Mohamed Raza ni Msanii Maarufu wa kimataifa ambaye ni hazina Halisi ya Taifu letu la Tanzania, alianza kazi yake ya  sanaa za kuchora tokea enzi za Uhuru wa Tanganyika. Vizazi zaidi ya viwili vimenufanika na kuelimika kwa kusoma vitabu vyake tokea shule za msingi mpaka secondary hasa vya kiingereza kama familia ya Mr & Mrs Daudi na Mtakuja Primary School. Mbali na hapo Mzee Raza aliwahi kumchora Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere Miaka ya 1960 na kufanikiwa kupata kazi katika chama cha TANU. Pia aliwahi kufaya kazi katika ubalozi wa Marekani Hapa Tanzania miaka ya 70.Zaidi tizama video hii
You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Dr.Salim Ahmed Salim, former Secretary-General of the Organisation of African Unity and former Prime Minister of Tanzania, has been appointed Chair of the Prize Committee of the Ibrahim Prize for Achievement in African Leadership, on which he currently serves as a member. Dr Salim, who is also a member of the Board of the Mo Ibrahim Foundation, takes over from former United Nations Secretary-General and Nobel Laureate, Kofi Annan, who has chaired the Committee for the last four years.

In his new role, Dr Salim will oversee the selection of winners of the Ibrahim Prize, which recognises and celebrates excellence in African leadership.

The 2008 Ibrahim Prize Laureate, former President of Botswana, H.E. President Festus Mogae, will join Dr Salim on the Prize Committee. President Mogae is currently also the Chairperson of the Coalition for Dialogue on Africa and Founder of Champions for an HIV Free Generation. He was awarded the 2008 Ibrahim Prize for his outstanding leadership in ensuring Botswana’s continued prosperity in the face of an HIV/AIDS pandemic and for his careful stewardship of Botswana’s natural wealth for the benefit of citizens.

Dr Salim Ahmed Salim said of his appointment to Chair, “The success, or failure, of African countries is a function of our political leadership. It is no coincidence that visionary leaders such as our previous Laureates Presidents Chissano, Mandela and Mogae, have transformed their countries’ fortunes or amplified success in the face of huge challenges. That is why the Prize is so important – we have to recognise the vital role that leadership plays on the continent. I am delighted to be able to take forward the deliberations on what constitutes exceptional leadership, and to help provide a platform for African role models to be recognised and celebrated, and to continue in a life of public service after office.”

H.E. Mr Kofi Annan said, “It has been a great privilege and honour to serve as the first Chair of the Prize Committee of the Ibrahim Prize for Achievement in African Leadership. If there is one area, which above all will determine the direction of Africa’s future, it is the quality of its governance and leadership. For a continent at peace with itself requires more than the absence of war. It requires leaders to embrace respect for human rights, the rule of law, and transparent, effective and accountable governance. This is why the Ibrahim Prize is so important: it celebrates excellence in African leadership and encourages progress across the whole continent.”‘

read more

Miongoni mwa marais barani Afrika ambao walikuwa wananivutia sana ni pamoja na Rais mstaafu wa Ghana,Jerry Rawlings. Kilichonivutia zaidi ni historia yake na jinsi ambavyo alianza kuiongoza nchi ya Ghana.

Hivi leo inaaminika kwamba mafanikio ya kiuchumi na kidemokrasia iliyonayo Ghana ya leo, yalichangiwa kwa kiasi kikubwa na uongozi wa Jerry Rawlings. Hivi leo Ghana ni nchi yenye uchumi unaokua kwa kasi zaidi barani Afrika na hivi karibuni iliingia katika orodha ya nchi zinazozalisha mafuta ulimwenguni. Katika siasa au demokrasia,nchi hiyo inasemekana kuwa na demokrasia iliyokomaa zaidi barani Afrika baada ya kushuhudia mabadiliko kadhaa ya vyama vinavyoongoza. Alipokuwa anaondoka madarakani,chama chake ambacho ndicho kilikuwa chama tawala,kilishindwa kabla ya kuweza kurejea tena madarakani miaka nane iliyofuata.

Jerry Rawlings aliiongoza nchi ya Ghana kwanza kama “dikteta” kuanzia mwaka 1981-1992 kufuatia mapinduzi ya kijeshi aliyoyaongoza hapo awali.

Ilikuwa May 15,mwaka 1979 alipowaongoza maofisa kadhaa wa ngazi za chini kutoka Jeshi la Anga la nchi hiyo(akiwa miongoni mwa maofisa hao). Wakati huo Ghana ilikuwa ikiongozwa kijeshi. Kwa hiyo unaweza kusema yalikuwa mapinduzi ya maofisa wa ngazi za chini dhidi ya maofisa wa ngazi za juu. Kilichomsukuma Rawlings ilikuwa ni kupinga rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma uliokuwa umetapakaa kila kona( Unaweza kuita “ufisadi” ukipenda.)na kuporomoka kwa uchumi.

Jaribio la kufanya mapinduzi halikwenda vizuri.Jerry Rawlings alikamatwa na kupitia mahakama ya kijeshi, akawekwa ndani akisubiri kusikiliza kwa kesi yake. Lakini akiwa jela na kabla hukumu rasmi haijatolewa, kundi lingine la maofisa wa kijeshi lilivamia jela na kumtoa likimtaka awaongoze katika mapinduzi.

Baada ya kutolewa au kutoka jela,Rawlings akatangaza kupitia radio kwamba anaunda Armed Forces Revolutionary Council maalum kwa ajili ya kumuondoa madarakani kiongozi wa kijeshi aliyekuwepo madarakani.Alikuwa akiitwa William Fred Akuffo.

Zoezi hilo lilifanikiwa na Jerry Rawlings aliongoza harakati za aina yake katika “kuisafisha” Ghana ambayo yeye na wenzake waliamini ilikuwa imeoza kwa rushwa na ufisadi. Mghana mmoja ambaye alishuhudia harakati hizo anasema Jerry Rawlings alipewa support kubwa na vijana wasomi kutoka vyuo vikuu  ambao nao walikuwa wamechoshwa na mambo yalivyokuwa.

Vijana hao wakiongozana na maofisa wa kijeshi waliokuwa chini ya Rawlings,wakaingia kila kona ya nchi wakikagua vitabu vya kumbukumbu za kifedha nk. Endapo itaonekana kwamba wewe ndio chanzo cha rushwa na ubadhirifu moja kwa moja unakwenda mahakamani. Kwa sababu wakati huo nchi ilikuwa ni ya kijeshi,wengi miongoni mwa watu waliothibitishwa kuwa chanzo cha rushwa walikuwa maofisa wa kijeshi. Adhabu yao ilikuwa KIFO kwa kutandikwa risasi hadharani!

Miongoni mwa watu waliouawa hadharani ni pamoja na viongozi wa kijeshi waliopita. Hawa kimsingi walikuwa marais waliomtangulia wakiwemo Akwasi Afrifa, Ignatius Acheampong na William Fred Akuffo.

Wote waliuliwa hadharani ndani ya kipindi cha miezi mitatu tu tangu Rawlings na wenzake walipoanza zoezi la “kuisafisha” Ghana. Baada ya kuamini kwamba zoezi la “kuisafisha” Ghana limekamilika, Rawlings alijiweka pembeni na kupisha kuitishwa kwa  uchaguzi wa kitaifa huku yeye akiwa hayumo miongoni mwa wagombea. Yeye alirejea jeshini na kuendelea na kazi yake kama pilot wa ndege za kijeshi kazi ambayo inasemekana aliimudu vizuri sana.

Uchaguzi ulifanyika na Dr.Hilla Limann, akashinda kwa tiketi ya chama cha National People Party(PNP) na hivyo Ghana ikawa imerejeshwa katika serikali ya kawaida. Baada ya muda mfupi tu (September 1979 mpaka December 1981) Jerry Rawlings akaona Dr.Hilla Limann, anairudisha tena nchi kule ilikotoka.Rushwa ikawa imeanza tena kutapakaa. Ufisadi ukaanza tena kuota mizizi. Baada ya kuona hivyo,akaipindua serikali ya Dr.Limann na kutwaa madaraka tarehe siku ya mkesha wa mwaka mpya mwaka 1981.Akaitupilia mbali katiba iliyokuwepo,akalivunja bunge na kuweka sheria kuondoa vyama vya kisiasa.

Jambo la kwanza alilolifanya baada ya kutwaa madaraka ni kuunda   Provisional National Defence Council(PNDC) ukiwa na mchanganyiko wa wajumbe kutoka uraiani na jeshini na yeye Jerry Rawlings akiwa Mwenyekiti.Baraza hilo ndio likawa chama pekee cha kisiasa.

Kazi ya kwanza ya baraza hilo ilikuwa ni kuanzisha mchakato wa kuirudisha Ghana kwenye utawala wa kiraia ambapo kila M-Ghana angejisikia kwamba anacho cha kuchangia katika maendeleo ya nchi. Suala la huduma ya afya kwa wote lilipewa kipaumbele ambapo sera ya kuzuia maradhi ilitiliwa mkazo.

Mwaka 1992, Rawlings alistaafu rasmi kutoka jeshini na kuanzisha rasmi chama cha National Democratic Congress(NDC) baada ya kukubalika kuundwa kwa mfumo wa vyama vingi kufuatia mchakato uliofanywa na tume ya demokrasia(National Commission for Democracy) aliyoiunda Rawlings.

Katika uchaguzi mkuu uliofanyika baada ya hapo,Jerry Rawlings alishinda kwa kishindo. Alishinda tena uchaguzi mkuu miaka minne iliyofuata(1996) na hivyo kutokana na katiba akaiongoza tena Ghana kwa kipindi kingine cha miaka minne mpaka mwaka 2001 alipostaafu.

Jerry Rawlings alizaliwa tarehe 22 June mwaka 1947. Baba yake alikuwa ni mkemia kutoka nchini Scotland aliyekwenda kufanya kazi nchini Ghana(wakati huo ilikuwa ikiitwa Gold Coast).Alijiunga na jeshi la anga la nchi hiyo mwaka 1967. Yeye na mke wake Nana Konadu Agyemah-Rawlings wana watoto wanne.

Pichani ni Jerry Rawlings akisalimiana na Rais wetu Dr.Jakaya Mrisho Kikwete walipokutana hapo juzi nchini Ethiopia wakati wa mkutano wa Umoja wa Afrika(AU).Picha kwa hisani ya Mawasiliano Ikulu.

A few months ago when we were busy working on creating the few new pages that now appears on top (including this one of /on Health,Beauty and Fashion),one of our readers sent us an e-mail with a tough question; Who are Top 10 Fashion Designers in Tanzania?? It was a tough question because,with so many fashion designers in the industry right now,how do you pick just 10 best?

We promised to give it a try and finally we can answer that question not only in private but also in public for the benefit of others including yourself. But before we reveal our top 10,I’d like to mention that our list is in no particular order. It is random…

Second, what rationale  did we use in picking up our top 10? Just to mention a few of them…first it was creativity. Then we looked at how active a designer is in terms of his/her own work as well as the community at large. Participation and international recognition was also a  piece that we pushed into consideration.And of course marketability of the products was a factor. In marketability we considered how well someone’s designs are doing in local markets and also their online presence…things like that.

Below is our top 10. Who do you think we missed and in your opinion they should have made it into our list? Your comments.

Manju Msita

Fatma Amour

Khadija Mwanamboka

Mustafa Hassanali

Jamilla Vera Swai

Farha Sultan

Ally Rhemtullah

Zamda George

Ailinda Sawe

Asia Idarous Khamsin

Wenzetu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo(zamani ilikuwa inaitwa Zaire),leo wanasheherekea miaka 50 ya Uhuru! D.R.C walipata Uhuru kutoka kwa mkoloni Mbelgiji.Tunawapongeza.

Pichani ni Patrice Lumumba, Waziri Mkuu wa kwanza wa Zaire. Yeye ndiye aliyeongoza harakati za kujipatia uhuru.Wiki chache tu baada ya Uhuru na kuwa madarakani,aliuawa.Unaweza kusoma zaidi kuhusu historia yake kwa kubonyeza hapa.

Imeandikwa na Na Angela Semaya wa Habari Leo

MAISHA yake sasa yamebadilika, amelazimika kuwa mtumwa wa kujificha kwa kuvaa vazi aina la Hijab ambalo anasema kwake limegeuka kuwa vazi analoliheshimu na kulithamini kwa kuwa ndio msiri wake mkubwa siku hizi, hii yote ni gharama inayotokana na moyo wake wa ujasiri na ushupavu uliotokana na kutumia kalamu yake kufichua uovu na unyanyasaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi kwa kuuawa kwa imani za kishirikina.

Kwa walio wengi ndani na nje ya Tanzania, jina la Vicky Ntetema sio geni masikioni mwao kwani ni mwandishi mahiri wa Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

Ntetema aliyezaliwa miaka 51 iliyopita ameibuka kuwa mwandishi mahiri, jasiri na shupavu baada ya kufichua siri ya kutisha kutokana na uchunguzi wa mauaji ya albino na familia zao akitaka kujua kwa undani sababu hasa za mauaji na ukatili dhidi ya albino. Hatimaye kazi yake hiyo imemuwezesha kupata Tuzo ya Ujasiri katika fani ya Uandishi wa Habari inayotolewa na International Women’s Media Foundation.

HABARI LEO Jumapili iliamua kumtafuta Vicky baada kutaka kufahamu kwa undani wa kilichomsukuma kufuatilia habari hiyo na kwa kiwango gani amefanikiwa, maisha yake kwa ujumla na kuhusiana na tuzo hiyo.

Ntetema ambaye alifanya uchunguzi wake kwa siri bila woga anasema Novemba, 2007 alipokea ujumbe wa maneno ukimuelezea kuhusu matukio ya kuuawa albino na kukatwa viungo vyao kwa imani za kishirikina, lakini awali naye hakuamini kama hicho kitu kinawezekana.

Na baada ya kufuatilia kwa muda na kujithibitishia habari hizo, alianza kuishawishi BBC, lakini walionekana kusitika wakiwa na mashaka kwamba kweli inawezekana kuwepo kwa matukio hayo? Hata hivyo anasema hakukata tamaa aliwasiliana na waandishi wengine walioko katika maeneo husika nao walimsaidia kuchunguza na kumpa taarifa zaidi.

Wakati akiendelea na uchunguzi wake aligundua kuwa waganga wa kienyeji ndio waliokuwa wakisababisha mauaji ya albino kwa kuwaambia wateja kuwa wanaweza kupata utajiri kwa kutumia viungo vya walemavu hao, ndipo alipoamua kuishawishi tena BBC huku akiendelea na uchunguzi wake kwa njia ya simu kwa kuwasiliana na watu wa Kanda ya Ziwa.

Kile alichokuwa amekusudia kukifanya na kukifichua, kilithibitishwa na Rais Jakaya Kikwete ambaye Mwezi Machi, 2008 alikemea vitendo hivyo vya kikatili dhidi ya albino na kuweka wazi kuwa tayari watu 19 walishauawa.

“Baada ya Rais kutangaza hivyo, nikasema kama kiongozi wa nchi amekemea kiasi hili na ametaja hadi maeneo yanayohusika na matukio hayo…kwa sababu ya kuwa na uhusiano mzuri na wahariri nilipeleka maombi yangu bila kusita wanisaidie ili niweze kwenda kabisa eneo husika ingawa waliniambia kwa kipindi hicho hawakuwa na bajeti,” anasema.

Dhamira yake ilimsukuma Ntetema kuchukua fedha zake za mshahara na kuamua kwenda Mwanza kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi wake. Anasema kazi hiyo ilimlazimu kuzunguka sehemu mbalimbali hadi akajikuta ameishiwa fedha na kulazimika kuomba kwa mama yake. read more

She is famously known as a Goodwill Ambassador for Tanzania. Her name is Tausi Likokola, one of the most successful international models that Tanzania has ever produced. In her modeling career, she has graced the catwalk stages of international shows and showcased some of the most renowned labels such as Gucci, Escada, Tommy Hilfiger, Christian Dior, Issey Miyake and many more.

However, Tausi is not just a model or a Goodwill Ambassador for Tanzania. She is an activist, an author and a mother. She is the founder of the not-for-profit organization, Tausi AIDS Fund, which supports prevention and awareness programs against HIV/AIDS in Africa. It is actually her efforts to support prevention and awareness of HIV/AIDS in Africa that landed her the title of a Goodwill Ambassador for Tanzania as a recognition and encouragement from the Government of Tanzania.

Recently, Tausi added yet another book in her list of books that she has authored. Her most recent book is titled The Touch of An Angel. About this book, Tausi says; “This is the closest and most private part of my life. This is my story of loss and how I am reconciling that loss. This is a memoir of my angel, AMANI. It is a story of life’s joy and pain”.

I recently caught up with Tausi to talk about her new book and also a couple of other things. Here is the interview;

BC: Congratulations for the launch of your latest book, The Touch of An Angel and welcome to BongoCelebrity.com. How are you doing today?

Tausi: Doing very well, thank you for all your support over the years.

BC: When did you decide to write a The Touch of an Angel? Did you have any particular reason for starting to write at that very moment?

Tausi: I have been writing as long as I can remember and always expressed myself through writing….likewise with this book….I was working my feeling and emotions through my writing. I started writing the book in Japan in 2005 following the death of my first born “Amani”….this book is on the incident that unfolded during that time.

BC: How was your writing process like? Did you have to get up early morning everyday to write or how did it go? read more

Anaitwa Irene Sporah Njau, ni mtangazaji wa Kipindi cha Sporah Show ambacho kinazidi kujipatia umaarufu na mashabiki.Lakini Sporah ni nani,ametokea wapi,ana malengo gani na ni kwanini anafanya anachokifanya? Ili kupata majibu ya maswali hayo na mengineyo bonyeza hapa kutembelea Spoti Starehe ili kucheki mahojiano kamili.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

KanumbaFrontKatika siku kama ya leo,miaka 26 iliyopita pale mkoani Shinyanga, alizaliwa kijana na kupewa jina la Steven. Hivi leo ni maarufu kama Steven Kanumba au kama mwenyewe anavyojiita wakati mwingine “The Great”. Kwa maana hiyo,leo ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Steven Charles Kanumba.Happy Birthday!

Kwa mtu yeyote ambaye anafuatilia maendeleo ya tasnia ya filamu nchini Tanzania,bila shaka atakubaliana na mimi nikisema kwamba Kanumba ni miongoni mwa waigizaji wa filamu(Film Actors) ambao ni maarufu zaidi nchini Tanzania. Leo hii ni vigumu kuiongelea sanaa ya filamu nchini bila kumhusisha Kanumba kwa njia moja ama nyingine.

Kwa hivyo,haishangazi sana kuona kwamba,katika mwaka uliopita jina lake lilikuwa takribani la kudumu katika vyombo mbalimbali vya habari vikiwemo vya mtandaoni,mitaani nk. Bila shaka unakumbuka jinsi habari ya Kiingereza Vs Kiswahili ilivyozua mjadala wa kitaifa. Kila mtu akasema lake.

Baada ya mambo kama yale,mijadala kama ile,watu hupenda kujua what next? Nilimtafuta Steven Kanumba ili kujua machache kuhusu mipango yake ya mwaka huu.

Unajua Kanumba angependa kupata chakula cha mchana (lunch) na actors gani maarufu hapa ulimwenguni? Una habari kwamba katika Curriculum Vitae(CV) yake ameongeza cheo cha “Blogger”? Unajua ana malengo gani mwaka huu? Una habari kwamba Kanumba hivi sasa amedhamiria kuibua vipaji vingine katika ulimwengu wa uigizaji filamu? Fuatana nami;

BC: Mpaka sasa unalionaje soko la filamu nchini Tanzania? Kumekuwa na mabadiliko gani ya kimsingi ukilinganisha toka ulipoanza mpaka hivi leo?

SK: Soko limetanuka kiasi kwamba tunatambulika kimataifa. Pia hivi sasa makampuni ya kusambaza kazi zetu yameongezea ikiwemo na pesa kwa kiasi fulani tofauti na hapo mwanzo.Safari bado ni ndefu lakini angalau inatia moyo.

BC: Mwaka 2009 ndio tumeumaliza.Jina lako liligonga vyombo vya habari kwa mambo kadha wa kadha.Unaweza kusema umejifunza mambo gani katika mwaka ulioisha? read more

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page