Mwezi wa kwanza wa mwaka 2012 ndio huo tumeshaanza kuuwashia indicator.Upo ukingoni.Wakati tukihesabu siku,kwenye tasnia ya Bongo Fleva,tayari wasanii kadhaa wameshaanza kuachia ngoma zao ambazo itakapofika Desemba mwaka huu,zitakamilisha orodha ya nyimbo zilizotoka mwaka huu.
Leo hapa tunao wimbo kutoka kwa Godzilla,msanii ambaye ana style inafanana kwa karibu na 50….(malizia mwenyewe kama unaafikiana nami).Hapa anakuja na wimbo Milele akiwa amemshirikisha Ally Kiba.Milele ni production nyingine kutoka pale MJ Records chini ya Marco Chali(wenyewe siku hizi wanapenda kumuita Dr.Chali). Usikilize hapo chini
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Wiki hii kwa kiasi kikubwa imekuwa ya taratibu sana hapa kwetu BC.Mambo yamekuwa mengi kupita kiasi.Bahati nzuri ni kwamba mambo yote hayo ni katika kuhakikisha kwamba wewe msomaji wa BC unakuwa unapata kitu ambacho kimefanyiwa kazi na sio copy and paste.Sisi tunaamini kwenye kupashana habari,kuelimishana,kuburudishana,kukosoana,kurekebishana bila kusahau kuheshimiana.
Sasa leo tunaanzisha kitu kipya.Kitakuwa kinaitwa BC Flashback Friday.Kila Ijumaa tutakuwa tunaweka burudani ya muziki ya kutoka miaka ya nyuma kidogo.Itakuwa ni aidha 70s,80s,90s,20S.Nia ya hiki kipengele ni kuburudisha na kukumbushana ilivyokuwa enzi hizo.
Leo tunao kina dada wa kundi lilikuwa linaitwa Zhane.Hawa walitamba sana miaka ya 90s.Hapa wanacho kibao Hey Mr.DJ ambacho ni maalumu kabisa kwa Ijumaa.Je,kibao hiki kinakukumbusha wapi?Ilikuwaje enzi hizo.Usiwe mchoyo wa “soga”.Tuambie.Tunakusikiliza.Ijumaa Njema

Bendi maarufu ya muziki wa dansi ya Twanga Pepeta, inatarajiwa kuzindua album yake inayokwenda kwa jina Dunia Daraja mnamo tarehe 6 Novemba(next weekend) pale katika viwanja vya Leaders-Kinondoni jijini Dar-es-salaam.Pichani ni baadhi ya watunzi wa nyimbo zilizomo katika album hiyo.Unaweza kuwatambua kwa majina baadhi ya unaowaona hapo? Na labda kwa kuongezea tu,ni kibao gani cha Twanga Pepeta ambacho unakikumbuka au kukipenda zaidi?Binafsi nakizimia sana Kisa Cha Mpemba.



Ukiwa nje ya mipaka ya Tanzania hususani katika nchi za Ulaya na Marekani ya Kaskazini ukazungumzia Hip Hop ya kutoka Afrika Mashariki,basi usishangae ukaulizwa kama unawajua X-Plastaz.Ni kundi linalojulikana sana nje ya nchi.Ndio utambulisho wa Hip Hop ya ukanda huu huko kunako “walami”.Staili wanayoitumia wanaiita Maasai Hip Hop.Hapo sasa.Utakumbuka mwaka jana msanii kutoka kundi hilo alikuwepo katika BET Awards Cypher sambasamba na KRS-One kitu ambacho kilizidisha mileage za kundi hilo kimataifa.
Hapa wanakuletea video mpya ya wimbo “Africa” ambao wamemshirikisha Fid Q na Bamba Nazar.

Kampuni ya African Stars Entertainment imeandaa tamasha kubwa la burudani kwa ajili ya kusherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara na Uzinduzi rasmi wa Albamu ya 11 ya Bendi yake ya African Stars “Twanga Pepeta”.
Tamasha hilo linataraji kuwahusisha wasanii wa fani mbalimbali za Muziki wa hapa nchini na kutoka nje ya nchi. Fani zitakazohusishwa ni pamoja na Taarab, Muziki wa Kizazi kipya na Muziki wa Dansi na msanii mmoja kutoka Nchini Kenya ambaye bado uongozi wa ASET unaendelea kufanya naye mazungumzo.

Tamasha hilo la uzinduzi linataraji kufanyika katika viwanja vya Leaders Club vilivyopo maeneo ya Kinondoni Jijini Dar es salaam siku ya Jumapili ya tarehe 06-11-2011 kuanzia saa sita za mchana.
Albamu itakayozinduliwa bado haijapatiwa jina ila nyimbo zilizopo kwenye albamu hiyo ni pamoja na “Mapenzi hayana Kiapo” utunzi wake Saleh Kupaza, “Penzi la Shemeji” utunzi wake Mwinjuma Muumini au Kocha wa Dunia, “Umenivika umasikini” utunzi wake Luizer Mbutu, “Dunia Daraja” utunzi wake Charlz Baba, “Mtoto wa Mwisho” utunzi wake Dogo Rama na nyimbo ya mwisho ni “Kauli” iliyotungwa na Rogart Hegga.
Nyimbo zote zimesharekodiwa katika CD kwenye studio ya Metro chini ya Mtengenezaji Allen Mapigo na nyimbo tatu zinatamba redioni na kwenye stesheni za redio mbalimbali hapa Nchini na nje ya nchi.
Maandalizi ya Tamasha yanaendelea vizuri na katika kufanikisha Tamasha hili, ASET imeandaa ligi ndogo itakayoshirikisha timu 12 ikiwemo Timu ya Twanga Pepeta FC iliyoundwa na wanamuziki na wadau wa karibu wa Bendi.
Uzinduzi wa mwaka huu tumeamua kuuweka tofauti kama zinduzi zilizopita ili kuenda sambamba na maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania Bara. Bendi inataraji kuingia kambini wiki moja kabla ya tarehe ya uzinduzi ili kujitayarisha vizuri kwa ajili ya shoo kali.
HASSAN REHANI.
MENEJA ASET.

The Ladies of Twanga Pepeta

Ni mwendo wa kutwanga na kupepeta.


Kwa Tanzania naweza kuwa sahihi nikisema kwamba “napenda kumtambulisha” kijana Chris Mhina,mtanzania anayefanya vizuri katika anga za muziki kutokea nchini Sweden kwani naamini sio watu wengi sana ambao wameshapata nafasi ya kumsikia Chris Mhina.Lakini kwa pande za kule Sweden,Chris Mhina hahitaji utambulisho sana kwani tayari ni miongoni mwa wanamuziki vijana wanaofanya vizuri sana katika za muziki.
Hivyo basi kwa heshima na taadhima,naomba nimtambulishe kwako wewe msomaji kijana huyu ambaye kwa mapana anapeperusha bendera ya Tanzania kupitia muziki huko Sweden na kote kwingineko hususani barani Ulaya.Ukitaka kujua mengi kumhusu Chris unaweza kufanya hivyo kwa kutembelea tovuti yake kwa kubonyeza hapa. Ili kupata kionjo kidogo tizama video hiyo hapo chini ya wimbo wake Last Dance.

Katika tuzo za muziki za Kilimanjaro(Kilimanjaro Music Awards) mwaka huu, alijinyakulia tuzo tano kwa mpigo na hivyo kuweka historia ya aina yake katika muziki wa kizazi kipya na kwa uhakika tuzo hizo.
Kilichofurahisha zaidi wananchi na hususani wapenzi wa muziki ni kwamba 20 Percent alistahili tuzo hizo kutokana na kuwa na albamu yenye mantiki na utamu halisi wa muziki.Inasemekana kwamba albamu ya Ya Nini Malumbano huenda ndio albamu iliyouzwa zaidi nchini Tanzania kwani hata kabla ya kumpatia tuzo hizo,ilikuwa ikienda kama njugu.
Kama nilivyodokezea hapo juu,kilichokuwa kinaiuza albamu hiyo ni nyimbo kali zenye ujumbe mkali na hivyo kuchukua jukumu la sanaa la kuelimisha,kuburudisha,kuonya,kushawishi,kusifia nk.Binafsi ninaisikiliza mara kwa mara album hii.
Akiendeleza kilichompa tuzo tano za Kili,20 Percent ameachia wimbo mwingine kutoka kwenye album hiyo hiyo ya Ya Nini Malumbano.Wimbo huu ambao uko katika mahadhi ya Reggae unaitwa Si Mfano. Ni production nyingine kutoka Combination Sound.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Pindi tu alipotwaa tuzo zake tano za Kili,nilifanikiwa kufanya mahojiano na 20 Percent.Kama hukuwahi kuyasoma,basi unaweza kufanya hivyo kwa kubonyeza hapa.Mahojiano hayo yalikuja kutumiwa pia na Jarida maarufu la Kitangoma.

Siku chache zilizopita nilipokea taarifa kutoka kwa Msanii Nonini kutoka nchini Kenya kwamba ameachia wimbo mpya unaokwenda kwa jina la Colour kwa Face kutoka katika album yake ya tatu aliyoipa jina The Godfather of Genge(ipo sokoni hivi sasa) akimshirikisha mwanadada Christine Apondi.
Kwa bahati mbaya sikupata muda wa chapchap wa kuusikiliza wimbo huu mpaka hivi leo.Kwa kawaida huwa siweki wimbo mpya hapa mpaka niwe nimeshausikiliza na kuupitisha(kuna watoto wanaingia hapa,lazima tuzingatie maadili fulani)
Baada ya kuusikiliza ilinibidi kusitisha vyote nilivyokuwa nafanya,kwenda ndani,kutoka nje na kuketi tena.Katika wimbo huu Nonini ambaye ni mwanaharakati wa kutetea watu wenye ulemavu wa ngozi(albino)anatuma ujumbe mpana sana kupitia wimbo huu.Kama mtakumbuka,Taifa letu la Tanzania liliingiwa na kashfa ya kimataifa pale ulimwengu ulipogundua kwamba kuna binadamu fulani wenye roho za ajabu wanawageuza watu wenye ulemavu wa ngozi “deal”.Nonini anaongelea hilo pamoja na mambo mengine ya kubaguana.Anaasa kupendana.Mpende kaka yako,mpende jirani na mpende kila mtu.Kwanini kubaguana?
Wimbo umetengenezwa na Musyoka kutoka Decimal Records.Usikilize…
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Unaweza kutizama picha za Nonini akiwa katika harakati zake za kupinga ukatili wowote dhidi ya albinos kwa kubonyeza link hii http://www.noninimusic.com/v2/national-albinism-day-may-4th/

Msanii anaitwa WESU, na hii ndio kazi yake ya kwanza kutoka rasmi kwa ajili ya kumtambulisha. Wesu ni msanii kutokea Dar,jiji lenye kila aina ya raha na karaha..a city.
Huu wimbo unaitwa “NGOJA KUKUCHE”. Ni story ambayo inajieleza yenyewe kama ukiisikiliza kwa makini, hivyo tunaamini itaeleweka na itawagusa watu wengi kwa sababu imewakilisha maisha ya kawaida.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
CREDITS:
Tittle: NGOJA KUKUCHE
Artist : WESU
Written by: YAKI & WESU
Arranged by: AMBA
Produced by: AMBA
Mixed by: AMBA
Studio: AMBA RECORDS
SEPTEMBER 2011



sending...
