Anavyoonekana hivi sasa Dr.Harrison Mwakyembe
Kwa muda sasa,hali ya afya ya Naibu Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Jimbo la Kyela mkoani Mbeya,Dr.Harrison Mwakyembe, imekuwa ni gumzo lisiloisha.Yanasemwa mengi kuhusu ugonjwa unaomsumbua.Yeye mwenyewe hajaweka bayana juu ya ugonjwa wake.Serikali nayo,kwa kuzingatia taratibu za kitabibu,haiwezi kusema kitu.Bado anaugua.
Pamoja na kwamba bado anaugua,hali yake inaendelea vizuri.Mwishoni mwa wiki alithibitisha hilo pale alipoweza kuhudhuria ibada katika Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mch.Josephat Gwajima lililopo maeneo ya Kawe jijini Dar-es-salaam.Hizi hapa ni baadhi ya picha kutoka katika tukio hilo ambalo pia lilihudhuriwa na wabunge kadhaa kama inavyoonekana katika picha hizi ambazo BC imezipata kwa hisani ya John Bukuku wa Full Shangwe.
Baadhi ya Wabunge waliohudhuria misa hiyo katika kumsindikiza mwenzao: Kutoka kushoto ni Mbunge wa Same-Mashariki,Mh.Anne Kilango Malecela, Waziri wa Afrika Mashariki,Samuel Sitta,Mbunge wa Kahama,Mh.James Lembeli,Dr.Harrison Mwakyembe na Mch.Gwajima
Dr.Mwakyembe akiondoka baada ya kumalizika kwa ibada hiyo.Katika salamu zake alisema tangu Octoba 9 mwaka jana alikuwa hajawahi kuweza kuvaa viatu.Kama inavyoonekana katika picha hii,sasa anaweza kuvaa viatu.
Mwaka jana mwezi wa nane(August),tuliuliza swali katika post hii hapa.Kichwa cha habari kilikuwa katika lugha ya Kiingereza kwamba Dr.Asha-Rose Migiro:The Next President? Swali lile tuliliuliza kufuatia kilichokuwa kikiendelea katika duru za kisiasa wakati ule. Kulikuwa na tetesi kwamba Dr.Migiro,huenda akajitupa ulingoni kuwania Urais mwaka 2015.Wadau mbalimbali wakawa wakiongelea uwezekano wa Tanzania kupata Rais wa Kwanza Mwanamke na mambo kama hayo.
Kwa bahati nzuri au mbaya,wakati ule Dr.Asha-Rose Migiro bado alikuwa akishikilia cheo chake cha U-naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(United Nations) na hivyo kufanya tetesi zile ziishie hewani kama vile mvuke wa maji ya moto tu. Mambo yamebadilika kidogo hivi majuzi ilipojulikana kwamba Dr.Migiro atakiachia cheo cha U-Naibu Katibu Mkuu wa UN kwa sababu muda wake umemalizika.Haijawekwa wazi kwamba kwanini yeye aondoke wakati Katibu Mkuu wake,Ban-Ki Moon bado yupo na kama walikuwa na ajenda basi ni yao wote kuitekeleza.Anyway,hayo ni mambo mengine,tuyaache kwa sasa.
Sasa kwa sababu Dr.Migiro anaondoka UN na hivyo kumaanisha kwamba atakuwa na nafasi zaidi ya kuwania Urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2015, tayari fukuto la maoni ya wananchi limeanza kutanda. Je,agombee mwaka 2015? Je anafaa?Je,Tanzania ipo tayari kwa Rais Mwanamke? Hayo ni baadhi ya maswali yasiyo na majibu ya moja kwa moja ambayo yamekuwa yakisikika iwe ni mtaani,mitandaoni,katika vyombo mbalimbali vya habari hususani Radios nk.Nini maoni yako wewe msomaji wa BC?

Unaowaona pichani,wote ni wanasiasa.Wote ni vijana.Nape Nnauye(kushoto katika picha) ni Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM )anayesimamia Itikadi na Uenezi.Kulia ni Mh.John Mnyika(MB) ambaye ni Mkuu wa Habari na Uenezi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA). Kazi zao zinafanana.Wanaongea na sisi tunawasikiliza.Wanaeneza itikadi na kunadi sera za vyama vyao.
Lakini suala la siasa ni imani.Unaamini kwamba anachokisema yule ni cha kweli na anayo dhamira nzuri kuhusu maendeleo yangu. Sasa wanaposimama hawa wawili kuongea,unamwamini yupi zaidi? Ni kitu gani kinachokufanya umwamini zaidi huyo unayemwamini? Tungependa kupata maoni yako.
NB: Vipima joto hivi vya BC,ni sehemu ya kuhakikisha kwamba viongozi na wananchi wanajua wapi wanaposimama au wanapobidi kusimama kila wakati na sio wakati wa uchaguzi tu.
Zaidi ya mwaka mmoja umeshapita sasa tangu Rais Jakaya Mrisho Kikwete aingie madarakani katika muhula wake wa pili wa kuliongoza taifa hili. Ingawa mwaka mmoja sio muda wa kutosha kwa kiongozi kukamilisha malengo na ahadi zote,ni muda wa kutosha kutoa picha ya mfumo na mtindo wa ki-uongozi.
Je,mwaka mmoja baadae,uchaguzi ungefanyika unadhani kura yako ungempa nani katika ya Rais Jakaya Kikwete na aliyekuwa mpinzani wake mkuu katika uchaguzi uliopita,Dr.Wilbrod Slaa?Kwanini?
Ninapoandika post hii, Dr.Wilbroad Slaa,kupitia tamko la CHADEMA wametoa msimamo wao kuhusu uongozi wa Rais Kikwete mwaka mmoja baadae.Gazeti la Mwananchi limeandika kwa kirefu kuhusu hilo na unaweza kulisoma kupitia hapa.
NB: Unaweza kutumia fursa hii kutoa maoni ya kujenga kwa maana ya kwamba kutoa maoni yenye tija na sio lawama na matusi.
TAREHE 31 DESEMBA, 2011
Ndugu Wananchi;
Leo tunauaga mwaka 2011 na kuukaribisha mwaka 2012. Naungana nanyi Watanzania wenzangu kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uhai na bahati ya kuiona siku ya leo. Wapo ndugu, jamaa na marafiki zetu wengi ambao hawakujaaliwa kuwa nasi kwa kuwa wametutangulia mbele ya haki. Tuzidi kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu awape mapumziko mema na sisi tuendelee kumuomba Mola wetu atujaalie rehema na neema tele katika mwaka ujao.
Mapitio ya Mwaka 2011 na Matarajio kwa Mwaka 2012
Miaka 50 ya Uhuru
Ndugu wananchi;
Mwaka 2011 ulikuwa mwaka wa aina yake na wa kihistoria kwa nchi yetu na wenye mchanganyiko wa mambo. Kulikuwa na matukio ya furaha na majonzi na ulikuwa mwaka tuliopata mafanikio mengi na changamoto mbalimbali. Tumeweza kusherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara kwa heshima stahiki kama nilivyoelekeza katika hotuba yangu ya kuuaga mwaka 2010 na kuukaribisha mwaka 2011. Tumezitumia vizuri sherehe hizo kufanya tathmini ya maendeleo tuliyoyapata tangu Uhuru mpaka hapa tulipo sasa pamoja na kutambua changamoto zilizo mbele yetu.
Hakika tumepata mafanikio makubwa sana katika miaka 50 hii ya Uhuru wetu kuliko yale yaliyopatikana katika miaka 77 ya ukoloni wa Wajerumani (miaka 34) na Waingereza (miaka 43). Pamoja na mafanikio hayo tuliyoyapata bado nchi yetu ni miongoni mwa nchi maskini sana duniani hivyo bado tunayo kazi kubwa sana ya kufanya mbele yetu. Katika tathmini iliyofanywa na kila Wizara na Idara za Serikali, mambo yanayostahili kufanyika miaka ijayo pamoja na mikakati ya kufikia malengo hayo, yameainishwa vizuri.
Mpango wa Maendeleo
Ndugu Wananchi;
Bahati nzuri, mambo yote yaliyoainishwa kufanywa yanakuwa sehemu ya mambo ya kutekelezwa katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2011/2012 mpaka 2015/2016. Kama mtakavyokumbuka miongoni mwa matukio muhimu katika mwaka 2011 ni kukamilika kwa kazi ya kufanya tathmini ya kuhuisha Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025 na kutengenezwa kwa Mpango wa Kwanza wa Maendeleo wa Miaka Mitano wa kutekeleza Dira hiyo. Tumejipanga vizuri kutekeleza Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano katika Bajeti ijayo. Pia nimeunda Kikundi Kazi kinachoongozwa na Prof. Benno Ndulu cha kushauri juu ya vipaumbele na kufuatilia utekelezaji wa Mpango huo.
Ndugu Wananchi;

Kufuatia habari tarehe 28 Novemba kuhusu ‘kupanda kimya kimya kwa posho za wabunge kwa zaidi ya asilimia 150’ tarehe 29 Novemba 2011 nilitoa kauli yangu kama mbunge na katibu wa wabunge wa CHADEMA kuhusu suala husika.
Katika kauli hiyo nilieleza kuwa: “ Wabunge wa CHADEMA hatujapokea taarifa rasmi kwamba masharti ya kazi ya ubunge yamebadilika na kwamba viwango vya posho vimeongezwa. Wala kamati ya wabunge wa CHADEMA haijawahi kuridhia ongezeko lolote la posho ya vikao (sitting allowance) kwa wabunge. Napenda kutumia fursa kusisitiza msimamo wetu wa kutaka posho za vikao (sitting allowance) ziweze kufutwa kwa wabunge na katika mfumo mzima wa malipo ya wakati wa kazi miongoni mwa watumishi wa umma”.
Hivyo, kama mbunge na katibu wa wabunge wa CHADEMA nilitoa mwito kwa Rais Jakaya Kikwete kwa niaba ya Serikali na Spika Anna Makinda kwa niaba ya Bunge kutoa kauli kuhusu suala hili ili kuondoa hisia zinazojengeka kwamba ‘wabunge wote tumekaa bungeni na kukubaliana kujiongezea posho ya vikao’.
Kufuatia Spika Makinda kutoa kauli na kunukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari tarehe leo tarehe 7 Novemba 2011 naomba kutoa msimamo wangu kama ifuatavyo:
“ Ongezeko la posho ya vikao lilofanyika linapaswa kusitishwa kwa kuwa limefanyika kinyume na taratibu na pia halina uhalali wowote kimantiki na halijazingatia uhalisia wa maisha ya wananchi na uchumi wa nchi kwa ujumla; nyongeza hiyo ya posho ya vikao ni haramu (Illegitimate).
Rais Jakaya Mrisho Kikwete jioni ya leo tarehe 27 Novemba 2011,amekutana na viongozi wa chama kikuu cha upinzani,CHADEMA,Ikulu jijini Dar-es-salaam ili kuzungumza nao juu ya musuada uliopitishwa hivi karibuni Bungeni kuhusu sheria ya kuundwa kwa tume ya kukusanya maoni ya wananchi juu ya uundwaji wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kama utakumbuka wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) walisusia upitishwaji wa musuada huo mjini Dodoma.Hii hapa ni SLIDESHOW ya picha mbalimbali kutoka katika mkutano huo ambao bado haijawekwa wazi juu ya yale yaliyoamuliwa.Lakini kutokana na muonekano wa picha tu,yaelekea ulikuwa mkutano mzuri!
Picha zote na Ikulu.Ukitaka kuiona picha katika ukubwa wake,bonyeza juu yake.

Mtaani kuna maneno mengi.Kuna huyu anayeongea kwa uhakika zaidi kama vile wewe na yeye asubuhi mnatokea katika mlango mmoja.Kuna mwingine anakaa kimya kisha baadae ahamie “kijiwe” kingine na kusema ee bwana eeh,leo kule kimesemwa hiki na kile.Kumbe fulani na fulani wako hivi na vile.Sijui wewe utamuita nani.Wajuaji wengine humuita mbea au mpenda udaku.
Kuna Siasa na Kuna Politrics.Kuna maneno lukuki.Eti huyu hapatani na yule.Eti huyu na yule hawapikiki chungu kimoja.Ni utata kuwaweka katika chumba kimoja.Dhahma yaweza anguka. Kuna ukweli?
Eti ukiitazama picha hiyo hapo juu na ukasikia maneno yaliyopo pale mkwajuni unawaza nini?Ni kweli?

Bila shaka unafuatilia siasa za nchi yetu.Ni nani asiyefuatilia?Kila kitu hapa kinaenda “kisiasa”.Kila kukicha vichwa vya habari vinavyopamba kurasa za mbele za magazeti na majarida yetu vimejaa “siasa”.Siasa ndio sisi na sisi ndio siasa.Bahati mbaya zaidi ni kwamba hata mambo ambayo kimsingi hayahitaji siasa bali weledi,sisi tunayapindishia kwenye siasa.Ni kama vile hakuna imani kwamba kuna yanayowezekana bila siasa.
Katika ulingo huo wa siasa,yupo mtu ambaye siasa yaweza kuwa ndio kazi yake.Ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),Nnape Nnauye(pichani). Ni kijana.Bado ana nguvu ya kuongea na kukitumikia chama tawala.Nikiwa kama mtazamaji wa siasa za nchi(kama wewe), nasikia mengi kutoka kwa Nnape Nnauye.Nasikia habari za kujivua gamba.Nikigeuka nasikia habari za maamuzi mazito.Ninapoanza safari ya ndotoni,nasikia habari za uongozi uliotukuka,habari za marais watarajiwa,vijana. Kisha nasikia kuhusu mmeguko ndani ya Chama Tawala.Kwamba kuna makundi.Kuna hujuma nzito miongoni mwa wanachama…wengine wakongwe.
Kwanini naandika hili?Najaribu kumuelewa Nnape Nnauye.Ni kiongozi au mtendaji wa aina gani?Anasimamia itikadi zipi?Nini kinamsukuma? Kwa sababu bado sina hata sembuse ya majibu kwa maswali niliyonayo kichwani kwangu,nataka kuanzia kwako msomaji.Ningependa zaidi kusikia kutoka kwa wanachama au wapenzi wa CCM.Mnazungumziaje utendaji wa Nnape? Na kwa wale wenzangu na mie tunaotazama kutoka pembezoni mwa fensi,mnaonaje? Miaka 10 ijayo,unadhani Nnape atakuwa wapi?


sending...





