
Wenzetu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo(zamani ilikuwa inaitwa Zaire),leo wanasheherekea miaka 50 ya Uhuru! D.R.C walipata Uhuru kutoka kwa mkoloni Mbelgiji.Tunawapongeza.
Pichani ni Patrice Lumumba, Waziri Mkuu wa kwanza wa Zaire. Yeye ndiye aliyeongoza harakati za kujipatia uhuru.Wiki chache tu baada ya Uhuru na kuwa madarakani,aliuawa.Unaweza kusoma zaidi kuhusu historia yake kwa kubonyeza hapa.

Imeandikwa na Na Angela Semaya wa Habari Leo
MAISHA yake sasa yamebadilika, amelazimika kuwa mtumwa wa kujificha kwa kuvaa vazi aina la Hijab ambalo anasema kwake limegeuka kuwa vazi analoliheshimu na kulithamini kwa kuwa ndio msiri wake mkubwa siku hizi, hii yote ni gharama inayotokana na moyo wake wa ujasiri na ushupavu uliotokana na kutumia kalamu yake kufichua uovu na unyanyasaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi kwa kuuawa kwa imani za kishirikina.
Kwa walio wengi ndani na nje ya Tanzania, jina la Vicky Ntetema sio geni masikioni mwao kwani ni mwandishi mahiri wa Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).
Ntetema aliyezaliwa miaka 51 iliyopita ameibuka kuwa mwandishi mahiri, jasiri na shupavu baada ya kufichua siri ya kutisha kutokana na uchunguzi wa mauaji ya albino na familia zao akitaka kujua kwa undani sababu hasa za mauaji na ukatili dhidi ya albino. Hatimaye kazi yake hiyo imemuwezesha kupata Tuzo ya Ujasiri katika fani ya Uandishi wa Habari inayotolewa na International Women’s Media Foundation.
HABARI LEO Jumapili iliamua kumtafuta Vicky baada kutaka kufahamu kwa undani wa kilichomsukuma kufuatilia habari hiyo na kwa kiwango gani amefanikiwa, maisha yake kwa ujumla na kuhusiana na tuzo hiyo.
Ntetema ambaye alifanya uchunguzi wake kwa siri bila woga anasema Novemba, 2007 alipokea ujumbe wa maneno ukimuelezea kuhusu matukio ya kuuawa albino na kukatwa viungo vyao kwa imani za kishirikina, lakini awali naye hakuamini kama hicho kitu kinawezekana.
Na baada ya kufuatilia kwa muda na kujithibitishia habari hizo, alianza kuishawishi BBC, lakini walionekana kusitika wakiwa na mashaka kwamba kweli inawezekana kuwepo kwa matukio hayo? Hata hivyo anasema hakukata tamaa aliwasiliana na waandishi wengine walioko katika maeneo husika nao walimsaidia kuchunguza na kumpa taarifa zaidi.
Wakati akiendelea na uchunguzi wake aligundua kuwa waganga wa kienyeji ndio waliokuwa wakisababisha mauaji ya albino kwa kuwaambia wateja kuwa wanaweza kupata utajiri kwa kutumia viungo vya walemavu hao, ndipo alipoamua kuishawishi tena BBC huku akiendelea na uchunguzi wake kwa njia ya simu kwa kuwasiliana na watu wa Kanda ya Ziwa.
Kile alichokuwa amekusudia kukifanya na kukifichua, kilithibitishwa na Rais Jakaya Kikwete ambaye Mwezi Machi, 2008 alikemea vitendo hivyo vya kikatili dhidi ya albino na kuweka wazi kuwa tayari watu 19 walishauawa.
“Baada ya Rais kutangaza hivyo, nikasema kama kiongozi wa nchi amekemea kiasi hili na ametaja hadi maeneo yanayohusika na matukio hayo…kwa sababu ya kuwa na uhusiano mzuri na wahariri nilipeleka maombi yangu bila kusita wanisaidie ili niweze kwenda kabisa eneo husika ingawa waliniambia kwa kipindi hicho hawakuwa na bajeti,” anasema.
Dhamira yake ilimsukuma Ntetema kuchukua fedha zake za mshahara na kuamua kwenda Mwanza kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi wake. Anasema kazi hiyo ilimlazimu kuzunguka sehemu mbalimbali hadi akajikuta ameishiwa fedha na kulazimika kuomba kwa mama yake. (more…)

She is famously known as a Goodwill Ambassador for Tanzania. Her name is Tausi Likokola, one of the most successful international models that Tanzania has ever produced. In her modeling career, she has graced the catwalk stages of international shows and showcased some of the most renowned labels such as Gucci, Escada, Tommy Hilfiger, Christian Dior, Issey Miyake and many more.
However, Tausi is not just a model or a Goodwill Ambassador for Tanzania. She is an activist, an author and a mother. She is the founder of the not-for-profit organization, Tausi AIDS Fund, which supports prevention and awareness programs against HIV/AIDS in Africa. It is actually her efforts to support prevention and awareness of HIV/AIDS in Africa that landed her the title of a Goodwill Ambassador for Tanzania as a recognition and encouragement from the Government of Tanzania.
Recently, Tausi added yet another book in her list of books that she has authored. Her most recent book is titled The Touch of An Angel. About this book, Tausi says; “This is the closest and most private part of my life. This is my story of loss and how I am reconciling that loss. This is a memoir of my angel, AMANI. It is a story of life’s joy and pain”.
I recently caught up with Tausi to talk about her new book and also a couple of other things. Here is the interview;
BC: Congratulations for the launch of your latest book, The Touch of An Angel and welcome to BongoCelebrity.com. How are you doing today?
Tausi: Doing very well, thank you for all your support over the years.
BC: When did you decide to write a The Touch of an Angel? Did you have any particular reason for starting to write at that very moment?
Tausi: I have been writing as long as I can remember and always expressed myself through writing….likewise with this book….I was working my feeling and emotions through my writing. I started writing the book in Japan in 2005 following the death of my first born “Amani”….this book is on the incident that unfolded during that time.
BC: How was your writing process like? Did you have to get up early morning everyday to write or how did it go? (more…)

Anaitwa Irene Sporah Njau, ni mtangazaji wa Kipindi cha Sporah Show ambacho kinazidi kujipatia umaarufu na mashabiki.Lakini Sporah ni nani,ametokea wapi,ana malengo gani na ni kwanini anafanya anachokifanya? Ili kupata majibu ya maswali hayo na mengineyo bonyeza hapa kutembelea Spoti Starehe ili kucheki mahojiano kamili.
Katika siku kama ya leo,miaka 26 iliyopita pale mkoani Shinyanga, alizaliwa kijana na kupewa jina la Steven. Hivi leo ni maarufu kama Steven Kanumba au kama mwenyewe anavyojiita wakati mwingine “The Great”. Kwa maana hiyo,leo ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Steven Charles Kanumba.Happy Birthday!
Kwa mtu yeyote ambaye anafuatilia maendeleo ya tasnia ya filamu nchini Tanzania,bila shaka atakubaliana na mimi nikisema kwamba Kanumba ni miongoni mwa waigizaji wa filamu(Film Actors) ambao ni maarufu zaidi nchini Tanzania. Leo hii ni vigumu kuiongelea sanaa ya filamu nchini bila kumhusisha Kanumba kwa njia moja ama nyingine.
Kwa hivyo,haishangazi sana kuona kwamba,katika mwaka uliopita jina lake lilikuwa takribani la kudumu katika vyombo mbalimbali vya habari vikiwemo vya mtandaoni,mitaani nk. Bila shaka unakumbuka jinsi habari ya Kiingereza Vs Kiswahili ilivyozua mjadala wa kitaifa. Kila mtu akasema lake.
Baada ya mambo kama yale,mijadala kama ile,watu hupenda kujua what next? Nilimtafuta Steven Kanumba ili kujua machache kuhusu mipango yake ya mwaka huu.
Unajua Kanumba angependa kupata chakula cha mchana (lunch) na actors gani maarufu hapa ulimwenguni? Una habari kwamba katika Curriculum Vitae(CV) yake ameongeza cheo cha “Blogger”? Unajua ana malengo gani mwaka huu? Una habari kwamba Kanumba hivi sasa amedhamiria kuibua vipaji vingine katika ulimwengu wa uigizaji filamu? Fuatana nami;
BC: Mpaka sasa unalionaje soko la filamu nchini Tanzania? Kumekuwa na mabadiliko gani ya kimsingi ukilinganisha toka ulipoanza mpaka hivi leo?
SK: Soko limetanuka kiasi kwamba tunatambulika kimataifa. Pia hivi sasa makampuni ya kusambaza kazi zetu yameongezea ikiwemo na pesa kwa kiasi fulani tofauti na hapo mwanzo.Safari bado ni ndefu lakini angalau inatia moyo.
BC: Mwaka 2009 ndio tumeumaliza.Jina lako liligonga vyombo vya habari kwa mambo kadha wa kadha.Unaweza kusema umejifunza mambo gani katika mwaka ulioisha? (more…)

Bila shaka unaitambua sura yake na bila shaka umewahi kumsoma au kusoma vitabu vyake. Anaitwa Ngugi wa Thiong’o. Ni miongoni mwa wanazuoni na waandishi ambao bara la Africa linajivunia kuwa nao.Je nikikupa nafasi ya kumuuliza swali Ngugi ungependa kumuuliza nini? Tuma swali lako kupitia sehemu ya maoni(comments) au kwa kutumia barua-pepe info at bongocelebrity dot com

Just a couple of weeks ago, he started his career as an NBA player. But before long, he broke his jaw in an incident involving him and his teammate, Zach Randolph. He actually suffered a ridgeline fracture in his mandible- a bone in his lower jaw.
Since the incident, his fans and well wishers have been praying for his quick recovery while his critics have also used the same opportunity to nail him down or try to elevate him. It just depends on how one looks at criticism.
I recently caught up with him, whereby, he took time to talk about his health and also to answer some of what his critics have been saying. Here is how my mini-interview with him went down…
BC: A lot of your fans and supporters have been worried about you since the jaw-breaking incident. Can you briefly tell me and of course…your fans how are you doing now and whether you are back in training and all that?
Hasheem Thabeet: Niko powa kabisa… I’m doing great. I have been back to work/practice since Monday and I am looking forward to play tonight when we play against L.A Clippers. I am a tough kid and don’t like to sit on a bench. I wouldn’t miss a game if it was my choice. But this is a professional level and coaches go with what they have been having or players that have been there before me. For now I am an additional and don’t mind playing that role.
BC: Some critics have been saying that you are not or were not ready for NBA and all that. I am sure you have heard such comments and criticism. What is your reaction?
Hasheem Thabeet: I know people have been talking and saying that I am not ready and or I should not have been drafted by Memphis and therefore suggesting I should have joined another team where there are more veterans so as to learn more and stuff. My answer to them is that; that is not or can’t work for everybody. If you may recall, Memphis Grizzlies drafted Pau Gasol. He was young and almost by himself. But eventually he ended where he is now…with a ring (Lakers).
I look at the situation differently. They drafted me for a lot of different reasons such as potential, progress, presence and production. That is what pushes to me to go out there and learn and strive to be better every day. There is a good reason they pay me $4 M per year.
So while I thank everybody for their advises, comments and criticism and try to understand those who keep doubting me or just hating for no well founded reasons, I wish to inform everyone that I am definitely making a progress and that is why I am able to survive the everyday’s routines of practices and the league itself.
BC: Thank you very much Hasheem. Wish you all the best.
Hasheem Thabeet: Thanks Jeff

Watanzania Ali Kiba, Pretty Poet( Jacqueline Kweka Kibacha) na kampuni ya Bongo UK ni miongoni mwa watu waliochaguliwa kuwania Tuzo za BEFFTA (Black Entertainment,Film,Fashion,Television and Arts Awards) zinazotarajiwa kufanyikia jijini London tarehe 17 October mwaka huu ndani ya London Hilton Metropole.
Ali Kiba amechaguliwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha Best International Act huku Pretty Poet akichaguliwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha Best Spoken Word Artist/Poets. Kampuni ya Bongo UK imechaguliwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha Best Event Promoters.
Kwa orodha kamili ya waliochaguliwa kuwania tuzo hizo,tafadhali bonyeza hapa. Ili kuona kazi za Jacqueline Kweka Kibacha,bonyeza hapa na hapa na hapa.
Kama ilivyo kawaida ya tuzo siku hizi,kura zinapigwa na wananchi.Wakati ukiwadia kwa zoezi hilo,BC itakujulisha.Kwa sasa tunapenda tu kuwapongeza Ali Kiba,Pretty Poet na Bongo UK for the nomination.

Christabel Swai(Silipa) standing on the “Roof of Africa”
Kila mwaka maelfu ya watu hutoka kila pande za dunia na kuja nchini Tanzania na hususani mkoani Kilimanjaro wakiwa na nia ya kuupanda Mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu kupita yote barani Afrika.
Pamoja na wageni wengi kuja nchini kwa lengo hilo,idadi ya watanzania ambao wameshawahi kuupanda mlima huo bado ni ndogo. Hapo ndipo suala zima la utalii wa ndani (internal tourism) linapokuja.
Lakini hivi karibuni yupo mtanzania ambaye ameonyesha mfano. Ni mtoto wa miaka 10! Anaitwa Christabel Swai. Mtoto huyo amefanikiwa kuupanda Mlima Kilimanjaro na kufika pale pale kileleni ambapo kina Kapteni Nyirenda(RIP) na wenzake waliuweka mwenge wa uhuru miaka takribani 48 sasa iliyopita.
Kwa maana hiyo,Christabel ambaye pia hujulikana kwa jina la Silipa,ameweka rekodi ya kuwa mtu mwenye umri mdogo zaidi nchini kuupanda mlima huo na kufika Uhuru Peak.
Mtoto huyo wa kike ni mwanafunzi wa darasa la nne katika shule ya Eden Garden ya mjini Moshi, alipewa cheti namba 60473 kinachoonyesha na kuthibitisha kwamba amefanikiwa kufika kilele cha mlima huo wenye urefu wa mita 5,895 kutoka usawa wa bahari.

Silipa at Gilman’s Point. Wengi huishia hapa lakini ilipokuja kwa Silipa,alipumzika kama dakika 20 hivi kisha akamwambia baba yake “Dad,Lets go to Uhuru”
Christabel alifanikiwa kupanda mlima huo kupitia njia ya Rongai(miongoni mwa njia zinazosemekana kuwa ngumu zaidi) akiwa ameongozana na baba yake, Cathbert Swai ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Uwakala ya Utalii ya Ahsante Tours ya mjini Moshi.
BC inapenda kumpongeza sana Christabel a.k.a Silipa.Well done!

