MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Jina la Madaraka Nyerere(pichani) sio geni miongoni mwa watanzania.Ukiachilia mbali ukweli kwamba yeye ni mtoto wa sita wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (kitu ambacho bila shaka kinampa automatic celebrity status), yeye pia ni mwandishi,mfanyabiashara na mtu ambaye huwa hasiti kuelezea hisia zake kuhusu mambo mbalimbali iwe ni katika nyanja za kisiasa,kijamii na hata kiuchumi kila mara fursa ya kufanya hivyo inapojitokeza.

Mwaka jana mwezi wa nne(April) yeye na Jaffar Amin(mtoto wa Iddi Amin-Rais wa zamani wa Uganda) waliingia katika vitabu vya kumbukumbu vya wapenda amani duniani walipokutana kwa mara ya kwanza ikiwa ni ishara ya amani na usuluhisho barani Afrika na kwingineko.

Hivi karibuni nilipata nafasi ya kuzungumza naye kuhusu mambo kadhaa yakiwemo ya kifamilia na pia kupata maoni yake kuhusu mambo mbalimbali.Je,ni kwanini mpaka leo hii hajajiingiza katika masuala ya siasa au uongozi?Anamuelezeaje Hayati Baba wa Taifa kama baba yake na kama kiongozi?Ana ushauri gani kwa wapiga kura katika mwaka huu wa uchaguzi? Ana mtizamo gani kuhusu viongozi mbalimbali ambao hupenda kumuenzi Baba wa Taifa kwa maneno huku vitendo vyao vikiwa tofauti kabisa? Unataka kujua kwanini alipewa jina la “Madaraka”? Ana ushauri gani kwa vijana kuhusu suala zima la kujiletea maendeleo? Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;

BC: Madaraka,asante sana kwa kukubali kufanya nami mahojiano haya. Kwa faida ya wale ambao hawawajui watoto wa Hayati Baba wa Taifa,Mwalimu Nyerere,nyumbani kwenu mmezaliwa watoto wangapi na wewe ulizaliwa lini,ukasomea wapi na kukulia wapi?

MADARAKA NYERERE: Tuko watoto nane. Mimi wa sita. Nimesoma shule

zifuatazo:

-Shule za msingi: Bunge, Forodhani, Arusha School, Isike (Tabora), Tarime.

-Sekondari: Mzizima, na Tambaza (Dar)

-Post-secondary: Shinyanga Commercial Institute

-Vyuo: Finafrica College (Milan, Italy); Algonquin College (Ottawa, Canada)

BC: Turudishe kidogo wakati wa utoto wako.Ni kitu au tukio gani unalolikumbuka zaidi kuhusu utoto wako?Na ulikuwa na ndoto za kufanya kazi gani utakapokua?

MADARAKA NYERERE: Sina tukio lolote kubwa ninalokumbuka la utotoni. Nahisi baada ya kuanza masomo ya biashara kuanzia kidato cha tatu, tayari nilianza kuwa na mawazo ya kuwa mfanyabiashara. Kabla ya hapo, sikumbuki kama nilikuwa na ndoto za kufanya kazi nyingine.

BC: Uliwahi kuelezwa kwanini ulipozaliwa ulipewa jina la Madaraka?Ilikuwaje kukua kama mtoto wa Rais au katika mazingira ya Ikulu na mambo kama hayo? (more…)

Upende,usipende,leo hii unapoongelea masuala ya nyanja ya habari na mawasiliano kupitia zana za blog kwa upande wa Tanzania(Tanzanian Blogsphere), huwezi kuepuka kumtaja Muhidin Issa Michuzi a.k.a Ankal,Mzee wa Libeneke.

Mwanzoni alipoanzisha blog yake maudhui yake yalikuwa zaidi ni picha na maelezo kidogo juu ya picha hiyo au picha hizo.Hiyo ilitokana na ukweli kwamba Michuzi ni seasoned professional photographer.

Baada ya muda fulani,na kutokana na mafanikio aliyokuwa ameyapata,ilimlazimu kutanua wigo wa blog yake na hivyo kutoishia katika picha na maelezo mafupi mafupi tu bali kujumuisha maelezo au habari zaidi.Leo hii,blog yake imekuwa kimbilio la wengi pale wanapotafuta habari motomoto kuhusu kinachoendelea nchini Tanzania,maeneo ya jirani na hata sehemu mbalimbali za ulimwengu.

Hivi sasa yupo mbioni(keshazianza mbio zenyewe) kuboresha zaidi kazi ngumu anayoifanya ya kuendeleza “libeneke”.Ameanzisha tovuti/blog mpya inayopatikana kupitia http://michuzipost.com

BC imepata nafasi ya kuongea naye machache kuhusu ujio huo wa MichuziPost na mambo mengine kuhusiana na tasnia ya habari na mawasiliano. Je,”wadau” watarajie nini katika uwanja huo mpya?Nini siri ya mafanikio yake mpaka hivi sasa?Ana ushauri gani kwa bloggers wapya na wale wanaofikiria kuanzisha blog?Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;

BC: Kwanza nikupe Hongera nyingi kwa kazi nzito unayoifanya.Mambo yanakwendaje?

MICHUZI: Ahsante sana, mambo mswano tu. Libeneke kwa kwenda mbele. Yaani baada ya miaka mitano ya tufanikio kiduchu tulikopatikana, sasa ni wakati muafaka wa kupiga hatua tano mbele, na kusaidia ujenzi wa taifa letu kwa njia ya habari.

Nitakuwa mtovu wa hisani na fadhila endapo kama nitaanza kujieleza bila kwanza kuwashukuru wadau wa Globu ya Jamii popote walipo duniani, kwani bila sapoti yao sidhani kama ningefikia robo tu ya hapa nilipo.

Naomba kwa heshima na taadhima wape AHSANTE SANA wadau. Waambie nawapenda, nawaheshimu na nitandelea kuwa mtumishi wao wakati wa raha na wakati wa shida. Pia naomba ninaowaudhi kwa njia moja ama nyingine wanisamehe kwani mie ni binadamu na si kamilifu. Pia si rahisi kumridhisha kila mdau kwa kila jambo. Napenda sana kutumia ule msemo wa ‘what’s good for the goose, is bad for the hen’. Hivyo naomba uvumilivu na kuelekezana pale palipo na dosari.

BC: Hivi karibuni utatimiza miaka mitano tangu ulipoanza ku-blog pale Helsink,Finland.Umepitia mengi,umeonana na wengi.Waliokuwa hawakujui,bila shaka hivi sasa wanakujua japo kwa sura tu.Unaielezea vipi safari hiyo ndefu tangu ulipoanza kwa maana ya kwamba umekabiliana na changamoto zipi nzito nzito na umejifunza mambo gani ya msingi katika uwanja mpana wa habari na mawasiliano? (more…)

Huu hapa ni ujumbe kutoka kwa Zitto Kabwe(MP)

Ndugu msomaji, nimekuwa na blogu hapo kabla lakini sikuweza kuifanyi kazi kama invyostahili. Nimeamua kuanzisha blogu hii mpya ili liwe jukwaa la kujadiliana jinsi ya kuimarisha demokrasia nchini kwetu Tanzania, Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Karibu kwa maoni, ushauri na hata makatazo! Bonyeza hapa kumtembelea.

Blog ya Muhidini Issa Michuzi ipo mbioni kuhama.Hivi punde itakuwa tovuti kamili inayojitegemea na hivyo kuondoka katika ulingo wa .blogspot.com.Ufuatao ni ujumbe kutoka kwake Issa Michuzi.

Asalaam Aleikhum, Bwana Asifiwe, Tumsifu Bwana, Shalom, Namaste, konnichiwa, Nihao, olá…..

Kwa heshima na taadhima nawaamkia  wadau wote popote mlipo ulimwenguni. Salamu nilizotoa hapo juu naomba ifahamike kuwa  hizo nilizozimudu ni kama kielelezo kwamba nia ni kumuamkua kila mmoja kwa nafasi yake popote alipo. Mie sijambo na naendelea na Libeneke kama kawaida.

Waama, baada ya salamu, napenda kuwafahamisha kwamba Globu ya Jamii hivi karibuni itaingia kwenye awamu mpya ya dot com, ikiwa katika jitihada za kuboresha Libeneke zaidi.

Imechukua muda kuchukua hatua hii kutokana na mazoea kwani toka September 8, 2005 hadi leo si kidogo ati. Hivyo mabadiliko kama yapo inabidi yafanywe kwa uangalifu wa hali ya juu ili kutoleta usumbufu wa aina yoyote kwa wadau wa Globu ya Jamii ambao kwangu ndiyo waajiri wangu wakuu.

Naam, wakati wowote kuanzia sasa libeneke la issamichuzi.blogspot.com litaingia katika awamu ya www.imichuzi.com. unakaribishwa kujaribu na kutoa maoni yako.

Mabadiliko haya  tayari (more…)

Hivi karibuni,pale jijini London,kulifanyika kongamano la watanzania wanaoishi ughaibuni. Lilikuwa ni kongamano la pili la namna hiyo na kwa sababu hiyo liliitwa Diaspora 2.

Miongoni mwa mambo mapya katika kongamano hilo,ilikuwa ni pamoja na kualika rasmi waandishi na hususani waandishi wa mitandaoni kama vile bloggers.Almaarufu Issa Michuzi alikuwa miongoni mwa sio tu waalikwa,bali pia watoa mada(mahojiano naye kuhusu uzoefu wake kufuatia kongamano lile yapo mbioni). Mwandishi mwingine mkongwe na blogger aliyekuwepo katika mkutano huo ni Freddy Macha. Mbali ya kuwa mwandishi,blogger,Freddy pia ni mwanamuziki na muelemishaji hususani katika masuala ya afya na michezo ya kujihami au kujikinga(self-defense). Unaweza kusoma mahojiano yangu ya kina naye kwa kubonyeza hapa na hapa.

Baada ya kongamano lile,Freddy aliketi chini na kuandika  kuhusu yaliyojiri kwenye kongamano na zinapoelekea zama hizi za tekinolojia ya habari na mawasiliano. Bonyeza hapa usome alichokiandika Freddy Macha. Usisahau pia kusoma makala zake katika gazeti la Mwananchi kila Jumapili.

Anaitwa Irene Sporah Njau, ni mtangazaji wa Kipindi cha Sporah Show ambacho kinazidi kujipatia umaarufu na mashabiki.Lakini Sporah ni nani,ametokea wapi,ana malengo gani na ni kwanini anafanya anachokifanya? Ili kupata majibu ya maswali hayo na mengineyo bonyeza hapa kutembelea Spoti Starehe ili kucheki mahojiano kamili.

Nimekuwa katika vuguvugu la habari na mawasiliano kwa njia ya blog kwa muda sasa.Kila siku huwa napitia blogs zaidi ya 500! Huwa natumia huduma ya www.bloglines.com. Ukiandika kitu basi naambiwa umeandika na hivyo napita na kusoma.Ukiwa hujaandika,basi siku hiyo napata muda wa kuperuzi au kutafuta blogs zingine,kuziingiza kwenye orodha yangu ya bloglines.Siku inakuwa imekwenda au naendelea na kazi zingine.

Leo nikiwa katika pitia pitia yangu mtandaoni,nimekutana na blog ya Madaraka Nyerere,mtoto wa Hayati Baba wa Taifa,Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Cha kwanza kilichonijia kichwani ni hasira fulani.Iweje siku zote hizi sikujua kuhusu blog ya Madaraka? Haikutangazwa au ilikuwaje? Hasira zangu ziliyeyuka kama vile barafu inapopigwa na jua baada ya kuanza kuipitia blog yake.Imesheheni habari kemkem.Madaraka ni mwandishi mzuri.Simulizi zake ni nyepesi kama pamba lakini maudhui yake ni mazito kuliko yale mawe yanaouzunguka mji wa Mwanza.

Bonyeza hapa ili kuitembelea blog hiyo. Nikisema mkaribishe nitakuwa nakosea kwani amekuwepo kwa muda sasa.Bravo Madaraka.

Pichani juu ni Madaraka Nyerere(kulia) akiwa na Jaffar Amin,mtoto wa Iddi Amini aliyewahi kuwa Rais wa Uganda. Soma zaidi kuhusu mkutano wao.

KanumbaFrontKatika siku kama ya leo,miaka 26 iliyopita pale mkoani Shinyanga, alizaliwa kijana na kupewa jina la Steven. Hivi leo ni maarufu kama Steven Kanumba au kama mwenyewe anavyojiita wakati mwingine “The Great”. Kwa maana hiyo,leo ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Steven Charles Kanumba.Happy Birthday!

Kwa mtu yeyote ambaye anafuatilia maendeleo ya tasnia ya filamu nchini Tanzania,bila shaka atakubaliana na mimi nikisema kwamba Kanumba ni miongoni mwa waigizaji wa filamu(Film Actors) ambao ni maarufu zaidi nchini Tanzania. Leo hii ni vigumu kuiongelea sanaa ya filamu nchini bila kumhusisha Kanumba kwa njia moja ama nyingine.

Kwa hivyo,haishangazi sana kuona kwamba,katika mwaka uliopita jina lake lilikuwa takribani la kudumu katika vyombo mbalimbali vya habari vikiwemo vya mtandaoni,mitaani nk. Bila shaka unakumbuka jinsi habari ya Kiingereza Vs Kiswahili ilivyozua mjadala wa kitaifa. Kila mtu akasema lake.

Baada ya mambo kama yale,mijadala kama ile,watu hupenda kujua what next? Nilimtafuta Steven Kanumba ili kujua machache kuhusu mipango yake ya mwaka huu.

Unajua Kanumba angependa kupata chakula cha mchana (lunch) na actors gani maarufu hapa ulimwenguni? Una habari kwamba katika Curriculum Vitae(CV) yake ameongeza cheo cha “Blogger”? Unajua ana malengo gani mwaka huu? Una habari kwamba Kanumba hivi sasa amedhamiria kuibua vipaji vingine katika ulimwengu wa uigizaji filamu? Fuatana nami;

BC: Mpaka sasa unalionaje soko la filamu nchini Tanzania? Kumekuwa na mabadiliko gani ya kimsingi ukilinganisha toka ulipoanza mpaka hivi leo?

SK: Soko limetanuka kiasi kwamba tunatambulika kimataifa. Pia hivi sasa makampuni ya kusambaza kazi zetu yameongezea ikiwemo na pesa kwa kiasi fulani tofauti na hapo mwanzo.Safari bado ni ndefu lakini angalau inatia moyo.

BC: Mwaka 2009 ndio tumeumaliza.Jina lako liligonga vyombo vya habari kwa mambo kadha wa kadha.Unaweza kusema umejifunza mambo gani katika mwaka ulioisha? (more…)

Model-Taji

Sitaki kusema mengi leo.Kama unapenda unachokiona pichani basi mtembelee Master Taji Liundi katika blog yake ya u-modo kwa kubonyeza hapa.

Ukitaka kusoma mahojiano yangu na Taji Liundi(Master T) hivi karibuni,bonyeza hapa.

summit-logo

Je wewe ni mwanablogu (Blogger) au mdau wa habari na mawasiliano kwa umma kwa kutumia mtandao? Kama jibu ni ndio, tafadhali unaombwa kujiorodhesha kwa ajili ya maandalizi ya Kongamano Maalumu la Kitaifa kwa ajili Wanablogu (Bloggers) na wadau wa habari na mawasiliano wa Tanzania (Tanzanians Bloggers Summit) linalotarajiwa kufanyika Desemba mwaka huu jijini Dar-es-salaam,Tanzania.

Dhumuni la kongamano hili ni Kuelimishana, Kufahamiana, Kuamsha Utambuzi Rasmi Kuhusu Tekinolojia ya Blogu na Mawasiliano ya Umma kwa Kutumia Mitandao, Kusaidia Utambuzi Rasmi juu ya mchango wa blogu nchini Tanzania kama chombo muhimu cha habari na mawasiliano, Kuelimishana jinsi gani blogu zinaweza kutumika katika kuleta maendeleo katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi, kuburudisha, kukuza utamaduni nk.

Wataalamu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wataalikwa kutoa mada na mafunzo mbalimbali kuhusiana na tekinolojia ya kublogu, zana nyinginezo za mawasiliano mtandaoni kama vile mitandao jamii(social networking), online forums nk.Kutakuwa na vipindi vya maswali na majibu.

Ili kufanikisha maandalizi ya Kongamano hili la kihistoria, kujiorodhesha kwako ni muhimu sana. Muda wa kujiodhoresha ni kuanzia tarehe 12/8/2009 (Jumatano) mpaka 12/9/2009 (Jumamosi) tu.

Kinachohitajika ili kujiandikisha ni :

Jina Lako, Anuani yako ya barua pepe (E-mail), Mahali Ulipo au unapoishi (Nchi,mji nk),Namba ya Simu (sio lazima) na Anuani au URL(Universal Resource Locator) ya blogu yako (mfano www.kongamano.blogspot.com/wordpress.com/.com/typepad nk). Vyeti vya Ushiriki vitatolewa kulingana na habari utakazoziorodhesha hapa.

Unaweza kujiorodhesha kwa kutuma ombi lako kwa barua pepe kwenda; summit@bongocelebrity.com.

Zingatia tarehe za kujiandikisha.

Ni mwezi mmoja tu! Asante kwa ushirikiano. UMOJA NI NGUVU!

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page