MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Tafadhali naomba usinichoke kwa kupenda kutundika masuala/hotuba za Obama.Nafanya hivyo kwa kuamini kwamba kila siku binadamu tunajifunza au tunatakiwa tujifunze mambo mapya.Hotuba za Obama zawezekana kuwa hazikufunzi mambo mapya ila kwa mapana na marefu naaamini zinatukumbusha mambo mbalimbali.Pia namfuatilia Obama kwa sababu angalau yeye ndio mwanasiasa ambaye namuona hapendi “kuongopa waziwazi”.Obama hawezi kukuambia kesho atakujengea daraja wakati moyoni mwake anajua kabisa hela za daraja alishakula. Hawezi pia kutoa ahadi za maisha bora kwa wote bila kukumbusha kwamba kazi ndio msingi wa maendeleo.

Obama anaweza kuwa anaongea na kundi fulani tu la watu lakini akawa anatoa ujumbe mkali kwa jamii mbalimbali.Cha msingi labda ni kusikiliza kwa makini na kufanya tathmini makini. Hivi majuzi Obama alialikwa na kutoa hotuba wakati wa kusherekea miaka 100 ya chombo muhimu cha Wamarekani Weusi kinachoitwa NAACP(National Association for the Advancement of Colored People)

Katika hotuba yake,Obama aliongelea mengi.Muhimu zaidi ambalo naamini hata sisi watanzania tunaweza kujihusisha nalo ni suala la elimu kwa watoto wetu,jamii zetu. Ulimwengu wa leo,wa ushindani wa namna hii,unahitaji elimu makini.Je tunafanyaje katika hilo? Viongozi wetu wanatupeleka wapi? Hebu tujiulize, tangu marais wetu waliofuatia baada ya J.K.Nyerere wametusaidia kujenga maktaba ngapi? Hivi unajua jiji la Dar-es-salaam lina maktaba ngapi?

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

haroubbc

weddingbcWeekend ndio imewadia tena. Kama ulidhani wiki hii ingekuwa kavu kavu nchini Tanzania bila mikikimikiki basi ulikosea.Ilikuwa ni wiki ya “mipasho”. Ilikuwa ni rusha kombora nirushe kombora au kama vile alivyowahi kuimba Prof.Jay ukimwaga ugali mimi namwaga mboga!

Bahati nzuri ni kwamba nadhani watu wazima wamejiona ovyo na kuamua kufuata njia zinazostahili. Mchezo sasa umegeuka kuwa wa kudaiana “vijisenti”. Bila shaka umesikia mmoja kadai fidia ya Tshs Bilioni 10 huku mwingine akidai fidia ya Tsh 1 tu. Kama ingewezekana huenda angedai ile ya mkoloni kabisa iliyokuwa na tundu katikati. Sijui tugange yajayo au bado tuendelee na nguvu ya hoja,uchambuzi nk.

Tuyaache hayo.Leo ni burudani ya kale.Wenyewe mnaziita Zilipendwa. Natamani tungeziita Tunazozipenda kwani ukweli ni kwamba bado nyimbo hizi zina mafundisho kemkem na ni kama zilitungwa jana. Leo tunaye Gwiji Marijan Rajab(RIP). Wimbo unaitwa Ndoa ya Mateso. Binti karudi kwao.Anasema ndoa imemshinda.Mume anamtesa.Pesa zote anamalizia kwenye makuku ya kukaanga akiwa na “vimwana’ wake huko nje wakati familia inakufa kwa njaa.Binti hana msaada wowote,hana ndugu wala jamaa hapo alipo.Kwa masikitiko anauliza kwani kuolewa ni utumwa? Binti anaomba talaka yake.Mjumbe ndie anaombwa kuwa shahidi. Kwa uchungu na aibu anasimulia yaliyokuwa yanamsibu.Anataka kurudi nyumbani kwao kwani anasema hakuzaliwa juu ya miti bali ana kwao.Ana baba na mama. Mateso.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Pata burudani,pata ujumbe na furahia weekend yako. Maisha mafupi haya.

maluwe

Majuzi wakati ulimwengu unasheherekea sikukuu ya wapendanao,mtangazaji maarufu nchini Tanzania,Michael Maluwe alihitimisha siku hiyo kwa kufunga ndoa na kipenzi chake Diana katika Kanisa Katoliki Parokia ya Msimbazi jijini Dar-es-salaam.

Pichani ni Michael na Diana wakati wa tafrija iliyofanyika katika ukumbi wa Sunset uliopo Mbezi jijini Dar-es-salaam.BC inawatakia ndoa bora yenye Baraka na maelewano tele.

Picha hii ni kwa hisani ya Father Kidevu ambaye kama unamuhitaji kwa shughuli yako unaweza kumpata kupitia simu yake namba +255 755 373999.

Mwimbaji na mnenguaji maarufu wa Twanga Pepeta,Luiza Nyoni pamoja na mumewe Mr.Mbutu.Luiza Nyoni Mbutu ni miongoni mwa wanamuziki ambao wamekuwepo kwenye fani kwa muda mrefu nab ado anaendelea kutesa.

Picha kwa hisani kubwa ya Global Publishers.

Katika nchi nyingi za magharibi,leo ni Mother’s Day au kwa maneno mengine Siku ya Mama.Leo ni siku maalumu ya kumkumbuka,kuutambua na kuuthamini rasmi mchango wa mama yako katika maisha yako.Huu ni utamaduni wa kimagharibi ambao unazidi kuenea kwa kasi ulimwenguni kote zikiwemo pia nchi zetu za kiafrika.Sasa hii sio kumaanisha kwamba katika siku zingine usimkumbuke,usiutambue wala usiuheshimu rasmi mchango wa mama yako.La Hasha!Kila siku,kwa walio wengi, ni siku ya mama. Kwetu sisi waafrika ndio kabisaa.Ndio maana kuna ule usemi kwetu wa Nani Kama Mama?

Itumie siku ya leo kumkumbuka mama yako.Kama kwa bahati mbaya alishaiaga dunia,basi chukua muda maalumu kumkumbuka,kumuombea na muhimu zaidi kumuenzi.Kama upo karibu na mama yako,basi mkumbatie na umkumbushe kwamba unampenda na unamtakia kila la kheri katika maisha.

Ni muhimu pia kukumbuka kwamba, kama binadamu,huwa inatokea wakati mwingine tukakosa kuelewana.Ndio.Huwa inaweza kutokea tukakosa kuelewana hata na mama zetu! Kama hali ipo namna hiyo katika maisha yako,itumie siku hii kusameheana na kuweka mambo sawa na mzazi wako.Jinsi moja nzuri ya kuweza kusamehe ni kujiuliza swali;Je kuna ulazima au manufaa yoyote ninayoyapata kutokana na kutokuelewana huku? Usiwe mgumu wa kusamehe ili nawe upate kusamehewa.Sote tunakosea katika maisha.Kama leo basi ni kesho.Usisite kutenda lililo jema leo.

Katika kuisindikiza siku hii,tumekuchagulia wimbo maalumu kutoka kwa mwanamuziki mkongwe wa nchini Nigeria, Prince Nicco Mbagga.Wimbo unaitwa Sweet Mother. Huu ni wimbo maalumu kwa kina mama wote.Kinamama,tunawapenda na tunawathamini.Bila ninyi dunia si dunia.Bonyeza player hapo chini upate burudani,sikiliza ujumbe uliomo ndani ya wimbo.Happy Mother’s Day!

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Pichani ni Mr and Mrs Juma Nature. Hivi karibuni blog ya Abdallah Mrisho imeripoti kwamba Sir Juma Nature na mkewe aitwaye Bi.Pili, wamebarikiwa kupata mtoto wa kike aliyazaliwa katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke.BC inaungana na wengine wote katika kuwapongeza.

Pichani ni Juma Nature na mkewe Pili siku ya harusi yao mwaka jana.Picha kwa hisani ya Global Publishers.

 

Bila shaka ushawahi kuusikia ule msemo wa “kulala masikini kuamka tajiri”.Nia au kiini cha msemo ule huwa ni kuzungumzia jinsi ambavyo maisha huweza kubadilika ghafla,bila hodi wala karibu.Hii ndio hali halisi kwa mke wa Waziri Mkuu(Mizengo Pinda),Tunu Pinda(pichani) ambaye miezi michache tu iliyopita sio watu wengi sana walikuwa wakimjua.Leo hii mambo sio hivyo tena.Bi Tunu keshaanza kulikwea jukwaa la wananchi maarufu.Wanapoketi wake wa “vigogo” wa nchi,huwezi kumkosa au kumuacha pembeni.That’s life!

 

Jana ndio ilikuwa jana.Kama ambavyo imekuwa ikiripotiwa,Banana Zorro na Suzy Walele jana walifunga pingu za maisha.Pichani ni Banana Zorro akimlisha keki mkewe Suzy Walele.Sherehe hiyo iliyofana ilifanyika katika ukumbi wa Msasani Beach Club jijini Dar-es-salaam.Banana na Suzy wamefungua ukurasa mpya.BC inawatakia kila la kheri.Kwa picha zaidi endelea hapa (more…)

Sehemu nyingi sana ulimwenguni hivi leo ni shamrashamra za sikukuu ya Christmas. Mitaani leo kuna kila aina ya shamrashamra.Leo ndio ile siku ya kuvalia zile mpya ulizonunuliwa na mzazi,mke,mume,rafiki,mjomba,shangazi,binamu nk. Harufu iliyotanda mitaani ni ile ya pilau(uh uh uh uh). Fukwe za jiji la Dar-es-salaam kwa mfano,leo zinapata habari yake. Simu za viganjani zinaita kuliko mfano, ni mwendo wa miadi ya kukutana na kufurahia siku hii ambayo hutokea mara moja tu mwaka. Hii ni tofauti na mitaa ya Ulaya au Marekani ya kaskazini. Mitaani hamna mtu, mall na maduka yote leo yamefungwa. Ni siku ya familia.Kila mtu kwao au kwake.Kimya kimya hivi.Usipojua style hizi za wazungu katika kusheherekea Xmas unaweza dhani kuna msiba fulani. Subiri kesho sasa,Boxing Day.Kila mtu mtaani,madukani.Kazi kweli kweli.

Kama anavyoimba mwanamuziki Dennis Kagia aka DNA(pichani) kutoka kwa majirani zetu Kenya, leo ni mwendo wa kubanjuka tu. Ni siku unayotakiwa kusahau matatizo yote,japo kwa muda. Toka nje,ingia mitaani.Jichanganye na wenzako. Usijitie upweke hivi leo. Ni sikukuu.

Mtizame DNA hapo chini kwenye wimbo wake Banjuka. Msikilize akisema “Weka shida chini,tupa mikono juu, Banjuka tu.Life ni fupi na mimi sijivungi” Kama vile haitoshi anasema ‘Sisi tuna shida zetu,tusikilize zako kwanini”? Xmas Njema.Furahia kwa sana lakini kuwa makini,hata kama maisha ni mafupi. Amani na upendo vitawale.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page