
Fikra za Umoja wa Waafika zilianza kuzungumziwa na kuchipuka kupitia Marcus Garvey- mwanarahakati wa Kijamaika aliyewasisimua viogozi wa mwanzo wa bara, miaka ya 1920 na 1930 . Garvey huzungumziwa sana katika Muziki wa reggae wa akina Bob Marley, Peter Tosh na Bunny Wailer. Alifariki na kuzikwa London mwaka 1940.

Marcus Garvey
Lengo lake mwandishi na mpiganaji huyu lilikua kuwaunganisha weusi wote duniani na kutupa moyo wa kujipenda na kutoogopa asilia yetu.

fursa hizi kwa umoja na maendeleo ambapo TWENZETU, inakuwa neno rasmi la
mawasiliano.Kama vile haitoshi kutakuwepo na kampeni ya matembezi ya hisani ya harakati rasmi za vita dhidi ya uharamia
wa kazi za wasanii yatakayofanyika kesho,wabunifu na wavumbuzi mbalimbali, mseto wa shuguli mbalimbali
zitahusishwa ikiwemo semina ya fursa kwa
watanzania,burudani hadhara ya sanaa za kisasa na za kitamaduni,mpira, chakula
na bidhaa mbalimbali za kitanzania zitapatikana uwanja wa jamhuri mapema leo mchana.
Mkurugenzi wa MISA-TAN Bw. Tumaini Mwailenge akizungumza na waalikwa kwenye Gala Dinner ya kuadhimisha siku ya Uhuru wa habari Duniani iliyoenda sambamba na uzinduzi wa Mfuko wa Mwangosi utakao kuwa ukisaidia waandishi wa habari pindi wapatapo matatizo wakiwa kazini. Kushoto ni Mzee Kassim Mapili wa Mjomba waliosherehesha usiku huo kwa buradani ya aina yake.(Picha na Dewji Blog).
Baadhi ya Wanahabari walioshiriki kwenye Gala Dinner ya siku ya Uhuru wa Habari iliyoenda sambamba na Uzinduzi wa Mfuko wa Mwangosi kusaidia waandishi wa habari ambao wamepata matatizo wakiwa kazini.
Blogger Pamela Mollel (katikati) wa Jamii Blog ya jijini Arusha akibadilishana wanahabari wenzake Tonia Kasoni( kushoto) wa Radio 5 pamoja na Mhariri wa Sibuka TV wakati wa hafla hiyo.
Mjane wa Marehemu Daudi Mwangosi na mtoto wa mwisho wa marehemu wakati wa uzinduzi wa Mwangosi Fund utakaokuwa ukisaidia waandishi wa habari wanaopata majanga wakiwa kazini vile vile utaenda sambamba na Tuzo ya Mwandishi ambaye atakuwa amepata matatizo, misukosuko katika kutafuta habari za uchunguzi na Tuzo hiyo itakuwa ikitolewa kila mwaka Septemba 6 siku aliyokufa Daudi Mwangosi na mshindi wa Tuzo hizo atajinyakulia Milioni 10 zitakazotolewa na waendeshaji wa mfuko huu UTPC.
Mzee Kassim Mapili wa Mjomba Band akikung’uta gitaa wakati akipiga wimbo wa Mbaraka Mwishe” Njoo mjionee Morogoro”….wakati wa hafla ya kuchangisha fedha za mfuko wa Daudi Mwangosi zilizoenda sambamba na uzinduzi wa mfuko huo katika hoteli ya Kibo Palace jijini Arusha.
Katika maadhimisho ya siku ya siku ya uandishi wa Vitabu na Hati Miliki Duniani Afisa Habari wa Kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa (katika ngazi ya Kimataifa) UNIC Bi. Stella Vuzo akizungumza na wanafunzi wa shule mbalimbali waliohudhuria semina fupi iliyoandaliwa na UNIC na kuwafafanulia umuhimu wa kusoma vitabu mbalimbali ambapo wanaweza kujifunza mambo tofauti ikiwemo kujua takwimu za ugonjwa hatari wa Malaria hapa nchini ambao umekuwa ukiongoza kwa kusababisha vifo vya watoto wenye umri chiniya miaka 5, hivyo kwa usomaji vitabu wanaweza kujua namna ya kujikinga na wanapogundua dalili kuweza kuwahi kupata matibabu.
Wanafunzi wa darasa la Saba shule ya msingi Oysterbay wakimsikiliza kwa makini Afisa Habari wa UNIC (katika ngazi ya Kimataifa) Bi. Stella Vuzo (hayupo pichani) wakati akielezea kazi zinazofanywa na Shirika la Afya Duniani WHO lililochini ya Umoja wa Mataifa katika kuhakikisha Ugonjwa wa Malaria unatokomezwa duniani katika nchini za kusini mwa Jangwa la Sahara. Ikiwa zimebaki siku mbili kuadhimisha siku ya Malaria duniani inayodhimishwa kila mwaka Aprili 25 wakati wa siku ya kuadhimisha siku ya uandishi wa vitabu na hati miliki duniani.
Msaidizi wa Maktaba ya UNIC Harriet Macha akiendesha chemsha bongo kwa wanafunzi walioshiriki semina hiyo kupima uelewa wao kuhusiana na Ugonjwa wa Malaria.
Picha juu na chini ni Mgeni rasmi Mh. Mstahiki meya wa Halmashauri ya manispaa ya Ilala Mh. Jerry Silaa akizungumza wananchi pamoja na washiriki wakati wa bonanza la timu ya Stakishari Veterans FC kutimiza miaka 5 ambapo amesema mpira wa soka unawakutanisha watu na kuwasidia kujenga mahusiano pamoja na kujenga afya za miili yao.
Picha juu na chini Mgeni rasmi Mh. Mstahiki meya wa Halmashauri ya manispaa ya Ilala Mh. Jerry Silaa akikabidhi jezi na mipira kwa baadhi ya timu 17 zilizoshiriki katika bonanza hilo.
Diwani wa Kata ya Kipawa Mheshimiwa Bonna Kaluwa akigawa jezi na mipira kwa timu zilizoshiriki Bonanza la Stakishari Veterans kutimiza miaka 5.
Mgeni rasmi Mh. Mstahiki meya wa Halmashauri ya manispaa ya Ilala Mh. Jerry Silaa akijiandaa kupiga penati kuashiria ufunguzi wa Bonanza hilo lililofanyika katika viwanja vya Stakishari kata ya Gongo la Mboto jijini Dar.
Mstahiki Meya Jerry Silaa akionyesha ufundi na kufunga goli wakati akipiga penati ya kuzindua rasmi bonanza la Stakishari Veterans FC kutimiza miaka 5.
Mstahiki Meya Jerry Silaa akipongezwa na Golikipa aliyemfunga goli kwa penati wakati akizundua Bonanza hilo.
Mwenyekiti wa kundi la wake wa mabalozi nchini (DSG) Juliana Parroni akifungua mkutano wa wake wa mabalozi nchini “Coffee meeting” uliyofanyika katika ukumbi wa Synergy Grill Oysterbay jijini Dar es Salaam.(Picha na Zainul Mzige wa Mo Blog)
Mke wa Balozi wa Japani nchini Tanzania Bi. Keiko Okada (kulia) akimtambulisha aliyewahi kuwa Miss Tanzania (2008) ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Duka la bidhaa za Kiutamaduni zinazotengenezwa kwa Mikono na wanawake wa Kimasai – ENJIPAI Nasreen Karim aliyepata fursa ya kuonyesha kazi za mikono zinazotengenezwa na wanawake wa Kimasai walioko katika kampuni hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa duka la ENJIPAI Nasreen Karim (wa pili kulia) lilipo barabara ya Kaunda Drive Oysterbay jijini Dar es Salaam akielezea namna anavyofanya kazi zake za ubunifu wa bidhaa za shanga na kinamama wa Kimasai.
Sehemu ya wake wa Mabalozi nchini na wageni waalikwa wakipiga makofi baada ya kusikia Utambulisho wa kazi anazofanya Nasreen Karim Mkurugenzi Mkuu wa Duka la ENJIPAI.
Picha juu na chini wake wa mabalozi nchini katika Coffee meeting yao.
Nasreen Karim akizungumza na mmoja wa wageni waalikwa kutoka Umoja wa Ulaya.
Nasreen Karim akimvisha moja ya bidhaa za Shanga mmoja wa wageni waalikwa kutoka World Bank Bi. Sharon Mitchell aliyetokea kuvutiwa na kazi za mikono ya kinamama wa Kimasai wa duka la ENJIPAI.
Mkurugenzi Mkuu wa Duka la ENJIPAI Nasreen Karim akimvisha mkufu wa shanga mmoja wa wake wa mabalozi wakati wa maonyesho ya bidhaa zake kwenye Coffee meeting ya wake wa mabalozi nchini.
Mke wa Balozi wa Nigeria Bi. Naomi Majnabu (kushoto) na Mke wa Balozi wa Rwanda nchini Bi. Mary Rugangazi (katikati) wakimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa duka la ENJIPAI Nasreen Karim kwa kazi nzuri ya ujasiriamali anayofanya.
Nasreen Karim akifurahi jambo na Mke wa Balozi wa Misri wakati wa maonyesho ya bidhaa za duka la ENJIPAI yakiendelea.
Nasreen Karim katika picha ya kumbukumbu na wageni waalikwa.
Mkurugenzi Mkuu wa duka la ENJIPAI Nasreen Karim katika picha ya pamoja na baadhi ya kinamama wa Kimasai anaofanya nao kazi za kutengeneza bidhaa za shanga mara baada ya maonyesho hayo wakati wa Coffee meeting ya wake wa mabalozi.
Na. Mwandishi wetu
Wanawake wajasiria mali haswa wa fani ya vifaa vya urembo vya asili kama vile mikufu ya shanga na vinginevyo nchini Tanzania wametakiwa kujitangaza zaidi kimataifa kwa kushiriki maonyesho mbalimbali ili kuonyesha uwezo wao.
Akitoa rai hiyo wakati akimtambulisha kwa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya inayotengeneza bidhaa hizo ya Enjipai Bi. Nasreen Karim kwa niaba ya wake wa mabalozi hao, Mke wa Balozi wa Japan hapa Tanzania Keiko Okada amesema bidhaa hizo zinazo tengenezwa kwa shanga zinapendwa na zinahitaji kutangazwa kimataifa.
Wake wa mabalozi hao wamesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa mikutano yao ya kila mwezi maarufu kama ‘Coffe Meeting’, kuzungumzia miradi wanayoifanya ambapo kila wakati huwa wanaalika wajasiria mali tofauti na kwa wakati huu wamealika kampuni iliyokusanya akimama wa kimasai wanaotengeneza bidhaa tofauti za shanga ya’Enjipai’.
Enjipai ni kikundi kilichoanzishwa miaka miwili iliyopita chini ya Bi. Nasreen Karim na leo kupata mualiko kutoka kwa wake za mabalozi kuonyesha bidhaa wanazozitengeneza..
Akizungumza Mimi niko Nasreen Karim kama unavyojua kazi zetu ni kwa wawezesha wanawake kwa namna hiyo hivyo nitazungumza na wageni hawa kuwaonyesha bidhaa zetu na baadae tukimaliza watatambua wapi tunataka kuelekea na kudhibitisha kuwa tukiwezeshwa tunaweza.
Afisa Habari wa kampuni ya usafi ya Green Waste Pro ltd Vidah Fammie.
Baadhi ya Dust bin zinazomilikiwa na kampuni ya Green Waste Pro ltd. zilizowekwa katika baadhi ya mitaa ya Manispaa ya Ilala ambazo pia mteja yoyote anapohitaji huuzwa.
Na.Mwandishi wetu.
Wananchi wa jiji la Dar es Salaam hususan wakazi wa manispaa ya Ilala wametakiwa kutambua kuwa suala la usafi na kutunza mazingira ni jukumu la watu wote na sio tu la kampuni zilizopewa kandarasi ya kukusanya taka.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Afisa Habari wa kampuni ya usafi ya Green Waste Pro ltd iliyopewa dhamana ya kufanya usafi katika manispaa ya Ilala Vidah Fammie amesema katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku wanakabiliana na changamoto nyingi zikiwemo watu kutochangia katika ulipaji wa ada ya taka na pia kutolipa kwa muda muafaka.
Akiendelea kuzitaja changamoto hizo amesema pia wangependa wananchi watambua kuwa suala la dust bin, watu wamekuwa wakielewa vibaya kuwa wao ndio wanaopaswa kuzimbaza jambo ambalo sio kweli, kampuni ya usafi ya Green Waste Pro wanaziuza na hawamlazimishi mteja wao yeyote kununua, ila anaruhusiwa kununua pale anapopenda, na kuwa zile dust bin zinazowekwa mitaani wao wanapata usaidizi kutoka manispaa.
Pia ameshauri kwa wale ambao hawana dust bin watumie mifuko maalum ya kuweka taka na gari litakapopita litachukuwa kama ulivyo utaratibu wa suala la usafi.
Bi. Vidah Fammie ameongeza kuwa tatizo jingine wanalokabiliana nalo ni suala la upeo mdogo wa wananchi kuhusu suala la usafi.
Mwandishi wa habari hizi alipotaka ufafanuzi kuhusu suala hilo, amesema inaonekana wapo wananchi wanaoelewa suala zima la usafi lakini wanapuuzia na kuna wale wasio elewa kabisa hivyo mtu akiwa na taka anatupa tu kwa kuwa anajua kuna mkandarasi wa kufanya usafi kitu ambacho si sawa.
Kingine amesema ni miundo mbinu mibovu na hali ya hewa hivyo wakati mwingine kwa mfano gari maalum la kusafisha barabara linashindwa kufika hivyo inabidi kutumika nguvu za ziada kama vile vibajaji na vitu vingine.
First Vice-President of Zanzibar Seif Sharif Hamad, DoubleTree by Hilton Regional Director Mr.Judd Lehmann, Director of Sales, DoubleTree by Hilton Florenso Kirambata in a group photo with Sober House Members.
DoubleTree by Hilton Resort in Zanzibar announced their partnership with Sober House, a grass roots organisation in Zanzibar that supports the recovery of drug addicts and conducts community awareness and prevention.
DoubleTree by Hilton has partnered with Sober House with the aim to educate the children of Zanzibar on drug awareness and prevention.
The Sober House volunteers (many former drug addicts) will visit schools every month for the next two years and facilitate a workshop that allows the children to learn about the facts and ask questions in a safe, supported space.
Each child will receive a booklet that features a comic written by the Sober House residence as well as factual information that was approved earlier this year during a workshop hosted by DoubleTree with the Ministry of Education, The Drug Commission of Zanzibar and representatives from The Ministry of Health.
Director of Sales, DoubleTree by Hilton Florenso Kirambata said Sober House Founder Members, Suleiman Mauly and Fatma Juma should be applauded for their dedication and efforts.
Added that we are proud to empower Sober House by building their capacity to make a larger impact in the community.
DoubleTree by Hilton Regional Director Mr Judd Lehmann insisted that “we hope that our campaign throughout schools will encourage the children to say NO to drugs because they understand the consequences.”
Wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari jijini Dar zikiwemo Makongo, Airwing, Mtakuja Beach na Chang’ombe wakiwa Safarini Kulekea katika ziara ya kutembelea Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara ambayo yapo kwenye orodha ya urithi wa Dunia katika safari ya iliyoandaliwa na Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) wakati wa kumbukumbu ya Biashara ya Utumwa na kuwaenzi waliopoteza maisha katika biashara hiyo iliyokuwa imeshamiri katika maeneo hayo.
Biashara hiyo ya Watumwa ilifanyika kwa miaka 400 na kuhusisha zaidi ya Waafrika milioni 15 na watu wenye asili ya Afrika ambao walikuwa waathirika wa ukatili wa Utumwa na kuendelea kuteseka na madhara yaa biashara ya Utumwa.(Picha na Mo Blog.)
Kiongozi wa msafara huo Afisa Habari wa ngazi ya kimataifa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Stella Vuzo (wa tatu kushoto) njiani kuelekea Kilwa Kisiwani.
Afisa Habari wa ngazi ya kimataifa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Stella Vuzo akitoa mwongozo wa ziara kwa wanafunzi baada ya kufika katika bandari ya Kilwa kabla ya kuelekea Kilwa Kisiwani kwa ziara ya mafunzo ya kumbukumbu za biashara ya Utumwa.
Ambapo alisema lengo la ziara hiyo ni kutaka Wanafunzi kujifunza madhara ya biashara ya Utumwa jinsi ilivyofanyika na madhara yake na ili waweze kusaidia katika jitihada za kuitokomeza biashara hiyo ambayo mpaka sasa bado inaendelea kufanyika kimya kimya katika maeneo mbalimbali nchini na kuwataka kuzijua haki zao za kibinadamu na kutogeuzwa bidhaa za kuuzwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa udanganyifu wa kupelekwa kufanya kazi nchini za kigeni.
Mwl. Mwasi wa shule ya Sekondari Chang’ombe (mwenye nyekundu) akiwa ndani ya boti na wanafunzi kuelekea Kilwa Kisiwani.
Wanafunzi wakiwasili Kilwa Kisiwani.
Picha juu na chini’ Tour Giude’ Dullah akitoa malekezo ya ramani ya sehemu watakazotembelea wanafunzi hao ili kupata ufajamu wa jinsi Historia ya eneo hilo ilivyokuwa hadi kufikia biashara ya Utumwa na majengo yaliyokuwa yakitumika Karne ya 9 baada ya kuzaliwa Kristo.
Wanafunzi wakichukua maelezo muhimu kutoka kwa Mtaalamu wa masuala ya Historia ya Asali ya Kilwa Kiswani na Songo Mnara wakiwa kwenye makaburi waliyozikwa viongozi waliotawala eneo la Kilwa Kisiwani.
‘Tour Giude’ Dullah akiendelea kutoa ufafanuzi wa maeneo mbalimbali yaliyotumika enzi za biashara ya Utumwa ikiwemo Misikiti, Gereza na Nyumba ya Sultan Hassan Bin Sultan ambaye alikuwa mtawala wa eneo hilo.
Wanafunzi wakielekea kwenye Gereza maarufu lililokuwa likitumiwa na kufunga watumwa.
Muonekano wa Gereza hilo kwa Nje Lango Kuu la kuingia.
Mhifadhi Mambo ya Kale Kilwa Kisiwani Yussuph Bakari Said (mwenye shati la zambarau) akionyesha Kisima kilichokuwa kikitumiwa na wafungwa ndani ya Gereza hilo.
Wanafunzi wakiangalia Kisima kimoja wapo ndani Msikiti wakati huo.
Mmoja ya wananfunzi wa shule hizo walioitembelea maeneo hayo ya kumbukumbu akishangaa Mzinga uliodumu mpaka leo toka Karne ya 9 baada ya kuzaliwa Kristo.
Mafunzo yakiendelea kutolewa kwa wanafunzi hao.
Moja ya Majengo ya Nyumba ya Sultan Hassan Bin Sultan aliyeoa wanawake 77 enzi za utawala wake.
Mhifadhi Mambo ya Kale Kilwa Kisiwani Yussuph Bakari Said katika picha ya kumbukumbu na Afisa Habari wa ngazi ya kimataifa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Stella Vuzo aliyeambatana na Phillip Musiba pamoja na wanafunzi wa shule mbalimbali za jijini Dar es Salaam katika siku ya kuwakumbuka wahanga wa biashara ya Utumwa.
Wanafunzi wakisindikizwa na Afisa Habari wa ngazi ya kimataifa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Stella Vuzo (mwenye kitenge) kupanda boti kurudi Bandarini baada ya kuhitimisha ziara yao Kilwa Kiswani.
Afisa Habari wa ngazi ya kimataifa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Stella Vuzo aliyeambatana na mfanyakazi mwenzake Phillip Musiba, walimu waliojumuika na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kilwa katika ziara hiyo katika picha ya pamoja.




sending...











































































