
Kila ifikapo tarehe 13 August, yeye hukumbuka na kusheherekea siku yake ya kuzaliwa. Alipozaliwa pale jijini Mwanza,kaskazini mwa Tanzania wazazi wake walimpa jina la Fareed. Leo hii kwa wengi anatambulika kama Fid Q.
Kama ambavyo umeshasikia,leo hii,tarehe 25 Feb 2010, album yake inayokwenda kwa jina Propaganda inaingia mtaani.Kwa hiyo leo ukizunguka mitaani,usishangae kukutana na mtu kabeba CD mpya ya Fid Q au ukasikia sauti yake kwenye gari,magari,usafiri wa umma.Jambo moja muhimu unaloweza kufanya ni kujipatia nakala yako halisi.Hakuna njia nzuri zaidi ya kuunga mkono juhudi za wasanii zaidi ya hiyo!
Hivi karibuni nilipata nafasi ya kuzungumza machache na Fid Q kuhusu ujio wa albamu hii ya Propaganda,muungano wa wasanii wa bongo fleva na pia suala zima la nyimbo nyingi za bongo fleva kuwa na maudhui ya mapenzi zaidi ya kitu kingine chochote.Kwanini ameiita album yake Propaganda? Anamaanisha nini? Je unajua Fid Q ana mtazamo gani kuhusu muungano wa wasanii?Je anasemaje kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika maendeleo au kifo cha muziki wa kizazi kipya? Fuatana nami katika mahojiano yafuatayo;
BC: Kwanza hongera kwa album mpya.Labda kwa ujumla tu,album hii umeitengenezea katika studio zipi,itakuwa na nyimbo ngapi na umewashirikisha wasanii gani wengine?
Fid Q: Asante sana kaka.Album hii nimeifanya katika studio 3 tofauti.Nimefanya kwa MJ Records, Tongwe Records na kwa Lamar.Nimewashirikisha wasanii kama AY, NCHA KALI, MZEE ZORRO, JUMA NATURE,QJ, NYLON WA MANZESE CREW, BI KIDUDE na wengine kibao bila kuwasahau MATONYA na MZUNGU KICHAA.
BC: Kwanini umeiita Propaganda?Kuna ujumbe wowote maalumu kutokana na jina la album? (more…)

Watanzania Ali Kiba, Pretty Poet( Jacqueline Kweka Kibacha) na kampuni ya Bongo UK ni miongoni mwa watu waliochaguliwa kuwania Tuzo za BEFFTA (Black Entertainment,Film,Fashion,Television and Arts Awards) zinazotarajiwa kufanyikia jijini London tarehe 17 October mwaka huu ndani ya London Hilton Metropole.
Ali Kiba amechaguliwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha Best International Act huku Pretty Poet akichaguliwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha Best Spoken Word Artist/Poets. Kampuni ya Bongo UK imechaguliwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha Best Event Promoters.
Kwa orodha kamili ya waliochaguliwa kuwania tuzo hizo,tafadhali bonyeza hapa. Ili kuona kazi za Jacqueline Kweka Kibacha,bonyeza hapa na hapa na hapa.
Kama ilivyo kawaida ya tuzo siku hizi,kura zinapigwa na wananchi.Wakati ukiwadia kwa zoezi hilo,BC itakujulisha.Kwa sasa tunapenda tu kuwapongeza Ali Kiba,Pretty Poet na Bongo UK for the nomination.

Wanenguaji wa kike wa Twanga Pepeta wakiwajibika wakati wa uzinduzi wa Dar-es-salaam.

Safu ya wanenguaji wa kiume wakiwa kazini.
Bendi maarufu ya muziki wa dansi nchini Tanzania, African Stars au maarufu kama Twanga Pepeta, majuzi walizindua albamu nyingine ambayo ni ya kumi tangu bendi hiyo ianze kuwapa burudani wapenzi wa muziki. Albamu hii wameipa jina Mwana-Dar-es-salaam. Sijajua kwanini wameipa jina hilo lakini nahisi ni kutokana na ukweli kwamba kwa muda sasa Twanga Pepeta wamekuwa wafalme wa burudani hususani jijini Dar-es-salaam yalipo makao yao makuu.Hongera Twanga Pepeta.
Lakini wakati albamu zinazinduliwa,muziki unakonga roho,watu wanaburudika yapo maswali ambayo baadhi ya watu wamekuwa wakiuliza. Tumeona nasi tuyalete hapa ili kama kawaida kila mtu atoe maoni au mapendekezo yake; Swali la kwanza ambalo lilianzia pale kwa Michuzi JR linauliza Eti Ni Kwanini Madensa Wengi wa Kibongo Wana Vitambi? Unaweza kusoma post hiyo na maoni yaliyotolewa kwa kubonyeza hapa. Kabla mada hiyo haijatulia msomaji wetu mmoja akatutumia e-mail akihoji kwanini wanenguaji wa kike huwa wanapenda kuvaa “nusu uchi” wakati wenzao wa kiume wakiwa wameficha karibu kila sehemu ya miili yao?
Kwa sababu tunaamini kwamba sisi hapa BC hatuwezi kuwa na majibu ya kutosheleza,hatuna budi kuomba msaada kutoka kwako msomaji.Unasemaje?Eti ni kwanini? Picha za hapo juu zikusaidie katika majibu.
Picha zote kwa hisani ya Charahani.

Tizama picha kwa makini. Unaweza kuwatambua wangapi kati ya hao waliopo pichani? Kwa ufupi ni kwamba wote ni wasanii. Kama sio sanaa ya muziki basi ni sanaa nyingine.

Pichani ni wabunifu wa mitindo ya mavazi Farha(kushoto) na Ally Rehmttulah(kulia).Picha hii ilipigwa na Mpoki Bukuku wakati wabunifu hao walipokuwa wanahudhuria onyesho la mavazi lililoitwa Lady in Red hivi karibuni jijini Dar-es-salaam.Ukitaka kupata vitu zaidi kuhusu kazi za Ally Rehmttulah unaweza kuitembelea tovuti yake kwa kubonyeza hapa.

UMAHIRI wa Mrisho Mpoto umekuwa ukiwakuna wengi hasa anapokuwa jukwaani akidondosha mashairi yake na mwaka jana alifanikiwa kushinda moja ya tuzo kubwa katika sanaa kwa Afrika ijulikanayo kama Slam, ambayo ilikuwa inashikiliwa na mmoja wa wasanii mahiri aitwaye, Steff H2K kutoka Mauritius.
Ushindi wa Mpoto umemfanya apate nafasi ya kushiriki fainali za tuzo za Slam za dunia, ambazo zinafanyika nchini Ufaransa Machi, mwaka huu lakini hiyo haitoshi wala haimzuii yeye kuendelea kusaka nauli ya kwenda Ikulu.
Baada ya kuwa ameshiriki katika wimbo wa ‘Salamu Zangu’ na kuweza kuchukua nafasi kubwa huku akimfunika mmliki wa wimbo huo Irene Sanga, Mpoto ameamua kuibukia upande wa pili na kutoa wimbo wa ‘Nikipata Nauli’.
[Usikilize wimbo "Nikipata Nauli" kwa kubonyeza player hapo chini kisha ndio uendelee kusoma makala hii hapo chini]JM
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Bongo,Bongo…ooh Bongo!Kila kukicha watu wanazidi kuwa wabunifu na wagunduzi. Kila siku akili zinazidi kuchemka, bongo zinazidi kutenda kinachotakiwa kutendwa.
Kama bado huamini kwamba Bongo inazidi kuja juu kwa ubunifu,basi jaribu kwanza kutizama hapo chini video mpya kutoka kwa Fareed Kubanda aka Fid Q(pichani) iitwayo I AM A PROFFESSIONAL ambayo ni single ya tatu kutoka kwenye albamu yake iitwayo Darwinz Naitmea.Kutoka kwetu hakuna la ziada bali pongezi kwa Fid Q kwa ubunifu na uchapa kazi.

Akiwa tayari na albamu zisizopungua tano kibindoni, Jennifer Mgendi(pichani) ni miongoni mwa wanamuziki wa muziki wa injili au kwa kiingereza Gospel nchini Tanzania ambao wamejijengea sifa na umaarufu mkubwa kutokana na kazi yake hiyo ya uimbaji na kumtukuza mola.
Lakini tofauti moja kubwa ya Jennifer na wanamuziki wengine wa muziki wa injili ni kwamba yeye pia ni mtunzi mzuri wa hadithi za filamu.Baadhi ya filamu alizowahi kutunga ni kama vile Pigo la Faraja, Joto la Roho na Teke la Mama.
Alianza rasmi kujishughulisha na kazi ya muziki wa injili mwaka 1995.Albam yake ya kwanza iliitwa ‘Nini?’. Baada ya hapo alitoka tena na albamu zake zilizokwenda kwa majina ‘Ukarimu wake’, ‘Yesu Nakupenda’,'Nikiona Fahari’ na ya hivi karibuni zaidi inayoitwa Mchimba Mashimo.
Hivi karibuni tulipata nafasi ya kufanya naye mahojiano ambayo utayasoma hivi punde. Katika mahojiano haya,Jennifer anakupa kwa undani kuhusu historia yake kimuziki na kibinafsi. Ni kweli kwamba muziki wa injili wa leo ni wa “kidunia” zaidi ya “kiroho”? Anasemaje kuhusiana na hoja hiyo? Je Jennifer anaongeleaje tofauti za muziki wa injili na ule wa Bongo Fleva?Unakubaliana naye?
Nini mipango yake kwa mwaka huu wa 2009 na ana ushauri gani kwa vijana?Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;
BC: Karibu Jennifer ndani ya BC.Sijui nikuambie mambo vipi au bwana asifiwe?
JM:Asante sana ndugu yangu. Yote mema tu kwani mambo ni safi na Bwana anaendelea kusifiwa…
BC:Kwa kifupi tu unaweza kutueleza historia ya maisha yako?
JM:Nilizaliwa miaka karibu 37 iliyopita hapa hapa jijini Dar es Salaam katika familia ya watoto watatu nikiwa nimetanguliwa na kaka wawili. Nimepata elimu yangu katika mikoa ya Dar es salaam na Tanga. Nilianza uimbaji rasmi mwaka 1995 na hapo katikati nilifanya kazi kadhaa za kuajiriwa kama Ualimu na Ukutubi lakini tangu mwaka 2007 niliacha kazi za kuajiriwa na mpaka hivi leo ninafanya shughuli zangu binafsi. (more…)

MWANAMUZIKI maarufu wa Hip Hop nchini, Joseph Haule maarufu kama Profesa Jay, anaondoka nchini kesho (Novemba 20, 2008) kwenda Abuja, Nigeria kutumbuiza kwenye tuzo za muziki za MTV Africa Music Awards with Zain (MAMA).Kwa undani zaidi wa habari hii bonyeza hapa.BC inamtakia kila la kheri Prof.Jay.
Anaitwa Nuru Magram.Makazi yake ni ndani ya jiji la Stockholm nchini Sweden. Bila shaka unamkumbuka kwa vibao vyake kama vile Walimwengu na Msela ambavyo ndivyo vilimtoa katika ulimwengu wa muziki.
Hivi karibuni amekuwa studio akikamilisha project yake mpya ya muziki ambayo itakamilika hivi karibuni.Lakini kuonyesha jinsi ambavyo bado hajajiweka kando na mambo ya muziki, hivi karibuni mnamo tarehe 22 Novemba anatarajiwa kufungua show ya mwanamuziki mwingine wa Bongo Flava, Ali Kiba.Show hiyo itafanyikia jijini Stockholm.
Ali Kiba inasemekana ameweka rekodi ya kuwa mwanamuziki wa kwanza wa muziki wa kizazi kipya kufanya tour ndefu kushinda zote zilizowahi kufanywa na mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya.Nuru ameahidi kufanya vitu visivyo vya kawaida hiyo tarehe 22 Novemba.Kazi kwenu wakazi wa Sweden na nchi zilizo jirani.Unaweza kumcheki Nuru hapo chini katika wimbo wake Walimwengu.Ni zouk iliyokuwa imetulia na yenye ujumbe mzuri.

