MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Miongoni mwa mambo ambayo yanatia moyo nchini kwetu ni pamoja na kuendelea kukua kwa tasnia ya filamu kama ambavyo tumekuwa tukishuhudia. Ukuaji huo unakwenda sambamba na kuona kwamba,siku baada ya siku, wapenzi wa filamu za “nyumbani” wanazidi kuongezeka na kwa maana hiyo industry nzima ya filamu inazidi kukua.

Lakini uungwaji mkono huo haukuja bure tu. Umetokana na tabia nzuri ambayo wasanii wengi wa sanaa hiyo wameionyesha.Wamekubali kukosolewa na kusikiliza maoni ya wadau mbalimbali wa masuala ya filamu na kuyafanyia kazi ipasavyo.

Miongoni mwa wasanii hao ni pamoja na Steven Kanumba ambaye bila shaka sote tunakubaliana kwamba kila kukicha ameonyesha kuwa na bidii kubwa kabisa katika kuboresha kazi zake na uigizaji wake kwa ujumla.

Mwezi ujao(August),Kanumba anatarajia kuendelea kuthibitisha jinsi anavyozidi kukomaa katika sanaa hiyo,itakapotoka filamu ambayo imepewa jina Crazy Love(Part 1 & 2). Kwa mujibu wake yeye mwenyewe kupitia blog yake,ili kuweza kuigiza katika filamu hiyo,ilimbidi kusoma vitabu mbalimbali vya wanafalsafa mashuhuri ulimwenguni kama vile Plato,Karl Max,Alexander The Great,Samuel Taylor nk ili kuelewa zaidi mambo yanayohusu tabia za binadamu,falsafa nk.

Je usomaji huo ulimsaidiaje Kanumba katika Crazy Love?Usikose kununua makala halisi ya filamu hiyo pindi itakapoingia sokoni mwezi ujao.

Photos Courtesy:Kanumba.

Kama unafuatilia masuala ya filamu hususani kutoka Hollywood,bila shaka utakuwa umesikia kuhusu “wazimu” uliowaingia wapenzi wa filamu(wengi wao ni vijana) kuhusu movie mpya inayoingia Theatre hivi leo ya The Twilight Saga:Eclipse. Ni movie kuhusu Vampires. Vijana wengi wa kizungu hupenda sana hadithi na mikasa kuhusu Vampires.Tizama Trailer ya filamu hiyo hapa chini;

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Kuna mtu kaniuliza swali ambalo sikuweza kuwa na jibu lake.Sasa kama unavyojua,BC ina watu.Watu kama wewe.Ninapokuwa sina jibu la swali au maswali,naomba msaada kutoka kwako.Ndio raha ya kuzungukwa na jamii.Penye wengi hapaharibiki neno. Mwenzetu kauliza;

Eti ni kweli Irene Uwoya na Jacquiline Wolper wanafanana kiasi kwamba wengine kuthubutu kumuita Jacquline kuwa ni pacha wa Irene Uwoya?

Pichani aliyepo kushoto ni Irene Uwoya na kulia ni Jacquiline Wolper.Wewe unasemaje?Wamefanana?

Bila shaka unaelewa kwamba kwa waafrika wengi,unene ndio deal.Ukiwa umekondeana au mwembamba,mara nyingi utadhaniwa kwamba umejawa na matatizo,umechacha,unaumwa nk.

Hali ni tofauti katika nchi za ughaibuni.Ukinenepeana ndio unaonekana una matatizo.Ukiingia tu kwa daktari wako swali lake linaweza kuwa “What is wrong,you have gained so much weight”. Suala la unene=afya na kupungua/kukonda=matatizo, ni mjadala ambao hata tukiamua kuuanza hivi leo hautoisha.

Ila kama wewe unaamini kwamba kupunguza uzito ndio afya(mimi naamini katika kuwa wastani) au unataka kupungua uzito kwa sababu zozote zile,basi unaweza kujifunza kutoka kwa mwanamuziki na mcheza filamu,Curtis Jackson au maarufu kama 50Cent.Pichani unaona jinsi alivyopungua.

Kwa mujibu wa mtandao wa ThisIs50.com, amepungua kwa ajili ya role ya filamu iitwayo Things Fall Apart(hakuna uhusiano na kitabu cha Things Fall Apart cha Achebe).Katika filamu hiyo,50 anaigiza kama mcheza Football(American Football-inatumia zaidi mikono) aliye na ugonjwa wa kansa. 50 Cent ameweza kupungua kutoka Paundi 214 mpaka Paundi 160(takribani kutoka kilo 97 mpaka kilo 72.5 hivi). Ametumia nini? Anasema ni Liquid Diet na kukimbia kwenye treadmill kwa masaa matatu kila siku kwa wiki tisa mfululizo!

Je,wacheza filamu wetu wanaweza kuiga mfano huu wa kupungua au kuongezeka ili ufit katika role fulani ya filamu? Changamoto.

Her name is Cynthia Masasi. She was born in Mwanza, Tanzania. Without a doubt, her name is among the most recognized name among Tanzanians especially abroad and even at home.

Although she has been in a limelight for a while through her career as a model, it is her appearances in a lot of rap/hip hop videos that made her popular. Those appearances, famously known as video vixen, have also been a point of attack and debates from her supporters and fans versus those who belong to the school of thought that claims; video vixen is something that degrade women and nobody’s daughter, mother or sister should be part of it.

She is now an aspiring actor, entrepreneur and continues being a model. In fact, she has already appeared in a couple of movies and has some serious upcoming projects this summer. We recently caught up with her to talk about her current career, her experiences as a video vixen and her entrepreneurship dreams and goals. How did she move from modelling to video vixen and now into much more serious acting? What is her motivation? What advice does she have for young models and artists? This is how it all went down;

BC: Cynthia, welcome to BongoCelebrity. It feels good to have you here. How are you doing?

CM: Thank you. I am doing great. How about yourself?

BC: I am doing great too Cynthia. Thanks for asking. Now I wish I could skip this question but because this is your first time on BC, there are tons of fans who’d like to know a bit about your life history. Can you briefly tell us where were you born, which schools did you go etc?

CM: I was born and raised in Mwanza. I come from a family of 6 children and I am the first born. I have one brother and four sisters. I started my academic journey at Progressive School which is in the city of Kampala in Uganda. Later on, I transferred to Nyanza Primary school in Mwanza. For secondary school, I went to Mwanza Secondary School in Mwanza. After that my mother suggested that I join Jitegemee Secondary School in Dar-es-salaam for A-Level studies. I therefore joined Jitegemee High School for the A-level. To this day I still have great memories of Jitegemee High School. Loved it! (more…)

Pichani juu ni Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akizungumza na waandishi wa habari kwenye Klabu ya Much More mapema hivi leo wakati alipozungumzia Filamu mpya inayoitwa Lovely Gamble iliyotengenezwa na kampuni ya ASET kwa kumtumia muigizaji Kanumba na watanzania kadhaa.

Asha amesema filamu hiyo imetengenezwa nchini Uingereza kwa kumtumia mtoto wao anyesoma huko ambaye ameiongoza, kurekodi na kuiediti filamu nzima kwa kutumia kampuni yake ya Buzzie Production.

Kanumba ameshirikiana na watanzania wanaoishi nchini Uingereza, wakenya pamoja na wazimbabwe na lugha zilizotumika katika filamu hiyo ni kiingereza na kiswahili.

Ameongeza kwamba filamu hiyo itazinduliwa aprili 25 kwenye ukumbi wa Billicanas wakati wa onyesho la kawaida la bendi ya African Stars inayopiga kwenye ukumbi huo kila jumatano katikati ya wiki.

Amemaliza kwa kusema kama ilivyo kampuni ya ASET imeendelea kuthamini vipaji vya wasanii wa nyumbani na baada ya kutoa filamu ya “Tone la Damu” imeamua kutoka na filamu hii mpya ya “Lovely Gamble” ambayo mara baada tu ya kuzinduliwa itaanza kusambazwa na kampuni ya KAPICO LTD na itakuwa ikiuzwa kati ya shilingi 2000 kwa bei ya jumla.

Habari na picha kwa hisani ya Full Shangwe. Itizame Trailer/Promo ya Lovely Gamble hapo chini.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

KanumbaFrontKatika siku kama ya leo,miaka 26 iliyopita pale mkoani Shinyanga, alizaliwa kijana na kupewa jina la Steven. Hivi leo ni maarufu kama Steven Kanumba au kama mwenyewe anavyojiita wakati mwingine “The Great”. Kwa maana hiyo,leo ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Steven Charles Kanumba.Happy Birthday!

Kwa mtu yeyote ambaye anafuatilia maendeleo ya tasnia ya filamu nchini Tanzania,bila shaka atakubaliana na mimi nikisema kwamba Kanumba ni miongoni mwa waigizaji wa filamu(Film Actors) ambao ni maarufu zaidi nchini Tanzania. Leo hii ni vigumu kuiongelea sanaa ya filamu nchini bila kumhusisha Kanumba kwa njia moja ama nyingine.

Kwa hivyo,haishangazi sana kuona kwamba,katika mwaka uliopita jina lake lilikuwa takribani la kudumu katika vyombo mbalimbali vya habari vikiwemo vya mtandaoni,mitaani nk. Bila shaka unakumbuka jinsi habari ya Kiingereza Vs Kiswahili ilivyozua mjadala wa kitaifa. Kila mtu akasema lake.

Baada ya mambo kama yale,mijadala kama ile,watu hupenda kujua what next? Nilimtafuta Steven Kanumba ili kujua machache kuhusu mipango yake ya mwaka huu.

Unajua Kanumba angependa kupata chakula cha mchana (lunch) na actors gani maarufu hapa ulimwenguni? Una habari kwamba katika Curriculum Vitae(CV) yake ameongeza cheo cha “Blogger”? Unajua ana malengo gani mwaka huu? Una habari kwamba Kanumba hivi sasa amedhamiria kuibua vipaji vingine katika ulimwengu wa uigizaji filamu? Fuatana nami;

BC: Mpaka sasa unalionaje soko la filamu nchini Tanzania? Kumekuwa na mabadiliko gani ya kimsingi ukilinganisha toka ulipoanza mpaka hivi leo?

SK: Soko limetanuka kiasi kwamba tunatambulika kimataifa. Pia hivi sasa makampuni ya kusambaza kazi zetu yameongezea ikiwemo na pesa kwa kiasi fulani tofauti na hapo mwanzo.Safari bado ni ndefu lakini angalau inatia moyo.

BC: Mwaka 2009 ndio tumeumaliza.Jina lako liligonga vyombo vya habari kwa mambo kadha wa kadha.Unaweza kusema umejifunza mambo gani katika mwaka ulioisha? (more…)

Imekuwa gumzo ulimwenguni kote.Ni filamu kutoka kwa Muongoza Sinema(Film Director),James Cameron. Huyu ndiye pia aliyetengeneza filamu maarufu ya Titanic.

Mpaka hivi sasa imeshaingiza zaidi ya $ 1 billion katika mapato ya sehemu mbalimbali za ulimwenguni.Rais Barack Obama na familia yake,waliitizama walipokuwa vacation huko Hawaii hivi karibuni. Ilibidi secret services watoe kila mtu kwenye jumba la sinema ili Obama na familia yake wapate kuiona bila bugudha au tishio lolote.Mambo ya wakubwa hayo!

Umeshaiona Avatar? Mimi sijaiona bado.Nipe ushauri.Nikaitazame pia au nisubiri tu kuiazima kwenye DVD? Tizama trailer yake hapo chini.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

baby-powder

Kila kukicha,watanzania mbalimbali waliotapakaa ulimwenguni kote wanazidi kuwa wabunifu na watu wanaothubutu kufanya mambo fulani fulani ambayo sio tu yanazidi kuiweka Tanzania mahali inapostahili katika ramani ya dunia ,bali pia kuongeza ujuzi,kuingiza vipato halali na zaidi to make us proud!

Hayo yanatokea katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya filamu!Bila shaka ulifuatilia filamu za Kibira za Bongoland.Ukipenda unaweza kusema ule ulikuwa ni mwanzo tu.Wengine wamefuata nyayo hizo na wanakuja na filamu inayokwenda kwa jina la BABY POWDER. Ni watanzania wanaoishi jijini Atlanta,GA.

Filamu hii inatarajiwa kuonekana kwa mara ya kwanza kabisa ndani ya jiji la Atlanta lililopo jimboni Georgia nchini Marekani tarehe 14 November,2009.Baada ya hapo itaonyeshwa jijini Houston huko Texas tarehe 26 November,2009 na kisha jijini Washington,DC tarehe 5 December 2009. Baada ya hapo itakuwa zamu ya watu wa Minnesota kuiona tarehe 19 December 2009 kabla ya tour ya Europe na Africa haijaanza tarehe 25 December 2009. Tarehe na miji itakapoonyeshwa filamu hiyo zitatangazwa baadaye.

BABY POWDER ni filamu inayogusa maisha ya kweli . PHILIP NKASA (Lambert “LBT” Tibaigana) ni kijana wa kitanzania ambaye anakwenda Marekani kwa matumaini ya kupata elimu ili kuweza kuboresha maisha yake na ya familia yake nyumbani. Philip ananzaa maisha yake ndani ya Marekani katika mji mdogo wa Wichita,KS na baada ya kumaliza shule na kushindwa kupata kazi ,Philip anakata shauri kwenda kujaribu bahati yake katika jiji la Atlanta, GA.

Mambo hayawi kama Philip alivyotegemea.Upatikanaji wa kazi jijini Atlanta unakua wa shida.Ili kuendesha maisha Philip anachukua kazi ya malipo kidogo pamoja na kuwa tayari ni msomi mwenye shahada ya kwanza(degree)Hali ya maisha ya wazee wake inaendela kuwa mbaya kutokana na mapato yake kuwa kidogo na hivyo kushindwa kuwasaidia.

Tizama Trailer hapa;

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Baada ya kugundua mfanyakazi mwenzake Mamdo (Albert Levasseur) anafanya biashara haramu, Philip anaona hiyo ndio nafasi ya kutatua matatizo yake.Baada ya kuonja asali anachonga mzinga. Anaingia katika biashara  haramu kwa nguvu zote. (more…)

vinara-voting3-copybc

TUZO ZA
VINARA WA FILAMU 2009 KUWASHIRIKISHA WANANCHI

Mchakato wa kutafuta vinara wa filamu Tanzania kwa mwaka huu utawahusisha wananchi kupitia upigaji kura.

Wapenzi wa tasnia ya filamu nchini watapendekeza filamu ambazo wanaona zinastahili kuingia tuzo za vinara wa filamu. Mbali an wananchi pia kuna taasisi mbali mbali kama vile kampuni ya uhasibu inayotambulika kimataifa litasimamia zoezi la mapendekezo ya filamu. Filamu zenye kura nyingi ndizo zitakazoingia katika tuzo hizi. Pia filamu zitakubaliwa kutokana na mapendekezo ya waandaaji na majaji.

Kuteua filamu ni kwa njia ya ujumbe mfupi ambapo mpenzi atatakiwa kuandika neon vinara kasha jina la filamu anayoipenda na kutuma kwenda 15551 kwa gharama ya Tshs 300.

Vipengele vitakavyowaniwa mwaka huu katika tuzo za vinara ni Mwigizaji bora wa kiume na wa kike wa mwaka, Mwigizaji chipukizi wa kiume na wa kike, Filamu bora ya mwaka, Muongozaji bora wa Mwaka, Mwandishi bora wa filamu, Adui bora, Msanii bora msaidizi wa kiume na wa kike, Mhariri bora wa mwaka, Mtunza Sauti bora, Mtunza Mwanga bora, Mpiga picha bora wa mwaka, Mtayarishaji bora wa filamu, Mtunzi bora wa filamu, Mapambo na maleba bora, msanii maarufu wa kiume na kike na Tuzo ya heshima.

Vipengele vilivyoongezwa ni mtunza taa bora, mtayarishaji bora wa filamu (producer) na wasanii maarufu wa kike na wakiume (People’s choice Award).

Mwaka huu kampuni mbali mbali zimejitokeza kudhamini mashindano haya lakini yatatajwa baada ya upigaji kura

Filamu zinazostahili kupendekezwa ni zile zilizotengenezwa kuanzia januari 2009. Filamu zitakazo ingia moja kwa moja ni zile ambazo bado hazijaingia sokoni lakini yatawasilishwa na watengeza filamu wenyewe.

Zoezi la kupendekeza filamu litafanyika hadi septemba 30 kabla ya kupatikana wahusika kwenye kila kipengele kabla ya wananchi kupiga kura kuwapata washindi.

Khadija Khalili

Mratibu


Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page