MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Unapoongelea sinema,hakuna ubishi kwamba majadiliano yako inabidi yaanzie Hollywood.Na unapokuwa Hollywood na kuamua kuanzisha mjadala wa Tuzo(awards) basi yakupasa uanzie kwenye tuzo maarufu za Academy au Oscars.

Muda mchache uliopita majina ya sinema,waigizaji,waongoza sinema na vipengele vingine walioteuliwa kuwania tuzo hizo kwa mwaka huu yametangazwa. Kama ambavyo ilitarajiwa, sinema ya Avatar iliyoongozwa na James Cameron pamoja na sinema ya The Hurt Locker ambayo imeongozwa na Kathryn Bigelow(mke wa zamani wa James Cameron) ndio zimepata teuzi nyingi zaidi katika kuwania tuzo hizo maarufu ambazo zinafanyika kwa mara ya 82 (miaka 82). Movie hizo zimeteuliwa mara 9 au katika vipengele 9.

Shughuli za mwaka huu za tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika tarehe 7 Mwezi Machi(takribani siku 33 zijazo).Zitaonyeshwa moja kwa moja(live) kupitia kituo cha televisheni cha ABC cha nchini Marekani.

Kwa orodha kamili ya Oscar Nominations kwa mwaka huu,bonyeza hapa. Je kuna movie,actor au actress ambaye ulitarajia angeteuliwa kuwania tuzo za mwaka huu ambaye hajatokea katika orodha?

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Movie inaitwa Legion. Mungu amekosa imani na wanadamu.Anatuma malaika kuja kuiangamiza dunia. Starring Paul Bettany, Dennis Quaid,Lucas Black,Tyrese Gibson etc.Imeongozwa na Scott Stewart

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Movie inaitwa Extraordinary Measures: Ni kisa cha kweli kinachowahusu wazazi John na Ailleen Crowley ambao wanajitolea kudhamini utatutwaji wa tiba kwa ugonjwa wa nadra ambao unawateketeza watoto wao wawili.Movie nzuri sana hii kwa wazazi.Starring Harrison Ford,Brendan Fraser, Courtney B.Vance nk.Imeongozwa na Tom Vaughan

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Movie inaitwa The Book of Eli. Starring Denzel Washington, Gary Oldman,Mila Kunis na wengineo.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Movie inaitwa The Spy Next Door.Starring Jackie Chan, Amber Valleta,Billy Ray Cyrus(baba yake Miley Cyrus),George Lopez na wengineo. Director ni Brian Levant.

mgonjabc1

Kama ulidhani ya mwaka 2008 ndio yashaisha basi ulikosea.Mambo yangali yakiendelea.Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Fedha na Mipango,Bw.Gray Mgonja leo ametinga kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Henzron Mwankenja, akikabiliwa na mashtaka mbalimbali.Mojawapo ya mashtaka anayokabiliwa nayo ni pamoja na matumizi mabaya ya madaraka kama ilivyokuwa kwa mawaziri wa zamani wa wizara hiyo nyeti, Daniel Yona na Basil Mramba waliofikishwa kizimbani wiki mbili zilizopita.

Habari hii inaendelea…stay tuned.

Muite Steven Kanumba.Hapa ilikuwa wiki iliyopita wakati wa utoaji wa tuzo za Vinara wa filamu Tanzania. Waandaaji wa tuzo hizo walimpa Kanumba Tuzo ya Heshima kutokana na mchango wake katika maendeleo ya filamu nchini Tanzania.Kuna watu wanakubaliana na uamuzi huo wa waandaaji wa tuzo hizo na kuna ambao hawakubaliani wakisema kwamba ni mapema mno kwa Kanumba kupewa “tuzo ya heshima”.Wewe unasemaje?

Mwingine aliyepewa tuzo ya heshima ni Ngumbagwe Misayo au maarufu kama Thea.Ukitaka kusoma mahojiano tuliyowahi kufanya na Steven Kanumba siku za nyuma,bonyeza hapa.

Photo/A.Mrisho

 

Moja kwa moja kutoka mjini Dar-Es-Salaam, tunafurahi kutangaza siku ya uzinduzi maalumu wa sinema ya Bongoland II. Tarehe ya uzinduzi ni mwezi April 5, 2008 hapa mjini Minnepolis, Minnesota katika ukumbi wa sinema wa Oakstreet Cinema.

Sinema hii ilitengenezwa mwaka jana July pale mjini Dar. Vitongoji maarufu vya mji huo kama Manzese na Magomeni vilitumika katika utengenezaji wa sinema hii. Kusema kweli, hii itakuwa ni hadhi kubwa ya wasanii wa ki-Tanzania maana sinema hii itaonyeshwa katika tamasha mbali mbali za sinema za kimataifa.

Sinema hii ni inamhusu Juma Pondamali ambaye baada ya maisha na malengo yake kutofanikiwa nchini Marekani, aliamua kurudi nyumbani. Lakini visakato alivyovikuta nyumbani vilimshangaza sana na hakuna kitu chochote hapa ulimwenguni ambacho kingemtayarisha kupambana na visakato hivyo.

Jitayarishe kuwaona wacheza sinema wakongwe wa Tanzania kama Mzee Kipara, Bi Chuma Selemani Mzee na Bi Thecla Mjatta. Vile vile pia kuwaona wachezaji chipukizi kutoka mjini Dar-es-salaam.

Msanii mhusika mkuu ni Peter Omari ambaye anacheza kama Juma. Peter, ambaye kwa sasa anishi Mwanza, aliwahi kucheza katika sinema yetu iliyopita iliyoitwa TUSAMEHE.

Habari hii ni kutoka kwa Kibira Films International

 

Pichani ni Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Dr.Rose Asha Migiro(kulia),akiwa na George Clooney(46),mwigiza filamu na mwanaharakati maarufu kutoka Marekani.

George Clooney aliteuliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Ban Ki-Moon hivi karibuni kuwa mjumbe au balozi mpya wa tisa wa amani wa Umoja wa Mataifa (U.N. Messenger of Peace ). Dr.Migiro alimkabidhi George Clooney Cheti Cha Mjumbe wa Amani.

Mwaka huu Clooney amechaguliwa kuwania tuzo maarufu ya Oscar kwa uigizaji wake katika filamu iitwayo Michael Clayton.

 

MWANAMUZIKI nyota wa muziki wa kizazi kipya, Banana Ally Zorro(pichani), baada ya kutesa vilivyo katika anga la muziki hivi karibuni anatarajiwa kuibuka kivingine katika filamu mpya ya ‘Kibongo’ inayokwenda kwa jina la ‘Mr. Handsome’, imefahamika. Habari zaidi bonyeza hapa.

 

With the success of twenty to thirty something artists in Tanzania, it is easy to forget that even before Bongo Flava or YouTube and, even the Internet for that matter – Mzee Kipara was there. When we went to film Bongoland II in Dar, the casting director – Gervas Kasiga told me that he found a perfect old man to play the imam in the movie. He then said – once you hear his voice you will know who he is. And, sure enough, once I heard him I recognized his voice immediately. Mzee Kipara is a veteran actor who worked for Radio Tanzania for many years. He was part of the talented cast that was heard weekly in thrilling radio drama productions.

As a kid growing up in Bukoba, the radio reception was never clear, and so sometimes all we could hear were pieces of an argument between two characters and the unmistakable deep voice of Mzee Kipara in most cases playing an elder, a teacher, or a grandfather. (more…)

 

Baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu hatimaye filamu ya Fake Pastors sasa inaingia mitaani. Kabla hata ya kutoka rasmi filamu hii tayari ilishakuwa gumzo mitaani kutokana na simulizi (hadithi) yenyewe ambayo kwa namna moja au nyingine imegubikwa katika jina la filamu yenyewe.Pichani juu ni cover ya filamu hiyo.

Kuanzia kesho jumatatu DVD’s na VHS’s za filamu hiyo zinapatikana madukani kote nchini Tanzania kwa bei ya Tshs 5,000(rejareja) na Tshs 3,500 kwa bei ya jumla.Filamu hii ni ya takribani masaa mawili na ina subtitles za kiingereza mahususi kabisa kwa wale wasiofahamu Kiswahili ambayo ndio lugha kuu iliyotumika. Wahi kuitazama na kisha utupe mapitio (review) yako.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page