike Tee (jina kamili Mike Mwakatundu)…siku hizi anajulikana pia kwa jina Daddy.Ni miongoni mwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye alitamba enzi zile na nyimbo kama vile Ningekuwa Star kabla hajajikita zaidi katika utayarishaji(production) akiwa na studio yake ya MyKey Records pale Mji Kasoro Bahari.
Sasa baada ya miaka kadhaa ya kuibua vipaji vya wengine,Mike T anarudi kwenye game na wimbo Let Me Know.Hii ni production kutoka B-Hitz Studio na MyKeY Records.Listen to the track below and you be the judge!
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
CREDITS;
SINGLE: MIKE TEE – LET ME KNOW (TANZANIA)
PRODUCED BY: PANCHO LATINO
COMPOSED BY: MIKE TEE
STUDIO: B-HITZ / MYKEY RECORDS
SOUND ENGINEER BY: PANCHO
VIDEO BY: SHOWBIZ VIDEOZ MEDIA CO.
Genre: Bongo Flava & Rap

Rais wa zamani wa Cuba,Fidel Castro,mwishoni mwa wiki hii ametimiza miaka 85 tangu azaliwe mnamo August 13 mwaka 1926 huko Biran nchini Cuba.Akiwa na miaka 32,Fidel Castro aliongoza mapinduzi yaliyomn’goa madarakani Fulgencio Batista aliyetambulika kwa wengi kama dikteta.Katika mapinduzi hayo,Fidel Castro alishirikiana kwa karibu na mdogo wake Rais wa sasa wa Cuba,Raul Castro na rafiki yake mwanamapinduzi maarufu mzaliwa wa Argentina,Che Guevara.
Cuba ni miongoni mwa nchi ambazo zina uhusiano wa karibu na Tanzania.Mpaka hivi leo tunao wasomi mbalimbali hususani madaktari waliopata na wanaoendelea kupata mafunzo yao nchini Cuba.Happy Birthday Fidel.

The Revolutionaries,Che Guevara and Fidel Castro

Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO
Check out this video from another production by Bongo Records.G-Scent is a Nigerian artist.East Meets West.

It’s a weekend and it’s a time “kujimwaga”.Here is a club fav. of today,tommorow and day after.The music is from Bongo Records under P-Funk aka Majani and the video is by Karabani


sending...
