Blogging for good 5 YEARS. You definitely deserve all the Congratulations.Hongera mdada.Kwa picha na habari zaidi,tembelea hapa.

Ingawa kila siku idadi ya bloggers wa kitanzania inazidi kuongezeka,idadi ya wanawake wanaoblog bado ni ndogo ikilinganishwa na wale wa kiume.Yawezekana ni kwa sababu wanawake bado hawajapata mwamko wa kutosha au pengine ni kitu ambacho bado wanakipa kisogo.

Lakini pamoja na idadi ya wanawake kuwa ndogo,wanaofanya hivyo wanafanya kazi nzuri sana ya kuwawakilisha wanawake wenzao.Miongoni mwa wanawake hao ni pamoja na Shamim Mwasha au Zeze kama anavyojulikana kwa watu wake wa karibu.

Iwe ni shughuli yenye mvuto wa kitaifa au wa mtu binafsi(hususani zile zenye kuwagusa wanawake zaidi),ukihudhuria na kutizamatizama katika watu waliopo mstari wa mbele katika kuchukua kumbukumbu iwe ni kwa kutumia picha za mgando(still photos) au videos,bila shaka waweza kumuona Zeze.Ukimsalimia atakujibu na kukurushia tabasamu ambalo naweza kusema ni “signature” yake.

Hivi karibuni nilipata nafasi ya kufanya naye mahojiano ambayo utayasoma hivi punde.Zeze ambaye blog yake inakwenda kwa jina www.8020fashions.blogspot.com, anaweka bayana mambo kadhaa kuhusu harakati zake kama mwandishi wa habari(taaluma yake) na pia blogger pamoja na ujasiriamali.

Yote tisa,kumi ni kwamba siku chache zijazo,Shamim kupitia blog yake ya 8020fashions,anasheherekea miaka mitano(5) tangu aanze shughuli ya kublog au Libeneke la kublog kama ambavyo rafiki yangu Issa Michuzi hupenda kuiita shughuli hii.Nimemuuliza pia maswali machache kuhusu siku hiyo maalum kwake na kwa wapenzi wa blog yake ambayo itafanyika pale Diamond Jubilee tarehe 30 October,2011.Twende pamoja katika mahojiano yafuatayo;

BC: Umekuwa uki-blog kwa muda gani mpaka hivi sasa?Nini kilikusukuma katika kuanzisha blog yako?

SM: Huu ni mwaka wangu wa tano sasa tangu nianze hili libeneke.Kikubwa kilichonisukuma kilikuwa ni nia yangu ya kutangaza biashara ya duka langu la nguo liitwalo 8020 Fashion lililopo Sinza.Nikaona nifungue blog ili niwe naweka nguo na bidhaa zingine kadiri zinavyowasili dukani.Sasa kama ujuavyo si kila siku naweza kuwa na new arrival na ili watu warejee kuangalia blog ndio nikaanza kuweka picha za matukio mbalimbali huku nikiwa nimejikita kwenye fashion zaidi katika kuonyesha nini kilivaliwa wapi na nani na mambo kama hayo.

BC: Kitaaluma wewe ni mwandishi wa habari. Sasa ukiwa kama blogger,unadhani kuna tofauti gani za kimsingi kati ya mwandishi wa habari wa kawaida na blogger? Je,kuna misingi ambayo wote (a journalist and a blogger) wanayotakiwa kuzingatia?

SM: Ni kweli kabisa,ipo tofauti kubwa sana. Kama ujuavyo blogger inakuwa ni mimi kama mimi ambapo nisipo-update ni blog inakuwa imelala doro. Hivyo kuwa kama blogger inabidi uwe na juhudi binafsi za kujituma kitu ambacho ni tofauti na mwandishi wa habari ambapo hata wewe usipoenda kazini au kufanya kazi gazeti ni lazima litoke tu.

BC: Blog yako imejikita zaidi katika kuandika habari za urembo,shughuli kama vile harusi,kitchen party,fashion shows nk.Ni kwanini uliamua kuwa na “niche” kama hiyo?

read more

Nestory Fedeliko — wengi wetu tunamfahamu kwa jina “FeDë” — ni mchoraji katuni chipukizi kiumri. Lakini kwa upande wa kazi, utasamehewa ukidhani ni mtu ambaye labda mvi zimeanza kuota utosini!

Jamaa zetu wa Vijana FM walipata nafasi ya kumuhoji; kama ilivyo desturi yao, walimuuliza maswali matano tu. Walichopata ni majibu mazuri na ya kina — tafadhali, usiruhusu uvivu ukuingie kwasababu mahojiano yanaonekana ni marefu. Kuna hadithi na visa vya hapa na pale vitakavyokufanya utabasamu na ucheke. Majibu mengine yatakukumbusha mbali. Mengine yatakushangaza. Bila kusahau, FeDë ameamua kutoa nasaha kuhusu fani ya uchoraji wa katuni na maisha kwa ujumla.

BONYEZA HAPA KUSOMA MAHOJIANO HAYO:

Kama wewe ni mfuatiliaji wa masuala ya watanzania mtandaoni,bila shaka utakubaliana nasi kwamba miongoni mwa mahali ambapo mengi hutokea na mengi huandikwa kama sio kujadiliwa basi mahali hapo ni katika blog inayokwenda kwa jina la U-turn.

Ni blog ambayo ingawa haina umri mkubwa(ilianzishwa mwaka mmoja na nusu tu uliopita), tayari imefanikiwa kuwa chanzo muhimu cha habari,michapo,maoni,matukio bila kusahau udaku wa hapa na pale.Ni mafanikio ambayo sio ya kubeza.It is what it is!

Mwendeshaji na mmiliki wa U-turn si mwingine bali Mange Kimambi ambaye miaka michache iliyopita ilikuwa ukisikia jina lake basi ilikuwa ni kupitia kurasa mbalimbali za magazeti hususani yale yanayoitwa “magazeti pendwa”. Leo hii mambo ni tofauti. Ni mama,mke,mwanafunzi na blogger mwenye idadi kubwa tu ya wasomaji na wafuatiliaji.

Hivi karibuni tulipata nafasi ya kufanya naye mahojiano ya kina. Hii ni mara ya kwanza kwa Mange kufanya mahojiano ya kina na chombo chochote cha habari.

Je,Mange ni nani hasa?Ametokea wapi mpaka kufikia alipo hivi sasa ambapo kila siku idadi ya wasomaji na wanaofuatilia maisha yake na anachokiandika inazidi kuongezeka? Ni matukio gani katika maisha yake ambayo kwa namna moja au nyingine yamechangia in making her who she is today?

Nini siri ya mafanikio yake au ya blog yake?Unataka kujua ana maoni gani kuhusu mambo mbalimbali kama vile uongozi wa Rais Jakaya Kikwete?Ana ushauri gani kwa wasichana wadogo(teen girls)? Kwa majibu ya maswali hayo na mengine mengi,fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;

BC: Mange,Karibu sana ndani ya BC.Mambo vipi?

MANGE: Asante sana.Feels good to be here!

BC:
Nimewahi kusoma mahali kwamba maisha yako ni kama vile kitabu kilicho wazi(an open book) ambapo kila anayetaka kusoma anayo nafasi ya kufanya hivyo.Lakini bila shaka utakubaliana nami kwamba wapo ambao hawajui lolote kuhusu historia ya maisha yako.Naomba tuanzie hapo…kwa kifupi tu ulizaliwa wapi,lini,ukasomea na kukulia wapi na mambo kama hayo.

MANGE: Nilizaliwa Hindu Mandal,Hospital- Dar es Salaam.Cheti changu cha kuzaliwa kina mwaka tofauti na passport yangu.According to my passport, I was born in 1980 lakini tukifuata Birth Certificate kuna difference ya 4years.Hii imetokana na kuna wakati mama yangu alitaka kunitoa kwa baba yangu akidai kwamba nina miaka chini ya 7.So kutokana na sheria za Tanzania natakiwa kuishi na mama. Baba yangu naye akawa na documents zake zinazosema nimeshapita miaka 7 kwa hiyo natakiwa kuishi na baba.So mama alikuwa na cheti changu cha kuzaliwa chenye umri tofauti na baba naye na passport yangu yenye umri tofauti.GO FIGURE.

Primary nilisoma Arusha School iliyoko Arusha- the best memories of my childhood came from my time there. Nilifanikiwa kufaulu mitihani ya darasa la 7 na nilichaguliwa kujiunga na Arusha Secondary.Baba yangu alifurahi sana na akanizawadia kwa kunipeleka kusoma Zimbambwe.So niliishi Harare miaka kadhaa kwa masomo yangu ya secondary.

Baada ya hapo nilikwenda Marekani kuanza masomo yangu ya juu.Kwa bahati nzuri (siwezi kusema bahati mbaya) nilijifungua mtoto wa kike,Bhoke, nikiwa Marekani jambo ambalo lilinifanya nirudi nyumbani kujipanga upya.

Then in 2004 nilijiunga na AVU-UDSM ambapo nilipata degree yangu ya Business Administration na sasa nipo Dubai nasoma Masters(MBA)

Mostly nimekulia Dar-es-salaam.

BC: Unakumbuka nini zaidi kuhusu maisha yako ya utotoni?Ulitaka kuwa nani,ulipenda michezo gani na tukio gani la utotoni ambalo hutokaa ulisahau?

read more

Ankal Michuzi (Issa Michuzi) ambaye ni mmoja wa waasisi wa mitandao ya habari ya jamii (blogs) hapa nchini amewashauri wadau wa sanaa hasa wasanii kuanza kuingia kwa kasi kwenye matumizi ya teknolojia hiyo kwani ni njia kubwa ya kujitangaza na kuuza kazi za sanaa kote duniani.

Akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa leo Jumatatu,Michuzi ambaye blog yake ya www.issamichuzi.blogspot.com imepata umaarufu mkubwa kutokana na kutembelewa na watu wengi aliweka wazi kwamba,blogs zimekuwa zikitembelewa na watu mbalimbali duniani hivyo wasanii hawana budi kuzitumia ili kujitangaza, kusambaza kazi zao na hata kujitambulisha katika masoko ya kimataifa.

Alisema kwamba, blogs tofauti na aina nyingine za vyombo vya habari inatumiwa kuhifadhi picha nyingi na kazi mbalimbali, kupata taarifa kuhusu tasnia ya sanaa, kupokea mawazo ya wateja wa kazi za sanaa na hata kuwa na wasaa wa kuwasiliana na wasanii wengine na hivyo kupanuka kimawazo na kiujuzi.

Akizungumzia historia ya blogs,Michuzi alisema kwamba ni teknolojia mpya hapa nchini na kwamba,ilianza kwa kuandika habari za kawaida lakini leo hii ni tegemeo katika kupasha habari kwa uharaka zaidi, kuwafikia watu wengi kuliko vyombo kadhaa vya habari na kimbilio la jamii kwani imekuwa kama sehemu ya jamii katika masuala mbalimbali.

Kwa ujumla Michuzi aliwataka wasanii na wadau wa Sanaa kuamka na kuanza kutumia teknolojia hiyo kwani wasanii mbalimbali duniani si tu wamekuwa wakitumia blog katika kujitangaza na kutambulisha kazi zao bali pia wamekuwa wakimilki mitandao na technolojia mbalimbali za mawasiliano.

Katika kuonesha kwamba, teknolojia hiyo ni muhimu Michuzi ameahidi kuwapa mafunzo ya bure wadau wa Jukwaa la Sanaa juu ya kufungua na kumiliki blog ambayo yataendeshwa Ijumaa ya Desemba 10,2010 kwenye Ukumbi wa BASATA.Wadau wote wa Sanaa mnakaribishwa.

Pichani juu ni Ankal Michuzi akiwaonyesha wadau wa Jukwaa la Sanaa jinsi ya kuweka video kwenye YouTube.

Jina la Madaraka Nyerere(pichani) sio geni miongoni mwa watanzania.Ukiachilia mbali ukweli kwamba yeye ni mtoto wa sita wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (kitu ambacho bila shaka kinampa automatic celebrity status), yeye pia ni mwandishi,mfanyabiashara na mtu ambaye huwa hasiti kuelezea hisia zake kuhusu mambo mbalimbali iwe ni katika nyanja za kisiasa,kijamii na hata kiuchumi kila mara fursa ya kufanya hivyo inapojitokeza.

Mwaka jana mwezi wa nne(April) yeye na Jaffar Amin(mtoto wa Iddi Amin-Rais wa zamani wa Uganda) waliingia katika vitabu vya kumbukumbu vya wapenda amani duniani walipokutana kwa mara ya kwanza ikiwa ni ishara ya amani na usuluhisho barani Afrika na kwingineko.

Hivi karibuni nilipata nafasi ya kuzungumza naye kuhusu mambo kadhaa yakiwemo ya kifamilia na pia kupata maoni yake kuhusu mambo mbalimbali.Je,ni kwanini mpaka leo hii hajajiingiza katika masuala ya siasa au uongozi?Anamuelezeaje Hayati Baba wa Taifa kama baba yake na kama kiongozi?Ana ushauri gani kwa wapiga kura katika mwaka huu wa uchaguzi? Ana mtizamo gani kuhusu viongozi mbalimbali ambao hupenda kumuenzi Baba wa Taifa kwa maneno huku vitendo vyao vikiwa tofauti kabisa? Unataka kujua kwanini alipewa jina la “Madaraka”? Ana ushauri gani kwa vijana kuhusu suala zima la kujiletea maendeleo? Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;

BC: Madaraka,asante sana kwa kukubali kufanya nami mahojiano haya. Kwa faida ya wale ambao hawawajui watoto wa Hayati Baba wa Taifa,Mwalimu Nyerere,nyumbani kwenu mmezaliwa watoto wangapi na wewe ulizaliwa lini,ukasomea wapi na kukulia wapi?

MADARAKA NYERERE: Tuko watoto nane. Mimi wa sita. Nimesoma shule

zifuatazo:

-Shule za msingi: Bunge, Forodhani, Arusha School, Isike (Tabora), Tarime.

-Sekondari: Mzizima, na Tambaza (Dar)

-Post-secondary: Shinyanga Commercial Institute

-Vyuo: Finafrica College (Milan, Italy); Algonquin College (Ottawa, Canada)

BC: Turudishe kidogo wakati wa utoto wako.Ni kitu au tukio gani unalolikumbuka zaidi kuhusu utoto wako?Na ulikuwa na ndoto za kufanya kazi gani utakapokua?

MADARAKA NYERERE: Sina tukio lolote kubwa ninalokumbuka la utotoni. Nahisi baada ya kuanza masomo ya biashara kuanzia kidato cha tatu, tayari nilianza kuwa na mawazo ya kuwa mfanyabiashara. Kabla ya hapo, sikumbuki kama nilikuwa na ndoto za kufanya kazi nyingine.

BC: Uliwahi kuelezwa kwanini ulipozaliwa ulipewa jina la Madaraka?Ilikuwaje kukua kama mtoto wa Rais au katika mazingira ya Ikulu na mambo kama hayo? read more

Upende,usipende,leo hii unapoongelea masuala ya nyanja ya habari na mawasiliano kupitia zana za blog kwa upande wa Tanzania(Tanzanian Blogsphere), huwezi kuepuka kumtaja Muhidin Issa Michuzi a.k.a Ankal,Mzee wa Libeneke.

Mwanzoni alipoanzisha blog yake maudhui yake yalikuwa zaidi ni picha na maelezo kidogo juu ya picha hiyo au picha hizo.Hiyo ilitokana na ukweli kwamba Michuzi ni seasoned professional photographer.

Baada ya muda fulani,na kutokana na mafanikio aliyokuwa ameyapata,ilimlazimu kutanua wigo wa blog yake na hivyo kutoishia katika picha na maelezo mafupi mafupi tu bali kujumuisha maelezo au habari zaidi.Leo hii,blog yake imekuwa kimbilio la wengi pale wanapotafuta habari motomoto kuhusu kinachoendelea nchini Tanzania,maeneo ya jirani na hata sehemu mbalimbali za ulimwengu.

Hivi sasa yupo mbioni(keshazianza mbio zenyewe) kuboresha zaidi kazi ngumu anayoifanya ya kuendeleza “libeneke”.Ameanzisha tovuti/blog mpya inayopatikana kupitia http://michuzipost.com

BC imepata nafasi ya kuongea naye machache kuhusu ujio huo wa MichuziPost na mambo mengine kuhusiana na tasnia ya habari na mawasiliano. Je,”wadau” watarajie nini katika uwanja huo mpya?Nini siri ya mafanikio yake mpaka hivi sasa?Ana ushauri gani kwa bloggers wapya na wale wanaofikiria kuanzisha blog?Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;

BC: Kwanza nikupe Hongera nyingi kwa kazi nzito unayoifanya.Mambo yanakwendaje?

MICHUZI: Ahsante sana, mambo mswano tu. Libeneke kwa kwenda mbele. Yaani baada ya miaka mitano ya tufanikio kiduchu tulikopatikana, sasa ni wakati muafaka wa kupiga hatua tano mbele, na kusaidia ujenzi wa taifa letu kwa njia ya habari.

Nitakuwa mtovu wa hisani na fadhila endapo kama nitaanza kujieleza bila kwanza kuwashukuru wadau wa Globu ya Jamii popote walipo duniani, kwani bila sapoti yao sidhani kama ningefikia robo tu ya hapa nilipo.

Naomba kwa heshima na taadhima wape AHSANTE SANA wadau. Waambie nawapenda, nawaheshimu na nitandelea kuwa mtumishi wao wakati wa raha na wakati wa shida. Pia naomba ninaowaudhi kwa njia moja ama nyingine wanisamehe kwani mie ni binadamu na si kamilifu. Pia si rahisi kumridhisha kila mdau kwa kila jambo. Napenda sana kutumia ule msemo wa ‘what’s good for the goose, is bad for the hen’. Hivyo naomba uvumilivu na kuelekezana pale palipo na dosari.

BC: Hivi karibuni utatimiza miaka mitano tangu ulipoanza ku-blog pale Helsink,Finland.Umepitia mengi,umeonana na wengi.Waliokuwa hawakujui,bila shaka hivi sasa wanakujua japo kwa sura tu.Unaielezea vipi safari hiyo ndefu tangu ulipoanza kwa maana ya kwamba umekabiliana na changamoto zipi nzito nzito na umejifunza mambo gani ya msingi katika uwanja mpana wa habari na mawasiliano? read more

Huu hapa ni ujumbe kutoka kwa Zitto Kabwe(MP)

Ndugu msomaji, nimekuwa na blogu hapo kabla lakini sikuweza kuifanyi kazi kama invyostahili. Nimeamua kuanzisha blogu hii mpya ili liwe jukwaa la kujadiliana jinsi ya kuimarisha demokrasia nchini kwetu Tanzania, Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Karibu kwa maoni, ushauri na hata makatazo! Bonyeza hapa kumtembelea.

Blog ya Muhidini Issa Michuzi ipo mbioni kuhama.Hivi punde itakuwa tovuti kamili inayojitegemea na hivyo kuondoka katika ulingo wa .blogspot.com.Ufuatao ni ujumbe kutoka kwake Issa Michuzi.

Asalaam Aleikhum, Bwana Asifiwe, Tumsifu Bwana, Shalom, Namaste, konnichiwa, Nihao, olá…..

Kwa heshima na taadhima nawaamkia  wadau wote popote mlipo ulimwenguni. Salamu nilizotoa hapo juu naomba ifahamike kuwa  hizo nilizozimudu ni kama kielelezo kwamba nia ni kumuamkua kila mmoja kwa nafasi yake popote alipo. Mie sijambo na naendelea na Libeneke kama kawaida.

Waama, baada ya salamu, napenda kuwafahamisha kwamba Globu ya Jamii hivi karibuni itaingia kwenye awamu mpya ya dot com, ikiwa katika jitihada za kuboresha Libeneke zaidi.

Imechukua muda kuchukua hatua hii kutokana na mazoea kwani toka September 8, 2005 hadi leo si kidogo ati. Hivyo mabadiliko kama yapo inabidi yafanywe kwa uangalifu wa hali ya juu ili kutoleta usumbufu wa aina yoyote kwa wadau wa Globu ya Jamii ambao kwangu ndiyo waajiri wangu wakuu.

Naam, wakati wowote kuanzia sasa libeneke la issamichuzi.blogspot.com litaingia katika awamu ya www.imichuzi.com. unakaribishwa kujaribu na kutoa maoni yako.

Mabadiliko haya  tayari read more

Hivi karibuni,pale jijini London,kulifanyika kongamano la watanzania wanaoishi ughaibuni. Lilikuwa ni kongamano la pili la namna hiyo na kwa sababu hiyo liliitwa Diaspora 2.

Miongoni mwa mambo mapya katika kongamano hilo,ilikuwa ni pamoja na kualika rasmi waandishi na hususani waandishi wa mitandaoni kama vile bloggers.Almaarufu Issa Michuzi alikuwa miongoni mwa sio tu waalikwa,bali pia watoa mada(mahojiano naye kuhusu uzoefu wake kufuatia kongamano lile yapo mbioni). Mwandishi mwingine mkongwe na blogger aliyekuwepo katika mkutano huo ni Freddy Macha. Mbali ya kuwa mwandishi,blogger,Freddy pia ni mwanamuziki na muelemishaji hususani katika masuala ya afya na michezo ya kujihami au kujikinga(self-defense). Unaweza kusoma mahojiano yangu ya kina naye kwa kubonyeza hapa na hapa.

Baada ya kongamano lile,Freddy aliketi chini na kuandika  kuhusu yaliyojiri kwenye kongamano na zinapoelekea zama hizi za tekinolojia ya habari na mawasiliano. Bonyeza hapa usome alichokiandika Freddy Macha. Usisahau pia kusoma makala zake katika gazeti la Mwananchi kila Jumapili.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page