MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Kila jambo lina mwisho wake. Kwa Bondia mkongwe na mahiri nchini Tanzania,Rashid Matumla au ukipenda “Snake Boy”, juzi ilikuwa ndio mwisho wake katika mchezo wa ndondi akiwa kama mchezaji.

Baada ya pambano lake na Bondia mwingine anayekuja juu katika mchezo huo,Mada Maugo,lililofanyikia katika Ukumbi wa PTA uliopo kwenye uwanja wa maonyesho wa Mwalimu Nyerere Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam, Matumla alitangaza kustaafu rasmi au kutundika “gloves” kama wenyewe wanavyosema.Katika pambano hilo,Matumla alipoteza kwa jumla ya pointi 98-95.Pambano hilo ambalo halikuwa la kuwania ubingwa wowote,lilikuwa la raundi kumi.

Matumla ambaye aliyewahi kufanya makubwa katika medani ya ngumi za kulipwa, alifikia hatua hiyo baada ya miaka kadhaa kushauriwa na wadau kadhaa akiwamo baba yake mzazi kuachana na mchezo huo kutokana na umri kumtupa mkono, bila mafanikio.

Rashid Matumla alizaliwa tarehe 16/5/1968 mkoani Tanga. Mpaka anastaafu na tangu aanze kupigana ngumi za kulipwa,ameshinda mapambano 40(kati ya hayo 30 kwa Knock Out) na ameshindwa katika mapambano 14(manne kati ya hayo alipigwa kwa KnockOut) na ametoka draw katika mapambano 2. Kwa ujumla amepambana katika raundi 373. Mpaka anastaafu katika ulimwengu wa ndondi za kulipwa katika uzito wa kati(Middle Weight),Matumla anashikilia nafasi ya 299 kati ya wanandondi 1107 wanaotambulika na walio active katika uzito huo.Kwa nchini Tanzania,amestaafu akiwa katika nafasi ya 5 miongoni mwa mabondia 29 wanaotambulika na ambao bado wapo active.Walio mbele yake ni Karama Nyilawila,Thomas Mashali,Mada Maugo, na Francis Cheka ambaye ndiye nambari 1 kwa hivi sasa nchini Tanzania.

Baada ya kustaafu Matumla amesema ushiriki wake katika mchezo huo namba mbili kwa kuwa na wapenzi wengi duniani nyuma ya soka,utakuwa katika nafasi ya ukocha.Amesema hivi sasa atajikita katika kuibua vipaji vya ndondi miongoni mwa vijana.

Tunamtakia Rashid Matumla au “Snake Boy” maisha mema katika kustaafu.

Dalili kwamba mashindano ya mwaka huu ya Kombe la Dunia yanayoendelea huko Afrika Kusini yanaweza kuwa machungu kupita yote kwa bara la Afrika yanaweza kuwa yameanza rasmi kuonekana hivi leo baada ya timu ya Taifa ya Cameroon,maarufu kama Indomitable Lions(Simba wasiofugika) kuwa timu ya kwanza kutolewa katika mashindano hayo.

Cameroon,timu ambayo ilikuwa miongoni mwa timu zilizokuwa zikitajwa kama “tumaini la Afrika”,imeyaaga mashindano hayo baada ya kufungwa jumla ya magoli 2-1 na Denmark.

Kwa maana hiyo kutoka kundi E,Uholanzi imejihakikishia kuendelea na mashindano(Best 16) huku Japan ikisubiri kuumana na Denmark katika mchezo ambao utaamua nani aendelee na nani atoke.Kutoka katika kila kundi timu mbili tu ndizo zinazoendelea.

Mwanaidi Hassan,akilia kilio cha furaha na kutoamini alipotangazwa kuwa Mwanamichezo Bora nchini Tanzania kwa mwaka uliopita wa 2009.Mwanaidi anacheza mchezo wa Netball.Anachezea timu ya JKT Mbweni na Timu ya Taifa ya Netball.Utoaji wa tuzo hizo ulifanyikia New Africa Hotel jijini Dar-es-salaam.

Mwanaidi Hassan(katikati) akikabidhiwa Tuzo ya Uanamichezo Bora na kitita cha shilingi Milioni Moja(1m Tshs).Anayemkabidhi ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania(BMT),Kanali Iddi Kipingu.Wanaoshuhudia pembeni,kutoka kulia kwenda kushoto ni David Nyombo,aliyechukua Ushindi wa Tatu kupitia mchezo wa kunyanyua vyuma vizito(body building),Juma Kaseja,aliyechukua ushindi wa pili kupitia mchezo wa Soka.Kaseja ni golikipa wa Simba Sports Club ya jijini Dar-es-salaam.Mwingine pichani ni Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari za Michezo(TASWA),Boniface Wambura.TASWA ndio waandaji wa tuzo hizo.

Juma Kaseja(kulia) akipokea Tuzo ya ushindi wa pili.Kaseja, golikipa nambari moja wa Simba.Anayemkabidhi ni Jaji Mark Bomani,Mwenyekiti wa Bodi wa Kampuni ya Serengeti ambao ndio wadhamini wakuu wa tuzo hizo.

David Nyombo,mnyanyua vyuma vizito,akikabidhiwa tuzo yake ya ushindi wa tatu.

Washindi wakiwa katika picha ya pamoja na wadhamini na wadau wa TASWA.

Picha zote na Richard Mwaikenda.

CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), leo kinatarajiwa kumtangaza mwanamichezo bora wa mwaka jana(2009) baada ya zoezi la kuwapigia kura wanamichezo waliofanya vema katika mwaka huo kukamilika jana.

Wanamichezo waliofanikiwa kuingia katika hatua ya fainali ni kipa mahiri wa Simba, Juma Kaseja, mfungaji mahiri wa timu ya netiboli ya Jeshi Stars, Mwanaidi Hassan na mtunisha misuli, David Nyombo. Kwa undani zaidi wa habarii hii bonyeza hapa.

David Nyombo

Juma Kaseja

Mwanaidi Hassan


Sijui wewe mwenzangu. Ukiniuliza mimi,mojawapo ya mambo ambayo najivunia sana kuwa nayo kama mtanzania ni suala zima la nchi yetu kuwa nchi ambayo imejaa wastaarabu na waungwana. Tunapingana kistaarabu. Tusipokubaliana katika mambo fulani fulani,tunaambiana kwa heshima. Tukishindwa kabisa kuelewana,tunapiga kura.Waache maadui zetu waifananishe hali hiyo na uzembe au ujinga.Shauri yao. Matunda yake tunayaona.

Ninachotaka kusema kinaweza kisiwe mfano hai au mfano muafaka zaidi.Pamoja nahayo naomba nikiseme. Ni kwamba nimependa uungawana,u-tanzania,uanamichezo na ustaarabu ulioonyeshwa na watanzania wakiongozwa na Rais Jakaya Kikwete kabla na hata baada ya mchezo wa soka kati ya timu yetu ya taifa(Taifa Stars) na Brazil. Hata yule jamaa aliyekimbilia uwanjani kumkumbatia mchezaji maarufu wa Brazil,Kaka,naamini alifanya vile kwa kuzidiwa tu na “mapenzi” na mchezo na mchezaji mwenyewe.

Pamoja na kufungwa jumla ya mabao 5-1, hatukukasirika. Tuliichukulia hali hiyo kama sehemu ya mchezo na nafasi ya kujifunza(hata kama matokeo siku za mbeleni yataonyesha kwamba hatukujifunza chochote,nafasi tumepata).Isitoshe,asiyekubali kushindwa,si….Kama unavyoona pichani, Rais wetu Jakaya Kikwete anaonekana akimkabidhi zawadi ya kinyago mchezaji timu ya taifa ya Brazil Kaka mara baada ya mchezo wao na Taifa Stars. Wametufunga lakini na zawadi za ukumbusho tumewapa.Kama sisi sio waungwana na wastaarabu,nani basi?

Bila shaka wa-Brazil hawa watakumbuka uungwana huu.I hope they remember this genuineand honesty hospitality. Hapo sijazungumzia tabasamu la Meneja Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa kampuni ya Bia ya Serengeti ambao ndiyo wadhamini wakuu wa Taifa Stars,pembeni. Ni tabasamu la kweli,lisilo na kinyongo cha kuchabangwa 5-1.After all,ulikuwa mchezo wa kirafiki.Tungekuwa tunashindania Kombe la Dunia,ah tungewafunga hawa! Au unasemaje?

Photo Credit/Full Shangwe

Kiungo mchezeshaji wa Timu ya Taifa ya Soka ya Ghana na klabu ya Chelsea ya Uingereza,Michael Essien(pichani), atazikosa fainali za Kombe la Dunia mwaka huu.

Kwa mujibu wa tovuti ya Chama cha Soka cha Ghana(GFA),kiungo huyo ambaye kwa muda sasa amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya goti,hatoweza kupona mpaka hapo mwishoni mwa mwezi wa saba(Julai) na hivyo kumaliza kabisa matumaini ya kuweza kucheza katika fainali hizo.

Uamuzi wa mwisho wa kumuondoa Essien katika kikosi cha Ghana(Black Stars) ulifikiwa na chama hicho cha soka kwa kushauriana kwa karibu na timu yake ya Chelsea pamoja na daktari wake na pia madaktari wa Timu ya Taifa ya Ghana.

Pamoja na kwamba hatocheza,habari zinazidi kupasha kwamba Michael Essien ataambatana na timu hiyo kwenda Afrika Kusini na kwamba atasaidia katika masuala mengine ya kiufundi.Ghana wapo kundi D pamoja na Ujerumani, Australia na Serbia. Wataingia uwanjani kwa mara ya kwanza tarehe 13 Juni kupambana na Serbia.

Hii ingekuwa mara ya pili kwa kiungo huyo kucheza katika fainali za Kombe la Dunia baada ya kufanya hivyo miaka minne iliyopita katika fainali zilizofanyikia nchini Ujerumani. Je,Ghana wataweza kufanya vizuri bila kiungo wao mahiri Michael Essien?

Taifa Stars

Brazil

Brazil are to play Tanzania on 7 June in a World Cup warm-up match ahead of this summer’s finals in South Africa.

The Brazilians have become the first non-African team to schedule a friendly in Africa in the build-up to the tournament, which kicks off on 11 June.

Tanzanian Football Federation (TFF) spokesman Florian Kaijage told BBC Sport that a contract would be signed within the next two to three days. For more information,click here.

Klabu ya Simba maarufu kama Watoto wa Msimbazi au Taifa Kubwa,wamepata mwenyekiti mpya wa klabu yao.Si mwingine bali ni Ismail Aden Rage(pichani) ambaye sio jina jipya katika medani ya soka nchini Tanzania. Aliwahi pia kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka nchini Tanzania katika zama ambazo ziligubikwa na rushwa na matumizi mabaya ya fedha kitu ambacho kilipelekea Rage kushtakiwa na kutiwa ndani.Kwa habari zaidi na picha kuhusu uchaguzi huu bonyeza hapa.

When the news surfaced that, Hasheem Thabeet, is headed to the Development League (D-League), the reaction among Tanzanians especially the users of social networks such as Facebook and blogs were overwhelming. I guess the big question in lots of folk’s minds was; what is a D-League? Does it suggest that he is no longer going to be playing in the usual NBA league? Well, it depends on a lot of things. You can read more about the D-League and its implications or benefits to Hasheem career by clicking here and also here.

The social networks such as Facebook and blogs were immediately stuffed with comments and opinions. Some were wishing him a “quick comeback “to the NBA, while some couldn’t hesitate to throw jabs on him in the sentiment of “we told you”.

I guess the news was “worth the talk”, because not only Hasheem is the first Tanzanian ever to play in the NBA, but also the highest draft pick ever to go to the D-League. Thabeet, who has played sparingly in his rookie season, averaging 2.5 points in 10.3 minutes over 50 games, has been optioned to the Dakota Wizards. He made his debut yesterday when Dakota Wizards played Erie Bayhawks. Dakota Wizards won 108-103.

Before his debut in the D-League, I had caught up with Hasheem with only one question in my mind; about his reaction following the demotion to the D-League. This is how it went;

BC: Hasheem, what is your reaction to this whole thing of moving to the D-League?

HASHEEM THABEET: My reaction about D-League…Uhmmm… well I’m excited to participate in the D-League. I’m looking forward to playing and maximizing this opportunity to be on court and use the skills that I have developed thus far rather than to be on the bench.

Right now the key for me is consistency court time as I am still learning the Pro Game. I know Coach Hollins has my best interest at heart so I’m happy with his decision which I believe is to make sure that I stay active.

Now I know this is the time for the haters and all the doubters to talk and say whatever they have because they have been waiting to bring me down for a minute. So it’s my downtime and I promise I’m not backing back. It’s a new saga that has started. Plus I’m still be getting the same cheque… it’s not like they are not gonna pay me the usual. So I’m still good and soon I’ll be back!!! And oh by the way, I’m only going there for 6 games. So I will be back sooner than they are thinking.

**BC would like to wish Hasheem all the best in the D-League and eventually his return to the NBA.

TigerMcheza golf maarufu,Tiger Woods,33 amepata ajali na kuumia karibu na nyumbani kwake huko Windermere,Florida. Tiger alikuwa akiendesha gari lake aina ya 2009 Cadillac SUV ambapo aligonga fire hydrant kabla ya kuuvaa mti uliokuwa pembeni.Ilikuwa mida ya saa nane na dakika ishirini na tano alfajiri. Ilibidi mke wake atumie golf club kupasua kioo cha nyuma cha gari la Tiger ili kumtoa. Mke wake alisikia mlio wa ajali kwani na kukimbilia nje kwani ajali ilitokea karibu kabisa na nyumbani kwa star huyo wa mchezo wa golf duniani.

Hata hivyo tofauti na habari zilizokuwa zimeenea hapo mwanzo,Tiger hakuumia sana katika ajali hiyo mbali ya kupata michubuko kadhaa usoni. Ametibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani kwake. Tovuti yake imeielezea ajali ya Tiger kuwa “ndogo”.

Historia ya Tiger Woods katika michezo ni miongoni mwa historia zenye mvuto wa aina yake.Kwa mujibu wa tovuti yake,ameshashinda zaidi ya mashindano 93. Aliweka historia ya kuwa kijana mdogo zaidi kushinda taji maarufu la Masters.Alikuwa na umri wa miaka 21. Tiger amesomea Chuo Kikuu cha Stanford.Alifundishwa kucheza mchezo wa golf na baba yake mzazi,Earl.Baba yake alikuwa mwanajeshi,mmarekani mweusi wakati mama yake ana asili ya Thailand.Mwaka jana Tiger Woods alitajwa kuwa mwanamichezo aliyelipwa zaidi akiwa amekusanya jumla ya dola milioni 110 kutoka katika michezo na matangazo ya biashara.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page