Jina lake unayemuona hapo juu ni Zuwena Mohamed.Ila kwa wengi anajulikana kama Shilole.Sina hakika kama Shilole jina lake la tokea utotoni au ni jina la kisanii.Ni muigizaji wa filamu nchini Tanzania na yes anaimba pia.
BC inajiandaa kuambaa na Shilole katika mahojiano maalum.Je,unalo swali au maswali ambayo ungependa Shilole ayajibu?Kama jibu lako ni NDIO basi usisite kuyatuma maswali yako kwenda bongocelebrity at gmail dot com(anuani pepe imewekwa hivyo ili kupunguza hackers).
ANGALIZO: Maswali yalenge katika kujenga na sio kubomoa
Picha kwa hisani ya Global Publishers.
Miezi kadhaa nyuma niliwahi kuuliza swali kuhusu nani aliye zaidi katika ya Steven Kanumba na Ray Kigosi.Mashabiki na wafuatiliaji wa Bongo Movies mkatoa ushirikiano mkubwa na kueleza bayana yule ambaye mnadhani ni zaidi ya mwenzake.Mpaka leo hii bado comments kuhusu hoja ile bado zinaendelea.Hiyo,kwa upande mwingine,inaonyesha ni kwa jinsi gani watu zaidi wanafuatilia sanaa ya filamu nchini Tanzania.Ni jambo zuri.
Leo naomba tuhamie kidogo upande wa waigizaji wa kike kwani ni wazi kabisa na wao wanafanya vizuri sana katika kuendeleza fani hii ambayo kwa miongo kadhaa ilipewa kisogo.Mchango wao ni dhahiri.Hapa naomba niwaweke “kikaangoni” Monalisa (Yvonne Cherryl) na Blandina Chagula maarufu kama Johari. Bila shaka umeshawahi kuwaona katika uigizaji wa aina mbalimbali.Endapo ungekuwa na filamu yako na ukawa unatafuta mwigizaji wa kike(lead actress) ungemchagua nani katika ya Monalisa au Johari.Kwa ufupi unadhani nani zaidi kati yao?Kwanini?
Johari
Muigizaji maarufu wa filamu za kibongo(Bongo Movies), Steve Kanumba, ana muonekano mpya.Sio muonekano mpya wa kubadili labda style ya nywele au rangi ya ngozi yake bali size ya mwili wake.Anasema baada ya kushauriwa na mashabiki wake kwamba ameanza kuelekea kwenye “michelin marathon”,akaamua kuitikia wito wa mashabiki wake waliomtaka apungue ili arudie zama zake. Sasa ameshapungua kama picha zinavyoonekana. Anauliza mashabiki wake kama aendelee kupungua au aishie hapo hapo.
Unaweza kumpa ushauri hapa au kwa kutembelea blog yake kwa kubonyeza hapa.Hizi hapa baadhi ya picha jinsi alivyo hivi sasa.





Kwa takribani miezi minne sasa,watanzania na watu wote wanaoongea au kutumia lugha ya Kiswahili wamekuwa wakiburudika na kuelimika kupitia channel mpya kabisa ndani ya DSTV inayokwenda kwa jina Africa Magic Swahili inayopatikana katika namba 127. Hivyo hutokosea ukiamua kuiita Channel 127 ya DSTV.Kama bado hujapata fursa ya kutazama Channel 127,nakushauri ufanye hivyo leo hii.
Nini kilipelekea kuanzishwa kwa Channel hiyo ambayo kila kukicha inazidi kujipatia umaarufu? Inawasaidiaje wasanii wa tasnia ya filamu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati katika kutimiza malengo yao na kupanua soko lao?Je,utaratibu wa kuingiza filamu yako katika Channel hiyo kama wewe ni muundaaji,muongozaji au msanii wa filamu ukoje?
Ili kupata majibu kwa maswali hayo na mengineyo,nilimtafuta Meneja Masoko wa DSTV-Tanzania,Furaha Samalu(pichani).Hapo chini ni maswali niliyomuuliza na majibu kutoka kwake;Fuatana nasi…
BC: Furaha,karibu sana ndani ya BC,pole na kazi.Mambo yanakwendaje?
FS : Mambo ni safi kabisa…Ahsante sana
BCÂ :Â Â Â Â Yapo mambo mengi sana ambayo tunaweza kuzungumzia kuhusiana na kazi yako au kazi zenu lakini kwa leo tumekutafuta ili kuzungumzia Channel 127 katika DSTV.Channel hii imeanza rasmi lini na kwanini mkaamua kuanzisha channel hii? Mchakato huo ulikwendaje?
FSÂ : Kwanza kabisa nishukuru sana BC kwa kunipa nafasi ya kuzumza na watanzania na kuwafahamisha zaidi juu ya chaneli yetu maarufu kabisa iitwayo AFRICA MAGIC SWAHILI inayopatikana katika vifurushi vyote vya DStv kwenye chaneli number 127.Africa Magic Swahili ilianza kurushwa kwenye DStv platform tarehe 1st of July 2011 na inaonekana masaa 24 katika nchi zifuatazo Tanzania, Kenya, Uganda, Ethiopia, Rwanda, Burundi, Congo and the DRC.
DStv iliamua kuanzisha chaneli hii mahususi kabisa kwa nchi za Afica Mashariki kama sehemu pekee ya kuonyesha kazi na utamaduni wa nchi hizi…kwa kuzingatia uwezo na utajiri mkubwa katika fani ya sinema na burudani mabalimbali uliopo katika nchi hizi.

BCÂ : Nimepitapita mitaani na kukuta watu wengi wakitizama Channel 127.Sasa huu wangu unaweza kuwa mtazamo ambao sio sahihi kwa njia moja au nyingine.Kwenu ninyi wenyewe,mpaka hivi sasa mwitikio umekuwaje?
FSÂ : Napenda kuwashukuru sana watanzania na hasa wasanii wa fani mbali mbali kama sinema, muziki na tamthilia kwa muitikio wao mzuri sana ambao unaifanya chaneli yetu hii ya Africa Magic Swahili iendelee kukuwa siku hadi siku.
Mpaka sasa watanzania ndio tunaoongoza kwa kutuma kazi zetu kwenye chaneli hii, nchi zingine za Africa mashariki zikifuata.
Msanii wa filamu za kitanzania maarufu kama Bongo Movies,Jacqueline Wolper Massawe,ana muonekano mpya kama picha zinavyoonyesha.Nini maoni yako?Amechemsha au ametoka swadakta?





Photos Courtesy of Ray The Greatest Blog

Ingawa historia ya filamu za kitanzania au Kiswahili ina historia ndefu(tangu enzi za kina Yombayomba,Chale Mwembamba na Mnene,Maangamizi nk),hakuna ubishi kwamba unapoongelea masuala ya sanaa hiyo hivi sasa,ni vigumu kuwaweka kapuni vijana wawili;Steven Kanumba na Ray Kigosi(kama wanavyoonekana hapo juu pichani).Kwa sababu mbalimbali,zikiwemo wingi wa filamu walizocheza na kuongoza(hili bado halinipi amani ya kweli),ndizo zinazowaweka mbele ya wenzao.
Mbaya au zuri ni kwamba Kanumba na Kigosi ni marafiki.Wenyewe wanapenda kutumia neno “swahiba” wanapotajana iwe ni hadharani au katika blog zao(Ya Kanumba hii hapa na ya Kigosi hii hapa).Pamoja na urafiki walionao,ninavyojua mimi Ray na Kanumba ni washindani. Wamewahi wenyewe kuongelea suala na “kufunikana” kama filamu.Kwamba mimi ni zaidi ya wewe na mambo kama hayo.
Hilo ndilo linalonifanya leo nikuletee wewe msomaji (natumaini u-mpenzi wa filamu za kitanzania[bongo films/movies]) nafasi ya kuwa jaji.Kwa mtizamo wako na kwa jinsi ambavyo umekuwa ukifuatilia filamu au uigizaji wa Steven Kanumba na Ray Kigosi nani unadhani ni zaidi ya mwenzake? Na je unaweza kusema ni kwanini unadhani huyo unayesema ni zaidi ni zaidi ya mwenzake?Una ushauri gani kwake au kwao?

Endapo unapenda kujua mengi kiasi kuhusu muigizaji Steven Kanumba,sasa papo pahala ambapo unaweza kufanya hivyo kirahisi hata kutoka kwenye simu yako ya kiganjani.Anayo tovuti mpya ambayo kwa mujibu wake mwenyewe,imeboreshwa na kuwa ya kimataifa zaidi.Ni www.kanumba.com. Unaweza kuitembelea kwa kubonyeza hapa.
Naomba nimpongeze Kanumba kwa hatua hii.Natumaini wengine nao watafuata kwani katika ulimwengu wa leo tovuti ni suala muhimu sana katika kujitangaza na kuwasiliana na mashabiki na wanunuzi wa kazi za sanaa kirahisi zaidi.Caution: Hakikisha inakuwa updated mara kwa mara.

Unaowaona pichani ni baadhi ya waigizaji wa filamu nchini Tanzania.Kuna jina lingine ambalo wanapenda kulitumia wakiwa pamoja.Ni Bongo Movies Stars.Kwa ufupi waigizaji hao ni watu ambao wana umaarufu kwenye jamii.Kuna wengine wana umaarufu kupitia majina yao ya uigizaji kuliko hata majina yao halisi.Je,kwa kuwatazama hapo pichani unaweza kuwataja au ku-tag picha hii?
Pichani ni wiki iliyopita walipokwenda Dodoma kukutana na watunga sheria wa nchi hii.Aliyepo pichani katikati ni Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko,Dr.Cyril Chami na Mbunge wa Viti Maalumu,Vicky Kamata ambaye pia ni msanii/mwimbaji.
Picha:PMO Office
A couple of weeks ago (almost a month), when browsing the internet and specifically on African Movies’ subject, I came across something that caught my profound attention. I came across a movie titled Taharuki that was/is scheduled to be screened at the New York African Film Festival. As you can guess, it is the name Taharuki Swahili word for Suspense, which generated my curiosity first. It is not very common to see “our films” in such prestigious festivals. And by “our films” I mean films from East Africa, made by East Africans.
It was then that I learned that Taharuki or Suspense in English, a short film, is actually written, produced and directed by one of our own, Ekwa Msangi-Omari (photo above) and one of the actresses in the film is Miriam Chemmoss whom I interviewed back in 2008.
I was then introduced to Ekwa by Miriam just to learn later that she is actually a distant relative of mine! Few weeks after that introduction, I had an opportunity to sit down with her for the interview you are about to read on the film Taharuki which is set against the backdrop of the start of the devastating post-election violence that took place in Kenya in 2007/2008 and has left tens of thousands of Kenyans homeless, traumatized or dead. This film is the fictional account of a man and woman from opposing ethnic tribes who’re working for an underground liberation movement to expose a child-trafficking cartel when something goes wrong, and they’re forced to make tough choices in order to stay alive and complete their mission.
Ekwa has directed for some of the biggest TV shows in East Africa including The Agency (MNET) a 13-part TV series which she created, show-ran, and directed; the hit show Block-D (KBC), and most recently co-created critically ac-claimed Higher Learning (NTV) along with several short films. She’s written for TV and film, and produced several shorts. Weakness, a short film she recently produced, has screened worldwide, including New York, Durban and Brazil and was nominated for a 2010 Kalasha Award and a 2011 AMAA-Award.
Watch the Trailer for Taharuki and then go ahead and read the full interview that follows. Pay close attention on the question of what she thinks about current state of African movies;

Bonyeza hapa kumtembelea mwenyewe ili ujue nini kinachojiri.It’s a Shock!


sending...



