MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Majuzi Tanzania imepoteza msanii hodari ambaye wengi tulianza kumsikia kupitia michezo ya radio. Huyo si mwingine bali Mzee Pwagu(Pumzika kwa Amani Mzee wetu). Lakini je,michezo ya radio ingalipo na nini nafasi yake katika jamii ya leo? Ukweli ni kwamba ndio,michezo ya radio ingalipo na bado ina nafasi na jukumu lile lile la kuelimisha,kubudurudisha, kuonya na hata kurekebisha jamii. Mfano mzuri wa michezo hiyo ni ule unaorushwa na Wahapahapa.

WAHAPAHAPA ni mchezo wa radio wenye nia ya kubadili mtazamo wa kimaisha kuwa chanya. Mchezo huu unalenga suala zima la mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI, matibabu na uangalizi.

Mchezo huu unarushwa kila wiki kwa namna ya kuvutia na kuelimisha, kwa njia ya mawasiliano ya radio.
Maisha yanayojiri katika mchezo huu yanatokea katika vijiji vya kufikirika vya KALUMBI na MAKATANI vilivyoko sehemu Fulani huko Tanzania.

“Homeboys” ni bendi ya muziki ambayo ndio kiunganishi cha matukio yote yanayojiri katika mchezo huu wa kusisimua. Bendi hii inaundwa na wavulana watano ambao baadae kidogo mwanamuziki wa kike anajiunga nao.

Bendi hii inaamini kuwa ikipiga muziki mzuri itafanikiwa kimaisha na hatimae watakuwa nyota kwa washabiki wao wa nyumbani. Bendi inakutana na changamoto kadhaa zinazokinzana na nia yao ya kuwa vinara wa muziki pamoja na kujitengenezea kipato. Kuna migogoro lakini haikosi suluhisho, maslahi ya bendi ni makubwa zaidi ya maslahi ya mtu mmoja mmoja.

Hatuishii kuona maisha ya wanabendi peke yake bali mchezo unazidi kunoga zaidi pale tunapokaribishwa kuona pia maisha ya ndugu, familia, jamaa, na marafiki wa wanabendi. Tunaona migogo na changamoto inayokabili jamii hii na jinsi inavyoamua kuungana pamoja kupambana kuelekea siku mpya.

Unaweza kuusikiliza mchezo huu wa kuvutia kwa kubonyeza hapa ili kwenda katika tovuti ya wahapahapa.com. Ukifika pale tafuta katika vichwa vya kurasa zilizopo pale utaona Mchezo wa Radio.

Msanii maarufu wa vipindi vya redio,maarufu kama Mzee Pwagu(jina lake halisi ni Rajab Kibwana Hatia),amefariki dunia hivi leo katika Hospitali ya Amana jijini Dar-es-salaam alipokuwa amelazwa kwa muda,akisumbuliwa na ugonjwa wa kwikwi(hiccups) pamoja na matatizo mengine yatokanayo na uzee.

Kama utakumbuka, kabla ya ujio wa televisheni au luninga nchini Tanzania kila mtu alikuwa akitegemea Radio Tanzania Dar-es-salaam(RTD) katika kupata habari,burudani na elimu kupitia sanaa ya kuigiza kupitia kitu kilichojulikana kama “michezo ya redio”. Hapo ndipo vipindi kama vya Pwagu na Pwaguzi vilipotamba.

Kipindi cha Pwagu na Pwaguzi kilikuwa kinarushwa hewani hewani kila Jumamosi kuanzia saa 11:45 hadi 12;00 jioni na Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) tangu mwaka 1966 mpaka miaka ya 1980.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kikundi cha Sanaa cha Kaole ambapo marehemu alikuwa mwanachama(kama mshauri) mpaka alipofariki, mazishi yanaweza yakafanyika kesho. Shughuli zote za msiba zinafanyikia nyumbani kwake maeneo ya Kigogo Mbuyuni jijini Dar-es-salaam.

Mzee Pwagu alizaliwa mwaka 1923 mjini Tabora. Ameacha mke na watoto wawili. Mmoja kati ya watoto wake ndiye mama mzazi wa msanii chipukizi Abdul Ahmad Salum maarufu kwa jina la Mr Benny wa kundi la Sanaa la Kaole.

Mwenzake,Pwaguzi, ambaye jina lake kamili ni Ali Said Keto,naye alishafariki dunia miaka kadhaa iliyopita.

MWENYEZI MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI,AMINA.

Picha na sehemu za habari/Habari Leo Ukitaka kujikumbusha kidogo mchezo wa Pwagu na Pwaguzi,Bonyeza hapa.

Anaitwa Yusuf Mlela.Aliwahi kutajwa kuwa Ijumaa Sexiest Bachelor.Ni miongoni mwa movie stars wanaokuja juu kwa kasi nchini Tanzania.Una ushauri wowote kwake kuhusiana na uigizaji wake kama umeshatizama japo moja miongoni mwa filamu alizocheza?

Photo:GP

Kila ifikapo tarehe 13 August, yeye hukumbuka na kusheherekea siku yake ya kuzaliwa. Alipozaliwa pale jijini Mwanza,kaskazini mwa Tanzania wazazi wake walimpa jina la Fareed. Leo hii kwa wengi anatambulika kama Fid Q.

Kama ambavyo umeshasikia,leo hii,tarehe 25 Feb 2010, album yake inayokwenda kwa jina Propaganda inaingia mtaani.Kwa hiyo leo ukizunguka mitaani,usishangae kukutana na mtu kabeba CD mpya ya Fid Q au ukasikia sauti yake kwenye gari,magari,usafiri wa umma.Jambo moja muhimu unaloweza kufanya ni kujipatia nakala yako halisi.Hakuna njia nzuri zaidi ya kuunga mkono juhudi za wasanii zaidi ya hiyo!

Hivi karibuni nilipata nafasi ya kuzungumza machache na Fid Q kuhusu ujio wa albamu hii ya Propaganda,muungano wa wasanii wa bongo fleva na pia suala zima la nyimbo nyingi za bongo fleva kuwa na maudhui ya mapenzi zaidi ya kitu kingine chochote.Kwanini ameiita album yake Propaganda? Anamaanisha nini? Je unajua Fid Q ana mtazamo gani kuhusu muungano wa wasanii?Je anasemaje kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika maendeleo au kifo cha muziki wa kizazi kipya? Fuatana nami katika mahojiano yafuatayo;

BC: Kwanza hongera kwa album mpya.Labda kwa ujumla tu,album hii umeitengenezea katika studio zipi,itakuwa na nyimbo ngapi na umewashirikisha wasanii gani wengine?

Fid Q: Asante sana kaka.Album hii nimeifanya katika studio 3 tofauti.Nimefanya kwa MJ Records, Tongwe Records na kwa Lamar.Nimewashirikisha wasanii kama AY, NCHA KALI, MZEE ZORRO, JUMA NATURE,QJ, NYLON WA MANZESE CREW, BI KIDUDE na wengine kibao bila kuwasahau MATONYA na MZUNGU KICHAA.

BC: Kwanini umeiita Propaganda?Kuna ujumbe wowote maalumu kutokana na jina la album? (more…)

befftabc1

Watanzania Ali Kiba, Pretty Poet( Jacqueline Kweka Kibacha) na kampuni ya Bongo UK ni miongoni mwa watu waliochaguliwa kuwania Tuzo za BEFFTA (Black Entertainment,Film,Fashion,Television and Arts Awards) zinazotarajiwa kufanyikia jijini London tarehe 17 October mwaka huu ndani ya London Hilton Metropole.

Ali Kiba amechaguliwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha Best International Act huku Pretty Poet akichaguliwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha Best Spoken Word Artist/Poets. Kampuni ya Bongo UK imechaguliwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha Best Event Promoters.

Kwa orodha kamili ya waliochaguliwa kuwania tuzo hizo,tafadhali bonyeza hapa. Ili kuona kazi za Jacqueline Kweka Kibacha,bonyeza hapa na hapa na hapa.

Kama ilivyo kawaida ya tuzo siku hizi,kura zinapigwa na wananchi.Wakati ukiwadia kwa zoezi hilo,BC itakujulisha.Kwa sasa tunapenda tu kuwapongeza Ali Kiba,Pretty Poet na Bongo UK for the nomination.

twangabc1

Wanenguaji wa kike wa Twanga Pepeta wakiwajibika wakati wa uzinduzi wa Dar-es-salaam.

twanga2bc

Safu ya wanenguaji wa kiume wakiwa kazini.

Bendi maarufu ya muziki wa dansi nchini Tanzania, African Stars au maarufu kama Twanga Pepeta, majuzi walizindua albamu nyingine ambayo ni ya kumi tangu bendi hiyo ianze kuwapa burudani wapenzi wa muziki. Albamu hii wameipa jina Mwana-Dar-es-salaam. Sijajua kwanini wameipa jina hilo lakini nahisi ni kutokana na ukweli kwamba kwa muda sasa Twanga Pepeta wamekuwa wafalme wa burudani hususani jijini Dar-es-salaam yalipo makao yao makuu.Hongera Twanga Pepeta.

Lakini wakati albamu zinazinduliwa,muziki unakonga roho,watu wanaburudika yapo maswali ambayo baadhi ya watu wamekuwa wakiuliza. Tumeona nasi tuyalete hapa ili kama kawaida kila mtu atoe maoni au mapendekezo yake; Swali la kwanza ambalo lilianzia pale kwa Michuzi JR linauliza Eti Ni Kwanini Madensa Wengi wa Kibongo Wana Vitambi? Unaweza kusoma post hiyo na maoni yaliyotolewa kwa kubonyeza hapa. Kabla mada hiyo haijatulia msomaji wetu mmoja akatutumia e-mail akihoji kwanini wanenguaji wa kike huwa wanapenda kuvaa “nusu uchi” wakati wenzao wa kiume wakiwa wameficha karibu kila sehemu ya miili yao?

Kwa sababu tunaamini kwamba sisi hapa BC hatuwezi kuwa na majibu ya kutosheleza,hatuna budi kuomba msaada kutoka kwako msomaji.Unasemaje?Eti ni kwanini? Picha za hapo juu zikusaidie katika majibu.

Picha zote kwa hisani ya Charahani.

names

Tizama picha kwa makini. Unaweza kuwatambua wangapi kati ya hao waliopo pichani? Kwa ufupi ni kwamba wote ni wasanii. Kama sio sanaa ya muziki basi ni sanaa nyingine.

ally-and-farha

Pichani ni wabunifu wa mitindo ya mavazi Farha(kushoto) na Ally Rehmttulah(kulia).Picha hii ilipigwa na Mpoki Bukuku wakati wabunifu hao walipokuwa wanahudhuria onyesho la mavazi lililoitwa Lady in Red hivi karibuni jijini Dar-es-salaam.Ukitaka kupata vitu zaidi kuhusu kazi za Ally Rehmttulah unaweza kuitembelea tovuti yake kwa kubonyeza hapa.

mrishompotobc

UMAHIRI wa Mrisho Mpoto umekuwa ukiwakuna wengi hasa anapokuwa jukwaani akidondosha mashairi yake na mwaka jana alifanikiwa kushinda moja ya tuzo kubwa katika sanaa kwa Afrika ijulikanayo kama Slam, ambayo ilikuwa inashikiliwa na mmoja wa wasanii mahiri aitwaye, Steff H2K kutoka Mauritius.

Ushindi wa Mpoto umemfanya apate nafasi ya kushiriki fainali za tuzo za Slam za dunia, ambazo zinafanyika nchini Ufaransa Machi, mwaka huu lakini hiyo haitoshi wala haimzuii yeye kuendelea kusaka nauli ya kwenda Ikulu.

Baada ya kuwa ameshiriki katika wimbo wa ‘Salamu Zangu’ na kuweza kuchukua nafasi kubwa huku akimfunika mmliki wa wimbo huo Irene Sanga, Mpoto ameamua kuibukia upande wa pili na kutoa wimbo wa ‘Nikipata Nauli’.

[Usikilize wimbo "Nikipata Nauli" kwa kubonyeza player hapo chini kisha ndio uendelee kusoma makala hii hapo chini]JM

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

(more…)

fid-qbc

Bongo,Bongo…ooh Bongo!Kila kukicha watu wanazidi kuwa wabunifu na wagunduzi. Kila siku akili zinazidi kuchemka, bongo zinazidi kutenda kinachotakiwa kutendwa.

Kama bado huamini kwamba Bongo inazidi kuja juu kwa ubunifu,basi jaribu kwanza kutizama hapo chini video mpya kutoka kwa Fareed Kubanda aka Fid Q(pichani) iitwayo I AM A PROFFESSIONAL ambayo ni single ya tatu kutoka kwenye albamu yake iitwayo Darwinz Naitmea.Kutoka kwetu hakuna la ziada bali pongezi kwa Fid Q kwa ubunifu na uchapa kazi.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page