MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Mwanamitindo maarufu ulimwenguni,Naomi Campbell,yaelekea akaingia matatani tena kwani hivi sasa polisi wa jijini New York nchini Marekani,wanamsaka!

Naomi,ambaye mwaka jana alitua nchini Tanzania na kushiriki katika onyesho la hisani kwa ajili ya akina mama, safari hii anatafutwa akikabiliwa na shutuma za kumchapa vibao dereva wake huko New York.

Mwanamitindo huyo ambaye inasemekana ni mpenda ugomvi sio mgeni na vyombo vya usalama.Siku za nyuma amekwisha kutwa na hatia ya kumpiga mfanyakazi wake wa ndani jijini New York, kumpa kibano msaidizi wake jijini Toronto na pia kumwangushia kisago polisi ndani ya ndege katika uwanja wa ndege wa Heathrow jijini London.Katika makosa yote hayo hapo juu,Naomi alikiri makosa yake na alihukumiwa kufanya kazi za kijamii(community services) kwa masaa zaidi ya 200.Kazi kweli kweli.Hivi kwanini kuna baadhi ya watu huwa wanadhani wanayo haki ya kuwaadhibisha watu wengine kiholela tu?Ni matunzo,jamii au?

NB:Hivi unajua Naomi Campbell alipokuwa mdogo alishiriki katika video ya Mfalme wa Reggae,Bob Marley katika wimbo One Love? Mtizame katika video hiyo hapo chini.Alikuwa na umri wa miaka 7 tu na hiyo ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kuwa katika spotlight.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

M-Net Face of Africa 2010 - The Top 12

Visura 12 wa M-Net wanaowania nafasi ya kuchuana kwenye fainali za kumtafuta kisura wa Africa(M-Net Face of Africa) zitakazofanyika katika jiji la Lagos, Nigeria, Februari 6, 2010.

East Africa

Ijumaa hii katika ukumbi wa Mlimani City,ni kivumbi na jasho.Mrembo wa Afrika Mashariki atakuwa akitafutwa. Zawadi kuu ni Toyota Celica Sports kama inavyoonekana pichani juu na huku warembo wanaowania taji hilo wakiwa wamelizunguka.

Nani atalinyakua gari hilo?Hilo ndilo swali la msingi. Kwa picha zaidi za warembo hao,na habari zaidi kuhusu tukio hili,bonyeza hapa.

Warembo wanaoshiriki katika mashindano ya kimataifa ya urembo ya Miss East Africa 2009 wataanza kuwasili nchini wiki hii(au wameshaanza kuwasili) tayari kwa mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika tarehe 18 mwezi wa 12 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.

Aidha, warembo watakaoiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo wanatarajiwa kutangazwa kesho kutwa baada ya kamati maalumu iliyopewa jukumu la kuratibu zoezi hilo kukamilisha kazi yake.

Mashindano ya Miss East Africa mwaka huu yanatarajiwa kuwa na mvuto wa aina yake kutokana na Nchi zinazoshiriki mashindano hayo kuchagua warembo wenye viwango vya hali ya juu ili kuziwakilisha katika mashindano ya mwaka huu

Miss East Africa 2009 itashirikisha warembo kutoka katika Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Eritrea, Somalia, Djibouti, na Mauritius ambazo zote zimeshathibitisha ushiriki wao.

Mashindano hayo makubwa ya urembo kwa ukanda huu wa Africa yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Limited ya jijini Dar es salaam.

Miongoni mwa makampuni yanayodhamini mashindano hayo kwa mwaka huu ni pamoja na Kunduchi Beach Hotel & Resort, EATV, Kings & Queens Worldwide, CMC Automobiles Limited na AKO Catering Services Ltd.

Hizi hapa chini ni picha,majina na umri wa baadhi ya washiriki wa mashindano hayo.

East1

Rebecca Getachew (23) Ethiopia,

East3

Asli Osman Mahamud(20)-Somalia

East4

Fatma Abdilahi (18)-Somalia

East5

Dalysha Nirena Doorga (21)-Mauritius

East7

Tabitha(20)-Kenya

East8

Queen Belle Monique (23)-Burundi


sheria1

If you are into fashion,you gotta watch Sheria Ngowi.Click Here.

elite-modelbc

INTRODUCING ELITE MODEL LOOK -TANZANIA

Compass Communications Company Limited introduces the largest and most prestigious modeling international competition in the world – Elite Model Look. Compass Communications Company Ltd is an independent TV production company that produces various TV programs and also is the organizer of Miss Universe Tanzania and other beauty pageant titles like Miss Earth, Miss International and Miss Tourism Queen International in Tanzania. The company has now branched out into a more specialized part of the industry namely professional modeling.

Elite Model Look contest was created in 1983 under the name Look of the Year. Elite Model Look competition is the largest model contest of its kind. This contest has become one of the most prestigious springboards for talents into the modeling industry. Up to now Elite Model Management is present in 5 continents and it represents more than 2,000 (Two Thousand) models internationally.

Each year, the Elite Model Look competition sees over 350,000 contestants attend regional and national castings that take place in more than 55 different countries, with at least one contestant of each country participating in the main event – the World Final..

The competition is made of several steps. Thus, through an intensive and rigorous selection process, which drives them from regional castings to national finals, at least one local contestant of each country gets a chance to participate in the World Final. Here in Tanzania Compass Communications will hold local auditions in Dar-Es-Salaam : where all applying contestants will be narrowed down to 10 to 15 semifinalists. No final event will be held this year in Tanzania and the 10 – 15 semifinalists will then be judged by a panel of judges including a representative from Elite Model Look headquarters in Paris, France, in order to find the Tanzanian model who will represent Tanzania in the World Finals in October in Sanya, China.

All girls are invited to make their dreams come true by participating in auditions of Elite Model Look Tanzania. The auditions are open to strictly girls aged 14 to 20 years, with the minimum height of 172 cm. The winner will be selected to meet the fast changing trends and needs of the fashion industry. She will be chosen based on photogenic quality, personality and natural beauty. From the approximately 70 finalists at the World Finals, 15 are chosen by an international panel of judges and they all sign an exclusive contract with Elite Model management. And out of the 15 luck ones, 3 are voted as winners. The top 3 winners will share a guaranteed remuneration of 325,000 USD in total as modeling contract.

This is the first time for Tanzania to hold the license and to select a finalist for Elite Model Look although in 1999 Miriam Odemba was selected and participated successfully in the Elite Model Look World Final in Nice, Paris through MNet Face of Africa.

For more information kindly contact Maria Sarungi Tsehai OR Mwanakombo Salim, Compass Communications, Tel: (022) 2182405, 2182596 Mob: 0784 305122


illuminata12bc

Mrembo ambaye ataiwakilisha Tanzania katika shindano la mwaka huu la Miss Universe,Illuminata James Wize amekwisha wasili huko visiwani Bahamas akiwa tayari kabisa kwa shindano hilo zito ambalo mwaka huu linafanyika hapo Bahamas tarehe 23 August(mwezi huu).

Shindano hilo linatarajiwa kurushwa moja kwa moja(live) katika kituo cha televisheni cha NBC siku hiyo saa tatu usiku (9.00pm) kwa saa za East Standard Time(US).

Kura za mtandaoni bado zinaendelea na unaombwa kuendelea kumpigia kura Illuminata.Bonyeza hapa ili kufanya hivyo. Hizi hapa ni baadhi ya picha za Illuminata akiwa huko Bahamas.

illuminata1bc

Illuminata akiwa na warembo wenzake wanaoshiriki shindano la mwaka huu wakiwa mitaani huko Bahamas.

illuminata3bc

Illuminata na warembo wengine walipotembelea hotel na mgahawa maarufu wa Graycliff huko Bahamas.

First Photo/MissUniverse.com

illuminata_mu5bc

Kindly visit www.missuniverse.com, log in and get a username then go to http://www.missuniverse.com/members/profile/41815 and click on Rate This Member and give Illuminata 5 Stars (It’s important to give her 5 Star for her stats to increase). With few 5 Stars votes,she can get ahead faster than with many 1 or 2 stars votes.Don’t forget to leave encouraging messages on the page for Illuminata. Go Tanzania!!

likokola

Pengine yeye ndio miongoni mwa warembo wa mwanzo kabisa kuiweka Tanzania katika ramani ya dunia katika masuala ya urembo. Anaitwa Tausi Likokola.

Kama ilivyo hapa kwetu,pengine na wewe umekuwa ukijiuliza,yuko wapi Tausi? Mbona kimya sana? Unaweza kutembelea tovuti yake ili kupata japo updates kidogo juu ya anachokifanya.Pia kama humkumbuki au hujawahi kumsikia,tembelea tovuti yake ili kujua mengi.

iluminata2009bc

Kama kuna mashindano ya urembo ya kimataifa ambayo Tanzania inaweza kujivunia bila shaka ni mashindano ya Miss Universe. Bila shaka bado tunakumbuka jinsi mrembo Flaviana Matata alivyoipeperusha vyema bendera ya Tanzania huko nchini Mexico mwaka 2007. Flaviana sio tu alishika mojawapo ya nafasi za juu bali style yake ya kuwa “mrembo mwenye upara” ilikuwa gumzo la dunia nzima kitu ambacho kwa namna yake kiliitangaza sana Tanzania.Kila mtu alikuwa akitaka kujua yule mrembo mwenye upara anatokea nchini gani? Jibu walilipata.

Mashindano ya mwaka huu yanatarajiwa kufanyika tarehe 23 August huko katika visiwa vya Atlantis Paradise ndani ya Nassau,Bahamas.Jumla ya warembo 84 wanatarajiwa kushiriki mashindano ya mwaka huu.

Tumaini letu na mwakilishi wetu huko ni binti unayemuona pichani. Anaitwa Illuminata James Wize. Bila shaka tayari waandaaji wa Miss Universe Tanzania walio chini ya uongozi hodari wa Maria Sarungi tayari wameshaanza maandalizi makali ili kuhakikisha kwamba kwa mara nyingine tena Tanzania inakwenda kushindana na sio kushiriki.BC inamtakia kila la kheri Illuminata James.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page