Mwimbaji nguli wa muziki wa tarabu nchini Tanzania Fatma binti Baraka, maarufu kama Bi Kidude amefariki Jumatano kisiwani Zanzibar akiwa na umri wa zaidi ya miaka 100.
Taarifa ya kifo chake ilitolewa na mjukuu wake Fatuma Baraka ambaye pia ni muimbaji wa Taraabu. Alisema Bi Kidude alifariki hospitalini kutokana na maradhi ya kisukari na uvimbe kwenye Kongosho.
Bi Kidude amekuwa katika fani ya muziki wa taarab ya kiasili pamoja na ngoma za unyago kwa zaidi ya robo tatu ya umri wake.
Katika miaka ya karibuni afya yake imekuwa ikizorota kiasi cha serikali ya Zanzibar kumzuia kupanda majukwaani kuburudisha japokuwa alionekana katika tamasha la Sauti za Busara mwezi Februari mwaka huu.
Mipango ya mazishi ya nguli huyu inafanywa nyumbani kwake Zanzibar.
Wengi, hasa vijana wa kizazi kipya wanamfahamu Bi. Kidude kwa uwezo wake mkubwa wa kuimba taarabu kwa kuchanganya lugha ya kiswahili na ile ya kiarabu. Nyimbo zake za kiarabu mara nyingi zimekuwa na ladha kama ile ya aliyekuwa mwimbaji gwiji wa Misri Ummu Kulthumu.
Sio uimbaji tu uliomfikisha Bi. Kidude alipofika, bali uwezo wake pia wa kutunga mashairi, kutumia ala za mziki kama vile kupiga ngoma na hata ngoma za unyago, vyote hivi vilimuweka Bi. Kidude katika nafasi tofauti katika jamii.
Alikuwa na tabia ya kumwita kila mtu ‘mwanangu,’ ingawa yeye mwenyewe hakubahatika kupata mtoto. Katika mahojiano aliyofanyiwa na vyombo mbali mbali vya habari, mwenyewe alisikika akisema, ingawa alikuwa na hamu ya kupata mtoto, lakini Mwenyezi Mungu hakumjaalia.
Katika miaka ya hivi karibuni, Bi. Kidude alishirikishwa sana na wasanii wengine katika kazi zao. Miongoni mwao ni Ahmada Amelewa, Fid Q Juhudi za Wasiojiweza.
Mbali na hayo, mashirika mbali mbali yakiwemo ya kibiashara na yale yasiyo ya kiserikali yaliona mvuto aliokuwa nao Bi. Kidude katika jamii, hivyo wakamtumia katika matangazo mbali mbali maarufu likiwa lile la kutokemeza Malaria.
Ni bibi aliyebahatika kusafiri takriban duniani kote, na vilevile katika maisha yake alijinyakulia tuzo lukuki. Miongoni mwa hizo ni ile ya 2005 WOMEX ikiwa ni kutambua mchango wake mkubwa katika tasnia ya muziki.
Katika siku zake za mwisho, Bi. Kidude alikuwa akiumwa, lakini wengi wanahusisha kuumwa kwake na utu uzima aliokuwa nao.
Kifo chake ni pigo kubwa kwa wote, lakini zaidi ni wanamziki wa kizazi kipya waliokuwa wakimuona Bi. Kidude ni nyanya yao.
Direct Source: BBC Swahili
Taarifa zilizopatikana jioni ya leo zinaeleza kuwa aliyewahi kuwa muigizaji katika kikundi cha Kaole,(pichani enzi za uhai wake) ,aliyekuwa akitambulika kwa jina la Mlopelo amefariki dunia mapema leo Hospitali ya Temeke,jijini Dar-es-salaam.
Kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa marehemu wameitonya kupitia Blog ya Jiachie, taarifa zinapasha kuwa Marehemu Mlopelo amefariki mchana wa leo kwenye hospitali ya Temeke mapema mchana wa leo, na kwamba shughuli zote za Msiba zipo nyumbani kwao Temeke Wailess mtaa wa Boko
Imeelezwa kuwa mazishi yake yatafanyika mapema kesho saa nne..Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi-Amen.
BC inaungana na watanzania wote na hususani wapenzi wa sanaa ya uigizaji kutoa pole nyingi kwa ndugu,jamaa na marafiki popote pale walipo.
Familia ya Bwana na Bibi Fredrick Kaduma wa Kimara-Dar-es-salaam,Tanzania na watanzania waishio Toronto,Canada wanasikitika kutangaza kifo cha mpendwa wao, Ritha Kaduma (Fatima) (pichani) kilichotokea hapo jana tarehe 9th August, 2012 huko Toronto,Canada.Fatuma au Rita amefikwa na mauti katika hospitali ya St.Michael’s ya Toronto alipokuwa amelazwa kwa muda mfupi.
Taratibu na mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda nyumbani Tanzania kwa mazishi zinafanyika nyumbani kwa marehemu alipokuwa akiishi na kaka yake huko huko Toronto,Canada.
Ukiwa kama mtanzania,ndugu,jamaa au rafiki,popote pale ulipo, unaombwa kuchangia fedha,hali na mali kwa ajili ya kuwezesha kuusafirisha mwili wa marehemu kurudi nyumbani kwa mazishi mapema kadri iwezekanavyo kwani kama wengi wenu mnavyofahamu, mwili unavyozidi kukaa Funeral-Home,gharama ndivyo zinavyozidi kuongezeka.
Mwili utasafirishwa punde tu zitakapopatikana fedha za kutosha kwa ajili ya kulipia gharama husika. Gharama zimekadiriwa kufikia kiasi cha $24,000 ambazo zinajumuisha kuutayarisha mwili,kuutunza na kuuhifadhi na pia kuusafirisha mpaka nyumbani Tanzania.
Unaweza kutuma mchango wako kwenye Account maalumu ya wafiwa kama ifuatavyo:
BANK : RBC (Royal Bank of Canada)
ACCOUNT NUMBER: 5122551
TRANSIT NUMBER: 06742
INSTITUTE NUMBER: 003
SWIFT CODE: L0YCCAT2
Vilevile unaweza kutumia E-mail Money Transfer kwenye anuani pepe gilfa36@hotmail.com .Pia unaweza kuwakilisha msaada wako kwa kutumia anuani hii:
5-7 DRIFTWOOD CRESCENT
NORTH YORK,ONTARIO
M3N 2R1
Kwa mawasiliano zaidi unaweza kuwasiliana na wafuatao:
Kaka yake Fatuma (Issa) kwa nambari hii-647-760-1051.
Flora- 647-622-6361
Emmanuel -416-835-6778.
Gabriel- 416-631-7762.
Kwa upande wa nyumbani Tanzania,tafadhali wasiliana na Fred Kaduma kupitia nambari 0655-888268 kwa taarifa zaidi.
Tafadhali chukua muda kuwafariji na kuwaombea ndugu,jamaa na marafiki waliofikwa na msiba huu. Tunatanguliza shukrani kwa misaada yote iliyotolewa na itakayotolewa. Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Amen.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete,jana mchana aliwaongoza viongozi mbalimbali wa serikali na maelfu ya wananchi katika mazishi ya aliyekuwa mnajimu maarufu Afrika Mashariki na Kati,Sheikh Yahya Hussein aliyefariki juzi kutokana na maradhi ya moyo.
Mbali na Rais Kikwete,viongozi wengine wa vyama mbalimbali vya siasa nchini wakiwemo Freeman Mbowe(Mwenyekiti-CHADEMA),John Cheyo(Mwenyekiti-UDP),Prof.Ibrahim Lipumba(Mwenyekiti-CUF) pia walihudhuria mazishi hayo yaliyofanyikia katika makaburi ya Tambaza jijini Dar-es-salaam. Kabla ya hapo dua ya kumuombea ilifanyika katika msikiti wa Manyema.Amefariki akiwa na umri wa miaka 79.Hizi hapa ni baadhi ya picha

Rais Kikwete akitia mchanga katika kaburi la Sheikh Yahya Hussein hapo jana.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lililobeba mwili wa Sheikh Yahya Hussein tayari kwa mazishi.

Baadhi ya wanafunzi wa Sheikh Yahya Hussein wakishiriki katika shughuli nzima ya mazishi yake nyumbani kwake Magomeni Mikumi.

Makamu wa Rais,Dr.Gharib Bilal alikuwa ni miongoni mwa viongozi mbalimbali wa serikali walioshiriki shughuli ya mazishi ya Sheikh Yahya.Pichani ni Dr.Gharib akimfariji mjane wa marehemu,Kate Yahya Hussein,nyumbani kwao Magomeni Mikumi jijini Dar-es-salaam.

SEASONED and veteran journalist, Adam Lusekelo (54) passed away while being rushed to Muhimbili National Hospital (MNH) on Thursday night, his wife Scolastica Lusekelo, said.
Ms Lusekelo said the deceased’s health deteriorated on Thursday night when relatives rushed him to MNH.
“He didn’t even reach the hospital, he breathed his last on the way at around 11pm,” Ms Lusekelo said. The ‘Sunday News’ columnist has been battling diabetes for a long time and was surviving on medication.
“Oh, no! We have lost a ‘Sunday News’ readers’ favourite,” lamented the newspaper’s Editor, Ichikaeli Maro upon receiving news of Mr Lusekelo’s death.
His column, a unique blend of writing serious issues of national importance with a soft touch, won many hearts and souls.
“My husband will miss him badly, he was his favourite columnist,” said Joyce Sabuni, Tanzania Standard Newspapers employee in the circulation section.
TSN Acting Managing Editor, Mkumbwa Ally also mourned the death of one of journalism’s most gifted writers. Burial arrangements are being made at his home at Ubungo Maziwa, but the body is likely to be transported to his home region of Rungwe in Mbeya, his wife said.
The late Lusekelo is survived by a wife and three children, two daughters and a son. He worked with TSN briefly in the 1980s before joining BBC as a correspondent based in Dar es Salaam.
News Source: Daily News
Photo Courtesy of Da Chemi @ Swahili Time
Adam was also a Blogger.Click Here to Check his Blog.His last post was 14th December,2010
THIS IS NOT APRIL FOOL’s PRANK.BC has confirmed.
Kama mnavyojua wenzetu wa Gongo la Mboto na maeneo mengine ya jiji la Dar-es-salaam walipatwa na janga la mabomu yaliyolipuka kutoka katika ghala nambari 5 la Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ)
Ni tukio la kusikitisha ambalo bado linatatiza wengi.Katika kuonyesha mshikamano na wote walioathirika,CEO wa Tongwe Records “Jay Murder” alijiwa na wazo la kuwaunganisha wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya ili kutengeneza wimbo ambao sio tu ni kama rambirambi kwa wote waliopoteza maisha au kuondokewa na ndugu,jamaa na marafiki bali pia kuelezea mambo kadhaa waliyonayo kama wasanii(kioo cha jamii).
Matokeo ya mkusanyiko huo wa wasanii ni wimbo uliopewa jina Toa Ndugu.Usikilize hapa.The Song was Produced By J-Ryder From Tongwe Records. To Know More About This Song, Contact Fid Q (Main Speaker of The Song)
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Mpangilio wa wasanii walioshiriki katika wimbo huu ni kama ifuatavyo;
Verse 1
Banana Zorro, G – Nako, Adam Mchomvu, Barnaba, Dj Fetty.
Chorus (Nurueli)
Verse 2
Cyrill, R.O.M.A, Domokaya, Jos Mtambo, Lord Eyez, Chege.
Chorus (Nurueli)
Verse 3
C Pwa, Ncha Kali, Bwana Misosi, Papaya, Darasa.
Chorus (Nurueli)
Verse 4
Anna, Soprano, Amini, Ditto.
Chorus (Nurueli)
Outro (Fid Q)
God Bless Tanzania, Bless Gongo La Mboto, and Bless Tongwe Records.

Kwa niaba ya Tanzanian Canadian Association (TCA), chama cha jumuiya ya Watanzania tunaoishi Toronto , Ontario , Canada na vitongoji vyake, tunapenda kuchukua fursa hii kwanza kabisa, kutoa rambirambi zetu kwa familia za wananchi waliopoteza wapendwa wao katika ajali ya mabomu yaliyolipuka katika kambi ya jeshi eneo la Gongo La Mboto, Dar-es- Salaam , Tanzania .
Tunawaombea wote waliopoteza maisha yao Mwenyezi Mungu awapumzishe kwa amani; tunawatakia majeruhi waugue pole, wapone haraka ili waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku. Vilevile, tunawatakia wote waliopotezana na ndugu zao hususan watoto waliopotezana na wazazi wao waweze kupatikana na kukutana tena.
Tumesikitishwa na taarifa za maafa hayo na kuhuzunishwa kuona kwamba ni mara ya pili tukio kama hili linatokea nchini kwetu. Wengi watakumbuka siku si nyingi janga kama hili lilitokea kule Mbagala. Tunapenda kuuomba uongozi wa jeshi uangalie upya namna silaha kali zinavyohifadhiwa; katika utaratibu wa kuhifadhi mabomu, tunapendekeza yafanyike marejeo na marekebisho yatakayozingatia usalama wa raia.
Katika kuhitimisha, tunalisisitizia Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), lichukue hatua madhubuti na za haraka katika kuhakikisha majanga yanayoweza kuepukika kama haya hayatokei tena.
Mungu Ibariki Tanzania .
Uongozi – Tanzanian Canadian Association (TCA)

Familia ya marehemu mwalimu Julius Banzi wa Mafiga Morogoro, inasikitika kuwatangazia msiba wa Mwalimu Innocentia Banzi kilichotokea alfajiri ya tarehe 12/01/2011 Dar-es-salaam-Tanzania.
Marehemu ni mama wa:
Dennis Londo wa Helsinki-Finland; Esther Londo na Walonzi Tatala wa Tampere-Finland;
Michael Gomela wa Reading-United Kingdom; Daniel Mtebe wa Stockholm-Sweden.
Habari za msiba huu ziwafikie wakuu wa shule zote za sekondari Tanzania, walimu na wanafunzi wa Kilakala sekondari, Morogoro sekondari na Masanze sekondari. Pia ziwafikie wanachama wote wa chama cha msalaba mwekundu Tanzania; wanachama wote wa chama cha maskauti Tanzania na wanamichezo wote wa Mkoa wa Morogoro.
Mazishi yanatarajiwa kufanyika Morogoro mara tu watoto wa marehemu watakapowasili.
Wale wote ambao mpo Finland msiba upo:
Lautamiehentie
2B 39 Vantaa (kwa maelezo zaidi piga simu 050 4863508, 040 5892123, 040 3750820)
Tanzania upo nyumbani kwa marehemu Mafiga-Morogoro, na Dar-es-salaam upo Mbezi Luis-njia panda ya kwenda Makabe (ulizia kwa Kunambi) Kwa maelezo zaidi piga simu namba: +255 732201098, +255 717365676, +255 713233843
One of the Tanzanian and African music legend,Dr.Remmy Ongala,is gone.He was laid to rest this afternoon in Sinza-Dar-es-salaam. Here are some of the photos from the farewell ceremony that took place at the Biafra Grounds in Dar-es-salaam.Rest in Peace Dr.Remmy Ongala.

10th February 1947-12th December 2010

Sehemu ya umati wa watu waliojitokeza kumuaga Dr.Remmy

Mjane wa Marehemu,watoto na wajukuu

Mtoto wa marehemu mwanasoka Kali Ongala akitoa heshima za mwisho kwa baba yake.

Baadhi ya viongozi wakitoa heshima zao.Wanaoonekana hapo ni John Mnyika,Mbunge wa Ubungo na Iddi Azan-Mbunge wa Kinondoni.

Waziri wa Utamaduni,Vijana na Michezo,Dr.Emmanuel Nchimbi akitoa heshima zake.

Mzee Makassy,mjomba wa marehemu ambaye ndiye alimshawishi Dr.Remmy kuja Tanzania akitokea DRC. 




sending...














