<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>BongoCelebrity &#187; Mtandao</title>
	<atom:link href="http://www.bongocelebrity.com/category/mtandao/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://www.bongocelebrity.com</link>
	<description></description>
	<lastBuildDate>Wed, 08 Feb 2012 14:28:26 +0000</lastBuildDate>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
	<generator>http://wordpress.org/?v=3.3.1</generator>
		<item>
		<title>ANSBERT NGURUMO ANAPOJADILI BLOGS</title>
		<link>http://www.bongocelebrity.com/2009/01/18/ansbert-ngurumo-anapojadili-blogs/</link>
		<comments>http://www.bongocelebrity.com/2009/01/18/ansbert-ngurumo-anapojadili-blogs/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 18 Jan 2009 18:50:01 +0000</pubDate>
		<dc:creator>bongocelebrity</dc:creator>
				<category><![CDATA[Blogging]]></category>
		<category><![CDATA[Blogs]]></category>
		<category><![CDATA[Mtandao]]></category>
		<category><![CDATA[Uandishi]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://bongocelebrity.wordpress.com/2009/01/17/ansbert-ngurumo-anapojadili-blogs/</guid>
		<description><![CDATA[Jina la Ansbert Ngurumo sio geni hata kidogo miongoni mwa wapenda habari na mawasiliano na hususani wapenzi wa habari za magazetini. Ansbert ni miongoni mwa waandishi wa habari mahiri nchini Tanzania ambao wamejijengea sifa na heshima kutokana na kazi zao za uandishi wa habari. Safu yake ya Maswali Magumu,inayochapishwa katika gazeti la Tanzania Daima kila [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><span style="font-family:Verdana;font-size:9pt;"><img class="size-full wp-image-2822 alignleft" title="ansbert-ngurumobc" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2009/01/ansbert-ngurumobc.jpg" alt="ansbert-ngurumobc" width="209" height="314" />Jina la <strong>Ansbert Ngurumo</strong> sio geni hata kidogo miongoni mwa wapenda habari na mawasiliano na hususani wapenzi wa habari za magazetini. Ansbert ni miongoni mwa waandishi wa habari mahiri nchini Tanzania ambao wamejijengea sifa na heshima kutokana na kazi zao za uandishi wa habari.<br />
</span></p>
<p><span style="font-family:Verdana;font-size:9pt;">Safu yake ya Maswali Magumu,inayochapishwa katika gazeti la <a href="http://www.freemedia.co.tz/" target="_blank">Tanzania Daima</a> kila jumapili inabakia kuwa safu yenye wasomaji lukuki huku kila mara ikizua mijadala ya aina yake jambo ambalo ni uthibitisho kwamba sio tu inapendwa bali pia hujibu na pia kuuliza Maswali Magumu.<br />
</span></p>
<p><span style="font-family:Verdana;font-size:9pt;">Ansbert ni blogger mzoefu pia.<a href="http://www.ngurumo.blogspot.com/" target="_blank">Blog yake</a> ambayo inaongozwa na kichwa cha habari, <a href="http://www.ngurumo.blogspot.com/" target="_blank"><strong>Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua</strong></a>, ni sehemu mojawapo nzuri ambapo unaweza kukuta kazi zake za uandishi,mitizamo na pia mikingamo.<br />
</span></p>
<p><span style="font-family:Verdana;font-size:9pt;">Hivi karibuni,jamaa wa mtandao wa <a href="http://www.rap21.org/rubrique163.html" target="_blank">Rap21</a>,walifanya naye mahojiano ambayo kwa kila hali ni &#8220;must read&#8221; kwa mtu yeyote ambaye yupo kwenye fani ya ku-blog au ni mfuatiliaji wa maendeleo ya tekinolojia hii ambayo mimi naiita mapinduzi ya karne katika ulimwengu wa habari na mawasiliano.<br />
</span></p>
<p><span style="font-family:Verdana;font-size:9pt;">Katika <a href="http://www.rap21.org/article20075.html">mahojiano hayo</a>,Ansbert ameongelea kwa mapana jinsi ambavyo blogs,ikiwemo ya kwake, zinazidi kuboresha mapinduzi hayo na pia jinsi gani blogs zinaweza kutumika katika kuboresha maisha ya wanajamii,kutunza historia zetu,kufichua maovu nk.<a href="http://www.rap21.org/article20075.html" target="_blank"><strong>Bonyeza hapa</strong></a> ili kusoma mahojiano hayo.<br />
</span></p>
<!-- Start Sociable --><div class="sociable"><div class="sociable_tagline"><a class='sociable_tagline' target='_blank' href='http://blogplay.com' style='color:#333333;text-decoration:none'>Be Sociable, Share!</a></div><ul class='clearfix'><li><a title="Twitter" class="option1_32" style="background-position:-288px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://twitter.com/intent/tweet?text=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS%20-%20http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F%20(via%20@sociablesite)"></a></li><li><a title="Facebook" class="option1_32" style="background-position:-96px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.facebook.com/share.php?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;t=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS"></a></li><li><a title="email" class="option1_32" style="background-position:-160px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="https://mail.google.com/mail/?view=cm&fs=1&to&su=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS&body=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&ui=2&tf=1&shva=1"></a></li><li><a class="option1_32" style="cursor:pointer;background-position:-128px 0px" rel="nofollow" title="Add to favorites - doesn't work in Chrome"  onClick="javascript:AddToFavorites();"></a></li><li><a title="StumbleUpon" class="option1_32" style="background-position:-224px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.stumbleupon.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&title=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS"></a></li><li><a title="Delicious" class="option1_32" style="background-position:-32px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://delicious.com/post?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;title=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS&amp;notes=Jina%20la%20Ansbert%20Ngurumo%20sio%20geni%20hata%20kidogo%20miongoni%20mwa%20wapenda%20habari%20na%20mawasiliano%20na%20hususani%20wapenzi%20wa%20habari%20za%20magazetini.%20Ansbert%20ni%20miongoni%20mwa%20waandishi%20wa%20habari%20mahiri%20nchini%20Tanzania%20ambao%20wamejijengea%20sifa%20na%20heshima%20kutokana%20na%20kaz"></a></li><li><a title="Google Reader" class="option1_32" style="background-position:-224px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/reader/link?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;title=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS&amp;srcURL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;srcTitle=BongoCelebrity+"></a></li><li><a title="LinkedIn" class="option1_32" style="background-position:-288px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.linkedin.com/shareArticle?mini=true&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;title=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS&amp;source=BongoCelebrity+&amp;summary=Jina%20la%20Ansbert%20Ngurumo%20sio%20geni%20hata%20kidogo%20miongoni%20mwa%20wapenda%20habari%20na%20mawasiliano%20na%20hususani%20wapenzi%20wa%20habari%20za%20magazetini.%20Ansbert%20ni%20miongoni%20mwa%20waandishi%20wa%20habari%20mahiri%20nchini%20Tanzania%20ambao%20wamejijengea%20sifa%20na%20heshima%20kutokana%20na%20kaz"></a></li><li><a title="BlinkList" class="option1_32" style="background-position:0px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.blinklist.com/index.php?Action=Blink/addblink.php&amp;Url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;Title=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS"></a></li><li><a style="cursor:pointer" rel="nofollow" onMouseOut="fixOnMouseOut(document.getElementById('sociable-post-2820'), event, 'post-2820')" onMouseOver="more(this,'post-2820')"><img style='margin-top:9px' src='http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/more.png'></a></li></ul><div onMouseout="fixOnMouseOut(this,event,'post-2820')" id="sociable-post-2820" style="display:none;">   

    <div style="top: auto; left: auto; display: block;" id="sociable">



		<div class="popup">

			<div class="content">

				<ul><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Myspace" class="option1_32" style="background-position:0px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.myspace.com/Modules/PostTo/Pages/?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;t=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Digg" class="option1_32" style="background-position:-64px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://digg.com/submit?phase=2&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;title=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS&amp;bodytext=Jina%20la%20Ansbert%20Ngurumo%20sio%20geni%20hata%20kidogo%20miongoni%20mwa%20wapenda%20habari%20na%20mawasiliano%20na%20hususani%20wapenzi%20wa%20habari%20za%20magazetini.%20Ansbert%20ni%20miongoni%20mwa%20waandishi%20wa%20habari%20mahiri%20nchini%20Tanzania%20ambao%20wamejijengea%20sifa%20na%20heshima%20kutokana%20na%20kaz"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Reddit" class="option1_32" style="background-position:-128px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reddit.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;title=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Google Bookmarks" class="option1_32" style="background-position:-192px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/bookmarks/mark?op=edit&amp;bkmk=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;title=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS&amp;annotation=Jina%20la%20Ansbert%20Ngurumo%20sio%20geni%20hata%20kidogo%20miongoni%20mwa%20wapenda%20habari%20na%20mawasiliano%20na%20hususani%20wapenzi%20wa%20habari%20za%20magazetini.%20Ansbert%20ni%20miongoni%20mwa%20waandishi%20wa%20habari%20mahiri%20nchini%20Tanzania%20ambao%20wamejijengea%20sifa%20na%20heshima%20kutokana%20na%20kaz"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="HackerNews" class="option1_32" style="background-position:-256px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://news.ycombinator.com/submitlink?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;t=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="MSNReporter" class="option1_32" style="background-position:-352px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reporter.es.msn.com/?fn=contribute&amp;Title=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS&amp;URL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;cat_id=6&amp;tag_id=31&amp;Remark=Jina%20la%20Ansbert%20Ngurumo%20sio%20geni%20hata%20kidogo%20miongoni%20mwa%20wapenda%20habari%20na%20mawasiliano%20na%20hususani%20wapenzi%20wa%20habari%20za%20magazetini.%20Ansbert%20ni%20miongoni%20mwa%20waandishi%20wa%20habari%20mahiri%20nchini%20Tanzania%20ambao%20wamejijengea%20sifa%20na%20heshima%20kutokana%20na%20kaz"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Sphinn" class="option1_32" style="background-position:-192px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://sphinn.com/index.php?c=post&amp;m=submit&amp;link=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Posterous" class="option1_32" style="background-position:-64px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://posterous.com/share?linkto=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;title=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS&amp;selection=Jina%20la%20Ansbert%20Ngurumo%20sio%20geni%20hata%20kidogo%20miongoni%20mwa%20wapenda%20habari%20na%20mawasiliano%20na%20hususani%20wapenzi%20wa%20habari%20za%20magazetini.%20Ansbert%20ni%20miongoni%20mwa%20waandishi%20wa%20habari%20mahiri%20nchini%20Tanzania%20ambao%20wamejijengea%20sifa%20na%20heshima%20kutokana%20na%20kaz"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Tumblr" class="option1_32" style="background-position:-256px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.tumblr.com/share?v=3&amp;u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2009%2F01%2F18%2Fansbert-ngurumo-anapojadili-blogs%2F&amp;t=ANSBERT%20NGURUMO%20ANAPOJADILI%20BLOGS&amp;s=Jina%20la%20Ansbert%20Ngurumo%20sio%20geni%20hata%20kidogo%20miongoni%20mwa%20wapenda%20habari%20na%20mawasiliano%20na%20hususani%20wapenzi%20wa%20habari%20za%20magazetini.%20Ansbert%20ni%20miongoni%20mwa%20waandishi%20wa%20habari%20mahiri%20nchini%20Tanzania%20ambao%20wamejijengea%20sifa%20na%20heshima%20kutokana%20na%20kaz"></a></li></ul>			

			</div>        

		  <a style="cursor:pointer" onclick="hide_sociable('post-2820',true)" class="close">



		  <img onclick="hide_sociable('post-2820',true)" title="close" src="http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/closelabel.png">

		  </a>

		</div>

	</div> 

  </div></div><div class='sociable' style='float:none'><ul class='clearfix'><li id="Twitter_Counter"><a href="https://twitter.com/share" data-text="ANSBERT NGURUMO ANAPOJADILI BLOGS - http://www.bongocelebrity.com/2009/01/18/ansbert-ngurumo-anapojadili-blogs/ (via #sociablesite)" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2009/01/18/ansbert-ngurumo-anapojadili-blogs/" class="twitter-share-button" data-count="horizontal">Tweet</a><script type="text/javascript" src="//platform.twitter.com/widgets.js"></script></li><li id="Facebook_Counter"><iframe src="//www.facebook.com/plugins/like.php?href=http://www.bongocelebrity.com/2009/01/18/ansbert-ngurumo-anapojadili-blogs/&send=false&layout=button_count&show_faces=false&action=like&colorscheme=light&font" scrolling="no" frameborder="0" style="border:none; overflow:hidden;height:32px;width:100px" allowTransparency="true"></iframe></li><li id="Google_+"><g:plusone annotation="bubble" href="http://www.bongocelebrity.com/2009/01/18/ansbert-ngurumo-anapojadili-blogs/" size="medium"></g:plusone></li><li id="LinkedIn_Counter"><script src="http://platform.linkedin.com/in.js" type="text/javascript"></script><script type="IN/Share" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2009/01/18/ansbert-ngurumo-anapojadili-blogs/" data-counter="right"></script></li><li id="StumbleUpon_Counter"><script src="http://www.stumbleupon.com/hostedbadge.php?s=2&r=http://www.bongocelebrity.com/2009/01/18/ansbert-ngurumo-anapojadili-blogs/"></script></li></ul></div><!-- End Sociable -->]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.bongocelebrity.com/2009/01/18/ansbert-ngurumo-anapojadili-blogs/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>8</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>UPDATE FROM MICHUZI AND GLOBAL PUBLISHERS</title>
		<link>http://www.bongocelebrity.com/2008/08/19/update-from-michuzi-and-global-publishers/</link>
		<comments>http://www.bongocelebrity.com/2008/08/19/update-from-michuzi-and-global-publishers/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 19 Aug 2008 23:40:43 +0000</pubDate>
		<dc:creator>bongocelebrity</dc:creator>
				<category><![CDATA[Blogs]]></category>
		<category><![CDATA[Mtandao]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://bongocelebrity.wordpress.com/2008/08/19/update-from-michuzi-and-global-publishers/</guid>
		<description><![CDATA[Blog ya Issa Michuzi hivi sasa inapatikana tena kwa kutumia anuani ile ile ya zamani ya www.issamichuzi.blogspot.com. Hiyo inafuatia matatizo ya kiufundi ambayo yamekuwa yakiikumba blog yake kwa muda wa takribani wiki nzima. Kwa hiyo kwa sasa Michuzi anapatikana kule kwa zamani mpaka hapo matatizo ya kiufundi yatakapopatiwa ufumbuzi wa kudumu. Wakati huo huo,kama ambavyo [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Blog ya Issa Michuzi hivi sasa inapatikana tena kwa kutumia anuani ile ile ya zamani ya <a href="http://www.issamichuzi.blogspot.com">www.issamichuzi.blogspot.com</a>. Hiyo inafuatia matatizo ya kiufundi ambayo yamekuwa yakiikumba blog yake kwa muda wa takribani wiki nzima. Kwa hiyo kwa sasa Michuzi anapatikana kule kwa zamani mpaka hapo matatizo ya kiufundi yatakapopatiwa ufumbuzi wa kudumu.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Wakati huo huo,kama ambavyo mmeona, tovuti ya Global Publishers,nayo inakabiliana na changamoto za kiufundi kidogo kwani hivi sasa haipatikani hewani kama ilivyokuwa.Hata hivyo,Global Publishers wametufahamisha kwamba mafundi wanajitahidi kwa kila hali kuhakikisha kwamba mambo yanarejea kuwa mswano mapema iwezekanavyo.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Wote wawili,Michuzi na Global Publishers, wanakushukuru kwa uvumilivu wako.<br />
</span></p>
<!-- Start Sociable --><div class="sociable"><div class="sociable_tagline"><a class='sociable_tagline' target='_blank' href='http://blogplay.com' style='color:#333333;text-decoration:none'>Be Sociable, Share!</a></div><ul class='clearfix'><li><a title="Twitter" class="option1_32" style="background-position:-288px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://twitter.com/intent/tweet?text=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS%20-%20http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F%20(via%20@sociablesite)"></a></li><li><a title="Facebook" class="option1_32" style="background-position:-96px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.facebook.com/share.php?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;t=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS"></a></li><li><a title="email" class="option1_32" style="background-position:-160px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="https://mail.google.com/mail/?view=cm&fs=1&to&su=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS&body=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&ui=2&tf=1&shva=1"></a></li><li><a class="option1_32" style="cursor:pointer;background-position:-128px 0px" rel="nofollow" title="Add to favorites - doesn't work in Chrome"  onClick="javascript:AddToFavorites();"></a></li><li><a title="StumbleUpon" class="option1_32" style="background-position:-224px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.stumbleupon.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&title=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS"></a></li><li><a title="Delicious" class="option1_32" style="background-position:-32px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://delicious.com/post?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;title=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS&amp;notes=Blog%20ya%20Issa%20Michuzi%20hivi%20sasa%20inapatikana%20tena%20kwa%20kutumia%20anuani%20ile%20ile%20ya%20zamani%20ya%20www.issamichuzi.blogspot.com.%20Hiyo%20inafuatia%20matatizo%20ya%20kiufundi%20ambayo%20yamekuwa%20yakiikumba%20blog%20yake%20kwa%20muda%20wa%20takribani%20wiki%20nzima.%20Kwa%20hiyo%20kwa%20sasa%20Michuzi"></a></li><li><a title="Google Reader" class="option1_32" style="background-position:-224px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/reader/link?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;title=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS&amp;srcURL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;srcTitle=BongoCelebrity+"></a></li><li><a title="LinkedIn" class="option1_32" style="background-position:-288px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.linkedin.com/shareArticle?mini=true&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;title=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS&amp;source=BongoCelebrity+&amp;summary=Blog%20ya%20Issa%20Michuzi%20hivi%20sasa%20inapatikana%20tena%20kwa%20kutumia%20anuani%20ile%20ile%20ya%20zamani%20ya%20www.issamichuzi.blogspot.com.%20Hiyo%20inafuatia%20matatizo%20ya%20kiufundi%20ambayo%20yamekuwa%20yakiikumba%20blog%20yake%20kwa%20muda%20wa%20takribani%20wiki%20nzima.%20Kwa%20hiyo%20kwa%20sasa%20Michuzi"></a></li><li><a title="BlinkList" class="option1_32" style="background-position:0px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.blinklist.com/index.php?Action=Blink/addblink.php&amp;Url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;Title=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS"></a></li><li><a style="cursor:pointer" rel="nofollow" onMouseOut="fixOnMouseOut(document.getElementById('sociable-post-1995'), event, 'post-1995')" onMouseOver="more(this,'post-1995')"><img style='margin-top:9px' src='http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/more.png'></a></li></ul><div onMouseout="fixOnMouseOut(this,event,'post-1995')" id="sociable-post-1995" style="display:none;">   

    <div style="top: auto; left: auto; display: block;" id="sociable">



		<div class="popup">

			<div class="content">

				<ul><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Myspace" class="option1_32" style="background-position:0px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.myspace.com/Modules/PostTo/Pages/?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;t=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Digg" class="option1_32" style="background-position:-64px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://digg.com/submit?phase=2&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;title=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS&amp;bodytext=Blog%20ya%20Issa%20Michuzi%20hivi%20sasa%20inapatikana%20tena%20kwa%20kutumia%20anuani%20ile%20ile%20ya%20zamani%20ya%20www.issamichuzi.blogspot.com.%20Hiyo%20inafuatia%20matatizo%20ya%20kiufundi%20ambayo%20yamekuwa%20yakiikumba%20blog%20yake%20kwa%20muda%20wa%20takribani%20wiki%20nzima.%20Kwa%20hiyo%20kwa%20sasa%20Michuzi"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Reddit" class="option1_32" style="background-position:-128px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reddit.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;title=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Google Bookmarks" class="option1_32" style="background-position:-192px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/bookmarks/mark?op=edit&amp;bkmk=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;title=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS&amp;annotation=Blog%20ya%20Issa%20Michuzi%20hivi%20sasa%20inapatikana%20tena%20kwa%20kutumia%20anuani%20ile%20ile%20ya%20zamani%20ya%20www.issamichuzi.blogspot.com.%20Hiyo%20inafuatia%20matatizo%20ya%20kiufundi%20ambayo%20yamekuwa%20yakiikumba%20blog%20yake%20kwa%20muda%20wa%20takribani%20wiki%20nzima.%20Kwa%20hiyo%20kwa%20sasa%20Michuzi"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="HackerNews" class="option1_32" style="background-position:-256px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://news.ycombinator.com/submitlink?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;t=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="MSNReporter" class="option1_32" style="background-position:-352px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reporter.es.msn.com/?fn=contribute&amp;Title=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS&amp;URL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;cat_id=6&amp;tag_id=31&amp;Remark=Blog%20ya%20Issa%20Michuzi%20hivi%20sasa%20inapatikana%20tena%20kwa%20kutumia%20anuani%20ile%20ile%20ya%20zamani%20ya%20www.issamichuzi.blogspot.com.%20Hiyo%20inafuatia%20matatizo%20ya%20kiufundi%20ambayo%20yamekuwa%20yakiikumba%20blog%20yake%20kwa%20muda%20wa%20takribani%20wiki%20nzima.%20Kwa%20hiyo%20kwa%20sasa%20Michuzi"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Sphinn" class="option1_32" style="background-position:-192px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://sphinn.com/index.php?c=post&amp;m=submit&amp;link=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Posterous" class="option1_32" style="background-position:-64px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://posterous.com/share?linkto=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;title=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS&amp;selection=Blog%20ya%20Issa%20Michuzi%20hivi%20sasa%20inapatikana%20tena%20kwa%20kutumia%20anuani%20ile%20ile%20ya%20zamani%20ya%20www.issamichuzi.blogspot.com.%20Hiyo%20inafuatia%20matatizo%20ya%20kiufundi%20ambayo%20yamekuwa%20yakiikumba%20blog%20yake%20kwa%20muda%20wa%20takribani%20wiki%20nzima.%20Kwa%20hiyo%20kwa%20sasa%20Michuzi"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Tumblr" class="option1_32" style="background-position:-256px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.tumblr.com/share?v=3&amp;u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F19%2Fupdate-from-michuzi-and-global-publishers%2F&amp;t=UPDATE%20FROM%20MICHUZI%20AND%20GLOBAL%20PUBLISHERS&amp;s=Blog%20ya%20Issa%20Michuzi%20hivi%20sasa%20inapatikana%20tena%20kwa%20kutumia%20anuani%20ile%20ile%20ya%20zamani%20ya%20www.issamichuzi.blogspot.com.%20Hiyo%20inafuatia%20matatizo%20ya%20kiufundi%20ambayo%20yamekuwa%20yakiikumba%20blog%20yake%20kwa%20muda%20wa%20takribani%20wiki%20nzima.%20Kwa%20hiyo%20kwa%20sasa%20Michuzi"></a></li></ul>			

			</div>        

		  <a style="cursor:pointer" onclick="hide_sociable('post-1995',true)" class="close">



		  <img onclick="hide_sociable('post-1995',true)" title="close" src="http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/closelabel.png">

		  </a>

		</div>

	</div> 

  </div></div><div class='sociable' style='float:none'><ul class='clearfix'><li id="Twitter_Counter"><a href="https://twitter.com/share" data-text="UPDATE FROM MICHUZI AND GLOBAL PUBLISHERS - http://www.bongocelebrity.com/2008/08/19/update-from-michuzi-and-global-publishers/ (via #sociablesite)" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2008/08/19/update-from-michuzi-and-global-publishers/" class="twitter-share-button" data-count="horizontal">Tweet</a><script type="text/javascript" src="//platform.twitter.com/widgets.js"></script></li><li id="Facebook_Counter"><iframe src="//www.facebook.com/plugins/like.php?href=http://www.bongocelebrity.com/2008/08/19/update-from-michuzi-and-global-publishers/&send=false&layout=button_count&show_faces=false&action=like&colorscheme=light&font" scrolling="no" frameborder="0" style="border:none; overflow:hidden;height:32px;width:100px" allowTransparency="true"></iframe></li><li id="Google_+"><g:plusone annotation="bubble" href="http://www.bongocelebrity.com/2008/08/19/update-from-michuzi-and-global-publishers/" size="medium"></g:plusone></li><li id="LinkedIn_Counter"><script src="http://platform.linkedin.com/in.js" type="text/javascript"></script><script type="IN/Share" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2008/08/19/update-from-michuzi-and-global-publishers/" data-counter="right"></script></li><li id="StumbleUpon_Counter"><script src="http://www.stumbleupon.com/hostedbadge.php?s=2&r=http://www.bongocelebrity.com/2008/08/19/update-from-michuzi-and-global-publishers/"></script></li></ul></div><!-- End Sociable -->]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.bongocelebrity.com/2008/08/19/update-from-michuzi-and-global-publishers/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>9</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>ANA KWA ANA NA “MWENYEKITI” MAGGID MJENGWA.</title>
		<link>http://www.bongocelebrity.com/2008/08/17/ana-kwa-ana-na-%e2%80%9cmwenyekiti%e2%80%9d-maggid-mjengwa/</link>
		<comments>http://www.bongocelebrity.com/2008/08/17/ana-kwa-ana-na-%e2%80%9cmwenyekiti%e2%80%9d-maggid-mjengwa/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 17 Aug 2008 22:32:50 +0000</pubDate>
		<dc:creator>bongocelebrity</dc:creator>
				<category><![CDATA[Blogs]]></category>
		<category><![CDATA[Elimu na Maendeleo]]></category>
		<category><![CDATA[Majarida/Magazeti]]></category>
		<category><![CDATA[Michezo]]></category>
		<category><![CDATA[Mtandao]]></category>
		<category><![CDATA[Photography/Picha]]></category>
		<category><![CDATA[Siasa]]></category>
		<category><![CDATA[Uandishi]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://bongocelebrity.wordpress.com/2008/08/17/ana-kwa-ana-na-%e2%80%9cmwenyekiti%e2%80%9d-maggid-mjengwa/</guid>
		<description><![CDATA[Kama wewe ni msomaji mzuri wa magazeti na majarida mbalimbali kutoka Tanzania,basi sina shaka kabisa kwamba jina Maggid Mjengwa (pichani) litakuwa sio geni kwako! Makala zake za kusisimua,kuchokoza hisia na kujenga hoja za nguvu ni miongoni mwa vivutio muhimu vya wasomaji wa magazeti ndani na nje ya Tanzania. Leo hii tunaweza kabisa kuthubutu kusema kwamba [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><img class="size-full wp-image-1954 alignleft" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/08/maggid001bc.jpg" alt="" width="408" height="336" /><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Kama wewe ni msomaji mzuri wa magazeti na majarida mbalimbali kutoka Tanzania,basi sina shaka kabisa kwamba jina <strong>Maggid Mjengwa</strong> (pichani) litakuwa sio geni kwako! Makala zake za kusisimua,kuchokoza hisia na kujenga hoja za nguvu ni miongoni mwa vivutio muhimu vya wasomaji wa magazeti ndani na nje ya Tanzania. Leo hii tunaweza kabisa kuthubutu kusema kwamba Maggid ni miongoni mwa wanahabari bora tulionao kwani hana uoga wowote pale anapokuwa anaandika au kuongelea jambo ambalo analiamini kwa dhati.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Lakini Maggid,kama ambavyo pengine unafahamu tayari, haishii magazetini tu bali pia ni blogger maarufu hivi sasa. <a href="http://mjengwa.blogspot.com/" target="_blank">Blog yake ya picha </a>ambayo mwenyewe anaiita &#8220;kijiji&#8221; na hivyo wasomaji wake na watembeleaji wake &#8220;wanakijiji&#8221;, imejipatia umaarufu sana kwa kuonyesha au kwenda kule ambapo ndiko kunahesabika kuwa kwenye hali halisi ya maisha ya mtanzania. Ukiitembelea na kuisoma blog yake vizuri kwa kutizama picha lukuki zinazoipamba blog yake,utaweza kuwa jaji mzuri kama &#8220;bongo ni tambarare&#8221; au bado zile ahadi za uchaguzi uliopita ni mbwembwe za kisiasa tu.Mwenyewe anasema blog yake ni kimbilio na sauti kwa wale ambao kila mara huwa wanasahauliwa!<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Maggid pia ni mjasiriamali.Yeye ndiye Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ijulikanayo kama Ikolo Investment Co ambao ndio wachapishaji wa Gozi Spoti; jarida la michezo, sanaa, maisha na burudani linalotoka kila Jumatano. Maggid pia ni mwanamichezo,mpenda michezo na shabiki mkubwa wa soka.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Hivi karibuni,baada ya kumsaka kwa muda mrefu kutokana na ratiba zake za kazi kumbana,tulifanikiwa kupata fursa ya kufanya naye mahojiano utakayoyasoma hivi punde.Kama ambavyo ungetegemea,Maggid anatoa &#8220;darasa&#8221; katika mahojiano haya.Mbali ya kukupa historia ya maisha yake kwa undani,Maggid anakumbusha vipengele fulani fulani vya historia ya nchi yetu ambavyo ni muhimu. Lakini kwa mapana, anaongelea kuhusu suala la uandishi na pia blog yake bila kusahau changamoto ambazo nchi yetu inakabiliwa nazo hivi leo katika nyanja mbalimbali. Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;</span><span id="more-1953"></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Maggid Mjengwa,karibu sana ndani ya BongoCelebrity<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA</strong>: Asante sana!<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Kwanza kabisa ningependa kupata kutoka kwako mwenyewe historia fupi ya maisha yako.Ulizaliwa wapi,lini,ukasomea wapi,unatoka kwenye familia ya watoto wangapi na mambo kama hayo.<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA</strong>: Awali ya yote, natanguliza shukran zangu za dhati kwako Jeff kwa heshima uliyonipa kwa kufanya mahojiano nami kupitia jukwaa hili la kijamii. Naitwa Maggid John Ramadhan Mjengwa. Nina bahati ya kuwa na asili zaidi ya moja.  Nina asili ya pwani na bara. Nimezaliwa Kliniki ya Ocean Road,  Dar Es Salaam. Mimi ni mmoja wa wale ambao huwaita wa kizazi cha Azimio la Arusha la mwaka 1967. Nimekulia Ilala, Mtaa wa Iringa nyumba namba 27.  Baadae familia yangu ilihamia Kinondoni Biafra, mwaka 1977.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Natoka katika familia ya watoto tisa. Wawili hawako tena duniani, mmojawapo ni kaka yangu, Grey John Ramadhan Mjengwa. Alifariki katika ajali ya basi mkoani Tanga zaidi ya miaka kumi iliyopita. Grey ndiye aliyenitangulia kwa kuzaliwa. Na mimi nilikuwa wa pili kuzaliwa. Elimu ya msingi na Sekondari nimesomea Dar. Nilimaliza Tambaza Sekondari mwaka 1987, baadae nilisoma Kidato cha Tano na Sita mkoani Mbeya pale Sangu Sekondari. Baada ya Sangu nilijiunga na JKT kwa mwaka mmoja ( Operesheni Kambarage 1990-91).  Kisha nikaamua kwenda kuishi na kufanya kazi za kujitolea wilayani Njombe, Iringa. Niliishi kijiji cha Igagala. Huko nilifundisha kwa kujitolea kwenye Chuo Cha Maendeleo ya Wananchi, Ulembwe. Kilomita 15 kutoka Njombe mjini. Nilipewa pia eka moja ya kulima.  Nililima mahindi, viazi na maharage. Vile vile nilipiga picha na kuandika habari za huko na kutuma kwenye magazeti, mojawapo ni Daily News.  Baada ya mwaka mmoja na nusu kijijiji hapo nilikwenda nchini Sweden. Huko nilikaa kwa miaka 12. Nimesoma kozi kadhaa kwenye vyuo vya Sweden na hatimaye kuhitimu shahada ya ualimu kwenye Chuo Kikuu cha Linköping.  Nimefanya kazi pia ya kufundisha kwenye baadhi ya vyuo vya maendeleo vya Maendeleo ya wananchi vya nchini Sweden.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Naam. Nimesema nina asili mbili; pwani na bara. Nitafafanua. Baba yangu alizaliwa kijiji cha Nyeregete, kwenye bonde la Usangu, Mbeya. Babu yangu, Chifu Mtenji Ramadhan Mjengwa alikuwa kiongozi wa kijadi mongoni mwa watu wa kabila la Wasangu.  Babu yangu mzaa mama, Fundi Pazi alitokea kwenye kabila la  Wahehe wa Iringa. Yeye alifanya kazi ya ujenzi wa  barabara.  Katika kazi yake akaja kukutana na bibi yangu mzaa mama,  Amina Binti Muhando Mwaruka. Hivyo basi, babu mzaa mama akalowea pwani na hususan Uzaramoni. Bibi yangu, Amina binti Muhando Mwaruka ( alifariki mwaka jana akiwa na umri wa miaka zaidi ya 87)  anatoka kwenye ukoo maarufu wa Mwaruka. Ni ukoo huu anaotoka mwanamuziki mahiri, Marehemu Mbaraka Mwinshehe Mwaruka. Mbaraka   alimwita bibi yangu shangazi. Nyumba ya marehemu bibi yangu kijijini Mzenga inapakana na nyumba ya Marehemu Mwinshehe Mwaruka, baba mzazi wa marehemu Mbaraka Mwinshehe Mwaruka.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Labda mpaka kufikia hapo kuna watakaoanza kunielewa kwanini napenda sana maeneo ya pwani kama vile Bagamoyo. Hakika, ni kutokana na asili yangu hiyo ya pwani kwa upande wa mama yangu. Kutoka Bagamoyo mpaka kijijini kwa mama yangu, Mzenga, Kisarawe ni mwendo wa dakika 45 kwa gari ndogo kwa kupitia njia ya mkato ya Bagamoyo-Miembe saba hadi Mlandizi.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Unakumbuka wakati ukiwa mdogo au ukiwa shule ya msingi ulitaka kuwa nani pindi ukimaliza shule? Na labda kuongezea tu,ni waandishi gani wa habari uliokuwa ukipenda zaidi kuwasoma enzi hizo?Kwanini?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA:</strong> Nilipenda masuala ya siasa, picha  na michezo tangu utotoni. Mazingira nayo yanachangia kumfanya mtu awe kama alivyo.  Pale Ilala tulikaa karibu kabisa na uwanja wa Karume. Nakumbuka niliingia uwanjani Karume kwa mara ya kwanza nikiwa na miaka sita nikiongozana na kaka yangu Grey. Ilikuwa ni mechi kati ya Simba na Cosmo Politans. Tuliingia uwanjani kwa kuruka ukuta kwenye moja ya kona za uwanja huo. Grey alinipandisha na kunishusha uwanjani. Nilishangaa mgambo hawakunifuata bali  waliwafuata  wengine.  Leo naelewa kuwa mgambo wale walikuwa ni watu wema sana. Wangefanya nini na mtoto wa miaka sita anayetamani kuona pambano la soka? Baadae ilikuwa rahisi zaidi kuingia uwanjani Karume na hata National Stadium. Ilikuwa ni kwenda getini, unamtafuta mtu mzima mmoja, unamuamkia kisha unamwomba akushike mkono muingie wote uwanjani kama mtoto wake. Mkishavuka geti hakuoni tena, wakati mwingine, kwa shauku ya mpira tulisahau hata kusema &#8216;asante&#8217; kwa waungwana wale waliotusaidia kuingia bure uwanjani.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Mapenzi yangu kwa klabu ya Simba yalianzia katika mechi ile ya kwanza niliyoiona maishani mwangu kati ya Simba na Cosmo. Simba walivaa jezi nyekundu na nyeupe. Cosmo walivaa bluu. Basi, cha kwanza kwangu ilikuwa kuchagua rangi. Nilichagua nyekundu na nyeupe. Lakini si rangi tu, Simba siku ile walicheza vizuri na kushinda pambano hivyo basi kutonifanya nibadili uamuzi wangu.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Hakika, tangu utotoni nilikuwa na mwelekeo wa kupenda  masuala ya kisiasa na kijamii. Kupenda michezo na picha. Kwa namna moja au nyingine, wazazi wangu walinisaidia sana kukuza vipaji vyangu. Nilianza kusikiliza redio nikiwa na miaka minne au mitano hivi, wazazi waliniruhusu kuchezea  redio. Mwanzoni nilidhani kuna watu wanaongea na kuimba ndani ya redio! ( Nadhani baadhi yenu mlifikiri kama mimi). Mapema sana nilianza kusikiliza vipindi vyenye kuelimisha. Miaka hiyo kabla hata sijatimiza miaka saba nakumbuka kuanza kusikiliza vipindi kama; mbiu ya mikoa, ujumbe wa leo na mazungumzo baada ya habari. Hicho cha mwisho ndicho ambacho Mzee Paul Sozigwa alikuwa akikiandaa.  Nakumbuka pia kila Jumapili Mkurugenzi wa RTD, Mzee David Wakati alikuwa na kipindi chake chenye kujadili masuala mbali mbali. Halafu nakumbuka kufuatilia kipindi cha &#8216; Umoja wa Mataifa Wiki Hii&#8217; ambapp &#8216;Born Again Pagan&#8217; maarufu kama BAP  na Abdalah Mbamba walikuwa wakikiendesha kwa nyakati tofauti.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Nilikuwa na kiu kubwa ya kusoma maandishi na kuangalia picha kwenye vitabu, majarida na magazeti. Nilifungua karibu kila kurasa ya kitabu kilichokuwa nyumbani. ( Hatukuwa na vitabu vingi sana). Nakumbuka kitabu cha Patrick Lumumba wa Kongo, sikuweza kusoma ( kiliandikwa kwa Kiingereza) lakini nilifuatilia picha za kitabuni na kumwuliza baba yangu. Nikafahamu kilihusu nini. Nakumbuka pia  kitabu cha John Okello( Zanzibar Revolution) Hiki nacho kilikuwa ni kwa Kiingereza, niliangalia picha na kumdadisi baba yangu, alinieleza kilihusu nini. Nilipofika Sekondari niliweza kuvisoma vitabu vyote hivyo. Hicho cha mwisho kilinifanya nifatute kila namna ili nifike Zanzibar kuona kwa macho yangu mazingira ya kisiwa yalikofanyika mapinduzi aliyoyaelezea Okello kwenye kitabu chake. Nilifika Zanzibar mara baada ya kumaliza kidato cha nne. Na nilikuwapo kwenye sherehe za mapinduzi Januari 12, 1989. Yote hii inaonyesha kwa namna moja au nyingine jinsi vitabu vinavyoweza kutujenga kama wanadamu.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Kuhusu picha nakumbuka pale Karume Stadium nilipenda sana kukaa nyuma ya goli na karibu kabisa na wapiga picha. Namkumbuka sana mpiga picha wa Daily News, Ernest Millinga. Nilifuatilia kazi zake uwanjani na hata magazetini. Siku moja baada ya mechi nilitafuta Daily News na kuangalia picha alizopiga Millinga. Zilinifanya nitake kujua pia maelezo ya picha hizo. Kwa namna moja au nyingine zilinisaidia kujifunza lugha ya Kiingereza.</span></p>
<p style="text-align:center;"><img class="size-full wp-image-1957 aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/08/maggid4bc.jpg" alt="" width="457" height="392" /></p>
<p style="text-align:center;">Maggid alipoitembelea Zanzibar enzi hizo.Unakumbuka hizo gari zilikuwa zinaitwaje?</p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Katika pekua pekua zetu kukuhusu tumegundua kwamba ulianza kuandika siku nyingi sana,tangu ukiwa shuleni Tambaza.Kwa msingi huo utakuwa ukifuatilia kwa karibu masuala ya maendeleo ya habari duniani na zaidi nchini Tanzania.Leo hii ukiangalia nyuma,unadhani pamekuwepo mabadiliko gani ya msingi tokea miaka ile ulipoanza kuandika mpaka hivi leo? Hapa nazungumzia mabadiliko kwako wewe binafsi na kwenye uandishi kwa ujumla.<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA:</strong> Ni kweli kuwa nimeanza kuandika tangu nikiwa Kidato cha Pili pale Tambaza. Lakini naweza kusema nimeanza kuandika tangu nikiwa shule ya msingi. Nakumbuka nilipenda sana pale mwalimu wa Kiswahili alipotupa kazi ya kutunga sentesi. Tukiambiwa tutunge sentesi tano mimi nilitunga kumi na tano!<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Hata hivyo, Tambaza ndipo hasa nilipoanzia uandishi wa kuonekana na wengine.  Mathalan, nilianzisha &#8216; kijigazeti&#8217; changu.  Niliandika kwa mkono juu ya mambo yanayotokea kwenye jamii yetu ya Tambaza, iwe michezoni au hata yanayotokea wakati wa kugawa chakula na matunda jikoni na darasani.  Nilivutiwa zaidi na kutiwa moyo nilipoona si wanafunzi wenzangu tu wanaosoma maandishi yangu, bali hata walimu walisoma pia. Sikupata  kumwona Mkuu wa Shule, Mzee Kalumuna akisoma maandishi yangu yale, lakini, Second Master wetu Mwaipopo alikuwa mmoja wa wasomaji wangu wakubwa.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Hata hili la kuandika kwa namna fulani linatokana na mazingira niliyokulia. Naamini uandishi unatokana na kusoma. Mama yangu alikuwa akifanya kazi Idara ya kupiga Chapa ya Serikali ( Government Press). Aliitambua mapema kiu yangu ya maandishi na kupenda kusoma na hata picha. Akitoka kazini alikuja na machapisho mbali mbali ya Kiserikali. Na hapa, kwa mara kwanza nabainisha, kuwa mama yangu aliniruhusu kusoma vitabu vya bajeti za Wizara za Serikali hata kabla ya wabunge hawajavitia machoni! Mama alikuja na kopi nyumbani akijua kuwa nilipenda sana kusoma, kudadisi na  kufuatilia mambo.  Ziada katika hilo ni kuwa niliweza pia kupata kopi ya gazeti maalum la serikali. ( Government gazette). Mara nyingi humo ziliandikwa habari za ndani ya Serikali kama vile uhamisho wa watumishi na mengineyo.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Wakati mwingine mama alirudi nyumbani na sahani ( plates) zenye picha mbali mbali zilizochapwa kwenye vitabu na mabango ya Serikali. Nilipenda sana kuziangalia kwa karibu picha zile. Hakika haya ya vitabu na picha yalinifanya nianze darasa la kwanza nikiwa najua kusoma na kuandika. Shida yangu ilikuwa siangalii vituo wakati nasoma &#8216; Juma na Roza&#8217;!<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Halafu linakuja suala la kupenda masuala ya siasa. Bila shaka, kwa namna moja au nyingine limechangiwa na hayo niliyoyaeleza hapo juu. Lakini pia pale Ilala tuliishi karibu kabisa na barabara kuu ya Uhuru na viwanja vya jangwani. Utotoni nilibahatika kuwaona viongozi wengi maarufu kutoka nje ya nchi  wakipita barabara hiyo.  Nakumbuka kuwaona viongozi maarufu kama vile Fidel Castro, Kaunda, Chu En Lai, Indira Gadhi ( Gandhi  alipita Pugu Road ) na wengine wengi.  Viwanja vya jangwani nilikwenda mara kadhaa kusikiliza mikutano ya kisiasa.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Kubwa kabisa la kisiasa nililopata kushuhudia katika maisha yangu ni kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi. Siku ile ya tarehe 5 Februari, 1977 nilikuwapo pale Ilala Bomani. Barabara ya Uhuru ilifungwa kwa magari. Kwaya ya Mzee Makongoro ilitumbuiza. Kulikuwa na gwaride la chipukizi na ngoma za asili. Ilikuwa ni shangwe na shamramshamra kila mahali. Tuliokuwa watoto wakati huo tuliingiwa na matumaini ya maisha bora ya baadae chini ya Chama kipya cha Mapinduzi.  Iliimbwa; &#8221; Chama Mapinduzi ee, Endeleza Kazi Ya Afro Na  TANU!&#8221;<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Miaka 30 imepita tangu kulishuhudia tukio lile kubwa maishani mwangu, ndio maana, siku zote najihisi ninayo ya kuandika kuhusu masuala ya siasa na kijamii, kwani, sikushuhudia tu kuzaliwa kwa CCM, bali tangu nikiwa na miaka saba nimekuwa nikifuatilia masuala ya kisiasa na kijamii katika nchi yetu bila kujihusisha na chama chochote cha siasa kwa maana ya kuwa mwanachama au mshabiki wa chama cha siasa.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Umekuwa mwandishi kwenye magazeti kwa muda mrefu sasa.Ingawa hivi sasa huandikii tena gazeti la Rai ambalo ulikuwa unaliandikia kwa muda mrefu,kuna watu ambao bado wanakutambua kama &#8220;Maggid Mjengwa wa Rai&#8221;.Kwa maana hiyo nadhani sio vibaya kama tutakuuliza kidogo kuhusu Rai.Ni kwanini uliamua kupumzika kuandikia Rai? Unadhani ulijifunza mambo gani ya msingi wakati wa uandishi wako kwenye gazeti la Rai?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA:</strong> Ah! &#8216; Maggid wa Rai&#8217;.  Sasa ni &#8216; Maggid wa Raia Mwema!&#8217;  Ndio, nilianza kuandikia Rai Agosti 8, 2004. Nakumbuka Agosti 4, 2004 nilikwenda Sinza Kijiweni kuwasalimia kaka zangu akina Bwire, Mbwambo, Salva  na jamaa wengine. Sikuwa na mawazo ya kuandikia Rai, maana nilikuwa na safu yangu ya &#8216; Gumzo la Ijumaa&#8217; kwenye gazeti la Majira. Mtu wa kwanza kukutana nae kabla sijaingia ndani alikuwa Salva Rweyemamu. Baada ya kumuamkia akaniambia; &#8221; Tena Maggid imekuwa vizuri umekuja,  njoo utuandikie kwenye Rai&#8221;. Nilishtuka kidogo, lakini nikaiona hiyo ni changamoto mpya.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">&#8221; Why not?&#8221; Nikamjibu. Kisha akanichukua na kunikabidhi kwa Bwire. Tangu hapo ikawa kama ilivyokuwa. Lakini, katika muda wote wa kuandikia Rai sikuwahi kushinikizwa kwa namna yoyote ile kuandika kile ambacho wengine walitaka niandike. Nimejisikia huru kuandika fikra zangu.  Rai ilinisaidia kutengeneza jukwaa na kuwafikia watu wengi zaidi ambao nisingeweza kuwafikia. Nitakuwa ni mwizi wa fadhila nisipowashukuru wale wote waliofanikisha hili na hususan Salva Rweyemamu aliyeuona uwezo wangu na kunipa changamoto. Huyu Salva Rweyemamu ni mmoja wa watu ninaowaheshimu sana hata kama kuna ambayo huwa hatukubaliani. Ana uwezo wa  kutambua vipaji na fursa zilizopo kwa wengine na namna ya kuzitumia vema. Ni Salva Rweyemamu, wakati akiwa Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mtanzania aliyenikaribisha ofisini kwake, pale Mtaa Mkwepu, si mara moja, na kunishauri mawili matatu katika fani hii ya uandishi ili niwe bora zaidi. Ni Salva Rweyemamu, Mhariri wa kwanza kabisa kunitumia faksi nikiwa Sweden mwaka 1995. Alifanya hivyo hata kabla ya kunitia machoni. Alinitumia faksi kunishukuru kwa kuchagua kuliandikia gazeti la Mtanzania.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Tangu 2004 nimeliandikia Rai hadi mwaka jana kunako mwezi Septemba. Naam. Ilifika mahali mazingira na upepo wa kiuandishi ulinilazimisha nimwandikie Mhariri wa Rai, kaka yangu Muhingo Rweyemamu kumshukuru na kumjulisha kuwa nimeamua kujipumzisha na kuwapisha wengine.  Nilikaa kijiweni kwa zaidi ya mwezi mmoja bila kuandika makala za magazetini. Nilibaki kuwa msomaji  kama wengine. Hatimaye nikapokea simu ya John Bwire akiniomba rasmi nijiunge na jarida jipya la Raia Mwema. Sikusita kuchukua changamoto hiyo.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Katika historia yako ya uandishi wa habari na makala magazetini,ilishawahi kukutokea ukaandika jambo ambalo baadaye ulipokaa na kutafakari upya ulitamani siku zirudi nyuma na jambo lile lisiwemo tena magazetini?Kama ndio ilikuwaje na ilikupa fundisho gani?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA:</strong> Hakika hilo kwa bahati nzuri halijanitokea.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Tukiwa bado kwenye suala hilo hilo la ukuaji wa nyanja za habari na mawasiliano nchini Tanzania.Unaliongeleaje suala zima la uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA:</strong> Ni swali gumu na zuri. Katika nchi yetu bado hatuna uhuru wa vyombo vya habari nikimaanisha uhuru wa kiuchumi. Tuna vyombo vya habari na wanahabari tegemezi. Hakuna ruzuku ya Serikali kwa vyombo vya habari vya binafsi. Hili linapelekea kushuka kwa viwango vya wanahabari na habari zenyewe.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Leo tuna mwanahabari anayetegemea lifti ya Mkuu wa Wilaya ili afike kwenye ziara ya DC. Hata hela ya kutuma faksi itoke kwa huyo huyo DC! Sasa unategemea mwandishi huyu ataandika jinsi wakazi wa eneo fulani walivyomweka kiti moto DC! Anajihatarishia kushushwa njiani kwenye ziara inayofuata ya DC!  Hakika hilo ni swali gumu na zuri  lenye kuhitaji makala nzima kuelezea.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Sasa tuongelee <a href="http://mjengwa.blogspot.com/" target="_blank">blog yako ambayo siku za hivi karibuni imezidi kujipatia umaarufu</a>. Katika mahojiano uliyofanya na jamaa wa Global Voices hivi karibuni ulikaririwa ukisema kwamba ulitaka upate mahali kama &#8220;kijiji&#8221; hivi ambapo watu wanaokosa pa kusemea wapate jinsi ya kufanya hivyo.Mbali na hilo,ni mambo gani matatu ambayo uliyatarajia na yepi matatu ambayo hukuyatarajia ulipokuwa unaanzisha blog hiyo?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA: </strong>Nilitarajia blogu iwe ni &#8216; jukwaa la maarifa&#8217;, mahali pa watu kukutana na kufahamiana, mahali pa burudani kupitia picha na mengineyo ili watu waweze kucheka na kutafakari. Binafsi napenda sana utani. Na wakati mwingine natumia blogu na picha kama kufanya utani huo. Si jambo rahisi sana kutaniana kwa njia ya blogu. Hutokea baadhi hawanielewi kama natania. Hata picha nyingine na maelezo huweka kwa makusudi mazima ya kuchokoza mjadala. Naona wajibu wangu ni kama wa mwalimu darasani, si kufundisha, bali kuandaa mazingira ya wanafunzi kujadili na kutoa maarifa waliyo nayo.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Sikutarajia; lingekuwa jukwaa kubwa hivi kwa muda mfupi, kuwa lingetoa fursa kwa wengine na hata kwangu mwenyewe kuwa na mahali pa kupata habari moto moto na kuwa jukwaa la kujieleza kwa uhuru na kupata maarifa mapya. Tatu, sikutarajia kuwa watu wengi hivi, ndani na nje ya nchi wangetumia blogu kama vile wanavyotumia magazeti katika kupata habari.</span></p>
<p style="text-align:center;"><img class="size-full wp-image-1965 aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/08/maggid003bc.jpg" alt="" width="591" height="329" /></p>
<p style="text-align:center;"><span style="font-size:small;color:#000000;"><span style="font-size:100%;color:#000000;">Novemba, 1996. Wafuasi wa CCM wakiandama kuingia Uwanja Wa Sokoine Mbeya kumsilikiza Rais Mstaafu Benjamin Mkapa. Maggid anasema; &#8220;Nilikuwepo uwanjani kushuhudia tukio lile. Watu hawakuwa wengi, wanafunzi wengi wa shule za Msingi waliletwa uwanjani. Wanafunzi hao wanaoonekana pichani sasa ni wapiga kura. Picha hii ni baadhi ya kazi zangu ambazo hazikuwahi kuchapishwa magazetini. Hakika, teknolojia hii ya blogu imetuwezesha baadhi yetu kupekua kwenye maktaba zetu na kukutana na kazi ambazo, huko nyuma tulizifanya kama hobby. Hakukuwa na vyombo vingi vya habari . Lakini sasa, kwa kutumia blogu tunaweza na tuna uhuru zaidi wa kuzichapa kazi hizo na wengi wakaziona.&#8221;</span> </span><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong></strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Pamoja na kwamba uandishi wa kiraia(citizen journalism) kwa mfano kupitia blogs nk umekuwa ukiendelea kukua kwa kasi na hivyo wakati mwingine kuwa news breaker wa mwanzo kabisa,kwa upande wa Tanzania bado blogs zenye habari mpya kila siku ni chache sana.Unadhani hii inatokana na nini?Nini kifanyike ili kushawishi watu wengi zaidi waanzishe blogs zao na kuzihudumia kila siku?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA: </strong>Nadhani hili la blogu inahusu mapenzi na nia ya mtu. Blogu inaweza kuanzishwa kwa madhumuni mbali mbali. Kuna wanaoanzisha kama photo album. Kuna wanaoanzisha wakiwa na nia ya kuihudumia kila siku, lakini muda hawana. Na kama ni blogu ya picha inabidi mtu uwe  na mapenzi na picha. Hakuna jibu la jumla la nini kifanyike isipokuwa kila anayeanzisha blogu ajiulize kwanini anaanzisha blogu.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Ni wanablog gani duniani,ikiwemo Tanzania, wanaokuvutia hivi sasa?Kwanini?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA: </strong>Navutiwa na wanablogu wengi, ndani na nje ya nchi. Nikiorodhesha watakuwa wengi. Lakini kwa nyumbani kaka yangu Issa Michuzi ni mmoja wa wanaonivutia sana. Kwa Michuzi si picha tu, ni zaidi ya picha. Mara nyingi nikikutana na Michuzi hufurahia sana, maana tunaongea lugha moja ( lugha ya picha) Tunavaa miwani  sawa ya &#8216;macho ya picha&#8217; ( Ingawa Michuzi yake ni 2.5 na miye 1.5!)<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Vinginevyo kazi kama za kwako Jeff na hata Haki Ngowi zinanifurahisha sana. Kwamba ubunifu wenu umewafanya muwe karibu sana na jamii yenu pamoja na tofauti ya maelfu ya maili kutoka ilipo jamii yenu. Kuna vijana wengine wanaoibukia na kufanya kazi ya kusifika, mfano ni  kijana  Bob Sankofa. Navutiwa na ubunifu na kazi zake. Halafu tuna vijana nje ya nchi, baadhi nimekutana nao nilipobahatika kutembelea ughaibuni. Nao wanafanya kazi ya nzuri kupitia majukwaa kama haya ya blogu na hata nje ya blogu. Tuwatambue na tuwape moyo kwa kazi zao.</span></p>
<p style="text-align:center;"><img class="size-full wp-image-1959 aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/08/maggid002bc.jpg" alt="" width="588" height="392" /></p>
<p style="text-align:center;">Maggid(kulia) akiwa na Issa Michuzi ndani ya uwanja wa Taifa jijini Dar-es-salaam.Wote ni wapenzi wa Michezo na wote ni bloggers.Raha ilioje.Maggid ni Simba wa kutupwa.Michuzi je?</p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Kwa sababu blog yako ni ya picha tungependa kukuuliza swali hili.Mpaka hivi leo ni picha gani ambayo uliipiga na kuitumia kwenye blog yako ambayo kila mara inakurudia mawazoni?Kwanini?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA: </strong>Swali zuri, kuna picha mbili, moja  niliipiga Morogoro. Mwenyeji wangu yule alinikaribisha vema nyumbani kwake. Nilisikitika sana pale aliponielezea matatizo ya wadudu wanaoharibu maharage yake shambani. Ilifika mahali aliwakusanya na kuwachoma moto akiamini kuwa harufu yake itawafukuza wadudu wengine. Ilisikitisha kwa vile aliko mwanakijiji yule ni mwendo wa saa moja tu kwa gari hadi kilipo Chuo Kikuu cha Kilimo Cha Sokoine. Unajiuliza, wataalam wetu wa kilimo wanafanya nini kumsaidia mkulima kama huyu?<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Picha nyingine ni  wakati nilipotembelea vijji viwili vya kandokando ya ziwa Nyasa. Moja ya kijiji hicho ni Ikolo.  Ni kijiji kisichofikika  kwa barabara. Wakati napanda mtumbwi kuelekea huko niliona hatari iliyopo, kwamba fikiri kama nahodha wangu atapatwa na kifafa au mshtuko wa moyo. Tulikuwa wawili tu kwenye mtumbwi. Katika hali hiyo nisingeweza kuungoza mtumbwi, nami ningezama katikati ya ziwa.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Lakini pamoja na fikra hizo niliona umuhimu wa kufika huko. Ni wajibu wangu kujaribu kuwafikia wasiofikika kirahisi. Nifanye hivyo ili sauti zao nao zisikike. Baada ya saa mbili ziwani  nilifika Ikolo. Nilipokewa vizuri. Nilikwenda na jarida la FEMA. Niliona jinsi vijana wa mahali pale walivyoligombania jarida lile. Vijana wale walikuwa na kiu kubwa ya kusoma. Ikolo hakuna magazeti wala majarida.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Nikiwa Ikolo, na katika mazingira yale, nilijiwa na fikra za kuanzisha kampuni itakayohusika zaidi na machapisho ya majarida na vitabu. Ndipo wazo la kuanza na jarida la michezo, sanaa, maisha na burudani  lilipoibuka. Haikupita miezi mingi, nikasajili  kampuni kwa jina la Ikolo Investiment Co. Ltd.  Mimi ni Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni hiyo. Kwa miezi minne sasa kampuni hiyo inazalisha jarida la  Gozi Spoti; jarida la michezo, sanaa, maisha na burudani linalotoka kila Jumatano. Gozi Spoti linafika hadi Ikolo na vijiji vya jirani kupitia mawakala wetu. Huko zinakwenda nakala kadhaa za bure kwa vijana wa Ikolo. Ikolo Investiment Co. Ltd pia imechapisha kitabu kuhusu maisha ya Barack Obama; alikotoka, aliko na anakokwenda. Machapisho zaidi yanatarajiwa kutolewa. Yote haya ni katika kujaribu kukata kiu ya kusoma kwa wananchi, lakini pia kuchangia katika kuwajengea Watanzania kiu ya kupenda kusoma. Mimi niliandaliwa mazingira ya kupata kiu ya kupenda kusoma. Nimesomeshwa na kufika hapa nilipo kwa gharama za wakulima na wafanyakazi walipa kodi wa nchi hii. Naliona ni jukumu langu na nina deni la kulipa kwa nchi yangu. Deni ni kubwa na sitalimaliza, lakini kushiriki kazi ya kuchapisha majarida na vitabu na kuwafikishia Watanzania hata walio vijijini kwa bei nafuu ni namna ya kupunguza deni hilo, ni wajibu wetu sote.</span></p>
<p style="text-align:center;"><img class="size-full wp-image-1962 aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/08/maggid2bc.jpg" alt="" width="523" height="392" /></p>
<p style="text-align:center;">Hali halisi ya maisha ya mkulima wa Tanzania.Je tutafika kweli?</p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Blog yako imejipatia umaarufu kwa sababu moja kuu;inaonyesha hali halisi ya mtanzania wa kawaida. Tangu uanze kufanya hivyo umekuwa ukitembelea vijiji na vijiji ambapo umekuwa ukikutana na watanzania wenyeji wa huko vijijini ambao bila kusita tunaweza kusema hali zao ni duni.Ukiongea nao wanakupa ujumbe gani wa msingi kuhusu hali zao?Nini unadhani kinatakiwa kufanyika ili kubadili hali zao?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA: </strong>Nimejitahidi kuifanya blogu yangu kuwa sauti kwa wasio na sauti. Kwamba ilenge kwenye kuelezea maisha ya kila siku ya Mtanzania wa kawaida. Ionyeshe mafanikio na changamoto zinazomkabili Mtanzania huyo. Kazi yangu imenipa fursa ya kutembelea vijiji vingi vya nchi yetu. Huko nimekutana na kuongea na Watanzania wa kada mbalimbali.  Wanavijiji wengi wa  nchi hii wanayajua matatizo yao na namna ya kukabiliana nayo. Wanachokosa ni nyenzo. Moja ya nyenzo hizo ni elimu. Cha kwanza wanachohitaji ni elimu, elimu, elimu. Na hapa sina maana ya elimu ya kuingia darasani tu, bali elimu kwa maana ya kusaidiwa kupata maarifa mbalimbali ya kukabiliana na matatizo yao ikiwamo kujua haki na wajibu wao.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Unadhani tekinolojia mpya kama hizi za blogs zinaweza kuwa na mchango gani katika maendeleo ya kijamii na kwa mfano kubadilisha hali za kimaisha za watanzania hususani waliopo vijijini ukizingatia kwamba tekinolojia hizi ni za mtandaoni jambo ambalo bado ni geni sana vijijini?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA: </strong>Ni kweli, kuwa teknolojia hii bado mpya sana sio  tu vijijini bali hata katika sehemu nyingi za mijini. Bado ni asilimia ndogo sana ya Watanzania wanaopata taarifa kupitia teknolojia hii.  Iko haja ya  kutafuta namna ya kuhamisha baadhi ya taarifa muhimu zinazopatikana katika mtandao zitoke pia katika magazeti na hata redio.</span></p>
<p style="text-align:center;"><img class="size-full wp-image-1963 aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/08/maggid3bc.jpg" alt="" width="523" height="392" /></p>
<p style="text-align:center;">Maggid,he often goes where our leaders don&#8217;t bother to go!</p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Maggid unajulikana kuwa mpenzi wa michezo hususani soka.Pia tunafahamu kwamba wewe ni shabiki mkubwa wa Simba Sports Club au wana Msimbazi.Sasa kama ujuavyo siku hizi watanzania wengi wana ushabiki wa timu za Uingereza.Kwa upande wako unaishabikia timu gani kule?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA: </strong>Mimi ni mpenzi wa Wekundu wa Msimbazi kwa maana ya Simba tangu nikiwa na miaka sita. Lakini zaidi ni mpenzi wa michezo kwa ujumla. Naamini katika fair play. Ndio maana kuna wakati hata Simba wenzangu hawanielewi pale ninapoandika fikra zangu zenye kuwatetea watani zetu wa jadi.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Nakumbuka kuna wakati niliandika makala kuishutumu Simba kwa kumfungia Athuman Idd na kupelekea mchezaji huyo kushindwa kuchezea Yanga, timu aliyotaka kuchezea. Katika makala hiyo niliandika kuwa mimi ni mpenzi wa Simba lakini nilikuwa na fikra tofauti katika suala la Athuman Idd. Basi, siku hiyo nilipigiwa simu nyingi na baadhi ya wapenzi wa Simba wenye hasira. Kuna walionitukana pia, mmoja aliniambia; &#8221; Acha upumbavu wewe, huwezi kuwa Simba bali ni kondoo unayejifanya simba!&#8221;<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;">Hata juzi hapa niliandika kupitia blogu yangu kuwataka Simba wenzangu tuwapiganie watani zetu Yanga wafutiwe adhabu yao ya kufungiwa au kupunguzwa kwa adhabu hiyo. Na laiti makala ile ingechapwa gazetini,  naamini kuna Simba ambao wangenipigia simu kunitukana. Nafuatilia pia kandanda ya England, huko naipenda sana Man United.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Mbali na uandishi na pia pia blog,unajishughulisha na nini?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA: </strong>Tangu mwaka 2004 nimekuwa mwajiriwa wa Shirika la Forum Syd lenye Makao yake Makuu Sweden. Mbali ya majukumu mengine nimekuwa nikifanya kazi ya kiushauri na hata kupanga na kuratibu semina za mafunzo kwa walimu wa Vyuo Vya Maendeleo ya Wananchi Tanzania. Mkataba wangu umemalizika Julai mwaka huu. Hata hivyo, mwajiri wangu ameniongezea miezi mitano zaidi, namaliza Desemba mwaka huu. Baada ya hapo nitatafuta kibarua mahali kwingine, kama mambo yatakuwa magumu nina kijishamba changu Bagamoyo, nitakwenda huko kulima mananasi.  Usisahau  nina ujuzi kidogo wa kuvua samaki, nitaishi tu!</span></p>
<p style="text-align:center;"><img class="size-full wp-image-1961 aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/08/maggid6bc.jpg" alt="" width="588" height="392" /></p>
<p style="text-align:center;">Mvuvi Maggid Mjengwa!</p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Unapenda kujishughulisha na nini baada ya kazi zako?<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>MJENGWA: </strong>Napenda kusoma vitabu na kuandika. Napenda kujumuika na marafiki na kuongea.  Napenda kupika vyakula. Napenda michezo. Hutokea nikachukua muda wangu kuangalia soka uwanjani au kwenye tv. Napenda kusikiliza muziki na kudansi pia. Nacheza pia mpira wa meza ( table tennis).  Lakini juu ya yote mimi ni mtu wa kawaida tu ninayefanya mambo mengine ambayo wengine watasema ni ya kijinga.  Ni binadamu ambaye kamwe siwezi kukamilika. Najifunza kila siku. Napokea shutuma na lawama kama sehemu ya kujifunza katika maisha.<br />
</span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong>BC: Shukrani sana Maggid.Nakutakia kila la kheri katika kazi zako.Endelea kuelimisha jamii.<br />
</strong></span></p>
<p><span style="font-size:9pt;font-family:Verdana;"><strong><br />
</strong></span></p>
<!-- Start Sociable --><div class="sociable"><div class="sociable_tagline"><a class='sociable_tagline' target='_blank' href='http://blogplay.com' style='color:#333333;text-decoration:none'>Be Sociable, Share!</a></div><ul class='clearfix'><li><a title="Twitter" class="option1_32" style="background-position:-288px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://twitter.com/intent/tweet?text=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA.%20-%20http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F%20(via%20@sociablesite)"></a></li><li><a title="Facebook" class="option1_32" style="background-position:-96px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.facebook.com/share.php?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;t=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA."></a></li><li><a title="email" class="option1_32" style="background-position:-160px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="https://mail.google.com/mail/?view=cm&fs=1&to&su=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA.&body=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&ui=2&tf=1&shva=1"></a></li><li><a class="option1_32" style="cursor:pointer;background-position:-128px 0px" rel="nofollow" title="Add to favorites - doesn't work in Chrome"  onClick="javascript:AddToFavorites();"></a></li><li><a title="StumbleUpon" class="option1_32" style="background-position:-224px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.stumbleupon.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&title=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA."></a></li><li><a title="Delicious" class="option1_32" style="background-position:-32px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://delicious.com/post?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;title=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA.&amp;notes=Kama%20wewe%20ni%20msomaji%20mzuri%20wa%20magazeti%20na%20majarida%20mbalimbali%20kutoka%20Tanzania%2Cbasi%20sina%20shaka%20kabisa%20kwamba%20jina%20Maggid%20Mjengwa%20%28pichani%29%20litakuwa%20sio%20geni%20kwako%21%20Makala%20zake%20za%20kusisimua%2Ckuchokoza%20hisia%20na%20kujenga%20hoja%20za%20nguvu%20ni%20miongoni%20mwa%20vivut"></a></li><li><a title="Google Reader" class="option1_32" style="background-position:-224px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/reader/link?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;title=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA.&amp;srcURL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;srcTitle=BongoCelebrity+"></a></li><li><a title="LinkedIn" class="option1_32" style="background-position:-288px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.linkedin.com/shareArticle?mini=true&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;title=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA.&amp;source=BongoCelebrity+&amp;summary=Kama%20wewe%20ni%20msomaji%20mzuri%20wa%20magazeti%20na%20majarida%20mbalimbali%20kutoka%20Tanzania%2Cbasi%20sina%20shaka%20kabisa%20kwamba%20jina%20Maggid%20Mjengwa%20%28pichani%29%20litakuwa%20sio%20geni%20kwako%21%20Makala%20zake%20za%20kusisimua%2Ckuchokoza%20hisia%20na%20kujenga%20hoja%20za%20nguvu%20ni%20miongoni%20mwa%20vivut"></a></li><li><a title="BlinkList" class="option1_32" style="background-position:0px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.blinklist.com/index.php?Action=Blink/addblink.php&amp;Url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;Title=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA."></a></li><li><a style="cursor:pointer" rel="nofollow" onMouseOut="fixOnMouseOut(document.getElementById('sociable-post-1953'), event, 'post-1953')" onMouseOver="more(this,'post-1953')"><img style='margin-top:9px' src='http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/more.png'></a></li></ul><div onMouseout="fixOnMouseOut(this,event,'post-1953')" id="sociable-post-1953" style="display:none;">   

    <div style="top: auto; left: auto; display: block;" id="sociable">



		<div class="popup">

			<div class="content">

				<ul><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Myspace" class="option1_32" style="background-position:0px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.myspace.com/Modules/PostTo/Pages/?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;t=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA."></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Digg" class="option1_32" style="background-position:-64px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://digg.com/submit?phase=2&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;title=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA.&amp;bodytext=Kama%20wewe%20ni%20msomaji%20mzuri%20wa%20magazeti%20na%20majarida%20mbalimbali%20kutoka%20Tanzania%2Cbasi%20sina%20shaka%20kabisa%20kwamba%20jina%20Maggid%20Mjengwa%20%28pichani%29%20litakuwa%20sio%20geni%20kwako%21%20Makala%20zake%20za%20kusisimua%2Ckuchokoza%20hisia%20na%20kujenga%20hoja%20za%20nguvu%20ni%20miongoni%20mwa%20vivut"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Reddit" class="option1_32" style="background-position:-128px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reddit.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;title=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA."></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Google Bookmarks" class="option1_32" style="background-position:-192px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/bookmarks/mark?op=edit&amp;bkmk=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;title=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA.&amp;annotation=Kama%20wewe%20ni%20msomaji%20mzuri%20wa%20magazeti%20na%20majarida%20mbalimbali%20kutoka%20Tanzania%2Cbasi%20sina%20shaka%20kabisa%20kwamba%20jina%20Maggid%20Mjengwa%20%28pichani%29%20litakuwa%20sio%20geni%20kwako%21%20Makala%20zake%20za%20kusisimua%2Ckuchokoza%20hisia%20na%20kujenga%20hoja%20za%20nguvu%20ni%20miongoni%20mwa%20vivut"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="HackerNews" class="option1_32" style="background-position:-256px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://news.ycombinator.com/submitlink?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;t=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA."></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="MSNReporter" class="option1_32" style="background-position:-352px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reporter.es.msn.com/?fn=contribute&amp;Title=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA.&amp;URL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;cat_id=6&amp;tag_id=31&amp;Remark=Kama%20wewe%20ni%20msomaji%20mzuri%20wa%20magazeti%20na%20majarida%20mbalimbali%20kutoka%20Tanzania%2Cbasi%20sina%20shaka%20kabisa%20kwamba%20jina%20Maggid%20Mjengwa%20%28pichani%29%20litakuwa%20sio%20geni%20kwako%21%20Makala%20zake%20za%20kusisimua%2Ckuchokoza%20hisia%20na%20kujenga%20hoja%20za%20nguvu%20ni%20miongoni%20mwa%20vivut"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Sphinn" class="option1_32" style="background-position:-192px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://sphinn.com/index.php?c=post&amp;m=submit&amp;link=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Posterous" class="option1_32" style="background-position:-64px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://posterous.com/share?linkto=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;title=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA.&amp;selection=Kama%20wewe%20ni%20msomaji%20mzuri%20wa%20magazeti%20na%20majarida%20mbalimbali%20kutoka%20Tanzania%2Cbasi%20sina%20shaka%20kabisa%20kwamba%20jina%20Maggid%20Mjengwa%20%28pichani%29%20litakuwa%20sio%20geni%20kwako%21%20Makala%20zake%20za%20kusisimua%2Ckuchokoza%20hisia%20na%20kujenga%20hoja%20za%20nguvu%20ni%20miongoni%20mwa%20vivut"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Tumblr" class="option1_32" style="background-position:-256px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.tumblr.com/share?v=3&amp;u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F08%2F17%2Fana-kwa-ana-na-%25e2%2580%259cmwenyekiti%25e2%2580%259d-maggid-mjengwa%2F&amp;t=ANA%20KWA%20ANA%20NA%20%E2%80%9CMWENYEKITI%E2%80%9D%20MAGGID%20MJENGWA.&amp;s=Kama%20wewe%20ni%20msomaji%20mzuri%20wa%20magazeti%20na%20majarida%20mbalimbali%20kutoka%20Tanzania%2Cbasi%20sina%20shaka%20kabisa%20kwamba%20jina%20Maggid%20Mjengwa%20%28pichani%29%20litakuwa%20sio%20geni%20kwako%21%20Makala%20zake%20za%20kusisimua%2Ckuchokoza%20hisia%20na%20kujenga%20hoja%20za%20nguvu%20ni%20miongoni%20mwa%20vivut"></a></li></ul>			

			</div>        

		  <a style="cursor:pointer" onclick="hide_sociable('post-1953',true)" class="close">



		  <img onclick="hide_sociable('post-1953',true)" title="close" src="http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/closelabel.png">

		  </a>

		</div>

	</div> 

  </div></div><div class='sociable' style='float:none'><ul class='clearfix'><li id="Twitter_Counter"><a href="https://twitter.com/share" data-text="ANA KWA ANA NA “MWENYEKITI” MAGGID MJENGWA. - http://www.bongocelebrity.com/2008/08/17/ana-kwa-ana-na-%e2%80%9cmwenyekiti%e2%80%9d-maggid-mjengwa/ (via #sociablesite)" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2008/08/17/ana-kwa-ana-na-%e2%80%9cmwenyekiti%e2%80%9d-maggid-mjengwa/" class="twitter-share-button" data-count="horizontal">Tweet</a><script type="text/javascript" src="//platform.twitter.com/widgets.js"></script></li><li id="Facebook_Counter"><iframe src="//www.facebook.com/plugins/like.php?href=http://www.bongocelebrity.com/2008/08/17/ana-kwa-ana-na-%e2%80%9cmwenyekiti%e2%80%9d-maggid-mjengwa/&send=false&layout=button_count&show_faces=false&action=like&colorscheme=light&font" scrolling="no" frameborder="0" style="border:none; overflow:hidden;height:32px;width:100px" allowTransparency="true"></iframe></li><li id="Google_+"><g:plusone annotation="bubble" href="http://www.bongocelebrity.com/2008/08/17/ana-kwa-ana-na-%e2%80%9cmwenyekiti%e2%80%9d-maggid-mjengwa/" size="medium"></g:plusone></li><li id="LinkedIn_Counter"><script src="http://platform.linkedin.com/in.js" type="text/javascript"></script><script type="IN/Share" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2008/08/17/ana-kwa-ana-na-%e2%80%9cmwenyekiti%e2%80%9d-maggid-mjengwa/" data-counter="right"></script></li><li id="StumbleUpon_Counter"><script src="http://www.stumbleupon.com/hostedbadge.php?s=2&r=http://www.bongocelebrity.com/2008/08/17/ana-kwa-ana-na-%e2%80%9cmwenyekiti%e2%80%9d-maggid-mjengwa/"></script></li></ul></div><!-- End Sociable -->]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.bongocelebrity.com/2008/08/17/ana-kwa-ana-na-%e2%80%9cmwenyekiti%e2%80%9d-maggid-mjengwa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>19</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>ISSA MICHUZI NA HATUA MBILI MBELE</title>
		<link>http://www.bongocelebrity.com/2008/07/02/issa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele/</link>
		<comments>http://www.bongocelebrity.com/2008/07/02/issa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 02 Jul 2008 14:17:55 +0000</pubDate>
		<dc:creator>bongocelebrity</dc:creator>
				<category><![CDATA[Blogs]]></category>
		<category><![CDATA[Mtandao]]></category>
		<category><![CDATA[News]]></category>
		<category><![CDATA[Sayansi na Tekinolojia]]></category>
		<category><![CDATA[Tangazo/Matangazo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://bongocelebrity.wordpress.com/?p=1589</guid>
		<description><![CDATA[Kuanzia usiku wa leo(saa sita usiku kwa saa za Afrika Mashariki),blog maarufu ya Muhidin Issa Michuzi,itabadilisha anuani.Badala ya kupatikana kupitia www.issamichuzi.blogspot.com sasa itapatikana kupitia www.michuzi-blog.com. Mbali na mabadiliko hayo ya anuani,yupo “mwana” mwingine ambaye naye anazaliwa.Hiyo ni tovuti nyingine chini ya usimamizi wa huyu huyu gwiji wa blog. Tovuti hiyo ambayo inapatikana kupitia www.bongotyube.com ni [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p style="text-align:center;margin:0 0 10pt;"><img class="size-full wp-image-1590 aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/07/michu1bc.jpg" alt="" width="588" height="392" /></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;">Kuanzia usiku wa leo(saa sita usiku kwa saa za Afrika Mashariki),blog maarufu ya Muhidin Issa Michuzi,itabadilisha anuani.Badala ya kupatikana kupitia <a href="http://www.issamichuzi.blogspot.com/">www.issamichuzi.blogspot.com</a> sasa itapatikana kupitia <a href="http://www.michuzi-blog.com/">www.michuzi-blog.com</a>. </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;">Mbali na mabadiliko hayo ya anuani,yupo “mwana” mwingine ambaye naye anazaliwa.Hiyo ni tovuti nyingine chini ya usimamizi wa huyu huyu gwiji wa blog. Tovuti hiyo ambayo inapatikana kupitia <a href="http://www.bongotyube.com/">www.bongotyube.com</a> ni maalumu kwa habari,burudani,michezo nk kupitia video.</span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;">Kama kawaida yetu,tulipopata habari kuhusiana na mabadiliko hayo katika blog hiyo ya jamii pamoja na tovuti mpya inayoanzishwa,tuliona ni heri tumtafute Michuzi mwenyewe ili atupe undani kidogo kuhusu mabadiliko hayo nk.Kwa uungwana kabisa akakubali kufanya nasi mahojiano utakayoyasoma hivi punde ingawa ukweli ni kwamba yuko bize <span> </span>ili kuhakikisha kwamba mabadiliko yaliyotajwa hapo juu yanakwenda salama kabisa.</span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;">Lakini pamoja na kuongelea mabadiliko hayo,Issa Michuzi,ametoa mafunzo na changamoto muhimu sana kwa wanablog na pia washika dau mbalimbali katika sekta au fani ya habari na mawasiliano.Je ni changamoto na mafunzo gani?Anawaambia nini “wadau” wakati huu anapojiandaa kuendeleza “libeneke” kwa mapana na marefu zaidi? Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;</span><span id="more-1589"></span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;"> </span></strong></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">BC:Kwa mara nyingine tena naomba nikukaribishe ndani ya BC.Mambo yanakwendaje?</span></strong><strong></strong></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">MICHUZI</span></strong><span style="font-size:9.5pt;">: Asante sana BC. Mambo mswano tu. Ila kwanza naomba nikupongeze kwa kazi nzuri mnayofanya. Kwa kweli ingawa wengi hawakubali kwa kuwa hawajafikiria hilo lakini staili yenu ya kipekee na haina mfano. Ningependa magazeti ya hapa nyumbani yaige mfano huu kwani habari ni watu na matukio sio viongozi pekee. Linalofanyika BC ni mfano wa kuigwa (sio wa ku-copy na ku-paste kama inavyoanza kujitokeza sasa ambapo naona magazeti yameanza kufanya hivyo) na wa kupewa sifa zote. Mie ni mpenzi sana wa BC na lazima nipitie humu kila siku na huwa siangushwi. Kila siku nakuta mahojiano mapya na kama si mahojiano muziki wa enzi hizo na za sasa. Hii inafurahisha sana. Hongera sana sana BC.</span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">BC:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;"> <strong>Kwanza kabisa hongera kwa kuzindua tovuti yako itakayokwenda kwa <a href="http://www.bongotyube.com/" target="_blank">www.bongotyube.com</a> na pia kuboresha uwezo wa blog yako maarufu ya Issa Michuzi kwa kuihamishia kwenye <a href="http://www.michuzi-blog.com/" target="_blank">www.michuzi-blog.com</a>. Kwa vyovyote vile mabadiliko haya yamefuatia au yanaelekea kwenye mipango fulani.Unaweza kutuambia kidogo kuhusu sababu zilizopelekea mabadiliko haya?</strong></span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">MICHUZI:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;"> Asante sana. Sababu ni rahisi sana; nayo ni kupiga hatua moja mbele zaidi. Naona furaha na fahari kwamba hivi sasa fani ya blogu imepiga hatua kubwa kwenda mbele kiasi ya kwamba blogu zimeanza kutambulika kama mojawapo ya vyombo muhimu vya habari. Hivi unavyozungumza hata stesheni zingine za redio zimeanza kupitia blogu kama zifanyavyo magazeti mengine. Nahisi muda si mrefu ujao stesheni za TV nazo zitafuatia kama wafanyavyo wenzetu wa magharibi.</span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;">Hivyo, kwa kujibu swali lako ni kwamba hii ni hatua moja kwenda mbele, na kama ilivyokuwa kwenye blogu yetu ya jamii nahisi nitapata wadau wa kufuata nyayo katika nia ya kuendeleza kile ambacho mie napenda kuita libeneke. Uwanja ni mpana sana mie peke yangu ama na watu kama BC hatuwezi kuujaza. Lazima wapatikane wengi wengine kama inavyojitokeza kwenye blogu. Inanifurahisha sana na kunitia moyo kwamba blogu zinakuwa nyingi. Natumai baada ya muda si mrefu bongotyube zingine pia zitaibuka.</span></p>
<p style="text-align:center;margin:0 0 10pt;"><img class="size-full wp-image-1591 aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/07/michu2bc.jpg" alt="" width="589" height="392" /></p>
<p style="text-align:center;margin:0 0 10pt;">Popote alipo huwa yupo kamili ili kuendeleza libeneke.</p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">BC: Ni miaka kadhaa sasa imepita tangu uanze kublog.Kwa mtu asiyehusika moja kwa moja na mambo ya blogs, anaweza kudhani kwamba pengine ku-blog hakuna changamoto tena hususani akizingatia uzoefu ambao unao.Unakubaliana na mtazamo kama huo? Kama jibu ni hapana,je ni changamoto gani unazokabiliana nazo hivi sasa tofauti na pale ulipoanza kublog?</span></strong><strong></strong></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">MICHUZI:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;"> Kwangu mimi kwa sasa changamoto kubwa zaidi sio za kiutendaji bali za kuhamasisha wadau wengi wafungue blogu na kuendeleza libeneke. Kama nilivyosema, sie tulio katika fani peke yetu hatutoshelezi. Ukiangalia blogu za wenzetu nje utakuta zina mambo tofauti tofauti na sio ya aina moja tu kama ilivyo sasa blogu zetu za hapa Tanzania. Nashangaa kukuta kwamba magazeti hayana blogu. Wenzetu wa ughaibuni wana blogu kwa kila mada kwenye habari zao, mfano michezo ina blogu yake. Hii inasaidia kufanya wasomaji wachangie na kujisikia wanahusika na hilo gazeti. Wakati umepita kwa wenye magazeti kuandika peke yao na kutegemea wasomaji waishie kusoma tu. Kwa taarifa yako kuna uchunguzi umefanyika mwanzoni mwa mwaka na kugunduliwa kuwa wasomaji hivi sasa ndio wanaoandika sana kuliko waandishi wenyewe kwenye hizo blogu, na kwamba blogu kwenye tovuti ya gazeti husaidia pia kuvuta wasomaji wengi, kwani mijadala inayoendelea huwa burudani na elimu tosha. </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;">Hivyo changamoto niliyonayo ni kujaribu kuiweka ndoto yangu katika hali halisi. Nataka magazeti na stesheni za redion na TV zifungue blogu kwa kila mada kwenye kurasa ama vipindi vyao. Pia kuhamasisha wadau wafungue blogu kwa kufuata fani zao. Mfano wachonga vinyago wawe na blogu zao watuonyeshe kazi zao pamoja na vinyago vyao, nasi tupate fursa ya kuvijadili. Wanamitindo, wanamuziki, hata madereva teksi. Unaonaje tukimpata mtu kama dereva wa daladala  ambaye atakuwa na blogu inayoelezea shughuli zake za siku hadi siku. Pamoja na kufaidika kwa kujua kinachoendelea pia hii ni njia rahisi na ya haraka ya kupashana habari.</span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">BC: Mara kwa mara tumekuwa tukishuhudia blogs mbalimbali za watanzania zikianzishwa.Hata hivyo,nyingi miongoni mwa blogs hizo huwa hazidumu.Unakuta blog inaanza leo na keshokutwa inakuwa ishakufa.Kwa uzoefu wako,nini huwa kinasababisha hali hiyo na unatoa ushauri gani kwa wanablog wapya au hata wale wa zamani ambao tunaweza kusema wamezitelekeza blogs zao?</span></strong><strong></strong></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">MICHUZI:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;"> Mie nachelea kuwalaumu sana wadau wote wa aina hiyo. Wengi huwa ni sababu ya kukosa nyenzo ama muda wa kutosha kuendesha blogu. Wengi wengine ni kuishiwa cha kuweka kwenye blogu, sababu kubwa ni kutaka kuiga ya blogu iliyofanikiwa bila kujua kwamba mwenye nayo huwa ameamua kuwa bloga kwa hali na mali. Hivyo inyeshe ama liwake ni lazima aweke mambo kwenye blogu. </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;">Sasa utakuta mtu akiishiwa cha kuweka kutokana na kutokuwa na aidha ubunifu wa kuendeleza libeneke, hukata tamaa. Lingine kubwa ni kukosa wasomaji ambako wengine hudhani kwamba wingi ama uchache wa <span> </span>maoni ni kupata ama kukosa wasomaji. Hilo ni kosa kubwa. Wadau kutokutoa maoni haimaanishi hawasomi blogu yako. Kwa mfano mimi blogu yetu ya jamii inaonesha kwamba wasomaji wasiotoa maoni ni wengi zadi kuliko wale wanaotoa maoni. Hilo ni funzo ambalo limenipa moyo sana kwani idadi ya wadau inaongezeka hata pale ambapo maoni yanakuwa haba. Tatizo lingine ni kukosekana kwa msisimko kwenye blogu zingine. Utakuta mtu anaposti mambo anayoyataka ama anayoyapenda yeye tu. Hapa pia mfano mwingine ni wa mimi kuchanganya mambo kwenye blogu ya jamii ikiwa ni pamoja na kukaribisha picha, habari na mawazo ama hata mada toka kwa wadau wengine. Hii ni moja ya siri za mafanikio ya blogu ya jamii ambayo kwa sasa siyo yangu tena kwani kila mdau anahisi ni yake pia na ana uhuru nayo kama kwamba ni yeye anayeiendesha. Hivyo ushauri wangu kwa wadau wasome na watafakari kwa makini niliyonena hapo juu, matokeo wataona pale watapoanza kuyatekeleza.</span></p>
<p style="text-align:center;margin:0 0 10pt;"><img class="size-full wp-image-1592 aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/07/bongotyubebc.jpg" alt="" width="448" height="305" /></p>
<p style="text-align:center;margin:0 0 10pt;">Muonekano wa www.bongotyube.com</p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">BC: Leo hii unapohamia kwenye makazi mapya na pia kuongeza &#8220;mwana&#8221; mwingine,una ujumbe gani kwa watembeleaji,wachangiaji wa blog yako au wadau kama ambavyo unapenda kuwaita?Watarajie nini?</span></strong></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;"> </span></strong></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">MICHUZI:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;"> Kwanza kabisa naomba hili la kuhamia makazi mengine niliweke sawa. Mie sihami, na blogu itabakia na mtazamo ule ule wa siku zote. Kinachobadilika hapa ni jina la anuani tu. Endapo kama ulikuwa unaipata blogu ya jamii kupitia <a href="http://issamichuzi.blogspot.com/" target="_blank">issamichuzi.blogspot.com</a> sasa utaweza kufanya hivyo kwa kufungua ama kutafuta kwenye google na injini zingine za kusachi kwa kutumia <a href="http://www.michuzi-blog.com/" target="_blank">www.michuzi-blog.com</a>. Itapofunguka utakutana na sura ile ile ya blogu ya buluu na kila kitu kinabaki kama kilivyo.</span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;">Kinachobadilika katika hiyo ni anuani tu. Pia kwa vile nafasi ya kuweka vitu zaidi kwenye <a href="http://blospot.com/" target="_blank">blospot.com</a> ni finyu, nimeamua kuinunulia blogu ya jamii nafasi ama space kubwa sana ambayo itaniwezesha kuweka mapicha na hata video kwa wingi na bila kuwa na wasiwasi wa kujaza space. Na hapa ningependa kuwatonya wana-blogu wote kwamba nafasi ama space kwenye blogu zao zina mwisho na kama mdau atataka aendeleze libeneke bila matatizo anunue space hiyo, vinginevyo itafikiwa wakati atakuta neno &#8216;you have exceeded your quota, your post cannot be published&#8217;. Mie yamenikuta hayo toka mwanzoni mwa mwaka huu na nikanunua nafasi ingine ambayo nayo baada ya kukaribia kujaa nimeona heri ninunue itakayodumu kwa miaka kama mitatu ama minne. Huko mbele ya safari tutajua kifanyike nini endapo kama itajaa tena.</span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;">Wadau watarajie mambo mengi zaidi kwa kila tukio, pamoja na video za aina mbalimbali. Mfano hapa BC haya mahojiano wadau wangekuwa wananiona na kunisikia badala ya kusoma maandishi peke yake. Kubwa la wadau kutarajia ni kuendelea kwa libeneke kama kawaida na kwa mapana zaidi. Vile vile watoa mada, habari na maoni wategemee uwanja mpana zaidi kwani space ni ya kutosha kuanzia leo Jumatano saa sita usiku kwa saa za Afrika Mashariki.</span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;">Kwenye hiyo <a href="http://www.bongotyube.com/" target="_blank">www.bongotyube.com</a> wadau watarajie kile walichokuwa hawana kwa muda wote wa historia ya blogu na tovuti za Bongo. Yaani sasa wadau wenye video ambazo wangependa kushea na wengine wajue kwamba mkombozi wao amefika na watajisajili na kuanza ku-posti video za matukio mbalimbali hapo. Hakuna kiingilio wala gharama yoyote, ni bure tu. Hivyo kazi kwao.</span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> <strong>BC: Michuzi,tunakutakia kila la kheri.</strong></span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><strong><span style="font-size:9.5pt;">MICHUZI:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;"> BC nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii.</span></p>
<p style="margin:0 0 10pt;"><span style="font-size:9.5pt;"> </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></p>
<!-- Start Sociable --><div class="sociable"><div class="sociable_tagline"><a class='sociable_tagline' target='_blank' href='http://blogplay.com' style='color:#333333;text-decoration:none'>Be Sociable, Share!</a></div><ul class='clearfix'><li><a title="Twitter" class="option1_32" style="background-position:-288px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://twitter.com/intent/tweet?text=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE%20-%20http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F%20(via%20@sociablesite)"></a></li><li><a title="Facebook" class="option1_32" style="background-position:-96px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.facebook.com/share.php?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;t=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE"></a></li><li><a title="email" class="option1_32" style="background-position:-160px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="https://mail.google.com/mail/?view=cm&fs=1&to&su=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE&body=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&ui=2&tf=1&shva=1"></a></li><li><a class="option1_32" style="cursor:pointer;background-position:-128px 0px" rel="nofollow" title="Add to favorites - doesn't work in Chrome"  onClick="javascript:AddToFavorites();"></a></li><li><a title="StumbleUpon" class="option1_32" style="background-position:-224px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.stumbleupon.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&title=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE"></a></li><li><a title="Delicious" class="option1_32" style="background-position:-32px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://delicious.com/post?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;title=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE&amp;notes=%0AKuanzia%20usiku%20wa%20leo%28saa%20sita%20usiku%20kwa%20saa%20za%20Afrika%20Mashariki%29%2Cblog%20maarufu%20ya%20Muhidin%20Issa%20Michuzi%2Citabadilisha%20anuani.Badala%20ya%20kupatikana%20kupitia%20www.issamichuzi.blogspot.com%20sasa%20itapatikana%20kupitia%20www.michuzi-blog.com.%20%0AMbali%20na%20mabadiliko%20h"></a></li><li><a title="Google Reader" class="option1_32" style="background-position:-224px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/reader/link?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;title=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE&amp;srcURL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;srcTitle=BongoCelebrity+"></a></li><li><a title="LinkedIn" class="option1_32" style="background-position:-288px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.linkedin.com/shareArticle?mini=true&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;title=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE&amp;source=BongoCelebrity+&amp;summary=%0AKuanzia%20usiku%20wa%20leo%28saa%20sita%20usiku%20kwa%20saa%20za%20Afrika%20Mashariki%29%2Cblog%20maarufu%20ya%20Muhidin%20Issa%20Michuzi%2Citabadilisha%20anuani.Badala%20ya%20kupatikana%20kupitia%20www.issamichuzi.blogspot.com%20sasa%20itapatikana%20kupitia%20www.michuzi-blog.com.%20%0AMbali%20na%20mabadiliko%20h"></a></li><li><a title="BlinkList" class="option1_32" style="background-position:0px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.blinklist.com/index.php?Action=Blink/addblink.php&amp;Url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;Title=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE"></a></li><li><a style="cursor:pointer" rel="nofollow" onMouseOut="fixOnMouseOut(document.getElementById('sociable-post-1589'), event, 'post-1589')" onMouseOver="more(this,'post-1589')"><img style='margin-top:9px' src='http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/more.png'></a></li></ul><div onMouseout="fixOnMouseOut(this,event,'post-1589')" id="sociable-post-1589" style="display:none;">   

    <div style="top: auto; left: auto; display: block;" id="sociable">



		<div class="popup">

			<div class="content">

				<ul><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Myspace" class="option1_32" style="background-position:0px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.myspace.com/Modules/PostTo/Pages/?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;t=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Digg" class="option1_32" style="background-position:-64px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://digg.com/submit?phase=2&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;title=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE&amp;bodytext=%0AKuanzia%20usiku%20wa%20leo%28saa%20sita%20usiku%20kwa%20saa%20za%20Afrika%20Mashariki%29%2Cblog%20maarufu%20ya%20Muhidin%20Issa%20Michuzi%2Citabadilisha%20anuani.Badala%20ya%20kupatikana%20kupitia%20www.issamichuzi.blogspot.com%20sasa%20itapatikana%20kupitia%20www.michuzi-blog.com.%20%0AMbali%20na%20mabadiliko%20h"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Reddit" class="option1_32" style="background-position:-128px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reddit.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;title=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Google Bookmarks" class="option1_32" style="background-position:-192px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/bookmarks/mark?op=edit&amp;bkmk=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;title=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE&amp;annotation=%0AKuanzia%20usiku%20wa%20leo%28saa%20sita%20usiku%20kwa%20saa%20za%20Afrika%20Mashariki%29%2Cblog%20maarufu%20ya%20Muhidin%20Issa%20Michuzi%2Citabadilisha%20anuani.Badala%20ya%20kupatikana%20kupitia%20www.issamichuzi.blogspot.com%20sasa%20itapatikana%20kupitia%20www.michuzi-blog.com.%20%0AMbali%20na%20mabadiliko%20h"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="HackerNews" class="option1_32" style="background-position:-256px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://news.ycombinator.com/submitlink?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;t=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="MSNReporter" class="option1_32" style="background-position:-352px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reporter.es.msn.com/?fn=contribute&amp;Title=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE&amp;URL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;cat_id=6&amp;tag_id=31&amp;Remark=%0AKuanzia%20usiku%20wa%20leo%28saa%20sita%20usiku%20kwa%20saa%20za%20Afrika%20Mashariki%29%2Cblog%20maarufu%20ya%20Muhidin%20Issa%20Michuzi%2Citabadilisha%20anuani.Badala%20ya%20kupatikana%20kupitia%20www.issamichuzi.blogspot.com%20sasa%20itapatikana%20kupitia%20www.michuzi-blog.com.%20%0AMbali%20na%20mabadiliko%20h"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Sphinn" class="option1_32" style="background-position:-192px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://sphinn.com/index.php?c=post&amp;m=submit&amp;link=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Posterous" class="option1_32" style="background-position:-64px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://posterous.com/share?linkto=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;title=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE&amp;selection=%0AKuanzia%20usiku%20wa%20leo%28saa%20sita%20usiku%20kwa%20saa%20za%20Afrika%20Mashariki%29%2Cblog%20maarufu%20ya%20Muhidin%20Issa%20Michuzi%2Citabadilisha%20anuani.Badala%20ya%20kupatikana%20kupitia%20www.issamichuzi.blogspot.com%20sasa%20itapatikana%20kupitia%20www.michuzi-blog.com.%20%0AMbali%20na%20mabadiliko%20h"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Tumblr" class="option1_32" style="background-position:-256px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.tumblr.com/share?v=3&amp;u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F07%2F02%2Fissa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele%2F&amp;t=ISSA%20MICHUZI%20NA%20HATUA%20MBILI%20MBELE&amp;s=%0AKuanzia%20usiku%20wa%20leo%28saa%20sita%20usiku%20kwa%20saa%20za%20Afrika%20Mashariki%29%2Cblog%20maarufu%20ya%20Muhidin%20Issa%20Michuzi%2Citabadilisha%20anuani.Badala%20ya%20kupatikana%20kupitia%20www.issamichuzi.blogspot.com%20sasa%20itapatikana%20kupitia%20www.michuzi-blog.com.%20%0AMbali%20na%20mabadiliko%20h"></a></li></ul>			

			</div>        

		  <a style="cursor:pointer" onclick="hide_sociable('post-1589',true)" class="close">



		  <img onclick="hide_sociable('post-1589',true)" title="close" src="http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/closelabel.png">

		  </a>

		</div>

	</div> 

  </div></div><div class='sociable' style='float:none'><ul class='clearfix'><li id="Twitter_Counter"><a href="https://twitter.com/share" data-text="ISSA MICHUZI NA HATUA MBILI MBELE - http://www.bongocelebrity.com/2008/07/02/issa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele/ (via #sociablesite)" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2008/07/02/issa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele/" class="twitter-share-button" data-count="horizontal">Tweet</a><script type="text/javascript" src="//platform.twitter.com/widgets.js"></script></li><li id="Facebook_Counter"><iframe src="//www.facebook.com/plugins/like.php?href=http://www.bongocelebrity.com/2008/07/02/issa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele/&send=false&layout=button_count&show_faces=false&action=like&colorscheme=light&font" scrolling="no" frameborder="0" style="border:none; overflow:hidden;height:32px;width:100px" allowTransparency="true"></iframe></li><li id="Google_+"><g:plusone annotation="bubble" href="http://www.bongocelebrity.com/2008/07/02/issa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele/" size="medium"></g:plusone></li><li id="LinkedIn_Counter"><script src="http://platform.linkedin.com/in.js" type="text/javascript"></script><script type="IN/Share" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2008/07/02/issa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele/" data-counter="right"></script></li><li id="StumbleUpon_Counter"><script src="http://www.stumbleupon.com/hostedbadge.php?s=2&r=http://www.bongocelebrity.com/2008/07/02/issa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele/"></script></li></ul></div><!-- End Sociable -->]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.bongocelebrity.com/2008/07/02/issa-michuzi-na-hatua-mbili-mbele/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>49</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>NI BINAMU13.COM</title>
		<link>http://www.bongocelebrity.com/2008/05/12/ni-binamu13com/</link>
		<comments>http://www.bongocelebrity.com/2008/05/12/ni-binamu13com/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 12 May 2008 04:06:37 +0000</pubDate>
		<dc:creator>bongocelebrity</dc:creator>
				<category><![CDATA[Bongo Flava]]></category>
		<category><![CDATA[Burudani]]></category>
		<category><![CDATA[Mtandao]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://bongocelebrity.wordpress.com/?p=1387</guid>
		<description><![CDATA[Kwa wengi siku hizi anajulikana kama Binamu.Lakini alipoingia rasmi kwenye ulimwengu wa muziki aliitwa MwanaFalsafa.Jina lake kamili ni Hamisi Mwinjuma(pichani).Ni mshindi wa tuzo maarufu za Kili. Tangu aingie kwenye fani ya muziki,sifa moja ambayo amekuwa nayo ni kuwa na mashairi au lyrics kali. Ilikuwa ni lazima uwe na uelewa mzuri wa lugha ya Kiswahili ili [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p class="MsoNormal"><img class="alignleft" style="float:left;" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/05/mwanafalsafabc.jpg" alt="" width="267" height="177" /><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">Kwa wengi siku hizi anajulikana kama Binamu.Lakini alipoingia rasmi kwenye ulimwengu wa muziki aliitwa MwanaFalsafa.Jina lake kamili ni Hamisi Mwinjuma(pichani).Ni mshindi wa tuzo maarufu za Kili.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">Tangu aingie kwenye fani ya muziki,sifa moja ambayo amekuwa nayo ni kuwa na mashairi au lyrics kali. Ilikuwa ni lazima uwe na uelewa mzuri wa lugha ya Kiswahili ili upate maana halisi ya nyimbo zake.Uwezo wake wa kwenda sambamba na mapigo (beats) za kimuziki huku akighani ipasavyo mashairi yake ni jambo linguine lililomfanya awe mmoja miongoni mwa wanamuziki wa B Flava wenye mashabiki lukuki..</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">Hivi karibuni MwanaFA amezindua <a href="http://www.binamu13.com/" target="_blank">tovuti yake rasmi</a>.BC tulipata nafasi ya kufanya naye mahojiano kuhusiana na ujio wa tovuti hiyo,muziki wake,mipango yake ya baadaye na mengineyo mengi.Kwanini ameiita tovuti yake <strong><a href="http://www.binamu13.com/" target="_blank">binamu13.com</a></strong>? Ana mipango gani katika miaka mitano ijayo? Anasemaje kuhusu ujio wa mwanamuziki 50 Cent nchini Tanzania hivi karibuni?Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;</span><span id="more-1387"></span></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">BC: Kwanza hongera sana kwa kuzindua tovuti yako rasmi hivi karibuni. Pia pongezi nyingi kwa mafanikio ambayo umeyapata tangu uanze kazi za muziki.Mambo yanakwendaje?</span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">MwanaFA</span></strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">:Thanx a lot cuz…Mungu anasaidia sana juhudi zangu zinatoa mwanga wa mafanikio!Nazingatia sana nguvu zake kwenye kila ninachofanya.Najua kila kitu kilishapangwa naye hata kabla sijazaliwa na ninachofanya ni kufumbua mafumbo aliyoniwekea kupata niliyopangiwa kuyapata humu kunako dunia yake.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">Mambo kama kawa ndugu yangu…</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">Labda kabla hatujaenda mbele sana naomba nimpe pongezi na shukrani zangu za dhati my boy Ahmed Babajide kwa kuweza kufanikisha kuwepo kwa tovuti hii.Mungu ataifanya kazi yako yenye thamani siku za karibuni Ahmed.Thanx a lot.</span></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">BC: Jambo la kwanza ambalo tumeliona pindi tulipopata habari kuhusu ujio wa tovuti yako rasmi ni kwamba tovuti yako umeiita binamu13.com.Wengi tunafahamu kuhusu jina Binamu lakini hatujui kuhusu namba 13.Unaweza kutuambia namba 13 inamaanisha nini?</span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">MwanaFA:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> 13 is my birthdate..March 13<sup>th</sup>!I am a Pieces,like Osama,MethodMan and many others…hahahaha..and I’ve been using the name binamu 13 sehemu kadhaa kwa muda sasa!sikiliza tena intro ya ‘hawajui’ utanifahamu…</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">BC: Mara nyingi mtu anapoamua kuanzisha tovuti yake anakuwa na malengo fulani maalumu.Kwa msanii kama wewe lengo mojawapo la wazi ni kutumia tovuti yako kujitangaza na kuwasiliana kirahisi na mashabiki wako wenye uwezo wa kutembelea mtandao.Mbali na lengo kama hilo,unategemea kupata nini zaidi kutokana na kuwa na tovuti yako mwenyewe/rasmi?</span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">MwanaFA</span></strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">: Sababu za wazi kabisa baada ya hizo ulizoziorodhesha awali ni kujaribu kuitumia kutafuta njia za kufanya biashara ipanuke.Kwa ulimwengu tulionao watu wengi zaidi wanaweza kukufikia kupitia mitandao kuliko sehemu nyingi nyingine,hasa walio mbali sana na Africa nilipo.Nikijaribu kuwa realistic,hakuna namna msanii wa uzito wangu ataeleweka bila ya kuwa na tovuti.Muda wa mimi kuwa na tovuti yangu rasmi ulishafika.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">BC: Kwa kiasi kikubwa tovuti yako imeandikwa katika lugha ya kiingereza kitu ambacho kwa kiasi fulani kinamnyima mshabiki wako asiyefahamu kiingereza nafasi ya kuitembelea na kuifurahia kama sio kusoma yaliyomo.Unaweza kutuambia kidogo kwanini sehemu kubwa umeiweka katika kiingereza?</span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">MwanaFA:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> Aaamh…kama nilivyosema katika swali lililopita,nalazimika kuwa karibu wa wapenzi wa kazi zangu,HASA WALIO MBALI NA NILIPO.Wengi wanaofahamu Kiswahili tu na sio kiingereza kilichotumika sana kwenye tovuti yangu wapo nilipo…Africa,na hasa Tanzania ambako wana namna nyingine lukuki za kupata habari za maendeleo ya kazi yangu kirahisi.Simaanishi hawatakuwa na nafasi ya kujua kupitia tovuti,no..kadri tunavyoendelea tutakuwa tukijaribu kumfanya kila mmoja ajisikie nyumbani kuipitia…kila mmoja ni binamu yangu!</span></p>
<p class="MsoNormal" style="text-align:center;"><img class="aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/05/fa-stagebc.jpg" alt="" width="523" height="392" /></p>
<p class="MsoNormal" style="text-align:center;">Binamu a.k.a MwanaFA akiwapa ladha murua mashabiki wake,mashabiki wa muziki wa kizazi kipya hivi karibuni.</p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">BC: Mashairi au lyrics za nyimbo zako, matumizi ya lugha ya Kiswahili ni mambo ambayo yanavutia sana wapenzi wa muziki kiasi kwamba wengine wamewahi kutania kwamba huenda kila<span> </span>unapokwenda huwa huiachi nyuma kamusi ya Kiswahili.Kuna ukweli wowote katika hilo? Je unadhani lugha ya Kiswahili ina nafasi gani kimataifa kupitia muziki?</span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">MwanaFA:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> Hahahahahaa…sina hata kamusi yenyewe mpwa!Nalichukulia hilo kama compliment anyway!..ukijaribu kuangalia kazi zangu za karibuni nimejaribu sana kurahisisha Kiswahili ninachokitumia ili kuondoa matatizo ya watu kutafuta kamusi ili waelewe nimesema nini…muziki tunaofanya yafaa uwe wa kumpumzisha mtu na sio kumuongezea mzigo wa mawazo..najua unanielewa kama uliwahi kuwa Africa.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">Nafasi ya lugha ya Kiswahili sio kubwa kwenye muziki wa kimataifa kwa kweli.Lakini muziki pia unaweza kutumika kukitangaza Kiswahili chenyewe kama utafanywa katika viwango vya kimataifa.Bado tunajaribu kuutoa huu muziki na Kiswahili kwa wakati mmoja.Hakuna namna tutashindana na kina Jay Z kufanya muziki mzuri kwa lugha yao.,so we better stick to ours!</span></p>
<p class="MsoNormal" style="text-align:center;"><img class="aligncenter" src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/05/mwanafab.jpg" alt="" width="392" height="591" /></p>
<p class="MsoNormal" style="text-align:center;">MwanaFA(kulia) akiwa na mshirika wako wa karibu,nyota mwingine wa muziki wa kizazi kipya, Ambwene Yesaya au AY.Kwa pamoja hivi karibuni walitoka na kitu,<a href="http://www.eastafricantube.com/media/4545/HABARI_NDIO_HIYO-MWANA_F_NA_AY/" target="_blank"><strong>Habari Ndiyo Hiyo</strong>.</a></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">BC: Tanzania hivi karibuni imekuwa ikipata bahati ya kutembelewa na wanamuziki mashuhuri kutoka nje na hususani Marekani. Hivi karibuni mwanamuziki 50 Cent na kundi lake la G-Unit walikuwepo nchini Tanzania na wewe ulikuwa mmojawapo miongoni mwa wahudhuriaji.Unadhani ziara kama zile<span> </span>zinawasaidia ninyi wanamuziki wa kizazi kipya kwa namna yoyote ile?Kwa maneno mengine tunaweza kusema kuna mambo yoyote ya msingi ambayo mnajifunza kutoka kwao?</span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">MwanaFA:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> Yeah,kiaina..Japo kitu haswa tunachoweza faidika nacho toka kwao ni kupata exposure.Nadhani waandaaji wa hayo matamasha wangekuwa wanajaribu kufanya utaratibu wa kutuunganisha nao kufanya kazi za pamoja.Naamini tutatangazika mno kwa mtindo huo!Imagine ujio wa Akon mathalan,angeweza fanya wimbo japo mmoja na msanii wa ‘bongo’,ingekuwa ni hatua ndefu ajabu…sawa 50 is expensive and all,hatuwezi mshawishi hata atupe Lloyd Banks ama Yayo afanye a single verse kwenye wimbo mmoja wa kibongo kweli?lol!Yafaa tuwashawishi watusaidie kujaribu kuuvusha muziki wetu.</span></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">BC: Ukitizama mbele kiasi,tuseme kama miaka kumi ijayo hivi,unadhani muziki wa kizazi kipya utakuwa wapi? Na wewe mwenyewe nini malengo yako katika miaka hiyo kumi ijayo?</span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">MwanaFA:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> Well,sina uwezo wa kuona sana mbali hivyo,ila kama kila kitu kitakuwa kwenye reli za juhudi zetu pengine tutakuwa kwenye nafasi ambayo raggatone ipo sasa…tuombe na kuwajibika!</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">Binafsi najaribu kujijenga vizuri nisishindwe japo kukumbukwa baada ya kuachana na muziki na pia nisitetereshwe na maisha pindi ujana utakapokwisha.Nafahamu sitaweza kufanya ninachokifanya milele hivyo najiandaa.I realy do,na namuomba Mungu sana anisaidie niweze fikia ama kuvuka malengo.</span></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">BC: Mwisho ungependa kuwaambia nini mashabiki wako,mashabiki wa muziki wa kizazi kipya?</span></strong></p>
<p class="MsoNormal"><strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;">MwanaFA:</span></strong><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> They should keep faith in me and I’ll never let them down.</span></p>
<p class="MsoNormal">Tembelea tovuti ya MwanaFA kwa <strong><a href="http://www.binamu13.com/" target="_blank">kubonyeza hapa</a></strong>.</p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;"> </span></p>
<!-- Start Sociable --><div class="sociable"><div class="sociable_tagline"><a class='sociable_tagline' target='_blank' href='http://blogplay.com' style='color:#333333;text-decoration:none'>Be Sociable, Share!</a></div><ul class='clearfix'><li><a title="Twitter" class="option1_32" style="background-position:-288px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://twitter.com/intent/tweet?text=NI%20BINAMU13.COM%20-%20http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F%20(via%20@sociablesite)"></a></li><li><a title="Facebook" class="option1_32" style="background-position:-96px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.facebook.com/share.php?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;t=NI%20BINAMU13.COM"></a></li><li><a title="email" class="option1_32" style="background-position:-160px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="https://mail.google.com/mail/?view=cm&fs=1&to&su=NI%20BINAMU13.COM&body=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&ui=2&tf=1&shva=1"></a></li><li><a class="option1_32" style="cursor:pointer;background-position:-128px 0px" rel="nofollow" title="Add to favorites - doesn't work in Chrome"  onClick="javascript:AddToFavorites();"></a></li><li><a title="StumbleUpon" class="option1_32" style="background-position:-224px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.stumbleupon.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&title=NI%20BINAMU13.COM"></a></li><li><a title="Delicious" class="option1_32" style="background-position:-32px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://delicious.com/post?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;title=NI%20BINAMU13.COM&amp;notes=Kwa%20wengi%20siku%20hizi%20anajulikana%20kama%20Binamu.Lakini%20alipoingia%20rasmi%20kwenye%20ulimwengu%20wa%20muziki%20aliitwa%20MwanaFalsafa.Jina%20lake%20kamili%20ni%20Hamisi%20Mwinjuma%28pichani%29.Ni%20mshindi%20wa%20tuzo%20maarufu%20za%20Kili.%0ATangu%20aingie%20kwenye%20fani%20ya%20muziki%2Csifa%20moja%20ambayo%20a"></a></li><li><a title="Google Reader" class="option1_32" style="background-position:-224px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/reader/link?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;title=NI%20BINAMU13.COM&amp;srcURL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;srcTitle=BongoCelebrity+"></a></li><li><a title="LinkedIn" class="option1_32" style="background-position:-288px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.linkedin.com/shareArticle?mini=true&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;title=NI%20BINAMU13.COM&amp;source=BongoCelebrity+&amp;summary=Kwa%20wengi%20siku%20hizi%20anajulikana%20kama%20Binamu.Lakini%20alipoingia%20rasmi%20kwenye%20ulimwengu%20wa%20muziki%20aliitwa%20MwanaFalsafa.Jina%20lake%20kamili%20ni%20Hamisi%20Mwinjuma%28pichani%29.Ni%20mshindi%20wa%20tuzo%20maarufu%20za%20Kili.%0ATangu%20aingie%20kwenye%20fani%20ya%20muziki%2Csifa%20moja%20ambayo%20a"></a></li><li><a title="BlinkList" class="option1_32" style="background-position:0px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.blinklist.com/index.php?Action=Blink/addblink.php&amp;Url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;Title=NI%20BINAMU13.COM"></a></li><li><a style="cursor:pointer" rel="nofollow" onMouseOut="fixOnMouseOut(document.getElementById('sociable-post-1387'), event, 'post-1387')" onMouseOver="more(this,'post-1387')"><img style='margin-top:9px' src='http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/more.png'></a></li></ul><div onMouseout="fixOnMouseOut(this,event,'post-1387')" id="sociable-post-1387" style="display:none;">   

    <div style="top: auto; left: auto; display: block;" id="sociable">



		<div class="popup">

			<div class="content">

				<ul><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Myspace" class="option1_32" style="background-position:0px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.myspace.com/Modules/PostTo/Pages/?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;t=NI%20BINAMU13.COM"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Digg" class="option1_32" style="background-position:-64px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://digg.com/submit?phase=2&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;title=NI%20BINAMU13.COM&amp;bodytext=Kwa%20wengi%20siku%20hizi%20anajulikana%20kama%20Binamu.Lakini%20alipoingia%20rasmi%20kwenye%20ulimwengu%20wa%20muziki%20aliitwa%20MwanaFalsafa.Jina%20lake%20kamili%20ni%20Hamisi%20Mwinjuma%28pichani%29.Ni%20mshindi%20wa%20tuzo%20maarufu%20za%20Kili.%0ATangu%20aingie%20kwenye%20fani%20ya%20muziki%2Csifa%20moja%20ambayo%20a"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Reddit" class="option1_32" style="background-position:-128px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reddit.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;title=NI%20BINAMU13.COM"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Google Bookmarks" class="option1_32" style="background-position:-192px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/bookmarks/mark?op=edit&amp;bkmk=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;title=NI%20BINAMU13.COM&amp;annotation=Kwa%20wengi%20siku%20hizi%20anajulikana%20kama%20Binamu.Lakini%20alipoingia%20rasmi%20kwenye%20ulimwengu%20wa%20muziki%20aliitwa%20MwanaFalsafa.Jina%20lake%20kamili%20ni%20Hamisi%20Mwinjuma%28pichani%29.Ni%20mshindi%20wa%20tuzo%20maarufu%20za%20Kili.%0ATangu%20aingie%20kwenye%20fani%20ya%20muziki%2Csifa%20moja%20ambayo%20a"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="HackerNews" class="option1_32" style="background-position:-256px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://news.ycombinator.com/submitlink?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;t=NI%20BINAMU13.COM"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="MSNReporter" class="option1_32" style="background-position:-352px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reporter.es.msn.com/?fn=contribute&amp;Title=NI%20BINAMU13.COM&amp;URL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;cat_id=6&amp;tag_id=31&amp;Remark=Kwa%20wengi%20siku%20hizi%20anajulikana%20kama%20Binamu.Lakini%20alipoingia%20rasmi%20kwenye%20ulimwengu%20wa%20muziki%20aliitwa%20MwanaFalsafa.Jina%20lake%20kamili%20ni%20Hamisi%20Mwinjuma%28pichani%29.Ni%20mshindi%20wa%20tuzo%20maarufu%20za%20Kili.%0ATangu%20aingie%20kwenye%20fani%20ya%20muziki%2Csifa%20moja%20ambayo%20a"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Sphinn" class="option1_32" style="background-position:-192px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://sphinn.com/index.php?c=post&amp;m=submit&amp;link=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Posterous" class="option1_32" style="background-position:-64px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://posterous.com/share?linkto=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;title=NI%20BINAMU13.COM&amp;selection=Kwa%20wengi%20siku%20hizi%20anajulikana%20kama%20Binamu.Lakini%20alipoingia%20rasmi%20kwenye%20ulimwengu%20wa%20muziki%20aliitwa%20MwanaFalsafa.Jina%20lake%20kamili%20ni%20Hamisi%20Mwinjuma%28pichani%29.Ni%20mshindi%20wa%20tuzo%20maarufu%20za%20Kili.%0ATangu%20aingie%20kwenye%20fani%20ya%20muziki%2Csifa%20moja%20ambayo%20a"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Tumblr" class="option1_32" style="background-position:-256px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.tumblr.com/share?v=3&amp;u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F05%2F12%2Fni-binamu13com%2F&amp;t=NI%20BINAMU13.COM&amp;s=Kwa%20wengi%20siku%20hizi%20anajulikana%20kama%20Binamu.Lakini%20alipoingia%20rasmi%20kwenye%20ulimwengu%20wa%20muziki%20aliitwa%20MwanaFalsafa.Jina%20lake%20kamili%20ni%20Hamisi%20Mwinjuma%28pichani%29.Ni%20mshindi%20wa%20tuzo%20maarufu%20za%20Kili.%0ATangu%20aingie%20kwenye%20fani%20ya%20muziki%2Csifa%20moja%20ambayo%20a"></a></li></ul>			

			</div>        

		  <a style="cursor:pointer" onclick="hide_sociable('post-1387',true)" class="close">



		  <img onclick="hide_sociable('post-1387',true)" title="close" src="http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/closelabel.png">

		  </a>

		</div>

	</div> 

  </div></div><div class='sociable' style='float:none'><ul class='clearfix'><li id="Twitter_Counter"><a href="https://twitter.com/share" data-text="NI BINAMU13.COM - http://www.bongocelebrity.com/2008/05/12/ni-binamu13com/ (via #sociablesite)" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2008/05/12/ni-binamu13com/" class="twitter-share-button" data-count="horizontal">Tweet</a><script type="text/javascript" src="//platform.twitter.com/widgets.js"></script></li><li id="Facebook_Counter"><iframe src="//www.facebook.com/plugins/like.php?href=http://www.bongocelebrity.com/2008/05/12/ni-binamu13com/&send=false&layout=button_count&show_faces=false&action=like&colorscheme=light&font" scrolling="no" frameborder="0" style="border:none; overflow:hidden;height:32px;width:100px" allowTransparency="true"></iframe></li><li id="Google_+"><g:plusone annotation="bubble" href="http://www.bongocelebrity.com/2008/05/12/ni-binamu13com/" size="medium"></g:plusone></li><li id="LinkedIn_Counter"><script src="http://platform.linkedin.com/in.js" type="text/javascript"></script><script type="IN/Share" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2008/05/12/ni-binamu13com/" data-counter="right"></script></li><li id="StumbleUpon_Counter"><script src="http://www.stumbleupon.com/hostedbadge.php?s=2&r=http://www.bongocelebrity.com/2008/05/12/ni-binamu13com/"></script></li></ul></div><!-- End Sociable -->]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.bongocelebrity.com/2008/05/12/ni-binamu13com/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>98</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>KWA KINA NA FREDDY MACHA</title>
		<link>http://www.bongocelebrity.com/2008/01/07/kwa-kina-na-freddy-macha/</link>
		<comments>http://www.bongocelebrity.com/2008/01/07/kwa-kina-na-freddy-macha/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 07 Jan 2008 05:10:57 +0000</pubDate>
		<dc:creator>bongocelebrity</dc:creator>
				<category><![CDATA[Blogs]]></category>
		<category><![CDATA[Historia]]></category>
		<category><![CDATA[Mahusiano/Jamii]]></category>
		<category><![CDATA[Majarida/Magazeti]]></category>
		<category><![CDATA[Mawazo/Tafakuri]]></category>
		<category><![CDATA[Mtandao]]></category>
		<category><![CDATA[Muziki]]></category>
		<category><![CDATA[Sanaa/Maonyesho]]></category>
		<category><![CDATA[Uandishi]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://bongocelebrity.com/2008/01/07/kwa-kina-na-freddy-macha/</guid>
		<description><![CDATA[&#160; Kwa miaka nenda rudi, tangu miaka ya sabini,jina la Freddy Macha (pichani) limekuwa sio geni miongoni mwa wasomaji mbalimbali wa magazeti, vitabu vya hadithi fupifupi,wapenzi wa muziki na pia sanaa ya ushairi nchini Tanzania. Iwe unamfahamu Freddy kupitia muziki wake,makala zake au mashairi yake, utakubaliana nasi kwamba Freddy ni mojawapo ya hazina tulizonazo linapokuja [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p class="MsoNormal">&nbsp;</p>
<div style="text-align:center;"><img src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/01/freddy-machabc1.jpg" height="336" width="448" /></div>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Kwa miaka nenda rudi, tangu miaka ya sabini,jina la <a href="http://freddymacha.com/" target="_blank"><b>Freddy Macha</b></a> (pichani) limekuwa sio geni miongoni mwa wasomaji mbalimbali wa magazeti, vitabu vya hadithi fupifupi,wapenzi wa muziki na pia sanaa ya ushairi nchini Tanzania. Iwe unamfahamu Freddy kupitia muziki wake,makala zake au mashairi yake, utakubaliana nasi kwamba Freddy ni mojawapo ya hazina tulizonazo linapokuja suala zima la usanii. Wengi miongoni mwa wasomaji wa makala zake katika magazeti ya  <i>The Guardian</i> na <i>Mwananchi</i> nchini Tanzania, wanakiri kwamba makala za Freddy huwa ni mojawapo ya sababu zinazowafanya wakati mwingine wadamke asubuhi na mapema ili mradi tu wasikose nakala za magazeti hayo hususani siku zinazochapishwa makala zake.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Wapenzi wengi wa muziki,ushairi, tamthiliya na ngoma mtakuwa mnamkumbuka Freddy Macha tangu  alipokuwa na kundi la <b>Sayari</b>. Kundi hilo ambalo lilitamba sana mwanzoni mwa miaka ya themanini, ni mojawapo ya vikundi vichache vya sanaa nchini Tanzania vilivyopata mafanikio sio tu nchini Tanzania bali pia katika medani za kimataifa. Sayari liliwahi kufanya ziara kadhaa za kimaonyesho katika nchi mbalimbali za nje hususani za Ulaya enzi hizo. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Kwa upande wa uandishi,Freddy Macha alianza kunoa kalamu katika magazeti ya <i>Uhuru na Mzalendo</i> na baadaye kuwa mwanasafu(columnist) wa gazeti la kila jumapili la <i>Sunday News</i> hadi mwaka 1984.Freddy amewahi kushinda tuzo kadhaa za uandishi ikiwemo ile ya Ushairi ya BBC mwaka 1981 na hadithi fupi fupi ya Jumuiya ya Madola( Commonwealth of Nations) ya mwaka 1996. </span></p>
<p class="MsoNormal"> <span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Hivi karibuni, baada ya kumsaka kwa muda mrefu, tulipata nafasi ya kufanya mahojiano ya kina na mwandishi/mwanamuziki/mwalimu huyu ambaye hivi sasa anaishi London nchini Uingereza. Sasa kutokana na ukweli kwamba Freddy ni mmojawapo miongoni mwa wale watu ambao tunaweza kuwaitwa &#8220;wenye vipaji vingi&#8221;,tumeamua kuyagawa mahojiano yetu naye katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza, ambayo ndiyo hii unayoisoma leo, tumeongea naye zaidi kuhusu kazi zake za uandishi.Sehemu ya pili ambayo itawajieni baadaye kidogo,tuliongea naye kuhusu muziki,jamii na mengineyo kadha wa kadha.  </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Unataka kujua Freddy ametokea wapi?Amepitia mambo gani mpaka kufikia hapo alipo? Anasemaje kuhusu uhuru wa vyombo vya habari, uandishi wa leo akilinganisha na ule wa zamani? Kwanini kitabu chake cha hivi karibuni amekiita <i>Mpe Maneno Yake</i>? Unafahamu kwamba Freddy aliwahi “kuzamia meli”?Ilikuwaje? Anasemaje kuhusu dhana za mawasiliano kama blogs? Kwa hayo na mengineyo mengi, fuatana nasi katika sehemu hii ya kwanza ya mahojiano yetu naye;</span><span id="more-802"></span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Karibu sana ndani ya BongoCelebrity</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Ahsanteni&#8230;mambo?</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Poa kabisa. Tunayo furaha kubwa kupata nafasi ya kuzungumza nawe hivi leo.Labda tuanze kwa kupata historia yako kwa kifupi.Ulizaliwa wapi,lini,ukasomea wapi nk</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">: Nilizaliwa Old Moshi, mwaka 1955; wazazi wangu walihama hama kutokana na kazi ya Baba ya udaktari na walipiga muziki, Mama akiwa mwimbaji. Tuliishi Moshi mgombani na Bumbuli kule Tanga. Nilisoma huko huko Mgombani (Wachagga tunaita shamba mgombani shauri ya migomba na kahawa na mifugo); hadi mwaka 1967. Nikiwa darasa la sita nilihamia Arusha, shule ya Kaloleni. Aliyekuwa sasa mlezi wangu ni Shangazi Sara Materu ambaye alikuwa Mwalimu Mkuu maarufu wa Shule ya sekondari ya Arusha &#8230;akiitwa Mama Materu enzi hizo. Alichanganya tabia na mwenendo (ambao hadi leo anao) wa elimu bora, nidhamu, mapenzi na alinishughulikia vizuri sana. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Nilifaulu na kuingia Sekondari Ilboru, hadi mwaka 1972, baadaye nikaendelea sekondari Mzumbe, Morogoro kidato cha tano na sita hadi 1974. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Enzi hizo tulitakiwa kisheria kujiunga na jeshi la kujenga taifa (JKT) baada ya masomo. Niliingia kambi ya Mafinga mkoani Iringa na kisha kuanza kazi kwenye gazeti la Uhuru mwaka 1976. Kazi yenyewe sikuiomba, niliitiwa kutokana na makala na barua nilizokuwa nikiandika tangu nikiwa shuleni.</span></p>
<p class="MsoNormal">&nbsp;</p>
<div style="text-align:center;"><img src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/01/freddymachabc3.jpg" height="299" width="448" /></div>
<div style="text-align:center;">Freddy Macha(wa pili toka kushoto) enzi akiwa kidato cha nne pale Lutheran Secondary School, Ilboru,Arusha mwaka 1972.Wengine kwenye picha kutoka kushoto ni Mohamed Miro, Tony Sarwatt(marehemu), Barnabas &#8220;Bandindo&#8221;Sengati(marehemu) na John Meciri(marehemu). Picha na Emmanuel Yuda.</div>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Ingawa una vipaji vingi mbalimbali,kama ambavyo tutaviongelea vyote katika mahojiano haya,wengi tunakufahamu zaidi kama mwandishi.Nini kilikuvutia kuingia katika fani ya uandishi?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">: Najulikana kama mwandishi nyumbani Bongo, lakini nchi za nje kazi yangu kuu ni mwanamuziki. Vitu hivi viko katika damu. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Nikiwa mdogo sikuwa mzungumzaji sana&#8230;nilipenda kusoma, kusikiliza, kutazama watu, kuchanganyikana nao lakini kuwasoma&#8230;Katika familia kulijaa waandishi, wataalamu na wanamuziki. Babu yangu (Mchungaji Anaeli Macha ) alikuwa mchungaji maarufu na mwandishi ,akachapisha vitabu kadhaa vya tabia, dini, familia na jamii. Pia shangazi zangu wengi walinipa moyo toka utotoni. Nakumbuka mmoja wao,Shangazi Eva, alikuwa akisifia barua zangu akisema “Freddy akiandika barua ni kama kitabu.”</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Uandishi rasmi wa kijumuiya ulianza nikiwa kidato cha pili. Ilikuwa hivi. Nilipokuwa Ilboru nilikuwa nikisaidia baadhi ya wenzangu kuandika barua zao za mapenzi kwa akina dada (“girlfriends”) nikaanza<span>  </span>kudai pesa. Wakati huo nilikuwa mwanachama wa kikundi cha vijana tukijiita “The Gringos.” Kuna wakati tulipigwa na wahuni na wanajeshi baada ya kuwaandikia wasichana fulani waliogombana na mmoja wetu barua. Zile barua nyingi niliziandika kutokana na ushauri wa kikundi hicho chetu.Zilikuwa si mchezo. Tuliishia kupigwa kishenzi na pia chapwa viboko vya faru na kulazwa hospitali.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Nilipokuwa nikisoma Mzumbe tulikuwa na bendi mbili. Ya walioimba Kiingereza, “Earthquakes” (niliyokuwepo) ikiongozwa na mkimbizi na mpigania Uhuru wa Afrika Kusini, Tabiso Leshoai na Mike Sikawa (aliyekuja kuwa mwandishi Daily News siku hizi yuko BBC anaandikia This Day)&#8230;ya pili ilikuwa ya muziki wa Kiswahili. Zote zilipewa moyo na marehemu Mbaraka Mwinshehe aliyekuwa akija pale Mzumbe kupiga piga dansi letu na dada zetu, wapenzi wetu wa shule ya Kilakala.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Lazima nisisitize suala la mtoto kuwa na waalimu wazuri. Moja ya mchango mkubwa katika elimu yangu ulikuwa pia waalimu. Mwalimu Mkuu, marehemu Lema na Mushi (“Chesti”) aliyemrithi, walikuwa wakali na walituchapa viboko na kutupa nidhamu ya kimaisha. Ilboru ilikuwa na waalimu wengi toka mataifa mbalimbali. Mmoja wao aliyenihamasisha kupenda zaidi fasihi ni Mama Chitepo aliyekuja kuwa Waziri wa Elimu nchini Zimbabwe.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Vile vile shule ya Mzumbe. Ilikuwa chimbuko la mwamko wangu kama mwandishi na mwana-jamii hasa kutokana na baadhi ya waalimu wazuri tuliokuwa nao. Namkumbuka mwalimu wangu wa fasihi marehemu John Mdakie(huyu bahati mbaya aliuawa baadaye na majambazi Dar Es Salaam ingawa alikuwa mtetezi mkubwa wa walalahoi) na mwandishi Nizar Visram. Visram alitufundisha kusoma vitabu na kuvijadili. Pia alikaribisha wataalamu mbalimbali wa ngazi za juu, kimataifa, kuja kuongea na kujibu maswali yetu. Kati yao ni mwandishi mashuhuri, mwanahistoria wa Kigayana, marehemu Profesa Walter Rodney (aliyeandika kitabu maarufu “How Europe Underdeveloped Africa”) na mshairi maarufu wa Afrika Kusini, Kgotsitsile. Huyu alifungwa mara kadhaa na makaburu.<span>  </span></span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Mbali na uandishi kuwa katika damu au katika familia yenu,kwa vyovyote vile kuna mwandishi au waandishi ambao ulikuwa ukipenda kuwasoma tangia utotoni.Unaweza kututajia majina yao?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Kwanza kabisa katika familia, Babu Mchungaji Macha mwenyewe. Halafu hapo hapo Bongo nakumbuka darasa la Sita nikisoma mashairi ya Shaaban Robert nikajiuliza hivi mtu anawezaje kuandika na kuwa na lugha nzuri kiasi hiki? Nakumbuka shairi la “Titi la Mama Litamu Hata likiwa la Mbwa.” Baadaye nilipenda sana kusoma magazeti&#8230;hasa kutoka Kenya. Moja liliitwa “Baraza” (miaka ya sitini).Gazeti lile lilikuwa la umbea na mastore kibao. Nina miaka 12-13 wakati huo. Lilinisisimua sana.</span><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Tulisoma pia magazeti ya “Film” yaliyokuwa na mbabe Spear na katili Rabon Zollo. Karibuni mwanablogu maarufu Michuzi katoa picha mbalimbali kusisitiza mchango wa magazeti haya ya zamani kusaidia lugha ya vijana enzi hizo.<b> </b></span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Baada ya hapo nilianza kusoma riwaya za Kiswahili na Kiingereza. Akina James Hadley Chase&#8230;Ian Fleming (aliyetunga James Bond) Kisha, Waafrika akina Chinua Achebe, Ngugi Wa Thiong&#8217;o (enzi hizo akiitwa James Ngugi), Euphrase Kezilahabi.Sasa niko sekondari&#8230;kidato cha pili&#8230;nasoma magazeti, <span> </span>riwaya, nakwenda sinema. Nakumbuka kidato cha kwanza na cha pili nilipewa tuzo na waalimu kama msomaji wa vitabu vingi. Sinema nilianza toka utotoni (wazazi wangu walikuwa wakinipeleka Plaza na Everest pale Moshi) nilipenda sana sinema na kujiunga na michezo ya kuigiza, Ilboru.</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Kwa hiyo mbali na uandishi unakumbuka ulitaka kuwa nani ukubwani?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Mbali na uandishi nilitaka, toka nikiwa mtoto, kuwa mwanamuziki. Nakumbuka nilikwenda kuona sinema ya Elvis pale Plaza, Moshi nikiwa na baba na mama. Nikaona yale magitaa, zile nyimbo, zile bichi na wanawake wakicheza nk. Wakati huo nina miaka minane nafikiri. Toka hapo nikasema lazima niwe mwanamuziki. Hii ni ukiachilia mbali kwamba kila siku Baba akitoka kazini au hata akiwa katika breki ya kula chakula cha mchana wakati akingojea mama amalize kupika (yuko na magwanda yake ya udaktari) anacharaza gitaa akisubiri msosi. Ile yote ilinipa hamasa; motisha.Wakati nikiwa sekondari gitaa na utunzi wa muziki ukaja kuwa moja ya njia za kujielezea hisia zangu. Nikikasirika au nikitaka kujieleza nachukua gitaa.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Baadaye ikawa kama natumia uandishi kupikicha muziki na muziki kupikicha uandishi. Nitafafanua mbele kwanini vitu hivi viwili havibandukani hadi leo.</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> <b>Nini kumbukumbu yako ya siku ya kwanza kama mwajiriwa wa gazeti la serikali,Uhuru,ulipoanza mwaka 1976?Ilikuwaje siku hiyo?</b></span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Duh&#8230;ilikuwa raha tupu. Niwakumbushe wasomaji miaka ya 70 ilivyokuwa Bongo. Lipo vuguvugu kila mahali. Vijana tuna hamasa,tunataka kubadili jamii.Tunamsikiliza Mwalimu Nyerere akisema nchi inahitaji kuondoa umaskini kuwa wakulima na wafanyakazi ni watu wa mbele.Tulikuwa wengi tuliotoka Mzumbe, Tabora, Mkwawa, nk.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Nilikuwa na akina marehemu Yahya Buzaragi (aliyekuja kuwa Mhariri wa Uhuru) , Marehemu Profesa Chachage (yeye aliingia fani ya uchapishaji vitabu baadaye akaendelea Chuo Kikuu na kuwa Mhadhiri maarufu). Akina Sengondo Mvungi, Harrison Mwakyembe,Palamagamba Kabudi.Wote hawa siku hizi wataalamu wakubwa nchini. Wana hamasa bab kubwa. Sasa siku hiyo ya kwanza&#8230;1976.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Nakumbuka nilikuwa nimevalia shati langu la kitenge na suruali ya mtumba nyeusi (niliinunua Kariakoo) viatu vya safari buti.Nimeingia,kijana mbichiiii, miaka 21. Nikawakuta akina Abdi Mushi, Salva Rweyemamu (bado yupo huyu) Mzee Stephen Msuya, na gwiji la uandishi Ndimara Tegambwage.Wamekaa pale wanatupa moyo. Sijui kutumia taipu wala nini.Enzi hizo mashine za kupiga taipu za kelele na zina vibonyezo vigumu.Wakawa wanatuonyesha mambo. Siku hiyo hiyo nikapewa kazi ya kwenda kumhoji mtu huku nimeongozana na mpigapicha bab kubwa marehemu Awadh Shebe.Huyu alikuwa si mchezo. Tuliewana sana. Awadhi alikuwa msanii wa kamera.Walikuwepo wengine akina Khatibu Ali <span> </span>lakini Awadh duh alikuwa pia kijana mwenzangu. Nakumbuka kuna picha alipiga mpirani wakati wa mechi ya Yanga na Simba (enzi hizo si mchezo). Picha ile ilizungumziwa miaka na miaka. Ilikuwa picha ya tikitaka.Brazili wanaita kipepeo (“Bolboleta”); kiingereza wanaiita “Mkasi”&#8230;. bahati mbaya Bongo hadi leo hatutoi tuzo kwa waandishi na wasanii bora. Awadhi alistahili.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Bila kusahau kusema, Awadhi ndiye aliyenifanya nianze kujifunza Kifaransa.Tulikuwa kila tukiwahoji watu wasiojua Kiingereza, anasema duh lazima tujifunze lugha zao.</span></p>
<p class="MsoNormal">&nbsp;</p>
<div style="text-align:center;"><img src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/01/freddymachabc2.jpg" height="298" width="448" /></div>
<p class="MsoNormal"><span>Freddy (katikati kalamu mkononi) , akifanya kazi Uhuru na Mzalendo, akimhoji Meya wa jiji la Amsterdam katika uwanja wa ndege wa Nyerere, Dar Es Salaam mwaka 1978. (Picha na Khatibu Ally)</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Tukiwa bado kwenye suala la uandishi.Unadhani waandishi na uandishi wa leo wana tofauti gani na ule wa enzi zile ulipokuwa unaanza kuandika?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM: </span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"><span> </span>Kitu kilichosukuma uandishi wa enzi zile ilikuwa Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Motisha wa kutaka kuendeleza jamii,kujenga nchi,kupambana na kile Mwalimu alichoita maadui watatu : umaskini, ujinga na maradhi. Leo waandishi wanafikiria fedha. Lakini enzi hizo kulikuwa pia na waandishi wa aina hiyo lakini haikuwa mtindo kama sasa. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Tofauti nyingine kubwa ni kwamba maduka ya vitabu yaliuza vitabu. Waandishi walisomwa. Uandishi ulikuwa na faida kwa vile ukiandika mtu unasomwa. Magazeti yalikuwa mawili tu Uhuru (Kiswahili) na Daily News. Kwahiyo magazeti hayakuwa mengi kama leo. Vitabu vilisomwa zaidi. Leo kuna magazeti elfu kidogo na vitabu havisomwi, lugha mbovu. Enzi hizo hadi uandikwe magazetini lazima uwe na lugha na uwezo mzuri sana; si holela<span>  </span>kama leo. Kila mtu anajiandikia tu. Leo kuna sinema, DVD, runinga, enzi hizo hakukuwa na vitu hivi. Mimi nimeona sinema mara ya kwanza katika runinga nikiwa Nairobi,niliona maajabu. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Lakini ule uvivu wa kutotafiti mambo baina ya waandishi bado upo hadi leo. Bado waandishi wa habari hawatafiti. Wakihoji hawatafiti mada sawasawa. Lugha imekwenda chini sana.Si kwa vile waandishi hawajasoma. Wandishi wa leo wamesoma kuliko wa zamani (wengi zamani walitokea kidato cha nne); Tatizo la leo waandishi wenyewe hawasomi vitabu. Vitabu vya fasihi na mashairi ndiyo huongeza msamiati wa lugha. Kiswahili na Kiingereza vimeghafilishwa, viko butu, vimejiinamia kama kuku aliyenyeshewa mvua.</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Unaliongeleaje suala la uhuru wa vyombo vya habari enzi zile ukiwa Uhuru na Daily News na hivi leo?Ni kweli kwamba enzi zenu kila mlichoandika ilikuwa ni propaganda kwa manufaa ya watawala?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Kweli kabisa. Leo kuna uhuru wa kuandika kuliko enzi zile. Enzi hizo Mhariri Mkuu alikuwa Rais wa nchi. Leo hata blogu zinasomwa, zinaandikwa na Wabunge kama akina Zitto Kabwe, bila wasiwasi. Mwaka niliokuwa Uhuru, mawazo kama anayoandika Zitto au huyu mwandishi wa This Day, Nkwazi Mhango (ana blogu kali sana http://</span><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"><a href="http://www.mpayukaji.blogspot.com/"><span>mpayukaji.blogspot.com</span></a></span><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> ) ingekuwa ni enzi zile wangetiwa ndani moja kwa moja. Sisi tulikuwa na wasiwasi sana.Na mara nyingi tulikuwa tukijihariri kabla ya kutoa makala. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Nakumbuka siku moja mhariri wangu Uhuru (marehemu Costa Kumalija) alivyokuja mkutanoni na gazeti limechorwa chorwa rangi nyekundu na Rais. Akasema Raisi kaudhiwa na habari fulani zilizoandikwa na gazeti. Visa vya aina hiyo vilitufanya waandishi tuwe na wasiwasi. Lakini kama nilivyosema sisi vijana tulikuwa na hamasa fulani, tukifikiria jumuiya, tukifikiria maendeleo. Mimi nilikuwa na safu zangu chungu nzima.Mojawapo iliitwa Wachapa Kazi ambayo nilitafuta wananchi waliokuwa wakijitahidi. Hadi leo napenda kuendeleza sana dhamira hiyo.Kwa upande mwingine ndiyo maana nilipiga muziki, maana yale ambayo hayakuandikwa gazetini niliyageuza ,muziki, niliyaandikia mashairi.</span></p>
<p class="MsoNormal">&nbsp;</p>
<div style="text-align:center;"><img src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/01/mutabaruka-1994.jpg" height="240" width="320" /></div>
<div style="text-align:center;">
<p class="MsoNormal"><span>Freddy Macha(kulia) akimhoji mshairi maarufu wa Jamaika ambaye huwa havai viatu, yaani Mutabaruka, Brazili mwaka 1994 (Picha na Amita Macha).</span></p>
</div>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Unaweza kukumbuka kisa chochote ambacho unadhani kilikuwa ni sumu kabisa kwenye dhana nzima ya uhuru wa vyombo vya habari enzi hizo?Kwa maoni yako unadhani nini kimechangia kuboresha uhuru wa vyombo vya habari tulionao hivi leo?Kuna madhara yoyote ya kuwa na uhuru wa vyombo vya habari na pia uhuru wa kujieleza?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Kwanza suala la sumu la Uhuru wa Habari. Kumbuka hali ilivyokuwa. Mwandishi wa habari anakwenda mahali kuchukua habari <span> </span>ili awe mdomo wa serikali na uongozi. Mara nyingi zilikuwepo karamu au pati ambazo pale mwandishi unapata chochote (cha kula na kuandika) .Sasa tatizo lilikuwa hapo. Mishahara yetu ilikuwa midogo sana. Uhuru bahati nzuri waandishi tulipewa pikipiki. Alhamdulilahi. Usafiri mbaya wa Dar ulisaidiwa na zile pikipiki. Lakini baada ya kazi (yaani kuandika store) mwandishi ulichofikiria ni wapi pa kwenda kupata pombe na makulaji ya bure.Huko huko kuna kitu kinaitwa ku-lobby (leo Ulaya wanasema “networking”, wanawake huita umbea wa kirafiki). </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Baadhi ya waandishi walitia aibu. Si wote, lakini ukweli hali ya umaskini ilikufanya mtu ujisahau. Mi nikiwa kijana iko siku nililewa nimempakia mtu tukaanguka na pikipiki. Saa za manane hizo. Ukiwa kijana unaona advencha hizo. Humo humo kuna visura wa kukata na shoka. Unaingia baa na vijisenti vyako unawaka. Unarudi&#8230; hilo doa la kulewa usiku ili kupata contacts (ambayo ni sehemu mahsusi ya uandishi wa habari) ilitufanya waandishi wa Bongo tuonekane wa njaa. Lakini si wote. Baadhi ya wageni hasa katika balozi walitujua. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Sasa ukija kwenye Uhuru wa kujieleza. Ikiwa mtu una mshahara mbaya, unategemea wakubwa kwa rasilmali na maisha ni wazi kwamba unakuwa huandiki kile unachokitaka. Matokeo waandishi wengi walikuwa walevi. Unajikuta unajua siri nyingi sana za nchi, unajua makosa mengi sana yanayofanyika, unawafahamu waongo na wakweli katika ngazi za juu, lakini huthubutu kutema, kutapika, wala kupiga chafya. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Ninawafahamu jamaa chungu nzima waliopotea. Wengine tukinywa pamoja sikuwaona hadi leo. Wanapotea tu. Wanafichwa. Kitabu changu cha kwanza (Twenzetu Ulaya) kilikuwa na kisa <span> </span>cha kweli cha mtu aliyeshukiwa kuwa “njagu” (shushushu), kinaitwa Masizi. Kumbe hakuwa lolote, maskini. Alikuwa tu na yake. Akauawa Uswahilini. Ile hali ya kuogopa kusema, kuogopa kuandika, kuogopa nani atakusikia, kuogopana hata waandishi kwa waandishi.Hali hii ilizua kitu kama hofu ya moshi na mvuke (“paranoia”) ambayo imewafanya watu wa rika langu hadi leo wawe wanaogopa ogopa na kuwa waangalifu kuzidi kiasi.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Kwa mfano mimi hadi leo nikiwa katika simu hata huku ughaibuni bado nina kawasiwasi kuwa kuna mtu ananisikiliza. Kumbe haiendi hivyo. Kawaida mashushushu wana watu wanaotaka kuwajua. Na leo ukitakiwa na serikali yeyote duniani utapatikana tu,huwezi kujificha. Lakini hapa nazungumzia ule wasiwasi uliokuwa umeenea ambao niliutungia kisa kilichoitwa Masizi katika mkusanyiko huo wa Twenzetu Ulaya mwaka 1984.</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Labda kabla hatujaendelea mbele..unakumbuka makala yako ya kwanza kuchapishwa gazetini ilikuwa lini na ilikuwa ikizungumzia nini?Unakumbuka nini zaidi kuhusu siku makala yako ilipochapwa gazetini?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"></span><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Sikuanza kama mwandishi wa makala, bali utenzi (mashairi) na barua.Ya kwanza ilikuwa barua nilizokuwa nikiandika magazetini,nikiwa bado shuleni.Nyingi sikumbuki lakini iliyovuma sana &#8230;nafikiri ilikuwa suala la vitabu vya Kizungu kuzidi kuuzwa nchini kuliko vya wananchi. Ilichapwa gazeti la Kiingereza, Daily News ikasifiwa sana. Nilikuwa kidato cha tano. Mhariri wa Uhuru alipoona akawa anatuma waalimu waniambie niwaandikie. Nilianza kuandika rasmi magazetini nikiwa kidato cha tano na sita.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Wakati huo kulikuwa na vuguvugu likivuma kila mahali.Mapinduzi ya Msumbiji (enzi Samora Machel kanyakua Uhuru Msumbiji), masuala ya Idi Amin akiua watu Uganda, Karume wa Unguja kauliwa Zanzibar, (1972) wakimbizi kibao wakija Bongo (toka Marekani enzi zile “Black Panthers” ikivuma) Wapalestina, Wasoweto (ndivyo tulivyoita wakimbizi toka Bondeni) hali ya vuguvugu, ukiwa mwana fikra unakuwa pia mwanajamii, unaona fahari kuitwa mwanamapinduzi. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Nilikuwa niko tayari hata kwenda Namibia kupigana, Palestina kushika bunduki&#8230;ilikuwa si bla bla&#8230;kila mtu alikuwa moto. Ndiyo miaka hiyo migomo ikapigwa marufuku Tanzania. Shule zilikuwa zinafungwa, mameneja waonevu wanafungiwa nje&#8230;hili vuguvugu ndiyo lilinipa mshawasha wa kuandika magazetini,kutunga mashairi, nyimbo, fasihi.</span></p>
<p class="MsoNormal">&nbsp;</p>
<div style="text-align:center;"><img src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/01/freddymachabc4.jpg" height="448" width="302" /></div>
<div style="text-align:center;"></div>
<p class="MsoNormal"><span>Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mafinga, mwaka 1975 (Picha na Harold Mhando)</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Unadhani moyo huo wa kujitolea mliokuwa nao vijana wa enzi hizo,moyo huo wa kizalendo,upo mpaka hivi leo?Kama haupo nini kimetokea?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Nafikiri Vijana wote wako sawa kiwakati. Vijana kwa jumla si watu waoga. Lakini vijana pia ni watu wasioona mbali. Wanataka mabadiliko lakini hawaangalii kila kitu. Kwa mfano kuna wakati nilichana chana noti ya shilingi mia moja mbele ya Mama yangu baada ya ubishi wa kifamilia. Hii ni eti miaka kabla sijaanza kazi, nimetoka jeshini, ninakosoa utawala unaowatesa maskini.Enzi hizo shilingi mia zilikuwa nyingi kama noti ya shilingi elfu kumi leo; hata zaidi. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Vijana wa leo wanao urahisi fulani ambao enzi zetu haukuwepo. Leo unaweza kufungua blogu, unaweza kuongea na mwenzako yeyote popote pale kwa SMS au barua pepe. Leo kuna Uhuru wa kuandika, kufanya mambo, kuna urahisi wa kuelewa mambo ya kidunia. Mimi kwa mfano miaka hiyo nilikuwa nakusanya habari kupitia wageni. Chukua suala la magazeti. Kuna majarida ya fasihi ambayo leo kijana anaweza kuyashusha kutokea “Google” kirahisi. Mi nilikuwa nakutana na mtalii,namwomba akirudi kwao anitumie jarida fulani kwa mfano gazeti mashuhuri la watu weusi la Marekani, “Ebony.” Nilikuwa nalihusudu sana. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Kwa hiyo urahisi ulioko leo unawafanya vijana waweze kufanya mengi ambayo sisi tulikuwa tunaotea. Ndiyo maana baada ya kujiuzulu kazi Uhuru mwaka 1978, nikaamua sasa na mimi nataka kuwa Baharia. Nikastoawei kama wengine wote. Tukashikwa India tukarudishwa mkuku.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Zote hizo zilikuwa jitihada ambazo leo, mtu unataka kwenda nje lakini unaweza pia kujaribu mambo ili mradi uwe na fedha.Enzi hizo hata haya mawazo ya kutoka nje ilikuwa unaulizia hujui uyapate wapi. Leo, ukiingia mtandaoni mambo kibao.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Ukija kwenye suala la kujitolea.Leo itikadi au fikra iliyopo kijamii sio uanamapinduzi, uanamabadiliko, bali kutaka kuukata, kutaka fedha.Hakuna wanamapinduzi wanaotia kichaa Afrika.Enzi hizo kila ukifungua gazeti unawaona akina Samora Machel. Unamsoma Steve Biko,unamsoma Mpalestina kafanya hili na lile. Leo marapa waliovalia suruali nusu uchi, chupi nje, kama wasenge, <span> </span>ndiyo wanaonekana wababe.Lakini ubabe wao ni wa “Bling Bling” wa kutumia: pombe, mabibi, magari, shari tupu. Kijana wa leo anafikiria Bling Bling au kuwa mjeuri, pesa, kuwa mtukutu. Sisi tulikuwa tunafikiria sana kubadili jamii iwe nzuri kwa maskini. Tulikuwa tukiwaangalia akina Che Guevara, Fidel Castro, Bob Marley, Malcolm X.Tukimzungumzia Mandela akiwa jela.Hapo hapo wapo waliotaka haya ma-Bling Bling lakini hayakuwa yakionekana kiwingi kama sasa kila kona yamejazana katika mtandao, runinga nk. Lakini vijana siku zote ni vijana,wana moto. Tofauti ni mazingira yao na wakati.</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Umegusia kidogo kisa cha kustoawei.Visa vya namna hii huwa vina msisimko wa aina yake miongoni mwa vijana.Unaweza kutusimulia kidogo ilikuwaje mpaka ukaamua kustoawei?Tupe mkasa huo japo kwa kifupi kisha tutaendelea na mada zetu za leo tafadhali.</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Hamna noma. Kwanza kabisa ilikuwa siri kubwa. Ukweli sijawahi kuliongelea suala hili katika hadhara hadi karibuni maana hata familia yangu haikujua. Wala girlfriend wangu enzi hizo hakujua. Nilikuwa nimechoka. Nimeacha kazi Uhuru shauri ya uzembe wa utawala. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Nilipoacha kazi, wenzangu kama wanane (au zaidi nasikia) wakafuata. Sasa hakukuwa na pengine pa kwenda. Nilitaka sana kuanzisha gazeti langu. Mtaji sina. Pesa itatoka wapi? Enzi ambazo biashara hazikuruhusiwa na uhuru wa kibiashara haukuwepo. Ah ikawa sasa wazo ni kuwa baharia. Zilikuwepo meli kibao pale bandarini. Kuingia ndani ni kuwapa jamaa chochote. Kifupi tulikuwa kama saba hivi. Tukajichomeka. Tumebeba mandazi,vitumbua, maji ya kunywa (enzi hizo hakuna haya maji ya chupa ya kuuzwa Bongo) tumeingia kule na nguo hizo hizo.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Kujisaidia ni humo humo baharini, mnapeana zamu ya kugadi usiku, mmejificha ndani ya mananihii ya kufunika bidhaa za meli. Wengine wanatapika, wengine wanaona baridi, hasa tulivyofika kati kati ya Bahari ya Hindi kupita visiwa vya Komoro. Mimi nilikuwa mtu wa mazoezi (hadi leo) nikishikwa kipipa ninapiga “mapush-up” yangu mia tatu&#8230;najisikia mwepesi na mwenye imani. Kufika Bombay sasa ikawa kazi ya kuvizia tutoke. Nchi yenyewe hatuijui. Lugha hatuongei. Pale kiama. Tumengoja usiku kucha. Kutoka mmoja mmoja.Wengine wakashikwa, wengine tukapotelea mitaani. Sasa pesa hatuna. Mtu unatafuta namna ya kupata kazi. Mipango hakuna. Tunajua tu kazi za meli rahisi.Inakuwa unaulizia kilibeneke,unabahatisha. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Tumekaa pale wiki moja.Namna tulivyokula wala haielezeki.Lakini tulikula. Wengine kama miye tulishapitia jeshini kwa hiyo &#8220;ujanja wa porini&#8221; tushajifunza.Lakini hatima yake ilikuwa kushikwa. Kurudishwa hadi Kenya. Kupigwa kishenzi. Hadi leo nina makovu. Kimya kimya kupandishwa katika mabasi, kutokea Tanga,kupotelea mitaani. Hapo ilibidi nivae kofia ya uandishi. Maana unaona ni kama “advencha” umepata cha kuandika. Lakini siri yake kubwa ni hii. Usitoke nchi yako kama hujui unakokwenda. Huna mpango. Hiyo ilikuwa moja ya nguzo zangu za kuandika Twenzetu Ulaya.Kuwaonya wenzangu kuwa usiondoke bila mpango.</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Duh..kisa cha kusisimua sana hicho.Tutapenda kusikia zaidi next time.Tuendelee</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> OK. Kuna mengi zaidi lakini iko siku labda&#8230;katika biografia yangu</span></p>
<p class="MsoNormal">&nbsp;</p>
<div style="text-align:center;"><img src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/01/freddy-machabc.jpg" height="322" width="448" /></div>
<div style="text-align:center;">
<p class="MsoNormal"><span>Freddy akitongoa moja ya shairi lake linalopendwa linalozungumzia urasimu liitwalo Papers! Papers! Papers! Katika tamasha la sanaa na muziki wa mtu mweusi, mjini Copenhagen, Denmark mwaka 1985 (Picha na Jørn Stjerneklar).</span></p>
</div>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Tukirudi kwenye uandishi.Kwa maoni yako unadhani uandishi ni kipaji au ni kitu ambacho mtu yeyote anaweza kujifunza na kuweza?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Uandishi ni kipaji, ni kuzaliwa hapo hapo ni kazi. Kila mwanadamu anao uwezo wa kuelezea jambo. Namna ya kuelezea inategemea kipaji, ufundi, silika na hulka. Wengine wazuri wa kusema. Wengine wazuri wa kuimba, wnegine wanachora, baadhi wanaandika. Kama nilivyosema nikiwa mdogo sikuwa mzungumzaji. Leo nimekuwa mzungumzaji sana, hususan shauri ya kufundisha, kuwa mwalimu na mwanamaonyesho.Lakini nimegundua siri moja kubwa. Ukitaka kuwa mzungumzaji mzuri, mwandishi mzuri, mstareheshaji mzuri, mwanafasihi poa, shurti uwe msikilizaji mzuri. Hakuna mpiga picha mzuri wa jamii kama mwandishi. Maana hukaa pale kimya wala hamumjui. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Kazi ya uandishi inaboreshwa pia na kusoma. Linton Kwesi Johnson, mshairi wa Kijamaika alikuwa akiwaasa waandishi chipukizi hapa London miaka michache iliyopita. Akasema mbona wanamuziki wanasikiliza sana muziki? Kusudi wawe mahiri. Mwandishi asiyesoma alisema Linton Kwesi, ni kama bubu asiyejua kutumia ishara za vidole. Maana msamiati utatoka wapi?</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Uandishi ni kazi lakini pia ni wajibu kwa watu wako, kwa jamii yako, kwa uhai na kwako wewe mwenyewe. Maana mwandishi unaopoandika unajijua zaidi. Unajielewa zaidi. Ni kama kuoga au kujichana nywele. Unajichana ili upendeze, lakini hapo hapo unajiangalia angalia unaelewa kichwa chako kiko hivi&#8230;</span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Sasa kumekuwepo na hoja kwamba siku hizi nchini Tanzania hakuna tena waandishi mahiri,hususani wa riwaya, kama ilivyokuwa enzi za akina Elvis Musiba, Katalambula, Kezilahabi nk.Je unakubaliana na hoja hiyo?Kwanini?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Kwanza kabisa vitabu haviuziki. Dar nzima kuna maduka mangapi ya vitabu au maktaba ngapi za vitabu vya Kiswahili? Utashangaa jinsi ambavyo sera ya elimu inahusisha tu wale walioko mashuleni. Lakini jamii inahitajika kuwa inasoma na kujielemisha hadi uzeeni. Ndiyo maana wenzetu wa nchi tajiri wanaendelea,wanatunga,wanagundua vitu, wanaishi maisha marefu sisi tunazidi kufa vijana (umri wa wastani leo ni miaka 45, Tanzania, ilhali Uingereza ni 75-80!) wanatajirika nk. Hii ni kwa sababu wanasoma. Sisi hatusomi, si kwa vile hatutaki, ila kwa kuwa hakuna sehemu ya kuuza vitabu. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Nilipomhoji mwandishi makini wa Unguja, Adam Shafi (mtunzi wa Kuli, Kasr ya Mwinyi Fuadi, Vuta Nkuvute na Haini) nilimuuliza swali hilo. Akasema ukisafiri mikoani siku hizi huwezi hata kituo kimoja kununua kitabu. Ukisafiri nchi za ughaibuni katika kila kituo utakuta maduka kadhaa ya aina kadhaa, ya kununua vitabu, majarida na vyakula. Kwetu kinachokutwa ni vyakula tu.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Kwa hiyo kwa kuanzia waandishi hawana pa kuuzia vitabu. Chukua kitabu changu cha karibuni, Mpe Maneno Yake&#8230;watu chungu nzima wananiandikia wanataka kukinunua lakini hawajui wapi wakipate. Nimewajibika mwenyewe (kama mfanyabiashara eti) kukiuza,utadhani, njugu.<span>  </span>Kutembea navyo&#8230;kazi gani hii? Waandishi ni wasanii wanachotaka ni kutunga&#8230;si kubeba soko la Kariakoo begani.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Ukiongea na wachapishaji leo Bongo wanakuambia vitabu vinavyouza ni vile vitavyotumika eti mashuleni. Si vibaya hata kidogo; lakini inapaswa viwepo pia vitabu vya watu wazima. Badala yake watu wazima wanachosoma ni chupa za bia, mitungi ya mbege, gongo na matap tap! Nchi itaendelea kweli?</span></p>
<p class="MsoNormal">&nbsp;</p>
<div style="text-align:center;"><img src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/01/freddymachabc5.jpg" height="252" width="448" /></div>
<div style="text-align:center;">
<p class="MsoNormal"><span>Baadhi ya kazi za mwandishi na mwanamuziki Freddy : vitabu vya hadithi fupi (Twenzetu Ulaya, Mpe Maneno Yake) albam ya Constipation na utenzi wa mashairi ya Kiingereza, Papers! Papers! Papers! (Picha na Ona Macha)</span></p>
</div>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Umegusia suala la kitabu chako cha hivi karibuni kiitwacho <i>Mpe Maneno Yake</i> ambacho nimemaliza kukisoma hivi karibuni.Kwanza kabisa nikupe hongera kwa kitabu hicho chenye visa motomoto.Pia ningemshauri msomaji yoyote wa mahojiano haya afanye juu chini akinunue na kukisoma.Swali; Mpe Maneno Yake ni mchanganyiko wa visa chungu mbovu,miaka nenda miaka rudi.Ulikuwa unajaribu kufikisha ujumbe gani hasa kwa jamii?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Kitabu kinapatikana maduka ya vitabu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam au TPH mtaa wa Samora Avenue. Ukitaka pia waweza kuwasiliana moja kwa moja na wachapishaji (E&amp; D Limited) kupitia simu namba ( +255) 78481-8282 au (+255) 754275347. Ongea na Kitunga au Lema, mjini Dar es Salaam</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Nashukuru kwa kusifia&#8230;maana wewe pia mwandishi mzuri napenda blogu zako zote&#8230;na hili ni suala muhimu sana&#8230;waaandishi kuelezana ukweli kuhusu maandishi. Bongo tunayo tabia ya kuogopa kusifiana eti utampa mwenzio kichwa.Kumbe si kumpa mtu kichwa bali kuendelezana. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Sikupanga niandike kitabu hiki. Kama nilivyosema awali, wakati nikiwa ripota wa Uhuru na Mzalendo baadaye nikawa naandikia magazeti mengine (New Outlook, Nchi Yetu, Daily News, Sunday News, Mfanyakazi, Kiongozi,nk) kuna habari au story ambazo hazikuwa zikichapwa. Hizi nilizigeuza nyimbo, mashairi (nikazitongoa kupitia kikundi changu enzi hizo cha Sayari) au kuzikusanya ili ziwe kitabu baadaye. Mwaka 1981 mathalani nilipata tuzo ya ushindi wa mashairi ya Kiingereza toka BBC, kati ya tenzi zilizoshinda zilitokana na visa ambavyo vilikataliwa kuandikwa magazetini. Sasa basi kwa kuwa nimezunguka sana, zipo store nyingi namna hii. Mpe Maneno Yake ni asilimia ndogo tu ya<span>  </span>mkusanyiko nilio nao. Kila siku miye huandika kitu : wimbo, shairi, hadithi, wazo au makala. Haipiti siku au juma bila kuwa na kitu. Uhai kwangu ni kalamu ya uandishi na utunzi.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Ukitazama kisa cha kwanza katika Mpe Maneno Yake ni mwaka 1976, wakati nikiwa Uhuru. Kilitokea kule Buguruni. Kisa cha mwisho ni Brazili, mwaka 1994, kuhusu mbwa koko. Katikati utakuta London miaka hii&#8230;Kanada&#8230;Mwananyamala, Mombasa&#8230;.Sweden&#8230;nk&#8230;Kitabu ni kama kumbukumbu ya safari na mielekeo yangu, kuna mambo mengi nimeyaona,mengine ya kusisimua sana. Lakini siri ni moja &#8230;dunia yote inafafana. Maafa yale yale. Majanga yale yale. Machungu na matamu yale yale. Kinachotofautiana ni sura, rangi za nyumba na nguo, lakini hisia zile zile; kwa hiyo basi nia yangu ni kumkumbusha msomaji kuwa dunia ni ndogo, binadamu ni wale wale na matatizo na raha zetu zile zile. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Hapo hapo lazima nikumbushe kuwa mimi napenda sana hadithi fupi maana ni rahisi kuelezea mambo ya aina nyingi katika maelezo mafupi kuliko riwaya. Kwangu hadithi fupi ni kama kamera. Tuseme Mpe ni kamera.Karibuni nimeanza kumenyana na uandishi wa riwaya. Nimemaliza riwaya ya Kiswahili inayoitwa &#8220;Hekaya za Masudi London&#8221; (wasomaji wa safu yangu Mwananchi lazima watakuwa wanamjua Masudi Pashamoto) na ninaandika riwaya yangu ya kwanza ya Kiingereza.Uandishi wa riwaya ni mtamu pia. Haina maana kuwa siupendi. Naupenda. Kila kitu kina nafasi yake.</span></p>
<p class="MsoNormal">&nbsp;</p>
<div style="text-align:center;"><img src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/01/freddy-machabc6.jpg" height="299" width="448" /></div>
<div style="text-align:center;">Freddy Macha(kushoto) akiwa na Andy Jones,mtengenezaji wa documentary inayohusu maisha ya Bi.Kidude ijulikanayo kama As Old As My Tongue.(Picha na Amita Macha)</div>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Kwa hakika visa vilivyomo kwenye Mpe Maneno Yake ni vya kusisimua.Hongera tena.Sasa kabla hatujamaliza kwenye masuala ya uandishi ningependa kukuuliza kuhusu tekinolojia mpya kama hizi blogs.Wewe pia siku hizi ni mwanablog.Unadhani blogs zina nafasi gani katika jamii na zinatoa changamoto ya aina gani kwenye uandishi uliokuwa umezoeleka miaka nenda,miaka rudi.Ule wa mhariri,waandishi na wasomaji?Na pia unadhani nini kitatokea ndani ya miaka kumi ijayo endapo blogs zitaendelea kukua kwa kasi hii?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> </span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">: Blogu ni hatari. Blogu inazidi kuwapa wananchi kijiko cha kuchotea na kula chakula&#8230;ajabu kuna magazeti hapo nyumbani bado yanaogopa blogu na hayazipi nafasi yake. Huku Uzunguni vyombo vya habari vimeanza kuona umuhimu wa blogu na kuzitumia. Ndiyo maana wanaziita Citizen Journalism. Maasi ya Burma mwaka jana yaliletwa na wanablogu kabla ya wanahabari wa kawaida. Mtu yeyote anaweza kuelezea alicho nacho.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Mimi nimeamua kuwa na blogu mbili kwa kuwa hutumia lugha mbili kuandikia nyumbani (kimuziki hutunga lugha kadhaa pia) yaani Kiingereza na Kiswahili. Tanzania tunatumia lugha hizi mahsusi, na sipendi kuzichanganya; ndiyo maana blogu ya Kitoto ni ya Kiswahili. Nalenga nyumbani na ile ya Kiingereza nalengesha wasomaji wowote duniani watakaotaka kunisoma. Sipendi kujiwekea vikwaazo kama mwandishi&#8230;</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Kuhusu suala la nini kitatokea baada ya miaka kumi&#8230;swali muhimu. Maana dola na serikali zitaamua (hata kabla ya hiyo miaka kumi kwisha) Kuzikamata. Ukweli dunia yetu inatawaliwa na wale wenye nguvu za uchumi na dola. Mawazo au fasihi yeyote inayohatarisha maslahi ya wenye nguvu lazima itazimwa. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Ukiangalia kwa mfano suala la tovuti zilizoanza kama nyenzo binafsi (My space au You Tube) leo zimeshanunuliwa na mabepari wakubwa (aliyenunua My Space) ndiye anayemiliki magazeti kama The Sun (hapa Uingereza gazeti hilo linasifika kwa kutojali sana maslahi ya wananchi hasa wasio weupe) sasa ikiwa watu hawa wanaona mahali pana fedha basi wananunua. Hilo ni suala la kiuchumi. Suala la kisiasa. Suala la mabavu.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Kadri tunavyoendelea ndivyo kadri blogu zitakuwa na nguvu. Wanablogu wataanza kuwa na sauti kali wataanza kutetemesha wenye nchi na vyombo vya dola vitaamua kuwasimamisha. Mchukue mwenzetu Saidi Yakubu. Blogu lake lilikuwa likiwika. Kalianza mwezi wa nne mwaka jana tulipofika mwezi wa Kumi akaanza kuwa maarufu sana.Wakubwa wake wa kazi wakamwambia linaingiliana na kazi yake. Hapo unaona mfano. Hakuna uhuru wa kudumu dunia yenye wanaotawala na waliotawaliwa. Kwa sasa blogu ni sauti ya wanyonge , sauti ya waandishi huria, lakini dunia si laini kama siagi. Ingekuwa laini na tamu kama fenesi kusingekuwa na vita wala viwanda vya bunduki na mabomu. </span></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">BC: Ungeshauri nini basi kifanyike ili blogs na vyombo vya habari vya kawaida visikingane bali vishirikiane kama ambavyo nchi za wenzetu magharibi vishaanza kufanya?</span></b></p>
<p class="MsoNormal"><b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">FM:</span></b><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';"> Dunia ya leo ni dunia ya mawasiliano. Hatuko enzi zile ambazo kiza kilitawala na viongozi wakawakata mikono waandishi (kama mafashisti walivyomkata mwanamuziki wa Chile, Victor Jara mwaka 1973).Dunia ya leo ni dunia ya teknolojia na habari. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Tatizo la baadhi ya vyombo vyetu vya habari (ukiacha labda Mwananchi wanaotangaza blogu) haviendi na wakati. Si shauri ya umaskini wa rasilimali bali umaskini wa kimawazo. Na haikuanza leo. Toka zamani. Hata nilipokuwa naanza uandishi wa habari hali ilikuwa vile vile. Uzuri mkubwa wa ubepari ni kukua kwa mawazo na uhuru huria wa kujieleza. Hapo hapo uhuru huu una mipaka. Anayetawala uchumi ndiye bosi; kwetu wanablogu lililopo ni kujiendeleza kila siku; kukimbia na kujua teknolojia. </span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Leo hapa Uingereza wametangaza vyombo vipya vya kuwacheki magaidi wanaopita pita katika matreni ya chini na vyombo vya usafiri. Aliyetengeneza zana hizi anaiuzia pia Marekani, na bwana usalama mmoja huko kwa Rais Bush kasema safi sana. Akaongeza kusema kuwa lazima tuwe hatua moja mbele ya magaidi. Lakini anasahau kitu kimoja.Siri ya ugaidi ni kutokuwa na usawa duniani; kuwepo maskini na matajiri. Blogu zikipigwa marufuku au kuwekewa pingu, wananchi hawatalala, wataendelea kugundua. Pale penye mchana pana usiku; penye hapana pana ndiyo, penye mwanamke pana mwanaume, penye njaa pana umaskini, penye tajiri pana mlala hoi.Uwiano huo ndiyo unaoongoza uhai. Kifupi basi blogu ni hatua fulani za harakati za mwanadamu kujiendeleza na kujieleza. </span><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">Kwa sasa ni kiwango cha juu sana cha sauti ya mwanadamu.</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-size:9.5pt;line-height:115%;font-family:'Verdana','sans-serif';">MWISHO WA SEHEMU YA KWANZA YA MAHOJIANO YETU NA FREDDY MACHA.HUTAKI KUIKOSA SEHEMU YA PILI.STAY TUNED.<br />
</span>
</p>
<p class="MsoNormal">Kwa habari zaidi kumhusu Freddy Macha usikose kutembelea tovuti yake kwa <b><a href="http://freddymacha.com/" target="_blank">kubonyeza hapa</a></b>. Blog za Freddy Macha unaweza kuzipata kwa kubonyeza <a href="http://kitoto.wordpress.com/" target="_blank">hapa</a> na <a href="http://www.freddymacha.blogspot.com/" target="_blank">hapa.</a></p>
<!-- Start Sociable --><div class="sociable"><div class="sociable_tagline"><a class='sociable_tagline' target='_blank' href='http://blogplay.com' style='color:#333333;text-decoration:none'>Be Sociable, Share!</a></div><ul class='clearfix'><li><a title="Twitter" class="option1_32" style="background-position:-288px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://twitter.com/intent/tweet?text=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA%20-%20http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F%20(via%20@sociablesite)"></a></li><li><a title="Facebook" class="option1_32" style="background-position:-96px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.facebook.com/share.php?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;t=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA"></a></li><li><a title="email" class="option1_32" style="background-position:-160px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="https://mail.google.com/mail/?view=cm&fs=1&to&su=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA&body=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&ui=2&tf=1&shva=1"></a></li><li><a class="option1_32" style="cursor:pointer;background-position:-128px 0px" rel="nofollow" title="Add to favorites - doesn't work in Chrome"  onClick="javascript:AddToFavorites();"></a></li><li><a title="StumbleUpon" class="option1_32" style="background-position:-224px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.stumbleupon.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&title=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA"></a></li><li><a title="Delicious" class="option1_32" style="background-position:-32px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://delicious.com/post?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;title=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA&amp;notes=%26nbsp%3B%0A%0A%0AKwa%20miaka%20nenda%20rudi%2C%20tangu%20miaka%20ya%20sabini%2Cjina%20la%20Freddy%20Macha%20%28pichani%29%20limekuwa%20sio%20geni%20miongoni%20mwa%20wasomaji%20mbalimbali%20wa%20magazeti%2C%20vitabu%20vya%20hadithi%20fupifupi%2Cwapenzi%20wa%20muziki%20na%20pia%20sanaa%20ya%20ushairi%20nchini%20Tanzania.%20Iwe%20unamfahamu%20"></a></li><li><a title="Google Reader" class="option1_32" style="background-position:-224px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/reader/link?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;title=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA&amp;srcURL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;srcTitle=BongoCelebrity+"></a></li><li><a title="LinkedIn" class="option1_32" style="background-position:-288px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.linkedin.com/shareArticle?mini=true&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;title=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA&amp;source=BongoCelebrity+&amp;summary=%26nbsp%3B%0A%0A%0AKwa%20miaka%20nenda%20rudi%2C%20tangu%20miaka%20ya%20sabini%2Cjina%20la%20Freddy%20Macha%20%28pichani%29%20limekuwa%20sio%20geni%20miongoni%20mwa%20wasomaji%20mbalimbali%20wa%20magazeti%2C%20vitabu%20vya%20hadithi%20fupifupi%2Cwapenzi%20wa%20muziki%20na%20pia%20sanaa%20ya%20ushairi%20nchini%20Tanzania.%20Iwe%20unamfahamu%20"></a></li><li><a title="BlinkList" class="option1_32" style="background-position:0px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.blinklist.com/index.php?Action=Blink/addblink.php&amp;Url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;Title=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA"></a></li><li><a style="cursor:pointer" rel="nofollow" onMouseOut="fixOnMouseOut(document.getElementById('sociable-post-802'), event, 'post-802')" onMouseOver="more(this,'post-802')"><img style='margin-top:9px' src='http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/more.png'></a></li></ul><div onMouseout="fixOnMouseOut(this,event,'post-802')" id="sociable-post-802" style="display:none;">   

    <div style="top: auto; left: auto; display: block;" id="sociable">



		<div class="popup">

			<div class="content">

				<ul><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Myspace" class="option1_32" style="background-position:0px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.myspace.com/Modules/PostTo/Pages/?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;t=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Digg" class="option1_32" style="background-position:-64px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://digg.com/submit?phase=2&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;title=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA&amp;bodytext=%26nbsp%3B%0A%0A%0AKwa%20miaka%20nenda%20rudi%2C%20tangu%20miaka%20ya%20sabini%2Cjina%20la%20Freddy%20Macha%20%28pichani%29%20limekuwa%20sio%20geni%20miongoni%20mwa%20wasomaji%20mbalimbali%20wa%20magazeti%2C%20vitabu%20vya%20hadithi%20fupifupi%2Cwapenzi%20wa%20muziki%20na%20pia%20sanaa%20ya%20ushairi%20nchini%20Tanzania.%20Iwe%20unamfahamu%20"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Reddit" class="option1_32" style="background-position:-128px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reddit.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;title=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Google Bookmarks" class="option1_32" style="background-position:-192px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/bookmarks/mark?op=edit&amp;bkmk=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;title=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA&amp;annotation=%26nbsp%3B%0A%0A%0AKwa%20miaka%20nenda%20rudi%2C%20tangu%20miaka%20ya%20sabini%2Cjina%20la%20Freddy%20Macha%20%28pichani%29%20limekuwa%20sio%20geni%20miongoni%20mwa%20wasomaji%20mbalimbali%20wa%20magazeti%2C%20vitabu%20vya%20hadithi%20fupifupi%2Cwapenzi%20wa%20muziki%20na%20pia%20sanaa%20ya%20ushairi%20nchini%20Tanzania.%20Iwe%20unamfahamu%20"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="HackerNews" class="option1_32" style="background-position:-256px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://news.ycombinator.com/submitlink?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;t=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="MSNReporter" class="option1_32" style="background-position:-352px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reporter.es.msn.com/?fn=contribute&amp;Title=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA&amp;URL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;cat_id=6&amp;tag_id=31&amp;Remark=%26nbsp%3B%0A%0A%0AKwa%20miaka%20nenda%20rudi%2C%20tangu%20miaka%20ya%20sabini%2Cjina%20la%20Freddy%20Macha%20%28pichani%29%20limekuwa%20sio%20geni%20miongoni%20mwa%20wasomaji%20mbalimbali%20wa%20magazeti%2C%20vitabu%20vya%20hadithi%20fupifupi%2Cwapenzi%20wa%20muziki%20na%20pia%20sanaa%20ya%20ushairi%20nchini%20Tanzania.%20Iwe%20unamfahamu%20"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Sphinn" class="option1_32" style="background-position:-192px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://sphinn.com/index.php?c=post&amp;m=submit&amp;link=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Posterous" class="option1_32" style="background-position:-64px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://posterous.com/share?linkto=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;title=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA&amp;selection=%26nbsp%3B%0A%0A%0AKwa%20miaka%20nenda%20rudi%2C%20tangu%20miaka%20ya%20sabini%2Cjina%20la%20Freddy%20Macha%20%28pichani%29%20limekuwa%20sio%20geni%20miongoni%20mwa%20wasomaji%20mbalimbali%20wa%20magazeti%2C%20vitabu%20vya%20hadithi%20fupifupi%2Cwapenzi%20wa%20muziki%20na%20pia%20sanaa%20ya%20ushairi%20nchini%20Tanzania.%20Iwe%20unamfahamu%20"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Tumblr" class="option1_32" style="background-position:-256px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.tumblr.com/share?v=3&amp;u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2008%2F01%2F07%2Fkwa-kina-na-freddy-macha%2F&amp;t=KWA%20KINA%20NA%20FREDDY%20MACHA&amp;s=%26nbsp%3B%0A%0A%0AKwa%20miaka%20nenda%20rudi%2C%20tangu%20miaka%20ya%20sabini%2Cjina%20la%20Freddy%20Macha%20%28pichani%29%20limekuwa%20sio%20geni%20miongoni%20mwa%20wasomaji%20mbalimbali%20wa%20magazeti%2C%20vitabu%20vya%20hadithi%20fupifupi%2Cwapenzi%20wa%20muziki%20na%20pia%20sanaa%20ya%20ushairi%20nchini%20Tanzania.%20Iwe%20unamfahamu%20"></a></li></ul>			

			</div>        

		  <a style="cursor:pointer" onclick="hide_sociable('post-802',true)" class="close">



		  <img onclick="hide_sociable('post-802',true)" title="close" src="http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/closelabel.png">

		  </a>

		</div>

	</div> 

  </div></div><div class='sociable' style='float:none'><ul class='clearfix'><li id="Twitter_Counter"><a href="https://twitter.com/share" data-text="KWA KINA NA FREDDY MACHA - http://www.bongocelebrity.com/2008/01/07/kwa-kina-na-freddy-macha/ (via #sociablesite)" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2008/01/07/kwa-kina-na-freddy-macha/" class="twitter-share-button" data-count="horizontal">Tweet</a><script type="text/javascript" src="//platform.twitter.com/widgets.js"></script></li><li id="Facebook_Counter"><iframe src="//www.facebook.com/plugins/like.php?href=http://www.bongocelebrity.com/2008/01/07/kwa-kina-na-freddy-macha/&send=false&layout=button_count&show_faces=false&action=like&colorscheme=light&font" scrolling="no" frameborder="0" style="border:none; overflow:hidden;height:32px;width:100px" allowTransparency="true"></iframe></li><li id="Google_+"><g:plusone annotation="bubble" href="http://www.bongocelebrity.com/2008/01/07/kwa-kina-na-freddy-macha/" size="medium"></g:plusone></li><li id="LinkedIn_Counter"><script src="http://platform.linkedin.com/in.js" type="text/javascript"></script><script type="IN/Share" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2008/01/07/kwa-kina-na-freddy-macha/" data-counter="right"></script></li><li id="StumbleUpon_Counter"><script src="http://www.stumbleupon.com/hostedbadge.php?s=2&r=http://www.bongocelebrity.com/2008/01/07/kwa-kina-na-freddy-macha/"></script></li></ul></div><!-- End Sociable -->]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.bongocelebrity.com/2008/01/07/kwa-kina-na-freddy-macha/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>29</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>BONGO FLAVA NA TEKINOLOJIA</title>
		<link>http://www.bongocelebrity.com/2007/12/10/bongo-flava-na-tekinolojia/</link>
		<comments>http://www.bongocelebrity.com/2007/12/10/bongo-flava-na-tekinolojia/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 10 Dec 2007 05:15:41 +0000</pubDate>
		<dc:creator>bongocelebrity</dc:creator>
				<category><![CDATA[Blogging]]></category>
		<category><![CDATA[Blogs]]></category>
		<category><![CDATA[Bongo Flava]]></category>
		<category><![CDATA[Burudani]]></category>
		<category><![CDATA[Mtandao]]></category>
		<category><![CDATA[Muziki]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://bongocelebrity.com/2007/12/10/bongo-flava-na-tekinolojia/</guid>
		<description><![CDATA[&#160; Pichani ni wasanii wa muziki wa kizazi kipya,Bongo Flava, Ilunga Khalifa a.k.a C Pwaa(kushoto) na Falid Kubanda a.k.a Fid Q(kulia). Ilunga Khalifa (CP)ni mmoja kati ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye anakwenda na wakati kwa kuhakikisha kwamba anazitumia tekinolojia za kisasa vilivyo kwa manufaa ya kibiashara na kimuziki.Tunasema hivyo kwa sababu C-Pwaa [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p class="MsoNormal">&nbsp;</p>
<p style="text-align:center;"><img src="http://bongocelebrity.files.wordpress.com/2007/12/fid-q.jpg" height="353" width="336" /></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-family:'Georgia','serif';">Pichani ni wasanii wa muziki wa kizazi kipya,Bongo Flava, Ilunga Khalifa a.k.a C Pwaa(kushoto) na Falid Kubanda a.k.a Fid Q(kulia).</span></p>
<p class="MsoNormal"><span style="font-family:'Georgia','serif';">Ilunga Khalifa (CP)ni mmoja kati ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye anakwenda na wakati kwa kuhakikisha kwamba anazitumia tekinolojia za kisasa vilivyo kwa manufaa ya kibiashara na kimuziki.Tunasema hivyo kwa sababu C-Pwaa kwa kutumia kamera ya simu yake ya mkononi anaendesha blog ambayo anaiita <strong>Simu Yangu Kamera.</strong>Unaweza kuitembelea blog yake kwa <strong><a href="http://simuyangukamera.blogspot.com/" target="_blank">kubonyeza hapa.</a></strong></span></p>
<p class="MsoNormal">Picha na <a href="http://michuzijr.blogspot.com/" target="_blank">MichuziJR.</a></p>
<!-- Start Sociable --><div class="sociable"><div class="sociable_tagline"><a class='sociable_tagline' target='_blank' href='http://blogplay.com' style='color:#333333;text-decoration:none'>Be Sociable, Share!</a></div><ul class='clearfix'><li><a title="Twitter" class="option1_32" style="background-position:-288px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://twitter.com/intent/tweet?text=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA%20-%20http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F%20(via%20@sociablesite)"></a></li><li><a title="Facebook" class="option1_32" style="background-position:-96px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.facebook.com/share.php?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;t=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA"></a></li><li><a title="email" class="option1_32" style="background-position:-160px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="https://mail.google.com/mail/?view=cm&fs=1&to&su=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA&body=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&ui=2&tf=1&shva=1"></a></li><li><a class="option1_32" style="cursor:pointer;background-position:-128px 0px" rel="nofollow" title="Add to favorites - doesn't work in Chrome"  onClick="javascript:AddToFavorites();"></a></li><li><a title="StumbleUpon" class="option1_32" style="background-position:-224px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.stumbleupon.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&title=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA"></a></li><li><a title="Delicious" class="option1_32" style="background-position:-32px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://delicious.com/post?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;title=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA&amp;notes=%26nbsp%3B%0A%0APichani%20ni%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%2CBongo%20Flava%2C%20Ilunga%20Khalifa%20a.k.a%20C%20Pwaa%28kushoto%29%20na%20Falid%20Kubanda%20a.k.a%20Fid%20Q%28kulia%29.%0AIlunga%20Khalifa%20%28CP%29ni%20mmoja%20kati%20ya%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%20ambaye%20anakwenda%20na%20wakati%20kwa%20kuhakikis"></a></li><li><a title="Google Reader" class="option1_32" style="background-position:-224px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/reader/link?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;title=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA&amp;srcURL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;srcTitle=BongoCelebrity+"></a></li><li><a title="LinkedIn" class="option1_32" style="background-position:-288px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.linkedin.com/shareArticle?mini=true&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;title=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA&amp;source=BongoCelebrity+&amp;summary=%26nbsp%3B%0A%0APichani%20ni%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%2CBongo%20Flava%2C%20Ilunga%20Khalifa%20a.k.a%20C%20Pwaa%28kushoto%29%20na%20Falid%20Kubanda%20a.k.a%20Fid%20Q%28kulia%29.%0AIlunga%20Khalifa%20%28CP%29ni%20mmoja%20kati%20ya%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%20ambaye%20anakwenda%20na%20wakati%20kwa%20kuhakikis"></a></li><li><a title="BlinkList" class="option1_32" style="background-position:0px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.blinklist.com/index.php?Action=Blink/addblink.php&amp;Url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;Title=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA"></a></li><li><a style="cursor:pointer" rel="nofollow" onMouseOut="fixOnMouseOut(document.getElementById('sociable-post-696'), event, 'post-696')" onMouseOver="more(this,'post-696')"><img style='margin-top:9px' src='http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/more.png'></a></li></ul><div onMouseout="fixOnMouseOut(this,event,'post-696')" id="sociable-post-696" style="display:none;">   

    <div style="top: auto; left: auto; display: block;" id="sociable">



		<div class="popup">

			<div class="content">

				<ul><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Myspace" class="option1_32" style="background-position:0px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.myspace.com/Modules/PostTo/Pages/?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;t=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Digg" class="option1_32" style="background-position:-64px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://digg.com/submit?phase=2&amp;url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;title=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA&amp;bodytext=%26nbsp%3B%0A%0APichani%20ni%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%2CBongo%20Flava%2C%20Ilunga%20Khalifa%20a.k.a%20C%20Pwaa%28kushoto%29%20na%20Falid%20Kubanda%20a.k.a%20Fid%20Q%28kulia%29.%0AIlunga%20Khalifa%20%28CP%29ni%20mmoja%20kati%20ya%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%20ambaye%20anakwenda%20na%20wakati%20kwa%20kuhakikis"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Reddit" class="option1_32" style="background-position:-128px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reddit.com/submit?url=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;title=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Google Bookmarks" class="option1_32" style="background-position:-192px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.google.com/bookmarks/mark?op=edit&amp;bkmk=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;title=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA&amp;annotation=%26nbsp%3B%0A%0APichani%20ni%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%2CBongo%20Flava%2C%20Ilunga%20Khalifa%20a.k.a%20C%20Pwaa%28kushoto%29%20na%20Falid%20Kubanda%20a.k.a%20Fid%20Q%28kulia%29.%0AIlunga%20Khalifa%20%28CP%29ni%20mmoja%20kati%20ya%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%20ambaye%20anakwenda%20na%20wakati%20kwa%20kuhakikis"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="HackerNews" class="option1_32" style="background-position:-256px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://news.ycombinator.com/submitlink?u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;t=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="MSNReporter" class="option1_32" style="background-position:-352px 0px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://reporter.es.msn.com/?fn=contribute&amp;Title=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA&amp;URL=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;cat_id=6&amp;tag_id=31&amp;Remark=%26nbsp%3B%0A%0APichani%20ni%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%2CBongo%20Flava%2C%20Ilunga%20Khalifa%20a.k.a%20C%20Pwaa%28kushoto%29%20na%20Falid%20Kubanda%20a.k.a%20Fid%20Q%28kulia%29.%0AIlunga%20Khalifa%20%28CP%29ni%20mmoja%20kati%20ya%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%20ambaye%20anakwenda%20na%20wakati%20kwa%20kuhakikis"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Sphinn" class="option1_32" style="background-position:-192px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://sphinn.com/index.php?c=post&amp;m=submit&amp;link=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Posterous" class="option1_32" style="background-position:-64px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://posterous.com/share?linkto=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;title=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA&amp;selection=%26nbsp%3B%0A%0APichani%20ni%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%2CBongo%20Flava%2C%20Ilunga%20Khalifa%20a.k.a%20C%20Pwaa%28kushoto%29%20na%20Falid%20Kubanda%20a.k.a%20Fid%20Q%28kulia%29.%0AIlunga%20Khalifa%20%28CP%29ni%20mmoja%20kati%20ya%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%20ambaye%20anakwenda%20na%20wakati%20kwa%20kuhakikis"></a></li><li style="heigth:32px;width:32px"><a title="Tumblr" class="option1_32" style="background-position:-256px -32px" rel="nofollow" target="_blank" href="http://www.tumblr.com/share?v=3&amp;u=http%3A%2F%2Fwww.bongocelebrity.com%2F2007%2F12%2F10%2Fbongo-flava-na-tekinolojia%2F&amp;t=BONGO%20FLAVA%20NA%20TEKINOLOJIA&amp;s=%26nbsp%3B%0A%0APichani%20ni%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%2CBongo%20Flava%2C%20Ilunga%20Khalifa%20a.k.a%20C%20Pwaa%28kushoto%29%20na%20Falid%20Kubanda%20a.k.a%20Fid%20Q%28kulia%29.%0AIlunga%20Khalifa%20%28CP%29ni%20mmoja%20kati%20ya%20wasanii%20wa%20muziki%20wa%20kizazi%20kipya%20ambaye%20anakwenda%20na%20wakati%20kwa%20kuhakikis"></a></li></ul>			

			</div>        

		  <a style="cursor:pointer" onclick="hide_sociable('post-696',true)" class="close">



		  <img onclick="hide_sociable('post-696',true)" title="close" src="http://www.bongocelebrity.com/wp-content/plugins/sociable/images/closelabel.png">

		  </a>

		</div>

	</div> 

  </div></div><div class='sociable' style='float:none'><ul class='clearfix'><li id="Twitter_Counter"><a href="https://twitter.com/share" data-text="BONGO FLAVA NA TEKINOLOJIA - http://www.bongocelebrity.com/2007/12/10/bongo-flava-na-tekinolojia/ (via #sociablesite)" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2007/12/10/bongo-flava-na-tekinolojia/" class="twitter-share-button" data-count="horizontal">Tweet</a><script type="text/javascript" src="//platform.twitter.com/widgets.js"></script></li><li id="Facebook_Counter"><iframe src="//www.facebook.com/plugins/like.php?href=http://www.bongocelebrity.com/2007/12/10/bongo-flava-na-tekinolojia/&send=false&layout=button_count&show_faces=false&action=like&colorscheme=light&font" scrolling="no" frameborder="0" style="border:none; overflow:hidden;height:32px;width:100px" allowTransparency="true"></iframe></li><li id="Google_+"><g:plusone annotation="bubble" href="http://www.bongocelebrity.com/2007/12/10/bongo-flava-na-tekinolojia/" size="medium"></g:plusone></li><li id="LinkedIn_Counter"><script src="http://platform.linkedin.com/in.js" type="text/javascript"></script><script type="IN/Share" data-url="http://www.bongocelebrity.com/2007/12/10/bongo-flava-na-tekinolojia/" data-counter="right"></script></li><li id="StumbleUpon_Counter"><script src="http://www.stumbleupon.com/hostedbadge.php?s=2&r=http://www.bongocelebrity.com/2007/12/10/bongo-flava-na-tekinolojia/"></script></li></ul></div><!-- End Sociable -->]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.bongocelebrity.com/2007/12/10/bongo-flava-na-tekinolojia/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>8</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>

<!-- Performance optimized by W3 Total Cache. Learn more: http://www.w3-edge.com/wordpress-plugins/

Page Caching using disk: enhanced

Served from: www.bongocelebrity.com @ 2012-02-09 16:37:31 -->
