Wakati suala zima la nani alileta mradi wa Zinduka nchini Tanzania,nani alianzisha idea hiyo na mchakato mzima wa mradi huo likiendelea,nadhani sio vibaya kama tukajionea kile ambacho wasanii waliweza kufanya.
Kimsingi,kampeni hii ina umuhimu wa aina yake.Malaria ni tishio la uhai wa mamilioni ya watu ulimwenguni.Inaua kuliko ugonjwa mwingine wowote.Inaua zaidi ya Ukimwi!Kuna haja ya kuendelea kusambaza ujumbe.Kuna haja ya kuendelea kupeana maarifa kuhusu jinsi ya kupambana na ugonjwa wa malaria.Mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria ni zaidi ya chandarua.Ni suala la mazingira.Vidimbwi vya maji yaliyotuama.Misitu ya majani inayoachwa bila matunzo.Ni pamoja na kutumia kila aina ya kinga zilizopo.Hongera kwa wasanii waliotengeneza na kushiriki katika video hii;Zinduka. Kwa msaada zaidi wa jinsi ya kupambana na malaria,bonyeza hapa.

Kila ifikapo tarehe 13 August, yeye hukumbuka na kusheherekea siku yake ya kuzaliwa. Alipozaliwa pale jijini Mwanza,kaskazini mwa Tanzania wazazi wake walimpa jina la Fareed. Leo hii kwa wengi anatambulika kama Fid Q.
Kama ambavyo umeshasikia,leo hii,tarehe 25 Feb 2010, album yake inayokwenda kwa jina Propaganda inaingia mtaani.Kwa hiyo leo ukizunguka mitaani,usishangae kukutana na mtu kabeba CD mpya ya Fid Q au ukasikia sauti yake kwenye gari,magari,usafiri wa umma.Jambo moja muhimu unaloweza kufanya ni kujipatia nakala yako halisi.Hakuna njia nzuri zaidi ya kuunga mkono juhudi za wasanii zaidi ya hiyo!
Hivi karibuni nilipata nafasi ya kuzungumza machache na Fid Q kuhusu ujio wa albamu hii ya Propaganda,muungano wa wasanii wa bongo fleva na pia suala zima la nyimbo nyingi za bongo fleva kuwa na maudhui ya mapenzi zaidi ya kitu kingine chochote.Kwanini ameiita album yake Propaganda? Anamaanisha nini? Je unajua Fid Q ana mtazamo gani kuhusu muungano wa wasanii?Je anasemaje kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika maendeleo au kifo cha muziki wa kizazi kipya? Fuatana nami katika mahojiano yafuatayo;
BC: Kwanza hongera kwa album mpya.Labda kwa ujumla tu,album hii umeitengenezea katika studio zipi,itakuwa na nyimbo ngapi na umewashirikisha wasanii gani wengine?
Fid Q: Asante sana kaka.Album hii nimeifanya katika studio 3 tofauti.Nimefanya kwa MJ Records, Tongwe Records na kwa Lamar.Nimewashirikisha wasanii kama AY, NCHA KALI, MZEE ZORRO, JUMA NATURE,QJ, NYLON WA MANZESE CREW, BI KIDUDE na wengine kibao bila kuwasahau MATONYA na MZUNGU KICHAA.
BC: Kwanini umeiita Propaganda?Kuna ujumbe wowote maalumu kutokana na jina la album? (more…)

Siku chache zijazo,tarehe 25 mwezi huu kwa uhakika,Fareed Kubanda au maarufu kama Fid Q anatarajia kuiweka sokoni albamu yake mpya ambayo ameipa jina Propaganda.
Hivi karibuni ametoa single moja kama utambulisho wa kitachokuwepo katika album hiyo. Single inakwenda kwa jina la Danger akiwa amemshirikisha J-Bryant.Usikilize kwa kubonyeza player hapo chini.Usikilize kwa makini.Sikiliza midundo,hisia,ujumbe uliomo na kisha sema usikike.Kwa ufupi ninachoweza kusema ni kwamba kuna utofauti…
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Nina imani kwamba hujawasahau Wagosi wa Kaya.Naam ni wale wale vijana kutoka Tanga ambao miaka ileee waliingia kwenye anga za muziki kwa kishindo pale walipohoji “Tanga Kunani Pale”?
Tangu pale Wagosi wa Kaya wakawa wamejikita katika ile aina ya muziki wa kizazi kipya ambao mimi hupenda kuuita “conscious” kwa maana ya kwamba unalenga kwa undani kile kinachoendelea katika jamii.Ukipenda uite “muziki tambuzi”.
Baada ya kuwa kimya kwa miaka kadhaa(hata wao wanakiri katika wimbo huu kwamba walikuwa kimya kwa muda mrefu) wamerudi.Na mara hii wamerudi wakiwa na timing ya aina yake.Wanagusia uchaguzi,siasa na mambo kama hayo. Kama unavyojua,mwaka huu,watanzania watajipanga foleni ili kuchagua tena viongozi.Demokrasia.Wao wanasema ni Maumivu ya Miaka 10!
Wasikilize Wagosi wa Kaya kwa kubonyeza player hapo chini.Sikiliza kwa makini ujumbe kwani kwa maoni yangu,kidogo sauti ya beats ni ya juu kuliko za wanaoghani.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Picha kwa hisani ya outhere.de.

Pichani ni Ilunga Khalifa (CP) au kwa wengi C-Pwaa. Ana style ya kipekepekee hivi Bongo. Kuna wakati C-Pwaa alikuwa anablog kwa kutumia simu yake(mobile blogging).Yeye alikuwa msanii wa kwanza kuamua kuanzisha blog. Sina uhakika kwanini aliacha kwani kwa muda sasa blog yake imekuwa parking lot.What happened C-Pwaa?

Tunapoelekea kuufunga mwaka 2009,yaelekea AY ameamua kwamba mwaka haushi bila kuonyesha kule anapojaribu kuelekea kisanii. Utakumbuka kwamba AY mwaka huu aliteuliwa kuwania tuzo za MTV Africa Music Awards na ndiye mwanamuziki ambaye amekuwa akipewa sifa na moyo zaidi kutoka kwa wasanii wengine wa kimataifa kama vile K9,Wyclef Jean,Akon na wengineo.
Safari hii anakuja na wimbo ambao ameuita Bed and Breakfast. Ni mchanganyiko kabambe wa Raga na Hip Hop. Wimbo umefanyika katika studio za B.Hitz Music Group chini ya Producer Hermy B huku mastering ikifanyika katika studio ya Ogopa Deejays ya nchini Kenya.
AY anasema video ya wimbo huu itafanyika mwezi huu ndani ya jiji la Johannesburg nchini South Africa chini ya kampuni ya Film Online ambayo ni miongoni mwa kampuni bora kabisa barani Africa katika utengenezaji wa videoz na mambo kama hayo.Miongoni mwa kazi walizowahi kuzifanya jamaa wa Film Online ni pamoja na Video Bora ya Mwaka ya MTV 2009 ya msanii S.A HHP.
Nilipoongea na AY hivi karibuni alinidokezea kwamba nia yake hivi sasa ni kuhakikisha kwamba Tanzania na wasanii wa kitanzania wanajikita na kuleta ushindani wa dhati katika soko la kimataifa la muziki na burudani kwa kwenda sambamba na wasanii wengine wanaofanya vizuri barani Africa kama vile kutoka nchi za South Africa,Nigeria etc.
Ukisikiliza wimbo wa Bed and Breakfast utagundua kwamba kuna kiitikio cha mwanadada fulani.Kwa bahati mbaya,mwanadada huyo hapendi kupewa credit zake kwa sababu zake binafsi.Kwa maana hiyo hatotajwa kwa sasa….labda baadaye. Pata burudani,sikiliza Bed and Breakfast.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Wikiendi iliyopita,jiji la Dar-es-salaam liligubikwa na homa ya “Fiesta”.Kuna ambao wamesema kama hukuhudhuria haifai hata kuomba kusimuliwa ilivyokuwa kwani hakuna jinsi ya kusimulia!
Wengi walikuwa wakielezea jinsi mwanamuziki mkongwe wa hip hop kutoka nchini Marekani,Busta Rhymes, alivyoweza kukonga nyoyo za mashabiki wa muziki.Wanasema japokuwa jamaa alilikwaa jukwaa wakati mida imeshakwenda sana,aliweza kuonyesha thamani yake kwa kuwapeleka mbio mashabiki wa mwanamuziki huyo.
Mimi sikuwepo.Nafuata ushauri wa kutokuomba hata kusimuliwa sana mambo yalivyokuwa.Niliyoyasoma katika vyombo mbalimbali vya habari yanatosha.Lakini donge nililonalo ni kutokuwepo kuwaona HBC(Hard Blasterz Crew) wakisimama tena jukwaani kwa pamoja.I would have loved that.HBC ni miongoni mwa makundi ambayo binafsi naamini kwa dhati kwamba yalichangia sana kuuweka muziki wa kizazi kipya hapo ulipo.Isitoshe nilibahatika kuwa mtu wa karibu kwa vijana hao wa HBC enzi hizo walipokuwa wanaanza kuiteka fani ya muziki wa kizazi kipya.
Napenda kuheshimu watu au vikundi vinavyoanzishwa na kisha kujenga msingi wa jambo fulani.HBC ni miongoni mwa makundi hayo.Swali ni je,HBC ndio wamerudiana na labda tutarajie albamu kutoka kwao? Najaribu kuwatafuta ili wajibu swali hilo hapo juu wenyewe. Makundi mengine ambayo yalikuwepo siku hiyo ni pamoja na Daz Nundaz…wale wazee wa Kaaamandaaa..unawakumbuka? Wateule pia walikuwepo…yaani Jafarai,Mchizi Mox bila kumsahau Jay Moe.
Wimbo waliouimba majuzi ni huu hapa unaoitwa Niamini.Sikiliza hapo chini.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Pichani kutoka kushoto ni Terry Msiagi(aka Baba Ray),William Shundi(Big Willy) na Joseph Haule(Professor Jay)
Sijawahi kupata nafasi ya kufanya nao mahojiano ili kujua kwa kina maana au chanzo cha jina Nako 2 Nako.Pamoja na hayo,wengi wanawakubali na kwa mambo mbalimbali,yakiwemo binafsi,wameshagonga vichwa vya habari mara kwa mara. Walianzia A-Town/City kabla ya kuweka kambi jijini Dar.
Hivi karibuni wamefyatua kitu kipya.Wimbo unaitwa Ndani ya Nyumba ambao kutokana na Producer wake,Hermy B(kutoka B’Hitz Music) ni wimbo wa kustarehesha zaidi kuliko kuelimisha au vitu kama hivyo.
Kitu ambacho kimekuwa kikinivutia kutoka Nako2Nako ni aina yao ya kughani.Ina utofauti fulani hivi ambao kimsingi ni muhimu.Nimewahi kusisitiza katika “kijiwe” fulani kwamba kama mtu anataka kupata mafanikio fulani katika chochote anachotaka kukifanya,ni muhimu akawa “mbunifu”.Kwenye muziki hali ni hiyo hiyo.Lazima utoke tofauti.La sivyo,watu watakusikiliza na kukuacha solemba haraka iwezekanavyo.Huna jipya.
Wasikilize Nako2Nako katika Ndani ya Nyumba
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Anajulikana kwa jina la Young D.Inasemekana ndiye hip-hop artist mdogo kupita wote nchini Tanzania.Tarehe 23 mwezi ujao(December) atafikisha miaka 17.Nimeweka neno ‘inasemekana” kwa sababu naamini wengine pia wapo ila huenda suala zima la “kujulikana na kukubalika” ndilo linalowaweka nyuma ya pazia.
Hivi karibuni kulikuwa na “ubishi” kwamba nani anamuandikia mashairi yake.Aliongea na Bongo5 na kuweka mambo wazi kwamba yeye anaandika mwenyewe tungo zake.Msikilize Young D hapo chini katika wimbo Teacher.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Photo/bongo5
Hivi karibuni makundi mawili ya wanamuziki wa kizazi kipya,TMK Wanaume Family na Tip Top Connections,kutoka jijini Dar-es-salaam walifanya Tour iliyojulikana kama Chama Kubwa Tour ambayo ilizunguka katika Kanda ya Ziwa.Tour yao ilianzia Tabora Mjini na kisha kuelekea Kahama,Geita,Mwanza Mjini,Sengerema,Chato,Kakola na kumalizikia mjini Bukoba.
Tour hiyo ilidhaminiwa na Vodacom. Hizi hapa ni baadhi ya picha kutoka katika Tour hiyo.

A light moment.

TMK Wanaume Family na Tip Top Connections wakiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kahama(katikati mwenye suti) aliyekwenda kuwatembelea hotelini walipofikia.

Ushabiki na upenzi wa Bongo Fleva sio mijini pekee.What can you say about this photo?

Time to deliver.

