Tanzania’s High Commissioner to the UK, Peter Kallaghe(right) presenting his credentials to The Queen at the Buckingham Palace yesterday.

Photo Credits:Press Association

Balozi Peter Kallaghe bado ni mgeni nchini Uingereza. Kwa maana hiyo ndio kwanza yupo katika ziara mbalimbali za kuwatembelea watanzania,washika dau mbalimbali nchini humo.Pia bado yupo katika kipindi cha kukaribishwa rasmi na wanajumuiya mbalimbali.

Hapo majuzi,ilikuwa ni zamu ya Britain-Tanzania Society kumkaribisha.Britain-Tanzania Society au kifupi BTS ni jumuiya yenye lengo la kudumisha ubadilishanaji wa maarifa,maelewano na heshima baina ya Uingereza na Tanzania kupitia shughuli mbalimbali.Hizi hapa ni baadhi ya picha kutoka katika shughuli hiyo iliyofanyikia katika ukumbi wa Westminster Central na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali hususani wawakilishi kutoka jumuiya mbalimbali za nchini Uingereza.

Balozi Kallaghe akiwashukuru wenyeji waliomkaribisha.

Mrs.Katanga(kushoto) akiwakabidhi Balozi Peter Kallaghe na mkewe,Mrs Joyce Kallaghe zawadi kutoka kwa wanachama wa BTS.

Baadhi ya Maofisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza wakijumuika na wanachama wa BTS katika tafrija hiyo.

Miezi michache iliyopita, Rais Jakaya Kikwete, alifanya mabadiliko na teuzi kadhaa za mabalozi wetu katika nchi mbalimbali. Miongoni mwa mabadiliko hayo ni pamoja na yale ya kumhamisha Balozi Peter A.Kallaghe kutoka nchini Canada kwenda kuwa Balozi mpya wa Tanzania nchini Uingereza.

Wakati akijiandaa kuondoka nchini Canada kuelekea katika kituo chake kipya cha kazi nchini Uingereza,BC ilipata nafasi ya kufanya naye mahojiano maalum utakayoyasoma hivi punde.

Balozi Peter Kallaghe anaelekea nchini Uingereza kuchukua nafasi iliyoachwa na Balozi Mwanaidi Maajar ambaye amehamishiwa nchini Marekani. Fuatana nasi katika mahojiano haya;

BC: Mheshimiwa Balozi,asante sana kwa kukubali kufanya nami mahojiano haya.Nafahamu kwamba una mambo mengi mengine ya kufanya hususan wakati huu unapojiandaa kuondoka hapa Canada.Kwa hiyo nashukuru sana kwa kunipatia fursa hii.

Kwa kuanzia na kwa sababu wewe ni Balozi wa kwanza kufanya nasi mahojiano,ningependa kukuuliza swali ambalo bila shaka lipo katika vichwa vya wasomaji na wafuatiliaji wetu.Ilikuwaje mpaka ukafikia hatua ya kuteuliwa kuwa Balozi?Katika historia yako ya utumishi wa umma(Public Service) umepitia ngazi zipi,milima na mabonde yapi?Hapa ninamaanisha ulisomea wapi,ukakulia wapi na nini kilikusukuma katika ajira ya serikalini au utumishi wa umma kwa ujumla?

Balozi Peter Kallaghe: Historia yangu kielimu ni kwamba nimehama hama sana shule, kwa sababu baba yangu, Marehemu Balozi Cecil A. Kallaghe, alikuwa mtumishi wa umma na alipata kufanya kazi nje ya nchi kama Balozi.

Kwa ufupi nilisoma elimu ya msingi katika shule za OysterBay na Arusha School katika miaka ya sitini. Na nilipata elimu ya sekondari katika shule ya Pugu Secondary School. Chuo Kikuu nilisomea Kieve State University ambapo nilihitimu na degree ya M.A. in International Relations. Aidha nina Post-Graduate Diploma kwenye Diplomacy, Negotiatiations and Strategic Communications.

Kikazi maisha yangu yote nimefanya kazi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ikulu, hususani kama msaidizi wa Rais kwa kipindi kirefu.

Niliteuliwa Balozi kwa mara ya kwanza mwaka 2004 nikiwa pale Ikulu, na mwaka 2007 niliteuliwa Balozi nchini Canada. Mwaka 2010 nimeteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza (UK).

Kuteuliwa kwangu kuwa balozi nakuchukulia kama fursa ya kipekee niliyopewa ya kutoa mchango wangu katika kulitumikia Taifa letu la Tanzania na watu wake. Na ninafanya hivyo nikitambua uzito wa dhamana hii hasa kwa nchi ambayo bado inakabiliana na changamoto nyingi za kimaendeleo.

BC: Sasa kama sikosei hii ilikuwa ni mara yako ya kwanza kuteuliwa kuwa Balozi kamili. Je,ulikuwa na matarajio gani kabla hujafunga safari kuja Canada? Je, ulichokitarajia ndicho ulichokutana nacho? read more

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Kikwete amemteua Balozi Francis Malambugi(pichani) kuwa Balozi mpya wa Tanzania nchini Brazil .

Uteuzi wa Balozi Malambugi umetokana na na kuteuliwa hivi karibuni kwa aliyekuwa Balozi wa nchi hiyo Balozi Daktari Joram Mkama Biswaro kuwa Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na kwenye Umoja wa Afrika.

Balozi Malambugi ambaye kwa taaluma ni Mwanasheria na Mwanadiplomasia alijiunga na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tarehe 1/1/1978 kama Wakili wa Serikali na amewahi kufanyakazi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Angola, Ofisi ya Umoja wa Mataifa iliyoko Geneva, Ujerumani,Ethiopia na Ubelgiji.

She is famously known as a Goodwill Ambassador for Tanzania. Her name is Tausi Likokola, one of the most successful international models that Tanzania has ever produced. In her modeling career, she has graced the catwalk stages of international shows and showcased some of the most renowned labels such as Gucci, Escada, Tommy Hilfiger, Christian Dior, Issey Miyake and many more.

However, Tausi is not just a model or a Goodwill Ambassador for Tanzania. She is an activist, an author and a mother. She is the founder of the not-for-profit organization, Tausi AIDS Fund, which supports prevention and awareness programs against HIV/AIDS in Africa. It is actually her efforts to support prevention and awareness of HIV/AIDS in Africa that landed her the title of a Goodwill Ambassador for Tanzania as a recognition and encouragement from the Government of Tanzania.

Recently, Tausi added yet another book in her list of books that she has authored. Her most recent book is titled The Touch of An Angel. About this book, Tausi says; “This is the closest and most private part of my life. This is my story of loss and how I am reconciling that loss. This is a memoir of my angel, AMANI. It is a story of life’s joy and pain”.

I recently caught up with Tausi to talk about her new book and also a couple of other things. Here is the interview;

BC: Congratulations for the launch of your latest book, The Touch of An Angel and welcome to BongoCelebrity.com. How are you doing today?

Tausi: Doing very well, thank you for all your support over the years.

BC: When did you decide to write a The Touch of an Angel? Did you have any particular reason for starting to write at that very moment?

Tausi: I have been writing as long as I can remember and always expressed myself through writing….likewise with this book….I was working my feeling and emotions through my writing. I started writing the book in Japan in 2005 following the death of my first born “Amani”….this book is on the incident that unfolded during that time.

BC: How was your writing process like? Did you have to get up early morning everyday to write or how did it go? read more

siscobc

Unapotaja jina la Balozi Cisco Mtiro bila shaka watu tisa kati ya kumi wanamtambua vyema. Hivi karibuni(kama inavyoonekana pichani) aliwakilisha hati zake za utambulisho wa kibalozi kwa Rais Gloria Aroyo wa Phillipines huko katika ikulu ya Phillipines jijini Manila.

Balozi Cisco Mtiro ndio mwakilishi(balozi) wetu katika nchi za Malaysia, Phillipines, Cambodia,Singapore na Laos.

Picha na habari kwa hisani ya Pius Mikongoti.

kofibc

Mwanamuziki maarufu kutoka DRC,Koffi Charles Olomide yupo nchini Tanzania kwa ziara ya siku mbili akiwa kama Balozi  maalumu chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya watoto, UNICEF.Katika ziara hiyo Koffi atatembelea sehemu mbalimbali ukiwemo mji wa kihistoria wa Bagamoyo hapo kesho.

Leo hii,kama inavyoonekana pichani,alitembelea kituo cha radio cha Clouds FM(Radio ya Watu) katika jengo lao jipya maeneo ya Mikocheni jijini Dar-es-salaam.Akiwa katika kituo hicho Koffi alifanya mahojiano mafupi na Gardner G.Habash kupitia kipindi chake cha Jahazi.

Pichani ni Koffi akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi wa Clouds FM, Joseph Kusaga

Bila shaka utakuwa bado unalikumbuka kundi maarufu la muziki lililokuwa linajulikana kama Destiny’s Child kutoka nchini Marekani. Miongoni mwa mabinti waliokuwa wanaunda kundi hilo ni Kelly Rowland(pichani).Wenzake walikuwa ni Beyonce Knowles(mke wa Jay Z hivi sasa) na Michelle Williams. Kundi hilo lilivunjika rasmi mwaka 2005 ingawa mara moja moja bado huwa inatokea wakafanya maonyesho pamoja.

Baada ya kuvunjika kwa kundi lao na kila mmoja kuendelea kivyake na shughuli za kimuziki,uigizaji nk, Kelly Rowland amekuwa akijitolea sana kwa huduma za kijamii.Hali hiyo ndio imemfanya achaguliwe hivi karibuni kuwa Balozi wa Taasisi ya MTV Staying Alive ambayo imejikita katika kupigana vita na maradhi ya ukimwi pamoja na matokeo yake kama vile kuwanyanyapaa walioathirika nk.

Ni katika wadhifa huo wa “ubalozi” ambapo Kelly Rowland anatarajiwa kutua nchini Tanzania hivi leo ikiwa ni katika ziara yake katika nchi kadhaa za Afrika ikiwa na nia ya kueneza ujumbe na kuendeleza kazi za taasisi hiyo.

Kwa mujibu wa Meneja Uhusiano wa Kampuni ya MultiChoice Tanzania ambao ndio wenyeji wake,Kelly Rowland anatarajia kutembelea vituo kadhaa vinavyojishughulisha na mapambano dhidi ya ukimwi na pia kuzungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ziara yake. Akimaliza ziara yake nchini Tanzania,Kelly Rowland anatarajiwa kuelekea Kenya na kisha Ghana,Msumbiji na Angola.

Halafu bonyeza hapa uone jinsi mwanamuziki huyu na nduguze walivyopewa heka heka na nyani katika mojawapo ya nchi za kiafrika anazozitembelea.

Pichani ni Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Balozi Mwanaidi Sinare Maajar.Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza kwa kushirikiana na Jumuiya ya Watanzania nchini humo,hivi karibuni uliandaa mkutano/au kongamano lililoitwa Tanzania Diaspora jambo ambalo limechukuliwa na wengi kama mfano wa kuigwa na balozi zingine za Tanzania duniani.

Tovuti ya Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza unaweza kuitembelea kwa kubonyeza hapa.

Picha kwa hisani ya TanzaniaOne UK

Tunaendelea na mfululizo wetu wa mabalozi wa Tanzania nchi za nje.Pichani ni Balozi Peter Kallaghe, balozi wa Tanzania nchini Canada. Kabla ya kuteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Canada, Peter Kallaghe alikuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano na Habari -Ikulu Tanzania.

Ukitaka kutembelea tovuti ya Ubalozi wa Tanzania nchini Canada bonyeza hapa.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page