Nilipokuwa kijana zaidi,miongoni mwa wanamuziki niliopenda kuwasikiliza alikuwa ni Sade.Niliupenda zaidi wimbo wa Smooth Operator Enzi hizo sikujua kama Sade pia ni jina la bendi anayoiongoza ambayo inabeba jina lake.
Huyu ni mzaliwa wa kule Ibadan,Oyo State nchini Nigeria aliyekulia nchini Uingereza.Wazazi walikutana nchini Uingereza kisha baadaye wakaenda kujaribu kuishi nchini Nigeria.Mambo hayakuwa mambo na hivyo akiwa bado kinda kabisa akarejea Uingereza na mama yake.Jina lake halisi ni Helen Folasade Adu na alizaliwa tarehe 16 Januari mwaka 1959.
Baada ya miaka kadhaa yenye mafanikio makubwa katika muziki,Sade walipotea.Sasa mwaka huu,mwezi wa Februari,wanarudi.Albamu inaitwa Soldier of Love.
Mpya kutoka kwa Joe Thomas

