
Kama mimi na wewe tunashabihiana kifikra, basi ulikuwa unatamani siku hii ifike.Siku ambayo angalau kwa muda mfupi,utapumzika kusikia kwamba kila production mpya ya Bongo Fleva, inakuwa imeelemea kwenye hadithi na visa kuhusu mapenzi.Sio kusema kwamba hadithi na visa vya mapenzi havina nafasi yake katika sanaa,La.Ni kuonyesha tu kwamba jamii ni pana na kuna mengi zaidi ambayo sanaa inaweza kuyagusia.
Aliyesikia kilio hicho ni Heavy-weight MC,Prof.Jay.Wimbo unaitwa Msilie akiwa amemshirikisha mkali mwingine wa hip hop nchini Tanzania,Chid Benz.Wimbo umetengenezwa na producer ambaye amekuja juu kwa sana.Ni Lamar kutoka Fish Crab Records.
Mambo kadhaa yamenifanya niusikilize wimbo huu siku nzima.Kikubwa ni ujumbe uliomo ndani yake.Kama ambavyo ungetarajia kutoka kwa Prof.kwa kina anaangalia yale yanayojiri katika jamii.Anatoa hoja,anafafanua,anaelekeza.Msikilize;
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Hey what’s up everybody! I thought the Producers in Tanzania have improved a lot but I guess I was wrong! Two and Half years ago, I made a beat and named it Block Running, I sold it to one of the Label called Koch Entertainment of New York with an agreement that wherever this beat goes my name gotta be there as a beat maker of this beat. Two days ago I was shocked when one of my friends from Tanzania sent me a song with the same beat I made 2 and half yrs ago! And I didn’t hear my name on the track. All I heard is Marco Chali.
So I called Koch Entertainment to ask what’s going on. Koch Entertainment management were so surprised to hear the news. So they told me to send the song to them and I did, they asked me if I ever sent the beat to MJ Records of Dar-es-salaam, Tanzania. I told them I never did but had put the beat on iTunes so people can buy and use it for promotions and not for any other type of business. But MJ Records used the beat without permission from Koch Entertainment and also they didn’t follow the agreement we signed that wherever this beat goes my name gotta be there as a beat maker!
I don’t have any rights of complaining this issue to MJ Records that why my name wasn’t on the song as a beat maker. All I will do is to take Koch Entertainment to court and they will deal with MJ Records. The only thing I am gonna deal with is if MJ Records bought this beat from iTunes. If they did why they used it for the business!!?
I put the song which Producer Marco Chali of MJ Records produced last year and my beat I made 2 and half years ago so you guys can compare and tell me if this beat is the same or not the same.Thanks.
Stiggo Ibrahim,
S&S Records-NY
Quick Rocka Ft QJ-Bullet
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
S&S Records & Koch Ent.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
BC is trying to reach MJ Records for their comment.Stay Tuned.

Za mwizi arobaini. Bila shaka ushausikia msemo huo.Sina uhakika sana na idadi ya siku (40) lakini nina uhakika kwamba msemo huo humaanisha kwamba uovu una kikomo.Ipo siku utakamatwa.Inaweza kuwa sio ndani ya siku arobaini(40) lakini ipo siku tu!
Lakini inakuwaje siku ukimfumania mtu ambaye haibi kunde na choroko zako shambani bali anaiba penzi au mpenzi wako? Utapigana au utamuacha aende zake.Yaani namaanisha utayamaliza kistaarabu tu au mtaani patakuwa hapatoshi kwa vurumai au songombingo utakalolianzisha?
Sijui utafanyaje…lakini Hussein Machozi(pichani) anasimulia jinsi siku za mwizi(wa penzi,mali au hali) zinavyofikia ukingoni.Baada ya siku arobaini mambo yanawekwa hadharani.Tyler Perry,yule muongoza sinema maarufu kutoka nchini Marekani,anao mchezo(play) unaoitwa What is Done In The Dark…Must Come Out to Light. Labda Hussein Machozi anamaanisha hivyo pia.
Wimbo unaitwa Za Mwizi 40,unapatikana katika album yake ya Kwa Ajili Yako. Hii ni single yake ya 3 kutoka katika album hiyo, single mbili zilizotangulia ni pamoja na Kwa Ajili Yako na Utaipenda.Usikilize hapo chini;
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
SONG’S DETAILS
Track Name: ZA MWIZI 40
Singer: HUSSEIN MACHOZI
Produced by: AMBA & KID BWOY
Written by: HUSSEIN MACHOZI
Song Arranged by: HUSSEIN MACHOZI & KID BWOY
Mixed by: KID BWOY
Studio: TETEMESHA RECORDZ / AB RECORDS

Kila ifikapo tarehe 13 August, yeye hukumbuka na kusheherekea siku yake ya kuzaliwa. Alipozaliwa pale jijini Mwanza,kaskazini mwa Tanzania wazazi wake walimpa jina la Fareed. Leo hii kwa wengi anatambulika kama Fid Q.
Kama ambavyo umeshasikia,leo hii,tarehe 25 Feb 2010, album yake inayokwenda kwa jina Propaganda inaingia mtaani.Kwa hiyo leo ukizunguka mitaani,usishangae kukutana na mtu kabeba CD mpya ya Fid Q au ukasikia sauti yake kwenye gari,magari,usafiri wa umma.Jambo moja muhimu unaloweza kufanya ni kujipatia nakala yako halisi.Hakuna njia nzuri zaidi ya kuunga mkono juhudi za wasanii zaidi ya hiyo!
Hivi karibuni nilipata nafasi ya kuzungumza machache na Fid Q kuhusu ujio wa albamu hii ya Propaganda,muungano wa wasanii wa bongo fleva na pia suala zima la nyimbo nyingi za bongo fleva kuwa na maudhui ya mapenzi zaidi ya kitu kingine chochote.Kwanini ameiita album yake Propaganda? Anamaanisha nini? Je unajua Fid Q ana mtazamo gani kuhusu muungano wa wasanii?Je anasemaje kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika maendeleo au kifo cha muziki wa kizazi kipya? Fuatana nami katika mahojiano yafuatayo;
BC: Kwanza hongera kwa album mpya.Labda kwa ujumla tu,album hii umeitengenezea katika studio zipi,itakuwa na nyimbo ngapi na umewashirikisha wasanii gani wengine?
Fid Q: Asante sana kaka.Album hii nimeifanya katika studio 3 tofauti.Nimefanya kwa MJ Records, Tongwe Records na kwa Lamar.Nimewashirikisha wasanii kama AY, NCHA KALI, MZEE ZORRO, JUMA NATURE,QJ, NYLON WA MANZESE CREW, BI KIDUDE na wengine kibao bila kuwasahau MATONYA na MZUNGU KICHAA.
BC: Kwanini umeiita Propaganda?Kuna ujumbe wowote maalumu kutokana na jina la album? (more…)

Pamoja na ushabiki wote wa soka nchini ambao siku hizi umejikita sio tu katika timu za Yanga na Simba bali pia timu mbalimbali zinazoshiriki ligi kuu ya nchini Uingereza(English Premier League), bado wengi tunakubaliana kwamba hakuna tukio la soka ulimwenguni linaloshinda mashindano ya kugombea Kombe la Dunia la Soka( Soccer World Cup).
Ubishi na ushindani wa Arsenal, Chelsea, Manchester United, Liverpool, Newcastle nk unapofikia ukingoni,macho na masikio huelekezwa katika Kombe la Dunia. Pale ndipo penye msisimko wa aina yake.Vipaji visivyo vya kawaida huonekana pale. Ndoto hutimizwa pale na pia ndoto huyeyuka au kuota mbawa na kupaa kama vile afanyavyo mwewe baada ya kukidakua kifaranga.
Kama unavyojua,mwaka huu kipute kipo barani kwetu. Hii ni mara ya kwanza kwa bara la Afrika kupewa nafasi ya kuandaa kombe la dunia. Ni mwaka ambao una matumaini mapya kwani ukitazama kwa makini,bara la Afrika lina wasakata kabumbu mahiri sana wanaocheza katika vilabu mbalimbali ulimwenguni hususani barani Ulaya.Mimi sina timu huko Ulaya;ila Real Madrid na Arsenal wakifungwa huwa sijisikii raha! Utaniita mshabiki?
Sasa kama ilivyo kwa matukio mengi makubwa ya michezo duniani,muziki huwa haukosi.Kunakuwa na wimbo maalumu kwa ajili ya mashindano(tournament’s official song). Kombe la dunia pia.Kwa mwaka huu, wimbo Waving Flags (kwa Kiswahili rahisi naweza kusema Kupeperusha Bendera) kutoka kwa mwanamuziki Knaan .Huu ndio World Cup 2010 Official Song.
Knaan ni mzaliwa wa Somalia. Kwa sasa makazi yake ni Toronto,Canada. Ni miongoni mwa wanamuziki wenye asili ya Afrika wanaofanya vizuri sana katika anga za muziki ulimwenguni. Bonyeza hapa ili kutembelea tovuti yake na pia hapa ili kusoma zaidi kuhusu historia yake.
Haya sasa,wimbo huo.Tupeperushe bendera.Je Afrika tutatoka kimasomaso huko Kusini mwa bara letu? Imebaki miezi michache.Usikilize wimbo Waving Flags hapo chini
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Picha na habari kwa hisani ya GetMziki.Watembelee kusikia pia Remix ya wimbo huu.

Siku chache zijazo,tarehe 25 mwezi huu kwa uhakika,Fareed Kubanda au maarufu kama Fid Q anatarajia kuiweka sokoni albamu yake mpya ambayo ameipa jina Propaganda.
Hivi karibuni ametoa single moja kama utambulisho wa kitachokuwepo katika album hiyo. Single inakwenda kwa jina la Danger akiwa amemshirikisha J-Bryant.Usikilize kwa kubonyeza player hapo chini.Usikilize kwa makini.Sikiliza midundo,hisia,ujumbe uliomo na kisha sema usikike.Kwa ufupi ninachoweza kusema ni kwamba kuna utofauti…
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Ndoto za mashabiki wa muziki kuwaona tena Nguza Viking(Babu Seya) na Papii Kocha(Mwana wa Mfalme) wakilipanda tena jukwaa la uraiani kutoa burudani,hususani katika wimbo wao maarufu wa Seya,leo zimefikia ukingoni.Rufaa yao imekataliwa.Hata hivyo,kwa mujibu wa mtandao wa Global Publishers,watoto wawili,Francis na Mbangu, wameachiwa huru!
Jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa, wakiongozwa na Jaji Natalia Kimaro, Salum Massati baada ya kupitia kwa makini rufaa hiyo, iliyosomwa na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufaa, Neema Chusi, wamewaachia huru vijana hao baada ya kuridhika na hoja za upande wa utetezi kuwa hawakuhusika katika tukio hilo lililohusisha familia hiyo mwaka 2003.
Kwa maana hiyo,Babu Seya na mwanae mmoja Papii Kocha,wamerudishwa Ukonga kuendelea kutumikia adhabu ya kifungo cha maisha inayowakabili.
Picha kwa hisani ya Global Publishers
Miongoni mwa kesi na hukumu ambazo zimekuwa na mawazo au maoni yanayopishana sana katika historia ya hivi karibuni ya nchini Tanzania,ni pamoja na ile ya Nguza Viking, maarufu kama Babu Seya na wanawe watatu ambao ni Papii Kocha Nguza,Nguza Mbangu na Francis Nguza. Lipo kundi kubwa tu la raia ambao wanasema Babu Seya na wanawe walionewa(set-up) na pia lipo kundi lingine linalosema kwamba walipo(jela) ndipo wanapostahili kuwepo kwani wana hatia.Katika siku za karibuni,wanaosema kwamba Babu Seya na wanawe hawana makosa, wameongezeka zaidi.
Wakati maoni na mtizamo wa raia ukizidi kujiweka sawa,kesho ni kesho kwa Babu Seya na wanawe kwani mahakama ya Rufaa nchini Tanzania,kesho inatarajiwa kutoa hukumu dhidi ya rufaa dhidi ya hukumu ya awali ya wanamuziki hao ambao wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Mabere Marando wa jijini Dar-es-salaam na Hamidu Mbwezeleni kutoka Zanzibar.
Je Babu Seya na wanawe wataachiwa huru hapo kesho?
Kwa undani zaidi wa kesi hii,hukumu za awali na mengineyo,bonyeza hapa

Hamis Ramadhan,maarufu kama H-Baba(pichani) yawezekana sio jina geni kwako.Huyu ni miongoni mwa wanamuzuki waliojikita katika mtindo ujulikanao kama TAKEU(Mr.Nice ndiye anasemekana kuwa mwanzilishi wake).
Ambacho unaweza kuwa hukijui ni kuhusu “imani” aliyonayo. Hivi karibuni H-Baba alinukuliwa na chombo kimoja cha habari akisema kwamba amelogwa na mmoja wa wasanii wenzake kitu ambacho anadai ndicho kilichosababisha mambo yake kwenda ‘kombo” katika siku za karibuni.
Kwa masikitiko na upole,H-Baba amenukuliwa akisema “Unajuwa mtu ataniona mimi kama naongopa lakini ukweli ni kuwa nilichezewa ila nilikuwa sijui nimekuja kugundua baada ya kupita pita kwenye tiba.Nilianza kujihisi hivyo mara baada ya kugombana na watu wengi sana nikiwa sijielewi”
H Baba anakiri kwamba hivi sasa ameshapona kutoka katika matatizo yaliyokuwa yakimsumbua baada ya kupata tiba toka kwa wataalamu wa miti shamba.
Bila kumtaja wazi huyo ‘mchawi” wake H-Baba alizidi kusema ” Unajuwa ni ukweli kabisa waswahili hawakukosea walivyosema kikulacho kinguoni mwako, kwani yote hayo yalikuwa yakifanywa na mtu wa karibu kabisa tena rafiki yangu mkubwa”.
Mfano mmojawapo wa matatizo yake,anasema “Matatizo mengi yalitokana na Irene(Uwoya), unajua watu wengi hawakupenda niwe na Irene, kwahiyo ili kunikomoa ikabidi waniroge, mimi na Irene tukawa hatuelewani, tunagombana mpaka tukaachana,”
Je,unaamini kwamba ni kweli yawezekana H-Baba amefanyiwa anachodai kufanyiwa au hii ni “publicity stunt”?

Yapo majina ya wasanii wa kizazi kipya ambao ukisikia wameshirikiana(collaborate)kutengeneza kazi fulani, basi unakuwa na imani kubwa kwamba kazi hiyo ina nafasi kubwa ya kuwa nzuri. Hiyo inatokana na uzoefu na pia zingatio za kazi zao zilizopita,nafasi waliyonayo katika uwanja mpana wa sanaa ya muziki na mambo kama hayo.
Hivi karibuni nilipoletewa kazi mpya na kuambiwa kwamba wasanii waliomo katika kazi hiyo ni TID(Top in Dar) na Chid Benz, nilikuwa na uhakika kwamba kazi hiyo itakuwa imesimama.TID na Chid ni miongoni mwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao binafsi nawaheshimu na sioni noma kusema kwamba nazipenda nyingi kati ya kazi zao.Habari nzuri ni kwamba hawakuniangusha katika kazi hii ya hivi karibuni inayokwenda kwa jina Huyu.
Kama zilivyo kazi nyingi za wasanii wetu siku hizi,hii pia ni hadithi ya mapenzi (bado natamani wigo wa yaliyomo(content) za kazi za wasanii upanuke zaidi na kugusa maeneo mengine yanayoizunguka jamii).Kinachoufanya wimbo huu uwe tofauti ni uwezo binafsi wa wasanii husika na hadithi yenyewe.
Kazi hii imepikwa pale Tetemesha Records(kule kule alikoibukia Hussein Machozi) chini ya George Mpanda au maarufu kama Kid Bwoy. Bonyeza player hapo chini usikilize wimbo Huyu.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

