MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

bc-logo-official

Mpenzi msomaji/mtembeleaji wa BC,

BC itakuwa chini ya matengenezo kwa siku mbili tatu zijazo.Kwa bahati mbaya,matengenezo hayo yatasababisha kutokuwepo kwa habari(posts) mpya katika muda huo wa matengenezo.Pamoja na hayo,maoni yako katika posts zilizopo yanakaribishwa na yataendelea kuwekwa hewani kama kawaida. Unakaribishwa pia kuzitizama posts mbalimbali zilizopita,yakiwemo mahojiano mbalimbali kwa kutembelea ukurasa wa “Archives”.

Matengenezo ni muhimu ili kuhakikisha kwamba BC inaendelea kupatikana kirahisi na kuwafikia watu wengi zaidi.Matengenezo haya hayatoathiri muonekano wa BC kwa namna yeyote ile kwa sasa.

Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Asanteni.

Jeff Msangi kwa niaba ya wana-BC wote.

 

Yawezekana umeshapata ujumbe uliosambazwa na Issa Michuzi mwenyewe au ule ambao Da’Chemi wa Swahili Times blog ameusambaza ikiwa ni tahadhari kuhusu e-mail ya kitapeli ambayo ilisambaa jana na bado inaendelea kusambaa hivi sasa ikidai Issa Michuzi amekwama hotelini huko nchini Nigeria na hivyo anaomba msaada wa kifedha.

Tungeweza kuipuuzia tu e-mail kama hiyo.Tatizo ni kwamba sio tu ni ya kitapeli,bali hivi sasa imemfanya Issa Michuzi ashindwe hata ku-update blog yake maarufu. Kimsingi e-mail ya issamichuzi at gmail ambayo ndio aliyokuwa akiitumia kuingia ndani ya blog yake haipo mikononi mwake tena! Ndio maana kama mnavyoweza kuona ukiitembelea blog yake tangu jana hajaweza kuweka picha mpya,jambo ambalo sio kawaida yake kabisa.

BongoCelebrity imewasiliana na Michuzi na kufanya naye mahojiano yafuatayo. Yasome na kisha mkumbushe na mwenzio kuhusu kwamba aipuuzie tu e-mail kama hiyo. Hapa Michuzi anaelezea nini kilitokea,lini ataweza tena kuendelea ku-update blog yake(archives zote bado zipo na zinapatikana online),vipi unaweza kuepuka yasikukute yaliyomkuta na anapatikana kwa njia gani hivi sasa? Majibu haya hapa chini;

BC:Nini hasa kimetokea? Ilikuwaje? (more…)

↑ Go Back to Top of Page