
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Song;Bye Bye
Download Link; http://www.hulkshare.
Prodyuza Tudd Thomas.
MASHABIKI wa mtayarishaji wa muziki (Producer), mwenye uwezo wa kipekee, aliyetayarisha wimbo wa Leka dutigite wa Kigoma All Stars na zingine nyingi, Tudd Thomas, wamekuwa wakiulizana maswali mengi wao kwa wao pasipo kupata majibu.
Safari ya Tudd Thomas katika muziki, ilianzia mkoani Iringa akiwa Iringa Records aliporekodi wimbo wa mwanamuziki Marlaw unaoitwa Bembeleza. Wimbo huo ulipata tuzo ya wimbo bora wa mwaka kutoka Kilimanjaro Tanzania Music Awards mwaka 2008 na pia kumfanya Marlaw apate tuzo ya msanii bora wa kiume kupitia tuzo hizo. Baadae alihamia jijini Dar es Salaam na ndipo alipoonesha uwezo wake zaidi kwa kusuka nyimbo zilizotikisa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla.
Hakuna asiyeufahamu wimbo wa Pii Pii (Missing my baby) wa Marlaw ambao aliutengeneza yeye kupitia Studio ya JML. Wimbo huo ulipata tuzo nyingi ikiwa ni pamoja na tuzo ya Nzumari nchini Kenya mwaka 2009 mbapo uliingia kwenye kipengere cha wimbo bora wa Afrika Mashariki, kumfanya Marlaw aingie kwenye kipengele cha msanii bora wa Afrika Mashariki na kunyakua tuzo hiyo. Baada ya hapo wimbo huo ulipata tuzo ya Kilimanjaro nchini Tanzania kama wimbo bora wa mwaka wa Afro pop mwaka 2010, tuzo ya Chaguo la Teneez Music nchini Kenya kama wimbo ulioongoza kwa kuchukuliwa kwa njia ya mtandao Afrika Mashariki “The most downloaded East African song” mwaka 2010, pamoja na tuzo ya Nigeria Sound City Video Music kama wimbo bora wa Afrika Mashariki mwaka 2010.
Aliendelea kutayarisha nyimbo ambazo zilipata umaarufu mkubwa na kuingia kwenye vipengele mbalimbali vya tuzo za muziki za Kilimanjaro. Mwaka 2012, nyimbo tatu zilizotokana na mikono yake zilipata nafasi ya kushiriki tuzo hizo. Nyimbo hizo ni Liz One wa Izzo Business ambao uliingia kwenye vipengele viwili ambavyo ni wimbo bora wa mwaka na wimbo bora wa Hip hop na pia kusababisha msanii huyo aingie kwenye kipengele cha msanii bora wa Hip hop. Milele daima wa Barnaba na Kizunguzungu wa Rachel, ambapo zote ziliingia kipengele cha wimbo bora wa Zouk/Rhumba pia ni nyimbo alizotengeneza mtayarishaji huyo.

Wapo wasanii ambao bado hawana majina makubwa.Hawa wanahitaji support yako hususani kwa wale ambao wana kipaji.Mfano mzuri ni huyu.Anaitwa Baridi.Single yake ambayo aliitoa mwaka jana inaitwa Nipe Nafasi.Tafadhali mpe support yako ili kumuwezesha kuendelea kufanya kile anachokifanya.Nunua kupitia iTunes,Amazon, Spotify ,Google Play,eMusic,etc.
Upo msemo wa Kiswahili unaosema “Mafahali wawili wapiganapo,ziumiazo ni nyasi”. Kama kuna ukweli wowote kwenye msemo huo, basi ni dhahiri kwamba wanapombana Yanga na Simba, nyasi lazima ziumie kwani wakongwe hao wa soka nchini Tanzania naweza kuwafananisha na mafahali.
Jumamosi hii, tarehe 18 Mei,2013,Yanga (watoto wa Jangwani) ikiwa tayari imeshanyakua ubingwa wa msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania inayodhaminiwa na Vodacom 2012/2013, inateremka dimbani kumenyana na watani wao wa jadi Simba (watoto wa Msimbazi) pale katika Uwanja wa Taifa jijini Dar-es-salaam.
Yapo mambo kadhaa yanayolifanya pambano la Jumamosi kuwa gumzo. Kwanza Yanga tayari ni mabingwa na hivyo kufungwa na Simba katika mpambano huu kitakuwa ni kitu ambacho kimeingiza “shombo” kwenye raha ya ubingwa. Lakini pia Yanga bado wana kisasi moyoni. Utakumbuka Yanga katika siku za hivi karibuni walifungwa 5-0 na Simba. Naam, bado wana donge.
Lingine kubwa linaloufanya mpambano huu kuwa tofauti ni kwamba huko mitaani na hata majumbani,badala ya kusikiliza matangazo ya mpambano huu kupitia radioni (kama tulivyokuwa tukifanya enzi zile za watangazaji kama vile Ahmed Jongo,Charles Hillary nk) safari hii Ulimwengu wa Mabingwa (SuperSport) ndani ya DStv wataonyesha mpambano huo Live kupitia channel ya SuperSport 9 East (Namba 219) kuanzia Saa 10 Jioni.
Kazi kwako mpenzi wa soka. Kazi kwako shabiki wa Yanga au Simba. Una kila sababu ya kulipia akaunti yako ya DStv na kuhakikisha kwamba unaona SuperSport 9 East (channel 219) ili ushuhudie “Live” kila kitakachokuwa kinaendelea kutoka Uwanja wa Taifa. Je ni Yanga au Simba?

“…Mwaka huu (2013), natimia miaka 13 tangu nianze kazi ya muziki. Namshukuru Mungu tuko pamoja na pia, nashukuru umma wa Tanzania kwa kuendelea kuni- support (unga mkono) muziki wa Tanzania na kunipa nguvu mimi kama msanii,”
“Nashukuru vyombo vyote vya habari vinavyoshiriki kikamilifu kukuza na kulinda sanaa ya Tanzania bila kujali maslahi binafsi. Tumeandaa sherehe kubwa na nzuri ya miaka 13 ya LADY JAYDEE, katika muziki.”
Sherehe ya miaka 13 ya Lady JayDee katika muziki itashirikisha show ya nyimbo zote bora za JayDee kwa kuwashirikisha pia baadhi ya wasanii wa nchini. Sherehe hizo zitafanyika Ijumaa tarehe 31 May 2013.
Sijui kama nikisema baada ya kimya cha muda fulani Nakaaya is back nitakuwa nimepatia au nimekosea. Kumbukumbu za haraka hazinijii kwamba mara ya mwisho aliachia single lini. Yote tisa. Kumi ni kwamba Nakaaya yupo tena hewani. Wimbo wake mpya huu hapa. Unaitwa Utu Uzima Dawa.
Yes ukikua na kuelewa kwamba wewe sasa ni mtu mzima na hivyo inabidi ufanye mambo yako kwa kutumia akili zako mwenyewe na sio kwa kutegemea “maisha ya kutengenezewa” basi hiyo ndio dawa. Ndio maisha na ndio utu uzima.
Hii ni production kutoka Fishcrab na Mandugu Digital.Usikilize.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Unapodhani kwamba Diamond amepunguza kasi. Unapodhani kwamba sasa mzigo wa kupamba kurasa za mbele za magazeti ya udaku umemuelemea. Unapodhani kwamba huenda sasa sifa za kupendwa na mashabiki na kinadada zimempanda kichwani.Unapodhani kwamba sasa theme za mapenzi zimemwishia, anasema Hapana.
Huu hapa ni wimbo mpya kutoka kwa Diamond. Unaitwa Mapenzi Basi. Ni kutoka AM Records chini ya Maneke. Listen
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Msanii Chege (ukipenda Chege wa Chigunda) anatarajiwa kuzindua rasmi video yake ya wimbo Uswazi Take Away hapo kesho kuanzia mitandaoni na keshokutwa katika vituo mbalimbali vya Televisheni. Wimbo wa Uswazi Take Away ambao unafanya vizuri producer wake ni Tuddy Thomas (huyu ndio mpikaji wa nyimbo nyingi za vijana pale THT) na Bass imepigwa na Dunga. Video imefanywa na Adam Juma kutoka Visual Labs( Next Level)…stay tuned..
The track is is called SHUT UP and it’s about playa haters who can’t treat their women good and when somebody steps up and treat their ladies like queens, they start hating. Love is divine, and when you have somebody with whom you can hold that, don’t let them down cause when they’re gone, it’s just you, yourself and misery. Sit back and enjoy good sounds from the factory of Hip hop and make sure you treat your lady with love and respect……PEACE!!!!!!!!!!!!!!
Ujumbe toka releasing studio, sio maneno yangu.Sikiliza Hapa
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Mara nyingi ukisikia nyimbo kutoka Arusha huwa inakuwa ni Hip Hop.Vijana kutoka katika jiji hilo lililopo kaskazini mwa Tanzania na ambalo mara nyingi limekuwa likiitwa “Geneva Of Africa”, wamekuwa wakiegemea zaidi katika upande wa Hip Hop.
Well…that is about to change kwani kuna kundi ambalo lenyewe limeanza kwa RnB. Linaitwa Dady Dadyz na linaundwa na Solomon Mwaigwisya {rapper wa kikundi}, Atufigwege Mwailunga {singer wa kundi} na Emanuel Mghase { huyu anadeal na vitu vingine vya kundi kama kusambaza nyimbo na kusimamia stage perfomance}
Huu hapa ni wimbo wao unakwenda kwa jina Mzuri ambao umerekodiwa pale FishCrab Studios chini ya Producer,Lamar. Usikilize hapa chini
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.




sending...



















