Recent Articles
SHUHUDIA FAINALI YA KOMBE LA UEFA JUMAMOSI HII KUPITIA DStv

SHUHUDIA FAINALI YA KOMBE LA UEFA JUMAMOSI HII KUPITIA DStv

  Jumamosi imekaribia. Mashabiki wa soka duniani wanalo la kuzungumzia, kujadili na kisha siku ya siku kujumuika kwa pamoja kushuhudia mechi kali na ya aina yake. ...

Read More

“KAMA ZAMANI”-MwanaFA Feat. THE KILIMANJARO BAND, MANDOJO & DOMOKAYA (BrAnD NeW)

KAMA ZAMANI-MwanaFA Feat. THE KILIMANJARO BAND, MANDOJO & DOMOKAYA (BrAnD NeW)

Huu wimbo ulitoka rasmi wiki iliyopita. Kwa makusudi sikuuweka hewani. Nilikuwa na bado nina maana yangu. Ukiendelea kusoma bila shaka utanielewa. Kila kizazi kina tabia au ...

Read More

WASANII KUTOKA NIGERIA, KENYA NA AFRIKA KUSINI KUPAMBA UZINDUZI WA BIG BROTHER AFRICA-THE CHASE

WASANII KUTOKA NIGERIA, KENYA NA AFRIKA KUSINI KUPAMBA UZINDUZI WA BIG BROTHER AFRICA-THE CHASE

Wasanii mbalimbali kutoka Nigeria, Kenya na Afrika Kusini wanatarajiwa kupamba shughuli ya kuanza kwa msimu mpya wa show kabambe ya Big Brother Africa siku ya ...

Read More

“SHANNI NA JENNY”-ABBY SKILLS Feat.CHEGE

SHANNI NA JENNY-ABBY SKILLS Feat.CHEGE

Ni muda kidogo hatujasikia kitu kutoka kwa Abby Skills ambaye kwa watu wanaokumbuka enzi zile Bongo Fleva inaanza kushika kasi, mtamkumbuka vizuri. Huu hapa ni ...

Read More

BREAKING NEWS: PROFESSOR JAY AJIUNGA NA CHADEMA/ AKABIDHIWA KADI YA UANACHAMA DODOMA

BREAKING NEWS: PROFESSOR JAY AJIUNGA NA CHADEMA/ AKABIDHIWA KADI YA UANACHAMA DODOMA

Pichani Professor Jay akiwa na Kiboya,mdau mkubwa wa muziki nchini ambaye pia ni mwanachama wa CHADEMA. Picha kwa hisani ya Twitter ya Professor. Habari ambazo zinatambaa ...

Read More

BILLBOARD MUSIC AWARDS: JUSTIN BIEBER AZOMEWA/ MIGUEL APIGA MWELEKA

Yawezekana hukupata nafasi ya kuangalia baadhi ya mambo yaliyojiri jana wakati wa Billboard Music Awards ambazo zilitangazwa kutokea Las Vegas,Nevada-mji wa kila aina ya dhambi ...

Read More

KINACHOMPONZA PRODYUZA TUDD THOMAS NI UCHAWI AU KUSAHAU?

KINACHOMPONZA PRODYUZA TUDD THOMAS NI UCHAWI AU KUSAHAU?

Prodyuza Tudd Thomas. MASHABIKI wa mtayarishaji wa muziki (Producer), mwenye uwezo wa kipekee, aliyetayarisha wimbo wa Leka dutigite wa Kigoma All Stars na zingine nyingi, Tudd ...

Read More

“NASHINDWA KULALA”- BONFACE MATEZA

NASHINDWA KULALA- BONFACE MATEZA

Huu hapa ni wimbo mpya kutoka kwa msanii Bonface Mateza. MSANII   :  BONFACE MATEZA WIMBO   :  NASHINDWA KULALA STUDIO  :   JAIM RECORD PRODUCER  :  GEORGE   JAMES

Read More

YANGA YAICHAPA SIMBA 2-0/ MASHABIKI BARANI AFRIKA WAFURAHIA MECHI KUPITIA SuperSport EAST 9

YANGA YAICHAPA SIMBA 2-0/ MASHABIKI BARANI AFRIKA WAFURAHIA MECHI KUPITIA SuperSport EAST 9

Yanga wakifurahia mojawapo ya magoli kutoka katika mechi hiyo. Picha kwa hisani ya Bin Zubeiry Blog Timu ya soka ya Yanga, jioni hii imewadhihirishia mashabiki wao ...

Read More

PERONI JAZZ SUNDAYS @ VELISA’s

PERONI JAZZ SUNDAYS @ VELISA's

Jumapili hii Mei 19 kuanzia saa Kumi na Moja jioni hadi Saa Mbili usiku karibu uburudike na muziki laini wa Jazz ukiletwa kwako na Wakwetu ...

Read More

EVE JUU YA ALBUM YAKE MPYA, BOYFRIEND WAKE MPYA, DMX NK

EVE JUU YA ALBUM YAKE MPYA, BOYFRIEND WAKE MPYA, DMX NK

Takribani miaka 11 imepita tangu Eve alipotoa album yake ya mwisho. Habari njema ni kwamba sasa amerejea tena katika ulingo. Album yake ambayo imeshatoka inaitwa ...

Read More

RAIS KIKWETE AZINDUA KAMPENI YA LISHE

RAIS KIKWETE AZINDUA KAMPENI YA LISHE

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Mama Maria Nyerere, Naibu Waziri wa Afya Dr. Seif Rashid wakipozi na wakuu wa mikoa ...

Read More

“RIZIKI YANGU”- LINEX Feat.WYRE

RIZIKI YANGU- LINEX Feat.WYRE

Linex ft. Wyre - riziki yangu Hakuna ubishi kwamba Linex ni miongoni mwa wasanii wa Bongo Fleva wenye kipaji cha hali ya juu katika uimbaji ...

Read More



Thatcher

 

Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Margaret Thatcher, amefariki dunia. Taarifa kutoka kwa msemaji wake ambayo imesambazwa na kuripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari ulimwenguni, inasema kwamba Bi. Margaret Thatcher amefariki kutokana na ugonjwa wa kiharusi (stroke). Alikuwa na umri wa miaka 87.

Thatcher ambaye kutokana na uhodari na ushapavu wake uliomfanya awe mwanamke wa kwanza kushika wadhifa wa Waziri Mkuu nchini humo alijulikana miongoni mwa wengi kama “Iron Lady” jina ambalo alipachikwa na vyombo vya habari vya Urusi. Aliiongoza Uingereza kuanzia mwaka 1979 mpaka mwaka 1990 akiwa pia kiongozi wa chama cha Conservative chama ambacho alikiongoza tangu mwaka 1975 wakati huo kikiwa ni chama cha upinzani.

Bi.Margaret Thatcher alijiuzulu rasmi kutoka katika siasa na maisha ya utumishi wa umma mwaka 2002 baada ya kupatwa na ugonjwa wa kiharusi. Tangu hapo amekuwa akionekana kwa nadra hadharani na hata mwaka 2010 alishindwa kutokea katika sherehe maalumu ya siku ya kuzaliwa kwake aliyokuwa ameandaliwa na Waziri Mkuu wa sasa wa Uingereza, David Cameron. Mwishoni mwa mwaka jana alilazwa hospitali na kufanyiwa upasuaji wa kuondoa uvimbe katika kibofu cha mkojo.

Margaret Thatcher alizaliwa tarehe October, 1925 katika mji mdogo wa Grantham(mashariki ya Uingereza). Baba yake alikuwa ni mfanyabiashara wa bidhaa ndogo ndogo za majumbani na baadae Mayor wa Grantham. Alisoma masomo ya Kemia katika chuo kikuu maarufu cha Oxford. Baadae alisomea Sheria.

Mume wake alikuwa Denis Thatcher, ambaye kwa pamoja walikuwa na watoto mapacha, Mark na Carol waliozaliwa mwaka 1953. Mumewe alifariki Juni 2003.

Mazishi yake ya kitaifa yanatarajiwa kufanyikia St.Paul Cathedral London na baadae katika shughuli ya faragha ya kifamilia, atazikwa kwa mwili wake kuchomwa moto.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

 

Be Sociable, Share!

Ismail rage

Mkutano wa Dharura ulioitishwa na wanachama wa klabu ya Simba umeung’oa uongozi wa juu wa klabu hiyo unaoongozwa na Mwenyekiti Ismail Aden Rage aliyepo kwenye matibabu nchini India.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, maamuzi hayo yamefikiwa kwenye mkutano huo uliofanyika na kumalizika mchana huu kwenye ukumbi wa Starlight Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
Majukumu ya kuiongoza kwa muda klabu hiyo yamekabidhiwa kwa kamati maalum inayoongozwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Usajili, Zakaria Hanspope na Rahma Al Kharoos. Hanspope na Bi Rahma maarufu kama Malkia wa Nyuki wataiongoza Simba mpaka pale utakapofanyika uchaguzi mkuu wa kupata viongozi wapya wa klabu hiyo.
Be Sociable, Share!

TARATIBU ZA KIMAHAKAMA ZAMKWAMISHA KURUDI NYUMBANI LEO!

Mahakama Kuu ya Tanzania mchana huu imeweka wazi masharti ya dhamana ya msanii  wa filamu anayejulikana zaidi kwa jina la Lulu,. Lulu ambaye jina lake halisi ni Elizabeth Michael anakabiliwa na mashtaka ya kuua bila kukusudia ya msanii mwenzake(ambaye inasemekana walikuwa na mahusiano ya kimapenzi), Steven Charles Kanumba, kilichotokea April mwaka jana huko Sinza-Vatican jijini Dar-es-salaam.

Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichokuwepo mahakamani mchana huu, dhamana ya mwigizaji Lulu ipo wazi endapo tu atatimiza masharti aliyotengewa ambayo ni

  • Kuwasilisha au kukabidhi hati yake ya kusafiria(passport)
  • Kutosafiri nje ya Dar es salaam.
  • Kuripoti mahakamani kila siku ya kwanza ya kila mwezi
  • Kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja atamdhamini kwa shilingi milioni 20 za kitanzania.

Pamoja na kwamba familia ya Lulu walikuwa wameshajiandaa kukabiliana na kutimiza masharti hayo, Lulu amerudi rumande leo kutokana na kwamba  watumishi wawili wa serikali(Mahakama) ambao wanahusika na sehemu ya dhamana hiyo kwa upande wa sahihi za kimahakama, hawakuwepo Mahakamani hapo kutokana na kuwa safarini mkoani Pwani kikazi. Hata hivyo, kwa mujibu wa mawakili wanaomwakilisha Lulu, masharti yote ya dhamana wameshayatimiza na kinachosubiriwa ni huo uthibitisho na utaratibu wa kimahakama ili Lulu arejee nyumbani na kuendelea kukabiliana na kesi hiyo akiwa uraiani.

Kwa maana hiyo, uwezekano ni wazi kabisa kwamba Lulu ataachiwa rasmi kesho January 29, 2013.

 

Be Sociable, Share!
Kwa taarifa zilizopatikana na za uhakika kutoka kwenye vyanzo vyetu vya habari,vinaeleza kuwa yule msanii aliyekuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya kwa muda mrefu,Sadick Juma Kilowoko ama aliyetambulika sana katika tasnia ya Filamu hapa nchini kwa jina la kisanii Sajuki,ambaye hivi karibuni Serikali ilijitolea kubeba jukumu la kugharamia matibabu yake na hatimaye hivi karibuni kulazwa kwenye kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU) kwenye hospitali ya Taifa ya Muhimbili,amefariki Dunia mapema leo asubuhi.

Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahali pema peponi-Ameni.


Picha na habari hii ni kwa mujibu wa Father Kidevu Blog
Be Sociable, Share!

Habari ambazo zimetufikia hivi punde zinapasha kwamba muigizaji na mwanamuziki, Hussein Ramadhan Mkieti almaarufu kama Sharo Milionea,amefariki dunia kutokana na ajali ya gari iliyotokea mida ya saa mbili usiku katika eneo la Maguzoni Songa katikati ya Segera na  Muheza mkoani Tanga.

Habari za ajali hii na tukio hili la kusikitisha zimethibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Constantine Masawe. Kwa mujibu wa Kamanda huyo, gari aina ya Toyota Harrier lenye namba za usajili T478 BBR alilokuwa akiendesha marehemu kutokea Dar-es-salaaam kwenda Muheza lilipofika katika eneo hilo liliacha barabara na kupinduka na hivyo kusababisha mauti yake.Mwili wake umehifadhiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali Teule ya Muheza.

BC inaungana na wapenzi wote wa sanaa nchini Tanzania kutoa pole za dhati kwa ndugu,jamaa na marafiki wa Sharo Milionea.Pumzika kwa Amani.

Be Sociable, Share!

Mbunge wa Njombe wa muda mrefu  na mwanasiasa wa siku nyingi nchini, Mzee Jackson Myangila Makweta,amefariki  dunia jioni hii jijini Dar-es-salaam, kutokana na matatizo ya moyo  ambayo yalikuwa yakimsumbua.

Mbali ya kuwa miongoni mwa wabunge walioongoza majimbo yao kwa muda mrefu zaidi katika historia ya Tanzania, Jackson Makweta pia aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali katika serikalini ya Tanzania zikiwemo zile za uwaziri(wa wizara mbalimbali),

BC inapenda kuungana na watanzania wote katika kuomboleza msiba huu na kutoa pole nyingi kwa ndugu,jamaa na marafiki na hususani familia yake. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.Amen

 

Be Sociable, Share!

NBC’s Managing Director,Lawrence Mafuru

Be Sociable, Share!

Habari ambazo zimetambaa, zinasema kwamba mtanzania anayecheza katika ligi ya kikapu nchini Marekani,(NBA) Hasheem Thabeet, atajiunga na timu ya Oklahoma City Thunders kwa mkataba wa miaka miwili.

Kwa mujibu wa Oklahoman, Ingawa mkataba kamili haujawekwa wazi inasemekana kwamba Hasheem ataingia kwa mkataba wa kulipwa mshahara usiopungua $880,000 katika mwaka wa kwanza wa mkataba huo.

Oklahoma City Thunders au OKC kama wanavyofahamika miongoni mwa mashabiki wa mpira wa kikapu na ligi ya NBA, itakuwa ni timu ya nne kwa Hasheem Thabeet kuichezea tangu aliposaini na Memphis Grizzlies kufuatia kuwa wa pili katika NBA Draft mwaka 2009 mbele kwa nafasi moja kutoka kwa mchezaji mwingine anayechezea Thunder hivi sasa,James Harden.

Hata hivyo,Hasheem ameonekana kutokuwa na mwanzo mzuri sana ndani ya NBA tofauti na alipokuwa chuoni Connecticut ambapo aliwahi kuwa Defensive Player Of The Year. Katika michezo 135 ndani ya NBA, Hasheem ana kiwango cha point 2.2, rebound 2.7 na 0.9 blocked shots.

Kwa muda mrefu OKC walikuwa wakimtaka Hasheem na walisikitika mwaka 2009 alipochukuliwa na Memphis.

Ni mwanzo mwingine kwa Hasheem Thabeet na kwa jinsi OKC walivyo,basi huenda tukashuhudia msimu tofauti kabisa wa NBA na bila shaka msimu tofauti kwa Hasheem Thabeet.

Be Sociable, Share!

Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe wakibeba jeneza la marehemu Bob Makani.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete,makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal pamoja na Mama Salma Kikwete leo waliungana na viongozi wa CHADEMA na viongozi wengine wa kitaifa kutoa heshima zao za mwisho kwa mmoja wa waasisi wa CHADEMA marehemu Bob Makani ambayepia aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini ikiwemo ya Naibu Gavana wa Benki kuu katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.(picha zote na Freddy Maro)

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpa pole Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Wilbroad Slaa katika viwanja vya Karimjee kufuatia msiba wa muasisi wa Chama hicho Bob Makani

Be Sociable, Share!

Taarifa ambazo zimetufikia muda si mrefu uliopita zinapasha kwamba Mwanasiasa mkongwe nchini,mwanasheria na miongoni mwa waasisi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA), Bob Makani, amefariki jioni hii katika hospitali ya Aga Khan jijini Dar-es-salaam.Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi.

Tutaendelea kuwaleteeni habari zaidi kadiri tunavyozidi kuzipata.

Be Sociable, Share!

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page