
Sijui kama nitakuwa nimekosea nikisema kwamba pengine AY na MwanaFA mpaka hivi sasa wanaweza kuwa wanashikilia rekodi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao wameshirikiana zaidi katika kazi zao.Kumbuka hawa wametoka mbali tangu enzi zao wakiwa East Coast Team iliyokuwa ikiongozwa na King Crazy GK ambaye sina uhakika yuko wapi siku hizi na anafanya shughuli gani.
Kuthibitisha kuzidi kukomaa kwa ushirikiano wao,AY na MwanaFA wakimshirikisha Hard Mad,wameachia single inayokwenda kwa jina Dakika Moja. Hii ni production kutoka B’Hitz Production iliyo chini ya Hermy B.
Sikiliza hapo chini;Ujumbe ni kwamba anaomba dakika moja tu aseme yaliyopo moyoni.Mmh,inawezekana kweli ndani ya dakika moja kikaeleweka?Sijui.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
“Kama maisha tumejaliwa,kama vipaji tumeshapewa,kwanini leo tuogope?Wanafiki tuwashangae,Wanachekesha”
Si maneno yangu bali maneno kutoka kwa vijana wa TMK Majita.Yamo katika wimbo wao walioutoa hivi karibuni unaokwenda kwa jina la Wanachekesha.Hii ni production kutoka Sound Crafters Studio chini ya Producer Enrico na Muba Touch.Burudika.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Miongoni mwa mambo ambayo nayapenda hapa BC ni pamoja na kupata nafasi ya kuwatambulisha wasanii wapya au wanaochipukia.Naamini katika kuwapa vijana nafasi ya kusikika.Naamini katika kuwezeshana kwa njia yeyote ile halali na inayowezekana.
Hivi karibuni nilipata nafasi ya kukutana na vijana wanaokwenda kwa jina la Sababisha Empire. Makazi ya vijana hao ni Tegeta mitaa ya Chanika/Namanga jijini Dar-es-salaam.Pichani ni vijana hao;BQ (mwenye rasta), Kimo (mwenye lowcut), na Zungu (aliyesuka).
“Bro,tuna nyimbo yetu ambayo tungependa uisikilize na kama vipi warushie wasomaji wako” Waliniambia vijana hao kwa kujiamini kwamba kazi yao si lelemama.
“Sisi tuna uwezo wa kufanya miziki ya R&B(Zungu), ku rap (Kimo), na kuimba reggae na dancehall (BQ). Na kama kikundi, wote pamoja tuna uwezo wa kuimba nyimbo za asili” alieleza Kimo akijifuta jasho kwenye paji la uso lililotokana na kijua kikali kilichokuwa kinawaka.
Well,niliwaahidi kwamba nitauweka wimbo wao hapa ili wasomaji na mashabiki wa muziki wapate kuusikia.Wimbo unaitwa Bongo Fleva Time(Friday Nite). Umetengenezwa na Producer Tudd Thomas kutoka pale Ngoma Records.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Miaka kama miwili hivi iliyopita,wasanii wachache sana walikuwa wameshtukia kitu kinachoitwa ‘blogs”.Leo hii mambo ni tofauti.Badala ya kujiuliza msanii gani ana blog,tunajiuliza nani hana!Maendeleo.
Lakini wapo ambao walikuwa na blog tangu enzi hizo au kwa maneno mafupi,walizishtukia tangu hapo mwanzo.Miongoni mwa wasanii hao ni Ilunga Khalifa au maarufu kama CPwaa(pichani).Siku hizi anaitwa King of BongoCrunk.Hii hata kwangu ni mpya.Nimepitwa kidogo kuhusu “bongocrunk”.Ntamtafuta Cpwaa anijulishe zaidi. Enzi hizo CPwaa ambaye tunaweza kusema alikuwa msanii wa kwanza wa muziki wa kizazi kipya kuwa na blog,alikuwa akiblog kwa kutumia camera ya kwenye simu yake ya mkononi tu.Ilikuwa ni kitu kipya na nakumbuka tuliandika kuhusu wasanii na tekinolojia.
Sasa Cpwaa bado anaendeleza kusambaza ujumbe na kazi zake kwa kutumia tekinolojia za kisasa.Hivi karibuni ameifanyia marekebisho na matengenezo tovuti yake rasmi.Mtembelee.

Unapoongelea wanamuziki wa muziki wa kizazi kipya ambao miziki yao na mashairi yao yametoa mchango mkubwa katika kuufanya muziki huo ukubalike na kupewa heshima na nafasi yake katika jamii,bila shaka huwezi kuthubutu kumweka pembeni Joseph Haule au kama anavyojulikana miongoni mwa washabiki na wadau wa muziki; Proffessor Jay,MC Shupavu,The Heavy Weight MC,Jay wa Mtulinga,Mti Mkavu,Jiizeh nk.
Hivi sasa Prof.Jay yupo nchini Marekani akiendelea na tour yake ndani ya taifa hilo ambalo hivi sasa linaongozwa na Barack Obama,Rais wa kwanza mweusi. BC ilipata nafasi ya kufanya naye mahojiano kuhusiana na ziara hiyo. Je unataka kujua atatua na kufanya shows katika miji na majimbo gani? Anasemaje kuhusu ambacho ameweza kukiona na kujifunza nchini humo mpaka hivi sasa? Kwa majibu ya maswali hayo na mengine,fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;
BC: Prof,asante kwa nafasi hii ya mahojiano mafupi.Mambo yanakwendaje?
PROF.JAY: Safi vipi mtu wangu?Na mimi nashukuru kwa kunipa nafasi hii adimu.
BC: Ni muda sasa umekuwa nchini Marekani kwa ajili ya American Tour yako kiasi kwamba mashabiki wako ambao hawajui uko wapi wamekuwa wakijiuliza maswali yasiyo na majibu ya haraka.Kupitia hapa BC unaweza kuwaeleza kwa sasa hapo Marekani makazi yako ni katika State au Jimbo gani?
PROF.JAY: Asante na naomba niseme samahani kwa wale ambao wamekuwa wakijiuliza kwamba nipo wapi na mambo kama hayo.Kwa sasa hapa nchini Marekani nipo Massachussets nikiwa nimeweka kambi na DJ wangu anayekwenda kwa jina la RICHMAKA.Na sababu ya kuweka kambi hapa ni ili kupata muda wa kutosha wa kufanya mazoezi kwa pamoja kama team ili shows ninazofanya ziwe katika kiwango cha hali ya juu na mashabiki wangu wapate thamani halisi ya pesa zao watakazotoa ili kuja kwenye shows.
BC: Ni kampuni gani inakusimamia katika hii tour yako hapo nchini Marekani?
PROF.JAY: Kampuni inayonisimamia inaitwa NGOME ENTERTAINMENT.Makao yake makuu yapo Dallas,Texas.Kampuni hii ipo chini ya CEO wake,Kitova Mungai.
BC: Ni miji gani ambako unatarajia kuwa na shows?
PROF JAY: Mpaka hivi sasa nimeshapiga show moja ambayo ilifanyikia pale Houston,Texas tarehe 4 Julai(siku ya kusheherekea Uhuru hapa nchini Marekani) Ratiba ya shows zinazofuatia ni kama ifuatavyo:
- Tarehe 31/8/2010 Washington,D.C
- Tarehe 7/8/2010 Boston,Massachusetts.
- Tarehe 13/8/2010 Dallas,Texas.
- Tarehe 19/8/2010 Kansas City,Missouri.
- Tarehe 20/8/2010 Witchita,Kansas.
- Tarehe 11/9/2010 Atlanta,Georgia.

Mpaka hivi sasa ratiba ndio hiyo. Lakini kuna shows zingine nyingi ambazo zinaweza kutokea kwa sababu Promoters kadhaa wameonyesha nia na kufanya majadiliano ya awali ingawa hatuja-confirm firm tarehe kamili za kufanya kazi. Pia naomba niweke wazi kwamba milango ipo wazi kwa promoters wengine ambao wanataka kubook shows.Wenye nia hiyo wanaweza kuwasiliana na Kitova kwa kutumia nambari ya simu +1 214 455 5082 au DJ Rich Maka kwa nambari +1 413 262 0400.Karibuni sana.
BC: Unawaambia nini mashabiki wako katika miji hiyo?Watarajie nini kutoka kwako?
PROF.JAY: Kama nilivyogusia hapo juu,mashabiki wategemee shows za kiwango cha juu kabisa ambayo hawajawahi kuiona kutoka kwa msanii yeyote kutoka kwenye ukanda wa Afrika Mashariki,kati na Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Ninachowaomba wajitokeze kwa wingi ili wasije wakayakosa yale niliyowaandalia.Pia nawaomba wapatapo habari hii wawaambie na wengine.
BC: Waswahili wanasema kutembea kwingi ni kuona mengi pia.Mpaka hivi sasa unaweza kusema umejifunza nini kutokana na ambacho umekiona nchini Marekani iwe ni kwa upande wa sanaa ya muziki au jamii kwa ujumla?
PROF.JAY: Kwanza kabisa nimejifunza professionalism. Huku watu wanaheshimu sana kazi zao. Muda wa kazi ni muda wa kazi. Pia muziki wa huku upo katika kiwango cha juu. Bila shaka na sisi tunahitaji marekebisho mengi sana ili nasi tuboreshe miziki yetu na kazi zetu za sanaa zifikie angalau robo tatu ya kiwango ambacho wenzetu wameshafikia.Nasema hivyo kwa sababu huku muziki ni kazi na ni ajira kubwa sana kwa vijana na hata wasio vijana.Inaheshimika kama kazi nyingine zingine zozote.

Kila anapofanya show,umati kumbi na viwanja huwa “vinatapika”.Hapo ilikuwa ndani ya CCM Kirumba-Mwanza.Can you do a count from this photo?
BC: Baada ya Tour yako nchini Marekani unatarajia kuelekea katika nchi nyingine kuendelea na tour au utarudi kwanza nyumbani kupumzika kidogo?
PROF.JAY: Baada ya kukamilisha hii tour,nitarudi nyumbani kwa mapumziko mafupi kisha nitaelekea Ulaya kwa tour nyingine.Mpaka sasa nimeshapata mwaliko kutoka nchi za Scandinavia(Sweden,Norway,Denmark na Finland).Pia nimepata mwaliko wa kwenda kutumbuiza nchini Uingereza. Nitakaporudi nyumbani ndio nitajua wapi pa kuanzia.Mashabiki na wadau watajulishwa kuhusu tour hizo kupitia vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo BongoCelebrity.
BC: Mbali na hiyo tour kuna shughuli nyingine unafanya huko Marekani?
PROF.JAY: Ni kweli kabisa.Mbali na tour pia narekodi miziki.Tumeshaongea na kampuni moja ya kutengeneza video ili tuweze kushoot video kadhaa huku huku.Pia nafanya mawasiliano na wanamuziki mbalimbali kutoka nchi nyingine duniani ili kubadlishana mawazo na pia kuangalia uwezekano wa kufanya kazi pamoja.
Mbali na yote hayo,kama unavyofahamu mimi ni Balozi wa MARALIA NO MORE.Wao pia wametumia nafasi hii kunialika New York yalipo makao yao makuu.Nitakuwa huko tarehe 28 na 29 July ili nikutane na staff wote kwa pamoja.Vyombo kadhaa vya habari vitakuwepo na hivyo bila shaka kutakuwa na media coverage.
BC: Kama Balozi wa Malaria No More,unaonaje kuhusiana na vita dhidi ya ugonjwa huo nchini kwetu? Utakuwa na ujumbe wowote maalumu utakapokutana na staff nzima ya Malaria No More?
PROF.JAY: Kwa kweli jitihada za kupambana na ugonjwa wa malaria zinakwenda vizuri.Kwa kutumia muziki,wananchi wengi wamepata nafasi ya kuelewa jinsi ugonjwa huo unavyoenea,mbinu za kupambana nao nk.
Nitakapokutana na staff wa Malaria No More,nitawaeleza zilipofikia jitihada zetu na jinsi tulivyofanikiwa kuwazindua watanzania kuhusiana na ugonjwa huu hatari ambao unaua mamilioni ya watanzania kila mwaka huku wengi wao wakiwa ni watoto chini ya miaka mitano(5) na akina mama wajawazito. Jitihada hizi zinaendelea kufanikiwa kutokana na mchango na support kubwa kutoka kwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.
BC: Je unatarajia kutoa albamu mpya mwaka huu? Kama sivyo,lini mashabiki wako watarajie album mpya?
PROF.JAY: Ni kweli,it’s about time.Hopefully ambo yote yakienda sawa mwakani mwanzoni nitatoa album mpya. Kwa hiyo mashabiki wangu vuteni subira kidogo. Kazi tumeshazi-record ila tunachozingatia ni lini muda muafaka wa kuzitoa.Nasubiri muongozo kutoka kwa Management yangu.
BC: Shukrani Prof.Tunakutakia kila la kheri katika American Tour yako.
PROF.JAY: Asanteni sana wakuu.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Angeris,akitoa burudani ya aina yake wakati wa Tamasha la kila mwaka la Fiesta.La mwaka huu limepewa jina la Fiesta Jipanguse. Hiyo ilikuwa Zenji wikiendi iliyopita.
Kwa picha chungu tele juu ya Tamasha hilo,Michuzi Jr,anakukaribisha uzicheki kwa kubonyeza hii link.

Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Aboubakar Shaaban Katwila ‘Q-Chiller‘, amevunja ukimya wake na kuweka bayana kwamba hana mpango wa kuimba Taarab kama ilivyokuwa imevumishwa kutokana na kimya chake.
Akiongea na safu ya Abby Cool & MC George ya Global Publishers,Q-Chief amesema yuko kimya kwa sababu kuna mambo yake anayaweka sawa na akikamilisha atawajulisha mashabiki wake.
Tusubiri tuone kwani kama unavyojua,subra huvuta kheri na angojeaye hupata!

Katika siku chache zijazo,nitafanya mahojiano na msanii wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul maarufu kama Diamond.
Je una swali au maswali ambayo ungependa niyajumuishe katika maswali yangu kwa msanii huyo ambaye mapema mwaka huu alibeba Tuzo 3 za Kilimanjaro (Kilimanjaro Music Awards).
Unaweza kutuma swali au maswali yako kupitia bongocelebrity at gmail dot com au info at bongocelebrity dot com. Asante.
Burudika kidogo na wimbo wake Kamwambie
Bila shaka mimi na wewe tunakubaliana kwamba miongoni mwa miradi ambayo imefanyika katika kuinua vipaji vya vijana nchini Tanzania katika miaka ya karibuni,miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na ile ya kuanzisha Tanzania House of Talent(THT).
Kama umewahi kuhudhuria shughuli fulani na vijana kutoka THT wakawa miongoni mwa watoa burudani,bila shaka utakubaliana nami katika kumpa pongezi Mkurugenzi wa THT,Bw.Ruge Muhataba ambaye pia ni Mkurugenzi wa PrimeTime Promotions na Clouds FM.
Lina(pichani) ni miongoni mwa vipaji vinavyokuzwa au kuendelezwa na THT.Hivi karibuni amekuja na kibao kinachoitwa Bora Nikimbie. Anasema amechoshwa na manyanyaso na vipigo na hivyo anaona bora atoke mkuku.Msikilize;
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
NB: Kiburudisho cha ziada: Pamoja na kuwa na kipaji cha usanii wa muziki,Lina ni shabiki wa soka.Lakini hivi majuzi alitoa kali ya mwaka alipoulizwa kitu kuhusu mashindano ya Kombe la Dunia yanayoendelea huko Afrika Kusini.Unajua aliulizwa nini na akajibu nini?Bonyeza hapa.
Hii ni Video ya nyimbo ya pili kutoka kwa Babu Sikare aka Albino Fulani baada ya single ya Barua kwa Mama. Ni moja ya nyimbo katika soundtrack ya movie inayoitwa Baby Powder ambayo pia ameshirikishwa kwenye uigizaji itakayotoka hivi karibuni. Video imetengenezwa na Karabani.
Albino Fulani ambae pia ni CEO wa Afrobino hivi karibuni aliongea kwene TedExDar kuelezea historia ya maisha yake na pia jinsi anavyotumia muziki kuonyesha jamii kuwa maalbino ni binadamu wa kawaida na wasitengwe kwenye jamii.


