
A couple of months ago, a friend asked me if I could come up with at least 100 songs that I consider to be most inspirational and motivational. This friend knows that I love music than a sleep. In fact, I have never imagined how the world could be without music. I have always said that there are three things that I run into whenever I feel like the skies are yellow and not blue; God, Family and Music!
However, I don’t love just any music even though I listen or could say I have listened to all genres of music available out there. I love music with lyrics that bears a message. It being good or evil, it gotta have a “message”. Of course, at the end of the day, I tend to stick with the ones that motivate and inspires.
I have therefore compiled a list of 120 songs that I consider to be both inspirational and motivational. I have already shared this list with a friend who asked and thought it’s not a bad idea if I share the same with you. I know some of you are also music fanatics.
These are the songs that keep me going even when things seem to get almost too tough to handle. Whenever I need to hear a voice different from the one from Heaven that tomorrow could be better, I tune in and listen to some of them.
Now before you start examining my list, please allow me to say this; I appreciate the fact that everyone will have their favorites and if none of the above is inspirational songs or motivational song, in your point of view, please accept my deepest regrets! This list is in random order. The numbers don’t have much meaning. Feel free to add some of your favorites through the comments section. I am planning to review this list in a couple of months. I will be happy to add some of your recommendations. Enjoy;
- One Love/People Get Ready- Bob Marley & The Wailers
- Three Little Birds- Bob Marley & The Wailers
- Smile- 2Pac Shakur Ft. Scarface
- A Beautiful Day- India Arie
- Don’t Worry ‘Bout A Thing-Stevie Wonder
- What’s Going On-Marvin Gaye
- Keep Ya Head Up-2Pac Shakur
- Beautiful Day-U2
- Beat It-Michael Jackson
- Beautiful Life-Ace of Base
- Sky Is The Limit- Notorious BIG Ft 112
- I Gotta A Feeling- Black Eyed Peas
- It’s My Life- Bon Jovi
- Soar- Christina Aguilera
- Keep Holding On-Avril Lavigne
- I Believe- Fantasia Barinno
- Sign Of Victory- R.Kelly
- You Gotta Be- Des’ree
- Redemption Song- Bob Marley
- Wind Beneath My Wings- Bette Midler
- Live Like You Were Dying-Tim McGraw
- Chariots Of Fire- Vangelis
- Win- Brian McKnight
- One Moment In Time-Whitney Houston
- When I Get Where I am Going-Brad Paisley Ft. Dolly Parton
- Unwritten- Natasha Bedingfield
- Walk On- U2
- True Colors- Cyndi Lauper
- Thugz Mansion- 2Pac Shakur
- Greatest Love Of All-Whitney Houston
- My Heart Will Go On- Celine Dion
- What A Feeling- Irene Cara
- Circle Of Life- Elton John
- That Is What Friends Are For- Dionne Warwick Ft Gladys Knight, Elton John and Stevie Wonder (more…)
Je,kuna siri ya watu wawili?Yawezekana.Haiwezekani.Ukishamwambia mtu mmoja sio siri tena!Kweli?
Ushawahi kuambiwa na mtu “hii ni siri,usimwambie mtu” au kwa kizungu “this is between you and me,don’t tell anyone”.Basi ni kwanini hakuna siri ya watu wawili?Ina maana katika watu wawili mmoja hawezi kukaa na kitu moyoni,asimwambie mtu?Ndivyo binadamu tulivyo?
Ninapoandika hapa,najaribu kuwaza kuhusu mambo mbalimbali ambayo niliwahi kuyafanya nikitegemea kwamba yangekuwa siri lakini yakageuka kuwa sio siri baada ya kuthubutu kumwambia mtu mmoja mwingine! Kwanini mtu yule au watu wale hawakuchukulia maanani maneno kama “hii naomba iwe siri baina yangu na wewe pekee,asijue mtu tafadhali”.Hivi ni kweli haiwezekani kutunza siri?
Maudhui hayo ndio yaliyopo kwenye Zilipendwa ya Ijumaa hii.Wimbo unaitwa Siri Yako kutoka kwao Bima Lee Orchestra. Burudika.Ijumaa Njema.Weekend Njema.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Unakumbuka Kisa Cha Mesenja Kuleta Balaa kutoka kwao hawa hawa Bima Lee?

Pichani juu ni Dr.Remmy Ongala.Tuliwahi kuandika kwa kirefu historia yake.Unaweza kuisoma kwa kubonyeza hapa. Katika miaka ya nyuma,yeye na Orchestre Super Matimila,ndio walikuwa kitambulisho kizuri cha muziki kutoka Tanzania katika nchi za Ulaya na hata Marekani ya Kaskazini.Alipendwa sana wakati alipokuwa akihudhuria matamasha ya WOMAD.
Mpaka leo hii,watu wengi wa ughaibuni ambao hawatoki Tanzania,hupenda kumuulizia na kutaka kujua yuko wapi na anafanya shughuli gani na kama bado anajishughulisha na muziki.Jibu la maswali hayo linaeleweka;Remmy Ongala siku hizi ni mlokole.Kama bado anajishughulisha na muziki,basi ni ule wa kiroho.Ule wa kumsifu na kumtukuza Muumba.
Remmy Ongala na Orchestre Super Matimila,ndio wanaotupa burudani ya wikiendi hii.Wimbo unaitwa Kipenda Roho.Anasema Kipenda Roho hula nyama mbichi.Kipenda Rohooo…msikilize na furahia mwisho wa wiki.Asante.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Anaitwa Kida Waziri.Enzi zake aliwahi kutamba sana na Vijana Jazz Band.Bila shaka wengi bado tunamkumbuka kwa wimbo wake Wifi Zangu.
Sasa kwa mujibu wa blog ya Brother John Kitime,Kida is back. Hivi karibuni ataingiza sokoni album mpya ambayo itakuwa na nyimbo 6.

Unaweza kuwaita FFU ukipenda.Lakini ukiwatambua au kuwatambulisha kama The Ngoma Africa Band,unakuwa hujakosea pia.Ni bendi inayoundwa na watanzania yenye makao yake makuu nchini Ujerumani.
Katika kuendeleza shamrashamra za majira ya kiangazi(summer), Jumamosi tarehe 7 mwezi wa Nane(August) vijana hao machachari watakuwepo jijini Frankfurt,huko huko Ujerumani katika tamasha kubwa linalojulikana kama Afrika & Karibik Festival litakalofanyika katika viwanja vya Robestock Park hapo Frankfurt.
Baada ya hapo FFU hao wanatarajiwa kuwasha moto katika tamasha lingine kubwa mjini Keiserslautern,Ujerumani.Hiyo itakuwa siku ya Jumapili tarehe 8-08-2010.
Kazi kwenu mashabiki wa muziki mliopo Frankfurt na Keiserslautern.Msikose kwenda kuwaunga mkono mabalozi hawa wa Tanzania kupitia muziki.
Unaweza kuwasikiliza The Ngoma Africa Band hapa www.myspace.com/thengomaafrica

Kufuatia post yetu ya jana kuhusu kutoelewana kulikoibuka kuhusiana na wimbo Nitafanya wa wanamuziki Kidum na Lady Jaydee na Producers wa wimbo huo Hermy B(original version) na RKay Kamanzi(second version),tumepokea maelezo kutoka kwa Kidum.Bila kuyahariri tunayaweka hapa chini;
Mimi ni Kidum .Nataka kutoa maelezo kikamilifu kuhusiyana na iyi muzozo wa uyu wimbo wangu na Lady Jaydee .Hakuna shida yeyote yipo kati yangu na Hermy B ambayo ni producer wa round ya kwanza ya recording ya uyu wimbo .
Kama vile munajuwa mimi naishi nairobi na hapa ndipo nafanya shuhuli za muziki wangu kwa muda mrefu .Sasa kama kwa mfano nime rekodi Dar es salaam alafu nisikiye kuna hitirafu kidogo kwa wimbo ni ngumu niwe nachukuwa ndege kila mara nikikuja Dar es salaam ingawa napapenda sana wakati hapa nairobi piya kuna studios .
Kwa mfano version ya kwanza Key ile tuliimbiya mimi na jaydee ni yenye ambao ilikuwa chini sana kuweza kuwa rahisi kwa mwana dada lakini tulipo rudiya sasa mwana Dada sauti yake ikatoka kama ya malaika .Hapakuwa ubaya wakurudiya ku rekodi tena uyu wimbo sababu mimi mwenyewe niko msanii na kuna kile kitu mimi natafuta kwa hali ya ubora zaidi kama sikipati bila shaka ata ku rekodi mara ya tatu siwezi kusita kufanya . Wimbo ni wangu mimi na lady jaydee sisi wenyewe tukielewana na tu amuwe kuwurudiya sioni kama kuna ubaya .
Hata Hermy B mwenyewe na amini munamusemeya uwongo ya kwamba anamatatizo kuhusiyana uyu wimbo sababu mimi mwenyewe naelewa vema kwenye radio stations nyingi wanacheza version yake ya Audio . bado ni uyo wimbo tu iwe video ama audio .Na pia bado ni Kidum na Lady Jaydee iwe ni video ama ni Audio

Tangu tuweke video ya wimbo unaoitwa Nitafanya ambao ni ushirikiano wa Kidum(mwanamuziki kutoka Burundi) na Lady JayDee hapo jana,tumepokea maoni tofauti tofauti. Maoni hayo yamekuja kutokana na ukweli kwamba kuna tofauti katika wimbo uliopo katika video na ule wa Audio ambao siku za nyuma tuliuweka baada ya kuupata kutoka kwa Producer Hermy B kama sehemu ya promotion ya wimbo huo.
Waliopata kuusikiliza wimbo huo katika Audio walielezea kukerwa kwao na jinsi wimbo huo ulivyobadilishwa au kuwa tofauti na ule wanaousikia katika video.Wengi waliupenda zaidi ule wa Audio.Kwanini nyimbo hizo zikawa tofauti? Je Producer wa nyimbo zote mbili ni mmoja?
Jibu kwa swali la kwanza nitakuachia wewe msomaji/msikilizaji.Ila jibu la swali la pili ni Hapana. Producer wa wimbo wa kwanza ni Hermy B akishirikiana kwa karibu na Kidum mwenyewe wakati ule wa video umetengenezwa na RKay Kamanzi,producer/videographer kutoka nchini Kenya. Huyu ndio pia producer wa nyimbo za msanii Wahu kama vile Sweet Love na Runnin’ Low.
Nini kilitokea? Kwa mujibu wa “Insider” kutoka B’Hitz Studio,kilichotokea ni kwamba,Kidum alipokuja Dar aliamua kumtafuta Hermy ambae siku za nyuma walikutana wakati wa Project Fame kule Nairobi.
Wakakutana na kufanya kazi pamoja huku Hermy B akiwa na jukumu la recording,engineering,adding instruments, mixing and mastering na Kidumu akitoa melodies. Drum Patern yote ikiwa ni ya Hermy B. Raundi ya kwanza ikawa imeisha.
Kidum aliporudi kule Nairobi akakutana na RKay.Dhumuni likiwa ni kutengeneza Video ya wimbo huu kwani RKay anayo pia kampuni ya kutengeneza video inayoitwa Maramoja Films. Cha ajabu RKay akamshawishi Kidum mpaka akakubali kurekodi au “kuutengeneza” upya wimbo huo. RKay akakopi karibuni kila kitu ila akabadili sauti tofauti kidooogo, kama ambavyo inasikika katika video tofauti na inavyosikika katika audio.Kimsingi idea ya kisanii ya Hermy B ikawa imetupwa nje(kwa kiasi fulani) bila yeye mwenyewe kuambiwa au kushirikishwa kama ambavyo sheria za kazi za kisanii zinavyokwenda.

Bila kujua kwa undani kinachoendelea, Hermy B aliutoa wimbo katika Radio Stations mbalimbali na pia blogs kama BC na nyinginezo. Hapo ndipo mambo yalipokwenda mrama kwani Kidum alizi-approach radio kadhaa ambazo tayari zilikuwa zimeshaanza kupiga original version ya wimbo akiwataka kuacha kuupiga. Alipoulizwa kwanini hakuwa tayari kuelezea kwa kina kilichotokea. Lakini stesheni kadhaa zikaendelea kuucheza ule ule wa kwanza ambao umetengenezewa Tanzania na sio Kenya. Kwa kifupi “Beef” likaanzia hapo!
Wakati yote hayo yanatokea, Hermy hakutaka kuongea chochote kile mpaka alipoona wimbo huo wa RKay ukichezwa na upo katika video iliyopigwa au kuongozwa na RKay kama tulivyoiweka hewani jana.
Je unaweza kutambua tofauti za kisanii/za kimuziki baina ya nyimbo hizo mbili?Tizama na kusikiliza kupitia video hapo juu. Kisha sikiliza audio version kwa kubonyeza player hapo chini.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Nini maoni yako?Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na “Insider”,kuna uharamia wa kisanii ambao Hermy B amechezewa na RKay? RKay na Kidum wanasemaje?Stay tuned!
Picha zinawaonyesha Hermy B na Kidum wakiwa studio wakitengeneza original version ya wimbo Nitafanya.


