Hii ni collaboration ya Kenya na Tanzania.Wimbo unaitwa Nimetoka Mbali.Ni kutoka kwa msanii Jaguar kutoka nchini Kenya akiwa amemshirikisha wa kwetu wenyewe,AY.Ni mojawapo ya track mpya mpya zinazotamba kwenye vituo vya radio,televisheni bila kusahau katika kumbi mbalimbali za raha.

Mojawapo ya mambo ambayo yanaweza kukufurahisha kama unapenda muziki kutoka Afrika Mashariki ni pale wasanii kutoka nchi zinazounda Afrika Mashariki wanapoamua kushirikiana katika kazi zao. Mifano ipo mingi kuonyesha jinsi gani mipaka iliyowekwa na mtawala wa enzi hizo inaweza kuvukwa japo kwa kutumia muziki.
Nimewahi kuandika siku za nyuma kwamba wakati viongozi wetu wanasuasua katika kukamilisha muundo wa jumuiya ya Afrika Mashariki(ukiniuliza mimi nitakwambia ni kwa sababu kila mmoja anaweka mbele maslahi binafsi badala ya faida nyingi za muungano makini) wasanii wao wameshavuka kizingiti hicho.Wanashirikiana.
Miongoni mwa mifano ya ushirikiano huo ni huu wa Juma Nature akimshirikisha Jose Chameleon(Uganda) katika wimbo unaokwenda kwa jina Mikiki Mikiki. Kama ujuavyo hawa wote ni ‘majina makubwa” katika muziki wa ukanda wetu. Wanaposhirikiana tunategemea kitoke kitu makini.Nakuomba uwe muamuzi.Sikiliza Mikiki Mikiki hapo chini.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Picha na Muziki kwa niaba ya GetMziki.

Yupo mwanamuziki mmoja wa zamani kidogo aliwahi kuimba kwamba “wivu katika mapenzi ni lazima….japo kidooogo”. Alimaanisha kwamba wivu ni sehemu ya mapenzi ingawa pia aliashiria kwamba ukizidi unaweza kuwa kero na wakati mwingine kuleta balaa kabisa. Si ushasikia mtu kamchinja mwenzake kisa wivu?
Swali la kujiuliza ni je nini husababisha wivu? Ni kutojiamini,kupenda kumiliki kitu mwenyewe au ni kweli kwamba mapenzi ndio husababisha wivu?Na kama jibu ni ndio je hayo huwa mapenzi ya dhati au ndio tulivyo tu sisi wanadamu?
Huo ni upande mmoja.Upande wa pili ni kuhusu “mpenzi wa zamani”. Hivi watu wakishaachana bado huwa wanaachana kweli au huwa wanapeana nafasi? Na inakuwaje unapoona mpenzi wako wa sasa anaendeleza sana mawasiliano na mpenzi wake wa zamani? Ni sababu tosha ya kuwa na wivu?
Ali Choki akishirikiana na msanii Nyota Ndogo anayetokea nchini Kenya maeneo ya Mombasa(Naamini unamkumbuka kutoka katika kibao chake Watu na Viatu) wanaimba kuhusu mambo ya wapenzi wa zamani na “wivu”. Mmoja anakuwa haelewi,wivu unamtatiza.Mwenzake anamwambia tulia,usiwe na papara wala wasi,hakuna kitu. Mwenzake anamsihi kwamba asimfiche na ndio maana wimbo unaitwa Usinifiche. Mimi najiuliza;akiambiwa ukweli ataweza kuhimili? Can he handle the truth? Usikilize wimbo Usinifiche kwa kubonyeza player hapo chini.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Wanaitwa Blue 3.Wanatokea nchini Uganda.Ni miongoni mwa makundi ya muziki yanayofanya vizuri katika anga za burudani na muziki katika ukanda wa Afrika Mashariki.Mara nyingi wamekuwa wakitoa burudani safi katika matamasha mbalimbali yanayofanyikia Afrika Mashariki ikiwemo hivi karibuni walipoalikwa kwenye utoaji wa tuzo za Kili.Nawatafuta kujua kwanini wanajiita Blue 3. Why Blue?
Niliwahi kusikia mahali fulani watu wa nchi jirani na Tanzania wakisema kwamba Tanzania huwa inachelewa kidogo kuanza mambo lakini pindi wanapoanza huwa wanakuja juu kwa kasi ya ajabu! Bila kuingilia mazungumzo yao,jamaa wakawa wanataja mifano kama vile jinsi ambavyo Tanzania imepiga hatua kwenye shughuli za kisanii kama vile muziki na hivi sasa filamu.
Kuna ukweli ndani yake; tunaweza kuanza mwisho lakini tukawa vinara. Yote inategemea jinsi ambavyo tunaamua kujiweka na kusonga mbele. Mojawapo ni kukubali kwamba kuna kukosea na pia kujirekebisha. Hivi sasa sanaa ya filamu inazidi kukua nchini Tanzania. Inatia moyo sana kuona watu wa mataifa mengine wanaangalia filamu ambazo zinaitwa “za kibongo”.
Pamoja na hayo kazi kubwa bado ipo mbeleni.Kama alivyowahi kusema Steven Kanumba tulipohojiana naye,kuna haja ya serikali kutoa support ya kutosha ili kuzidi kuinua sanaa hiyo. Marekani ipo hapo ilipo kwa sababu ilitangaza sanaa na sera zake za mambo ya nje kupitia kwenye filamu. Ikulu ya Marekani ina kitengo cha kushughulikia masuala ya filamu.Kama filamu itaonekana haijakaa “vizuri” kwa mujibu wa taratibu zao,basi haitoki.Mradi unakufa.
Lingine ni hili ambalo muigizaji Mohamed Mwikongi(pichani) almaarufu kama Frank katika uigizaji ameliongelea majuzi alipofanya mahojiano na jamaa wa Global Publishers. Frank anasema lazima wasanii na washika dau wote katika nyanja za filamu wakubali kukosolewa. Wazungu wanaita hii constructive criticism. Unapokubali kukosolewa unajipa nafasi ya ushindi kwani maana yake ni kwamba kesho utafanya kizuri zaidi.Lakini pia ipo haja ya wakosoaji kutokuwa “wabezaji”. Unapokosoa basi useme pia sababu zako na utoe ushauri wa kujenga kwamba nini kifanyike.Kwa mwendo huo filamu za kibongo zitazidi kupata jina na sio ajabu kabisa siku moja nasi tukaona Slumdog Millionare za kikwetu.

Kwa njia tofauti,katika nyakati tofauti,Raisi wa Kenya,Mwai Kibaki na mkewe Lucy Muthoni Kibaki wameongelewa sana katika vyombo mbalimbali vya habari ulimwenguni.Sote tunajua kwamba hivi karibuni jina la Mwai Kibaki lilitawala katika vyombo vya habari baada ya “muujiza’ wa uchaguzi wa Kenya.Lakini unajua kwanini Lucy Muthoni Kibaki ni mmojawapo miongoni mwa “First Ladies” wa Afrika wenye umaarufu wa kipekee pekee hivi?Unaweza kupata dalili kwa kubonyeza hapa.
BC inakutakia siku njema ya wajinga duniani.Kuwa makini leo,its April’s Fools Day.


Jiji la Dar-es-salaam lina historia ndefu sana.Tangu enzi hizo likiitwa Mzizima mpaka wajanja walipolibatiza jina maarufu la “Bongo” ingawa baadaye “Bongo” imekuja kuwa sio tu jiji la Dar-es-salaam bali Tanzania nzima.
Katika historia mbalimbali za jiji la Dar,mojawapo ni kuwa na wakuu wake wa mkoa ambao huwa na machachari na mbwembwe za aina yake.Nani anaweza kusahau kwamba kuna wakati jiji la Dar-es-salaam lilikuwa linajulikana kama “Jiji la Makamba” kutokana na uongozi wa Mheshimiwa Yusuf Makamba?
Historia ya Dar bado inaendelea kuandikwa.Kila kukicha Dar inazizima na mambo mapya.Kila siku kuna geni jijini Dar.Kila siku maelfu ya wananchi wanatoka mikoani na kuhamia jijini Dar kwani inasemekana Dar ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi.Haishangazi kwamba mpaka hivi leo,kuhamia Dodoma kwa serikali kumebakia kuwa sera isiyotekelezeka.
Hivi sasa jiji la Dar-es-salaam lipo chini ya uongozi wa Mheshimiwa Abbas Kandoro.Hivi sasa anapumua baada ya jiji lake/letu kufikwa na ugeni mzito wa George W.Bush.Historia yake ndio hivyo inaandikwa.
Pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Dar,Abbas Kandoro(kushoto) na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo kabla ya Kandoro,Mheshimiwa Yusuf Makamba.Makamba hivi sasa ndiye Katibu Mkuu wa CCM taifa.

Pichani ni Maimatha wa Jesse,mmoja kati ya watangazaji maarufu nchini Tanzania. Maimatha,kwa kushirikiana na mtangazaji mwenzake Ben Kinyaiya, huendesha kipindi cha Afro Beat kinachorushwa kila siku ya Jumamosi kuanzia saa moja mpaka tatu usiku kupitia kituo cha East Africa TV maarufu kama Chanel 5.Watch it.
Picha kwa hisani ya Mroki Mroki

