MWANAMUZIKI wa kizazi kipya wa Bongo Fleva nchini Abasi Kisinza wiki iliyopita alihukumiwa kifungo cha miaka saba au faini ya sh 200,000 baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na madawa ya kulevya aina ya bangi mwaka jana.
Kwa mujibu wa habari iliyoandikwa na Kennedy Kisula na kuchapwa katika gazeti la Habari Leo, Hakimu wa mahakama ya wilaya Kilwa mheshimiwa Arcado Chuwa alitoa hukumu hiyo baada ya kukamilisha kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili, za utetezi na mashataka.
Alisema ili kuwa fundisho kwa wengine baada ya mahakama kumtia hatiani anamhukumu kifungo cha miaka saba au faini ya sh 200,000.
Awali mwendesha mashitaka Inspector wa jeshi la polisi, wilayani Kilwa, Thomas alisema mtuhumiwa alikutwa na madawa ya kulevya aina ya bangi gramu 20 mwaka jana mwezi wa Desemba wakati akiwa safarini kwenye kijiji cha Nangurukuru katika gari lake, wilayani Kilwa.
Hata hivyo 20 per cent alikwepa kifungo baada ya kulipa kiasi hicho cha fedha .
OUR TAKE: Kuna haja ya wasanii na watu wengine wote maarufu kutambua kwamba kuitwa “kioo cha jamii” sio mzaha.Wachukulie vyeo hivyo kama karama kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa hivyo waishi kama mifano mizuri kwa faida ya vizazi vya sasa na vya baadae.Kwa msanii kama 20 Percent ambaye sio tu anasifika kwa tungo nzuri na zenye ujumbe,pia anayo sifa nzuri ya kujitwalia Kili Awards nyingi kwa mkupuo kitu ambacho bila shaka kuna wasanii wengi wengine wanakitamani na hivyo kutaka kujifunza mengi kutoka kwake.Watch Out 20%.Pole.
BC iliwahi kufanya mahojiano na 20%.Unaweza kuyasoma hapa.
Mwishoni mwa wiki iliyopita alifanya uzinduzi rasmi wa nyimbo hii.Huyu sio mwingine bali ni Barnaba,msanii ambaye yupo ameketi na ametulia kabisa katika orodha ya waimbaji ambao naamini kabisa kwamba wanaweza kuimba katika steji yoyote duniani na kuamsha hisia za mashabiki.He can sing!
Wimbo aliozindua pale Club Billicanas unaitwa Gube Gube.Sijajua bado kwa hakika nini maana ya neno hili.Ntamtafuta Barnaba nizungumze naye kuhusu undani wa wimbo huu katika siku za usoni.Lakini kwa haraka haraka nilipochungulia Kamusi ya Kiswahili niliyonayo inasema Gube au aghalabu Magube ni Hila au Ujanja Ujanja…Unaweza kusema Fanya Magube ukamaanisha fanya ujanja ujanja.Anyway,usikilize wimbo huu hapa chini. Hii ni production ya Tudd Thomas na Mosse Kinanda.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Wakati huo huo tunayo furaha kumtambulisha Ally Nipeshe,huyu ni msanii mpya ambaye bila kwere anaonekana kuwa na kipaji kizuri cha kuimba.Hapa anakuja na wimbo wake unaokwenda kwa jina Ntalila.Hii pia ni production ya Tudd Thomas na Mosse Kinanda.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Hii hapa chini ni video mpya kutoka kwa Dayna akiwa amemshirikisha Barnaba katika wimbo Nivute Kwako.Video imetengenezwa na Adam Juma pale Visual Lab(NextLevel) huku audio ikiwa ni kutoka pale Burn Records kwa Sheddy Clever.
Naomba itazame kisha uniambie kama umeweza kupatambua hapo kwenye maporomoko au maji.One of the best from Adam Juma in my opinion.Loved it.

Mwanzoni alimsihi “Ridhiwani” aongee na mshua.Naamini wawili hao wahusika walishafanya mazungumzo na huenda matokeo tutayaona soon.Lakini wakati bado Ridhiwani akiwa anaongea na mshua,Izzo Bizness,anakuja tena na kitu Barua.Hii ni barua kwenda kwa wanasiasa na viongozi kwa ujumla.
Wimbo umetengenezwa pale Fishcrab Records chini ya Lamar.Usikilize
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Endapo tutasema Professor Jay amerudi tena au hata tuiweke kwa kimombo kwamba Professor Jay is back ili kuonyesha msisitizo,bila shaka tutakuwa tunakosea.Nasema hivyo kwa imani moja nyepesi kabisa; Professor Jay alikuwepo,yupo na hakuna ubishi kwamba ataendelea kuwepo.
Hii ni kutokana na jinsi ambavyo kwa muda mrefu Professor Jay(jina kamili Joseph Leonard Haule) amekuwa akifanya kama kupotea hivi kabla hajaibuka upya kama sio kivingine kabisa kama ambavyo amefanya katika wimbo ambao nina furaha kuutambulisha kwako hivi leo.
Wimbo unaitwa Kamili Gado,ambalo ni neno la kimtaa kidogo lenye kumaanisha kitu au mtu aliyeko kamili katika mengi. Huu ni wimbo wa pili rasmi kutoka katika album yake mpya inayokwenda kwa jina Jaysco ambayo kwa mujibu wake,maandalizi kabambe ya kuiweka uwanjani yanaendelea.
Katika wimbo huu ambao umetengenezwa pale MJ Records(Masaki jijini Dar-es-salaam),Professor Jay amemshirikisha Producer wa wimbo huo,Marco Chali. Usikilize wimbo KamiliGado kwa kubonyeza player hapo chini na kisha tembelea tovuti maalumu ya wimbo huu,www.kamiligado.com kwa ajili ya kudownload wimbo wenyewe,Instrumental na Acapella.Kumbuka tu kwamba hiyo yote ni kwa ajili ya Promotions tu na sio matumizi mengineyo.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Solo Thang,one of the legendary Bongo Fleva artists is getting ready to release his highly anticipated new album “” I AM TRAVELLAH Vol 1″ which if all goes well will be out in January 2012. So far, he has released about four tracks from that album. He is now releasing his 5th and last track from the same album titled UWEZO MIA MIA”
In this track he collaborates with Godzilah one of the super fast ladder climbing young MC in Bongoland.Listen
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
SONG TITLE: UWEZO MIA MIA
ARTISTS: Â SOLO THANG ft GODZILAH

Kutoka pande za Temeke,Wanaume TMK wanaingiza karata yao.Wimbo unaitwa “Kichwa Kinauma“. Umetengenezwa pale Masaki kwa MJ Records chini ya Producer Marco Chali(Doctor Chali).
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Sina uhakika unaisomea wapi habari hii lakini nahisi unaisomea ukiwa katika mitkasi yako ya kila siku iwe ni kazini au katika sehemu zinginezo za kutafutia riziki.Kwa ufupi unafanya kitu! Lakini je,umeshawahi kuketi chini na kujiuliza kwa undani kabisa kwamba kwanini unafanya unachokifanya? Nini kinakusukuma kufanya hivyo?Unapohisi kukata tamaa na kitu unachokifanya,kwanini unaendelea?
Maudhui kama hayo hapo juu ndio yaliyomo katika wimbo mpya wa Mike Tee(Mnyalu) ambao amemshirikisha Fareed Kubanda au ukipenda Fid Q. Wimbo unazungumzia zaidi sanaa ya muziki.Ni wangapi wanafanya muziki kwa sababu wanapenda au wengi wanafanya kwa “Sababu Ya Njaa”?Msikilize kwa makini Mike Tee hapa.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Photo Courtesy:Get Mziki

Takribani mwezi mmoja ujao,Tanganyika(Tanzania Bara) kutakuwa na shangwe na vifijo kusheherekea miaka 50 ya kujitawala wenyewe(unapojitawala unaweza kujisimamisha au kujiangusha). Kauli mbiu ambayo inaongoza maandalizi ya kuelekea kwenye kilele cha sherehe hizo za kujitawala ni Tumethubutu,Tumeweza na Tunasonga Mbele.
Kwa sababu ambazo bado nazitafutia mantiki, kauli mbiu hiyo ndiyo iliyonijia mara nilipomaliza kusikiliza wimbo mpya kutoka kwa MwanaFA(jina halisi Hamisi Mwinjuma) unaokwenda kwa jina Yalaiti. Ni lazima kwanza uthubutu kisha uweze, ujiwezeshe au uwezeshwe ndipo utakapokuwa na moyo wa kusonga mbele.
Katika wimbo huu MwanaFA amemshirikisha mwanadada Linah ambaye sio tu anaitendea haki vilivyo chorus ya wimbo huo bali anatukumbusha ipasavyo kuhusu mwimbaji maarufu wa taarab aliyewahi kutokea.Namzungumzia Sitti Binti Saad kutoka Visiwani Zanzibar.Linah amenifanya nijiulize mara mbili mbili kwamba kwanini binti huyu asiimbe pia muziki wa mwambao? I believe she can!
Baadaye nilimtafuta MwanaFA nikitaka kujua kwanini akaamua ku-sample muziki huu wa Sitti Binti Saad? FA akanijibu
Because I wanted to keep the good music alive na huo ni miongoni mwa nyimbo nzuri kabisa nilizokuwa nazisikia wakati nakua.
I couldn’t agree more MwanaFA.It Is a good music and I am glad you are keeping it alive! Kama nilivyosema hapo mwanzo,umethubutu,umeweza na lazima usonge mbele.Natumaini more stuff like this are on the way.
Wimbo huu umekuwa produced na Marco Chali pale MJ Records.Sikiliza Yalaiti
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.



Ukiwa nje ya mipaka ya Tanzania hususani katika nchi za Ulaya na Marekani ya Kaskazini ukazungumzia Hip Hop ya kutoka Afrika Mashariki,basi usishangae ukaulizwa kama unawajua X-Plastaz.Ni kundi linalojulikana sana nje ya nchi.Ndio utambulisho wa Hip Hop ya ukanda huu huko kunako “walami”.Staili wanayoitumia wanaiita Maasai Hip Hop.Hapo sasa.Utakumbuka mwaka jana msanii kutoka kundi hilo alikuwepo katika BET Awards Cypher sambasamba na KRS-One kitu ambacho kilizidisha mileage za kundi hilo kimataifa.
Hapa wanakuletea video mpya ya wimbo “Africa” ambao wamemshirikisha Fid Q na Bamba Nazar.


sending...


