
Blogging for good 5 YEARS. You definitely deserve all the Congratulations.Hongera mdada.Kwa picha na habari zaidi,tembelea hapa.

Ingawa kila siku idadi ya bloggers wa kitanzania inazidi kuongezeka,idadi ya wanawake wanaoblog bado ni ndogo ikilinganishwa na wale wa kiume.Yawezekana ni kwa sababu wanawake bado hawajapata mwamko wa kutosha au pengine ni kitu ambacho bado wanakipa kisogo.
Lakini pamoja na idadi ya wanawake kuwa ndogo,wanaofanya hivyo wanafanya kazi nzuri sana ya kuwawakilisha wanawake wenzao.Miongoni mwa wanawake hao ni pamoja na Shamim Mwasha au Zeze kama anavyojulikana kwa watu wake wa karibu.
Iwe ni shughuli yenye mvuto wa kitaifa au wa mtu binafsi(hususani zile zenye kuwagusa wanawake zaidi),ukihudhuria na kutizamatizama katika watu waliopo mstari wa mbele katika kuchukua kumbukumbu iwe ni kwa kutumia picha za mgando(still photos) au videos,bila shaka waweza kumuona Zeze.Ukimsalimia atakujibu na kukurushia tabasamu ambalo naweza kusema ni “signature” yake.
Hivi karibuni nilipata nafasi ya kufanya naye mahojiano ambayo utayasoma hivi punde.Zeze ambaye blog yake inakwenda kwa jina www.8020fashions.blogspot.com, anaweka bayana mambo kadhaa kuhusu harakati zake kama mwandishi wa habari(taaluma yake) na pia blogger pamoja na ujasiriamali.
Yote tisa,kumi ni kwamba siku chache zijazo,Shamim kupitia blog yake ya 8020fashions,anasheherekea miaka mitano(5) tangu aanze shughuli ya kublog au Libeneke la kublog kama ambavyo rafiki yangu Issa Michuzi hupenda kuiita shughuli hii.Nimemuuliza pia maswali machache kuhusu siku hiyo maalum kwake na kwa wapenzi wa blog yake ambayo itafanyika pale Diamond Jubilee tarehe 30 October,2011.Twende pamoja katika mahojiano yafuatayo;
BC: Umekuwa uki-blog kwa muda gani mpaka hivi sasa?Nini kilikusukuma katika kuanzisha blog yako?
SM: Huu ni mwaka wangu wa tano sasa tangu nianze hili libeneke.Kikubwa kilichonisukuma kilikuwa ni nia yangu ya kutangaza biashara ya duka langu la nguo liitwalo 8020 Fashion lililopo Sinza.Nikaona nifungue blog ili niwe naweka nguo na bidhaa zingine kadiri zinavyowasili dukani.Sasa kama ujuavyo si kila siku naweza kuwa na new arrival na ili watu warejee kuangalia blog ndio nikaanza kuweka picha za matukio mbalimbali huku nikiwa nimejikita kwenye fashion zaidi katika kuonyesha nini kilivaliwa wapi na nani na mambo kama hayo.
BC: Kitaaluma wewe ni mwandishi wa habari. Sasa ukiwa kama blogger,unadhani kuna tofauti gani za kimsingi kati ya mwandishi wa habari wa kawaida na blogger? Je,kuna misingi ambayo wote (a journalist and a blogger) wanayotakiwa kuzingatia?
SM: Ni kweli kabisa,ipo tofauti kubwa sana. Kama ujuavyo blogger inakuwa ni mimi kama mimi ambapo nisipo-update ni blog inakuwa imelala doro. Hivyo kuwa kama blogger inabidi uwe na juhudi binafsi za kujituma kitu ambacho ni tofauti na mwandishi wa habari ambapo hata wewe usipoenda kazini au kufanya kazi gazeti ni lazima litoke tu.
BC: Blog yako imejikita zaidi katika kuandika habari za urembo,shughuli kama vile harusi,kitchen party,fashion shows nk.Ni kwanini uliamua kuwa na “niche” kama hiyo?

Kama wewe ni mfuatiliaji wa masuala ya watanzania mtandaoni,bila shaka utakubaliana nasi kwamba miongoni mwa mahali ambapo mengi hutokea na mengi huandikwa kama sio kujadiliwa basi mahali hapo ni katika blog inayokwenda kwa jina la U-turn.
Ni blog ambayo ingawa haina umri mkubwa(ilianzishwa mwaka mmoja na nusu tu uliopita), tayari imefanikiwa kuwa chanzo muhimu cha habari,michapo,maoni,matukio bila kusahau udaku wa hapa na pale.Ni mafanikio ambayo sio ya kubeza.It is what it is!
Mwendeshaji na mmiliki wa U-turn si mwingine bali Mange Kimambi ambaye miaka michache iliyopita ilikuwa ukisikia jina lake basi ilikuwa ni kupitia kurasa mbalimbali za magazeti hususani yale yanayoitwa “magazeti pendwa”. Leo hii mambo ni tofauti. Ni mama,mke,mwanafunzi na blogger mwenye idadi kubwa tu ya wasomaji na wafuatiliaji.
Hivi karibuni tulipata nafasi ya kufanya naye mahojiano ya kina. Hii ni mara ya kwanza kwa Mange kufanya mahojiano ya kina na chombo chochote cha habari.
Je,Mange ni nani hasa?Ametokea wapi mpaka kufikia alipo hivi sasa ambapo kila siku idadi ya wasomaji na wanaofuatilia maisha yake na anachokiandika inazidi kuongezeka? Ni matukio gani katika maisha yake ambayo kwa namna moja au nyingine yamechangia in making her who she is today?
Nini siri ya mafanikio yake au ya blog yake?Unataka kujua ana maoni gani kuhusu mambo mbalimbali kama vile uongozi wa Rais Jakaya Kikwete?Ana ushauri gani kwa wasichana wadogo(teen girls)? Kwa majibu ya maswali hayo na mengine mengi,fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;
BC: Mange,Karibu sana ndani ya BC.Mambo vipi?
MANGE: Asante sana.Feels good to be here!
BC:
Nimewahi kusoma mahali kwamba maisha yako ni kama vile kitabu kilicho wazi(an open book) ambapo kila anayetaka kusoma anayo nafasi ya kufanya hivyo.Lakini bila shaka utakubaliana nami kwamba wapo ambao hawajui lolote kuhusu historia ya maisha yako.Naomba tuanzie hapo…kwa kifupi tu ulizaliwa wapi,lini,ukasomea na kukulia wapi na mambo kama hayo.
MANGE: Nilizaliwa Hindu Mandal,Hospital- Dar es Salaam.Cheti changu cha kuzaliwa kina mwaka tofauti na passport yangu.According to my passport, I was born in 1980 lakini tukifuata Birth Certificate kuna difference ya 4years.Hii imetokana na kuna wakati mama yangu alitaka kunitoa kwa baba yangu akidai kwamba nina miaka chini ya 7.So kutokana na sheria za Tanzania natakiwa kuishi na mama. Baba yangu naye akawa na documents zake zinazosema nimeshapita miaka 7 kwa hiyo natakiwa kuishi na baba.So mama alikuwa na cheti changu cha kuzaliwa chenye umri tofauti na baba naye na passport yangu yenye umri tofauti.GO FIGURE.
Primary nilisoma Arusha School iliyoko Arusha- the best memories of my childhood came from my time there. Nilifanikiwa kufaulu mitihani ya darasa la 7 na nilichaguliwa kujiunga na Arusha Secondary.Baba yangu alifurahi sana na akanizawadia kwa kunipeleka kusoma Zimbambwe.So niliishi Harare miaka kadhaa kwa masomo yangu ya secondary.
Baada ya hapo nilikwenda Marekani kuanza masomo yangu ya juu.Kwa bahati nzuri (siwezi kusema bahati mbaya) nilijifungua mtoto wa kike,Bhoke, nikiwa Marekani jambo ambalo lilinifanya nirudi nyumbani kujipanga upya.
Then in 2004 nilijiunga na AVU-UDSM ambapo nilipata degree yangu ya Business Administration na sasa nipo Dubai nasoma Masters(MBA)
Mostly nimekulia Dar-es-salaam.
BC: Unakumbuka nini zaidi kuhusu maisha yako ya utotoni?Ulitaka kuwa nani,ulipenda michezo gani na tukio gani la utotoni ambalo hutokaa ulisahau?

Ankal Michuzi (Issa Michuzi) ambaye ni mmoja wa waasisi wa mitandao ya habari ya jamii (blogs) hapa nchini amewashauri wadau wa sanaa hasa wasanii kuanza kuingia kwa kasi kwenye matumizi ya teknolojia hiyo kwani ni njia kubwa ya kujitangaza na kuuza kazi za sanaa kote duniani.
Akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa leo Jumatatu,Michuzi ambaye blog yake ya www.issamichuzi.blogspot.com imepata umaarufu mkubwa kutokana na kutembelewa na watu wengi aliweka wazi kwamba,blogs zimekuwa zikitembelewa na watu mbalimbali duniani hivyo wasanii hawana budi kuzitumia ili kujitangaza, kusambaza kazi zao na hata kujitambulisha katika masoko ya kimataifa.
Alisema kwamba, blogs tofauti na aina nyingine za vyombo vya habari inatumiwa kuhifadhi picha nyingi na kazi mbalimbali, kupata taarifa kuhusu tasnia ya sanaa, kupokea mawazo ya wateja wa kazi za sanaa na hata kuwa na wasaa wa kuwasiliana na wasanii wengine na hivyo kupanuka kimawazo na kiujuzi.
Akizungumzia historia ya blogs,Michuzi alisema kwamba ni teknolojia mpya hapa nchini na kwamba,ilianza kwa kuandika habari za kawaida lakini leo hii ni tegemeo katika kupasha habari kwa uharaka zaidi, kuwafikia watu wengi kuliko vyombo kadhaa vya habari na kimbilio la jamii kwani imekuwa kama sehemu ya jamii katika masuala mbalimbali.
Kwa ujumla Michuzi aliwataka wasanii na wadau wa Sanaa kuamka na kuanza kutumia teknolojia hiyo kwani wasanii mbalimbali duniani si tu wamekuwa wakitumia blog katika kujitangaza na kutambulisha kazi zao bali pia wamekuwa wakimilki mitandao na technolojia mbalimbali za mawasiliano.
Katika kuonesha kwamba, teknolojia hiyo ni muhimu Michuzi ameahidi kuwapa mafunzo ya bure wadau wa Jukwaa la Sanaa juu ya kufungua na kumiliki blog ambayo yataendeshwa Ijumaa ya Desemba 10,2010 kwenye Ukumbi wa BASATA.Wadau wote wa Sanaa mnakaribishwa.
Pichani juu ni Ankal Michuzi akiwaonyesha wadau wa Jukwaa la Sanaa jinsi ya kuweka video kwenye YouTube.

Upende,usipende,leo hii unapoongelea masuala ya nyanja ya habari na mawasiliano kupitia zana za blog kwa upande wa Tanzania(Tanzanian Blogsphere), huwezi kuepuka kumtaja Muhidin Issa Michuzi a.k.a Ankal,Mzee wa Libeneke.
Mwanzoni alipoanzisha blog yake maudhui yake yalikuwa zaidi ni picha na maelezo kidogo juu ya picha hiyo au picha hizo.Hiyo ilitokana na ukweli kwamba Michuzi ni seasoned professional photographer.
Baada ya muda fulani,na kutokana na mafanikio aliyokuwa ameyapata,ilimlazimu kutanua wigo wa blog yake na hivyo kutoishia katika picha na maelezo mafupi mafupi tu bali kujumuisha maelezo au habari zaidi.Leo hii,blog yake imekuwa kimbilio la wengi pale wanapotafuta habari motomoto kuhusu kinachoendelea nchini Tanzania,maeneo ya jirani na hata sehemu mbalimbali za ulimwengu.
Hivi sasa yupo mbioni(keshazianza mbio zenyewe) kuboresha zaidi kazi ngumu anayoifanya ya kuendeleza “libeneke”.Ameanzisha tovuti/blog mpya inayopatikana kupitia http://michuzipost.com
BC imepata nafasi ya kuongea naye machache kuhusu ujio huo wa MichuziPost na mambo mengine kuhusiana na tasnia ya habari na mawasiliano. Je,”wadau” watarajie nini katika uwanja huo mpya?Nini siri ya mafanikio yake mpaka hivi sasa?Ana ushauri gani kwa bloggers wapya na wale wanaofikiria kuanzisha blog?Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;
BC: Kwanza nikupe Hongera nyingi kwa kazi nzito unayoifanya.Mambo yanakwendaje?
MICHUZI: Ahsante sana, mambo mswano tu. Libeneke kwa kwenda mbele. Yaani baada ya miaka mitano ya tufanikio kiduchu tulikopatikana, sasa ni wakati muafaka wa kupiga hatua tano mbele, na kusaidia ujenzi wa taifa letu kwa njia ya habari.
Nitakuwa mtovu wa hisani na fadhila endapo kama nitaanza kujieleza bila kwanza kuwashukuru wadau wa Globu ya Jamii popote walipo duniani, kwani bila sapoti yao sidhani kama ningefikia robo tu ya hapa nilipo.
Naomba kwa heshima na taadhima wape AHSANTE SANA wadau. Waambie nawapenda, nawaheshimu na nitandelea kuwa mtumishi wao wakati wa raha na wakati wa shida. Pia naomba ninaowaudhi kwa njia moja ama nyingine wanisamehe kwani mie ni binadamu na si kamilifu. Pia si rahisi kumridhisha kila mdau kwa kila jambo. Napenda sana kutumia ule msemo wa ‘what’s good for the goose, is bad for the hen’. Hivyo naomba uvumilivu na kuelekezana pale palipo na dosari.
BC: Hivi karibuni utatimiza miaka mitano tangu ulipoanza ku-blog pale Helsink,Finland.Umepitia mengi,umeonana na wengi.Waliokuwa hawakujui,bila shaka hivi sasa wanakujua japo kwa sura tu.Unaielezea vipi safari hiyo ndefu tangu ulipoanza kwa maana ya kwamba umekabiliana na changamoto zipi nzito nzito na umejifunza mambo gani ya msingi katika uwanja mpana wa habari na mawasiliano? 

Nimekuwa katika vuguvugu la habari na mawasiliano kwa njia ya blog kwa muda sasa.Kila siku huwa napitia blogs zaidi ya 500! Huwa natumia huduma ya www.bloglines.com. Ukiandika kitu basi naambiwa umeandika na hivyo napita na kusoma.Ukiwa hujaandika,basi siku hiyo napata muda wa kuperuzi au kutafuta blogs zingine,kuziingiza kwenye orodha yangu ya bloglines.Siku inakuwa imekwenda au naendelea na kazi zingine.
Leo nikiwa katika pitia pitia yangu mtandaoni,nimekutana na blog ya Madaraka Nyerere,mtoto wa Hayati Baba wa Taifa,Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Cha kwanza kilichonijia kichwani ni hasira fulani.Iweje siku zote hizi sikujua kuhusu blog ya Madaraka? Haikutangazwa au ilikuwaje? Hasira zangu ziliyeyuka kama vile barafu inapopigwa na jua baada ya kuanza kuipitia blog yake.Imesheheni habari kemkem.Madaraka ni mwandishi mzuri.Simulizi zake ni nyepesi kama pamba lakini maudhui yake ni mazito kuliko yale mawe yanaouzunguka mji wa Mwanza.
Bonyeza hapa ili kuitembelea blog hiyo. Nikisema mkaribishe nitakuwa nakosea kwani amekuwepo kwa muda sasa.Bravo Madaraka.
Pichani juu ni Madaraka Nyerere(kulia) akiwa na Jaffar Amin,mtoto wa Iddi Amini aliyewahi kuwa Rais wa Uganda. Soma zaidi kuhusu mkutano wao.
Sitaki kusema mengi leo.Kama unapenda unachokiona pichani basi mtembelee Master Taji Liundi katika blog yake ya u-modo kwa kubonyeza hapa.
Ukitaka kusoma mahojiano yangu na Taji Liundi(Master T) hivi karibuni,bonyeza hapa.

Je wewe ni mwanablogu (Blogger) au mdau wa habari na mawasiliano kwa umma kwa kutumia mtandao? Kama jibu ni ndio, tafadhali unaombwa kujiorodhesha kwa ajili ya maandalizi ya Kongamano Maalumu la Kitaifa kwa ajili Wanablogu (Bloggers) na wadau wa habari na mawasiliano wa Tanzania (Tanzanians Bloggers Summit) linalotarajiwa kufanyika Desemba mwaka huu jijini Dar-es-salaam,Tanzania.
Dhumuni la kongamano hili ni Kuelimishana, Kufahamiana, Kuamsha Utambuzi Rasmi Kuhusu Tekinolojia ya Blogu na Mawasiliano ya Umma kwa Kutumia Mitandao, Kusaidia Utambuzi Rasmi juu ya mchango wa blogu nchini Tanzania kama chombo muhimu cha habari na mawasiliano, Kuelimishana jinsi gani blogu zinaweza kutumika katika kuleta maendeleo katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi, kuburudisha, kukuza utamaduni nk.
Wataalamu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wataalikwa kutoa mada na mafunzo mbalimbali kuhusiana na tekinolojia ya kublogu, zana nyinginezo za mawasiliano mtandaoni kama vile mitandao jamii(social networking), online forums nk.Kutakuwa na vipindi vya maswali na majibu.
Ili kufanikisha maandalizi ya Kongamano hili la kihistoria, kujiorodhesha kwako ni muhimu sana. Muda wa kujiodhoresha ni kuanzia tarehe 12/8/2009 (Jumatano) mpaka 12/9/2009 (Jumamosi) tu.
Kinachohitajika ili kujiandikisha ni :
Jina Lako, Anuani yako ya barua pepe (E-mail), Mahali Ulipo au unapoishi (Nchi,mji nk),Namba ya Simu (sio lazima) na Anuani au URL(Universal Resource Locator) ya blogu yako (mfano www.kongamano.blogspot.com/wordpress.com/.com/typepad nk). Vyeti vya Ushiriki vitatolewa kulingana na habari utakazoziorodhesha hapa.
Unaweza kujiorodhesha kwa kutuma ombi lako kwa barua pepe kwenda; summit@bongocelebrity.com.
Zingatia tarehe za kujiandikisha.
Ni mwezi mmoja tu! Asante kwa ushirikiano. UMOJA NI NGUVU!

Je wewe ni mwanablogu (Blogger) au mdau wa habari na mawasiliano kwa umma kwa kutumia mtandao? Kama jibu ni ndio, tafadhali unaombwa kujiorodhesha kwa ajili ya maandalizi ya Kongamano Maalumu la Kitaifa kwa ajili Wanablogu (Bloggers) na wadau wa habari na mawasiliano wa Tanzania (Tanzanians Bloggers Summit) linalotarajiwa kufanyika Desemba mwaka huu jijini Dar-es-salaam,Tanzania.
Dhumuni la kongamano hili ni Kuelimishana, Kufahamiana, Kuamsha Utambuzi Rasmi Kuhusu Tekinolojia ya Blogu na Mawasiliano ya Umma kwa Kutumia Mitandao, Kusaidia Utambuzi Rasmi juu ya mchango wa blogu nchini Tanzania kama chombo muhimu cha habari na mawasiliano, Kuelimishana jinsi gani blogu zinaweza kutumika katika kuleta maendeleo katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi, kuburudisha, kukuza utamaduni nk.
Wataalamu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wataalikwa kutoa mada na mafunzo mbalimbali kuhusiana na tekinolojia ya kublogu, zana nyinginezo za mawasiliano mtandaoni kama vile mitandao jamii(social networking), online forums nk.Kutakuwa na vipindi vya maswali na majibu.
Ili kufanikisha maandalizi ya Kongamano hili la kihistoria, kujiorodhesha kwako ni muhimu sana. Muda wa kujiodhoresha ni kuanzia tarehe 12/8/2009 (Jumatano) mpaka 12/9/2009 (Jumamosi) tu.
Kinachohitajika ili kujiandikisha ni :
Jina Lako, Anuani yako ya barua pepe (E-mail), Mahali Ulipo au unapoishi (Nchi,mji nk),Namba ya Simu (sio lazima) na Anuani au URL(Universal Resource Locator) ya blogu yako (mfano www.kongamano.blogspot.com/wordpress.com/.com/typepad nk). Vyeti vya Ushiriki vitatolewa kulingana na habari utakazoziorodhesha hapa.
Unaweza kujiorodhesha kwa kutuma ombi lako kwa barua pepe kwenda; summit@bongocelebrity.com.
Zingatia tarehe za kujiandikisha.
Ni mwezi mmoja tu! Asante kwa ushirikiano. UMOJA NI NGUVU!

Unamjua Dina Marios kama mtangazaji maarufu wa Clouds FM kupitia kipindi chake cha Leo Tena. Ambacho unaweza kuwa hukijui kuhusu Dina ni kwamba yeye pia ni blogger. Dina ana-blog kupitia www.dinamarios.blogspot.com. Ninachopenda kuhusu blog ya Dina ni topics mbalimbali ambazo anazirusha kila mara.Mtembelee ujionee mwenyewe kwa kubonyeza hapa.


sending...