MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Kama mimi na wewe tunashabihiana kifikra, basi ulikuwa unatamani siku hii ifike.Siku ambayo angalau kwa muda mfupi,utapumzika kusikia kwamba kila production mpya ya Bongo Fleva, inakuwa imeelemea kwenye hadithi na visa kuhusu mapenzi.Sio kusema kwamba hadithi na visa vya mapenzi havina nafasi yake katika sanaa,La.Ni kuonyesha tu kwamba jamii ni pana na kuna mengi zaidi ambayo sanaa inaweza kuyagusia.

Aliyesikia kilio hicho ni Heavy-weight MC,Prof.Jay.Wimbo unaitwa Msilie akiwa amemshirikisha mkali mwingine wa hip hop nchini Tanzania,Chid Benz.Wimbo umetengenezwa na producer ambaye amekuja juu kwa sana.Ni Lamar kutoka Fish Crab Records.

Mambo kadhaa yamenifanya niusikilize wimbo huu siku nzima.Kikubwa ni ujumbe uliomo ndani yake.Kama ambavyo ungetarajia kutoka kwa Prof.kwa kina anaangalia yale yanayojiri katika jamii.Anatoa hoja,anafafanua,anaelekeza.Msikilize;

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Hey what’s up everybody! I thought the Producers in Tanzania have improved a lot but I guess I was wrong! Two and Half years ago, I made a beat and named it Block Running, I sold it to one of the Label called Koch Entertainment of New York with an agreement that wherever this beat goes my name gotta  be there as a beat maker of this beat. Two days ago I was shocked when one of my friends from Tanzania sent me a song with the same beat I made 2 and half yrs ago! And I didn’t hear my name on the track. All I heard is Marco Chali.

So I called Koch Entertainment to ask what’s going on. Koch Entertainment management were so surprised to hear the news. So they told me to send the song to them and I did, they asked me if I ever sent the beat to MJ Records of Dar-es-salaam, Tanzania. I told them I never did but had put the beat on iTunes so people can buy and use it for promotions and not for any other type of business. But MJ Records used the beat without permission from Koch Entertainment and also they didn’t follow the agreement we signed that wherever this beat goes my name gotta be there as a beat maker!

I don’t have any rights of complaining this issue to MJ Records that why my name wasn’t on the song as a beat maker. All I will do is to take Koch Entertainment to court and they will deal with MJ Records. The only thing I am gonna deal with is if MJ Records bought this beat from iTunes. If they did why they used it for the business!!?

I put the song which Producer Marco Chali of MJ Records produced last year and my beat I made 2 and half years ago so you guys can compare and tell me if this beat is the same or not the same.Thanks.

Stiggo Ibrahim,

S&S Records-NY

Quick Rocka Ft QJ-Bullet

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

S&S Records & Koch Ent.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

BC is trying to reach MJ Records for their comment.Stay Tuned.

Za mwizi arobaini. Bila shaka ushausikia msemo huo.Sina uhakika sana na idadi ya siku (40) lakini nina uhakika kwamba msemo huo humaanisha kwamba uovu una kikomo.Ipo siku utakamatwa.Inaweza kuwa sio ndani ya siku arobaini(40) lakini ipo siku tu!

Lakini inakuwaje siku ukimfumania mtu ambaye haibi kunde na choroko zako shambani bali anaiba penzi au mpenzi wako? Utapigana au utamuacha aende zake.Yaani namaanisha utayamaliza kistaarabu tu au mtaani patakuwa hapatoshi kwa vurumai au songombingo utakalolianzisha?

Sijui utafanyaje…lakini Hussein Machozi(pichani) anasimulia jinsi siku za mwizi(wa penzi,mali au hali) zinavyofikia ukingoni.Baada ya siku arobaini mambo yanawekwa hadharani.Tyler Perry,yule muongoza sinema maarufu kutoka nchini Marekani,anao mchezo(play) unaoitwa What is Done In The Dark…Must Come Out to Light. Labda Hussein Machozi anamaanisha hivyo pia.

Wimbo unaitwa Za Mwizi 40,unapatikana katika album yake ya Kwa Ajili Yako. Hii ni single yake ya 3 kutoka katika album hiyo, single mbili zilizotangulia ni pamoja na Kwa Ajili Yako na Utaipenda.Usikilize hapo chini;

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

SONG’S DETAILS

Track Name: ZA MWIZI 40

Singer: HUSSEIN MACHOZI

Produced by: AMBA & KID BWOY

Written by: HUSSEIN MACHOZI

Song Arranged by: HUSSEIN MACHOZI & KID BWOY

Mixed by: KID BWOY

Studio: TETEMESHA RECORDZ / AB RECORDS


Kila ifikapo tarehe 13 August, yeye hukumbuka na kusheherekea siku yake ya kuzaliwa. Alipozaliwa pale jijini Mwanza,kaskazini mwa Tanzania wazazi wake walimpa jina la Fareed. Leo hii kwa wengi anatambulika kama Fid Q.

Kama ambavyo umeshasikia,leo hii,tarehe 25 Feb 2010, album yake inayokwenda kwa jina Propaganda inaingia mtaani.Kwa hiyo leo ukizunguka mitaani,usishangae kukutana na mtu kabeba CD mpya ya Fid Q au ukasikia sauti yake kwenye gari,magari,usafiri wa umma.Jambo moja muhimu unaloweza kufanya ni kujipatia nakala yako halisi.Hakuna njia nzuri zaidi ya kuunga mkono juhudi za wasanii zaidi ya hiyo!

Hivi karibuni nilipata nafasi ya kuzungumza machache na Fid Q kuhusu ujio wa albamu hii ya Propaganda,muungano wa wasanii wa bongo fleva na pia suala zima la nyimbo nyingi za bongo fleva kuwa na maudhui ya mapenzi zaidi ya kitu kingine chochote.Kwanini ameiita album yake Propaganda? Anamaanisha nini? Je unajua Fid Q ana mtazamo gani kuhusu muungano wa wasanii?Je anasemaje kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika maendeleo au kifo cha muziki wa kizazi kipya? Fuatana nami katika mahojiano yafuatayo;

BC: Kwanza hongera kwa album mpya.Labda kwa ujumla tu,album hii umeitengenezea katika studio zipi,itakuwa na nyimbo ngapi na umewashirikisha wasanii gani wengine?

Fid Q: Asante sana kaka.Album hii nimeifanya katika studio 3 tofauti.Nimefanya kwa MJ Records, Tongwe Records na kwa Lamar.Nimewashirikisha wasanii kama AY, NCHA KALI, MZEE ZORRO, JUMA NATURE,QJ, NYLON WA MANZESE CREW, BI KIDUDE na wengine kibao bila kuwasahau MATONYA na MZUNGU KICHAA.

BC: Kwanini umeiita Propaganda?Kuna ujumbe wowote maalumu kutokana na jina la album? (more…)



Email for bands
Quantcast

Hii ni kutoka kwa DJ Fetty.Wimbo ninaoupenda zaidi ni wa kwanza hapo kutoka kwa kijana anayeitwa Roma.Wimbo ni Mr.President.Mtembelee DJ Fetty kwa kubonyeza hapa.

Ukumbi umefurika,watu wananyanyua na kushusha mikono.Wanaimba na kucheza.Wengi wamevalia nguo nyekundu.Siku ya siku ni Valentine’s Day au Siku ya Wapendanao.Kila mtu na wake. Ni siku ya kumuonyesha mwenzako kwamba unampenda.Kama alikuwa haamini huenda leo akaamini.Mwanamuziki aliyepo jukwaani ni TID.Mahali ni Platinum Club,Mikocheni.

Ghafla muziki unazimwa.TID anasema kuna kitu anataka sema.Waungwana wakatulia ili kumsikiliza.Anaanza kuongea “Wapendwa, muda umewadia,nataka kuuaga ukapela.Nataka kuoa”. Watu kimyaa, minong’ono ya chini kwa chini,shauku ya kutaka kujua na kusikiliza zaidi!

Kwa mujibu wa John Bukuku wa Full Shangwe,kilichofuata ni TID kumtambulisha mchumba.Anaitwa Kinana(pichani). TID akapiga goti na kutamka “Will You Marry Me”? Binti akakubali.TID and Kinana are engaged.

Hongera TID.Maisha ni hatua.Tunasubiri harusi.Kila la kheri.

Picha na chanzo cha habari:Full Shangwe.

Siku chache zijazo,tarehe 25 mwezi huu kwa uhakika,Fareed Kubanda au maarufu kama Fid Q anatarajia kuiweka sokoni albamu yake mpya ambayo ameipa jina Propaganda.

Hivi karibuni ametoa single moja kama utambulisho wa kitachokuwepo katika album hiyo. Single inakwenda kwa jina la Danger akiwa amemshirikisha J-Bryant.Usikilize kwa kubonyeza player hapo chini.Usikilize kwa makini.Sikiliza midundo,hisia,ujumbe uliomo na kisha sema usikike.Kwa ufupi ninachoweza kusema ni kwamba kuna utofauti…

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Hamis Ramadhan,maarufu kama H-Baba(pichani) yawezekana sio jina geni kwako.Huyu ni miongoni mwa wanamuzuki waliojikita katika mtindo ujulikanao kama TAKEU(Mr.Nice ndiye anasemekana kuwa mwanzilishi wake).

Ambacho unaweza kuwa hukijui ni kuhusu “imani” aliyonayo. Hivi karibuni H-Baba alinukuliwa na chombo kimoja cha habari akisema kwamba amelogwa na mmoja wa wasanii wenzake kitu ambacho anadai ndicho kilichosababisha mambo yake kwenda ‘kombo” katika siku za karibuni.

Kwa masikitiko na upole,H-Baba amenukuliwa akisema “Unajuwa mtu ataniona mimi kama naongopa lakini ukweli ni kuwa nilichezewa ila nilikuwa sijui nimekuja kugundua baada ya kupita pita kwenye tiba.Nilianza kujihisi hivyo mara baada ya kugombana na watu wengi sana nikiwa sijielewi”

H Baba anakiri kwamba hivi sasa ameshapona kutoka katika matatizo yaliyokuwa yakimsumbua baada ya kupata tiba toka kwa wataalamu wa miti shamba.

Bila kumtaja wazi huyo ‘mchawi” wake H-Baba alizidi kusema ” Unajuwa ni ukweli kabisa waswahili hawakukosea walivyosema kikulacho kinguoni mwako, kwani yote hayo yalikuwa yakifanywa na mtu wa karibu kabisa tena rafiki yangu mkubwa”.

Mfano mmojawapo wa matatizo yake,anasema “Matatizo mengi yalitokana na Irene(Uwoya), unajua watu wengi hawakupenda niwe na Irene, kwahiyo ili kunikomoa ikabidi waniroge, mimi na Irene tukawa hatuelewani, tunagombana mpaka tukaachana,”

Je,unaamini kwamba ni kweli yawezekana H-Baba amefanyiwa anachodai kufanyiwa au hii ni “publicity stunt”?

Mara ya kwanza tuliwasiliana mwaka jana.Akanieleza mipango yake,ndoto zake na mikakati aliyonayo katika kutimiza ndoto zake.Kama ilivyokuwa kwa mamilioni ya watu ulimwenguni, Babu Sinare ambaye kisanii anajulikana kwa jina la Albino Fulani, alikerwa na kuhuzunishwa na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi(albino) kwa imani za kishirikina. Kwake yeye,ilikuwa ni kama vile wametonesha kidonda ambacho alidhani kilishapona kwani Babu Sikare ni albino pia.

Miongoni mwa mipango yake ilikuwa ni pamoja na kuanzisha NGO yake ambayo italenga kusaidia albino wengine.Kupitia muziki wake,aliahidi kwamba atazidi kukemea mauaji ya albino.Hakuwa anatania.Alianzisha shirika lisilo la kiserikali na kuliita Afro-Bino. Matunda ya shirika hilo yameanza kuonekana.

Pichani juu ni Babu Sikare(kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa Huduma za Hospitali kutoka Wizara ya Afya, Dr. Magreth Mhando (kulia) karatasi yenye maelekezo ya msaada wa mafuta ya kuzuia ngozi isiharibike na jua kwa ajili ya watoto wenye ulemavu wa ngozi Tanzania (Albino) yenye thamani ya dolla 1,500. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ustawi wa Jamii Bi. Magreth Njimba.

Kutoka moyoni,naomba kumpongeza Babu Sinare na shirika zima la Afro-Bino.We salute you and we support you.

Albino Fulani anatamba pia na wimbo wake Barua Kwa Mama.Bonyeza hapa kuusikia.


Kama wewe ni mtizamaji au mpenzi wa sinema za kutoka nchini Nigeria,bila shaka umewahi kuwaona wachekeshaji wawili wajulikanao kama Aki na Ukwa.Wanasemekana ndio waigizaji wafupi kuliko wote nchini humo.Habari nzuri,kama wewe unapendezwa na vichekesho vya Aki na Ukwa ni kwamba wapo njiani kuja jijini Dar-es-salaam.

Kwa mujibu wa Gazeti la Mwanaspoti,wachekeshaji hao wanatarajiwa kufanya vitu vyao katika tamasha la watoto yatima, na wale wanaoishi katika mazingira magumu Februari 14 mwaka huu. Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika siku ya wapendanao(Valentine’s Day) katika viwanja vya TTCL, Kijitonyama jijini Dar es salaam.

Aki na Ukwa watakuwa nchini kwa lengo wa kucheza na kufurahi na watoto mbalimbali wahishio kwenye mazingira magumu.

Watasindikizwa na wasanii wengine wa ndani wanaotarajiwa kutumbuiza katika tamasha hilo ni pamoja na Ze Comedy, Q-Chief, Mr.Nice, Rose Mhando na Mrisho Mpoto. Kwa habari zaidi bonyeza hapa.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page