Suma Lee analia.Kwanini? Ni mapenzi. Anasemwa.Wanamsema. Mambo lukuki. Mapenzi yana machozi.Unashangaa? Hujawahi kupenda wewe. Au unachokipenda hujui kama unakipenda.Unaona kwa jicho la kioo cha lami. Ni kama vile unaona dimbwi la maji hivi lakini kumbe sio. Waliosoma Physics bila kukremu wanajua.
Suma Lee katika wimbo huu naamini anarudi kule kwenye upbeat za ki-Hakunaga kitu ambacho naamini ndicho alichokuwa anatakiwa kufanya au kuendelea kukifanya.
Safi hii…isikilize hapa chini
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Weekend inapofika ni muda wa Love Me. Nimeamua kuuweka wimbo huu mwishoni mwa wiki kwa makusudi kwani naamini kila mtu anahitaji mapumziko na kutafakari. Wimbo unaitwa Love Me. Ni kutoka kwa Izzo Bizness akiwa amewashirikisha Shaa na Barnaba.
Izzo aliibuka vyema kwenye anga za muziki na wimbo wa Rizwani ambao ulikuwa ni ujumbe mkali kwenda kwa “wanaopeleka nchi”(you now what I am talking about) .Kwa hiyo kutoka kwenye msimamo ule,kwa wimbo huu ni kwamba Izzo has gone soft kidogo.It’s time for Love. Take A Listen and Enjoy Your Weekend.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Huu hapa ni wimbo mpya kutoka kwa Ben Pol. Unaitwa Jikubali. Kimsingi ujumbe uliopo kwenye wimbo huu ni mzuri. Binadamu unatakiwa kujikubali. Unatakiwa kuwa shabiki namba moja wa wewe mwenyewe. Wengine watakwambia huo ni ubinafsi lakini mimi naamini charity starts at home. Ukijikubali ni rahisi kuwakubali wengine.
Lakini kwa upande wa mpangilio na jinsi Ben Pol alivyoimba….somehow I am not feeling this song as much as I expected. Ben Pol is one of the good singers we have and it is my humble opinion that he should produce tracks that allows him to showcase his talent. On this one Ben…we can walk miles apart. It’s Okay.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Here are the Lyrics
Verse1;
Unaweza kuwa Doctor, unaweza kuwa Star
Unataka kuwa Linah, unaweza kuwa Shaa
Kipaji Mali yako, Elimu Ngao yako
Usiache jambo Kati kwenye maisha yako
Unaweza kuwa Diamond, unaweza kuwa Jay
Unaweza kuwa JB, unaweza kuwa Ray
Mi Nakuasa it’s your time,
Huwezi kuwa chini you’ve got somethin’ special
Unampenda Lady Jay dee unamzimia Zitto
Trust me iko siku utatimiza ndoto yako
You can be a Boss, you can be a Lawyer
You can be the President
You’ll be successful

MAXI LOPEZ FT LINAH-i need you(pozo langu) 
Huu hapa ni mpya kutoka kwa Max Lopez akiwa amemshirikisha Linah. Wimbo unaitwa Pozo Langu. Usikilize hapo chini
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Sijui kama nikisema baada ya kimya cha muda fulani Nakaaya is back nitakuwa nimepatia au nimekosea. Kumbukumbu za haraka hazinijii kwamba mara ya mwisho aliachia single lini. Yote tisa. Kumi ni kwamba Nakaaya yupo tena hewani. Wimbo wake mpya huu hapa. Unaitwa Utu Uzima Dawa.
Yes ukikua na kuelewa kwamba wewe sasa ni mtu mzima na hivyo inabidi ufanye mambo yako kwa kutumia akili zako mwenyewe na sio kwa kutegemea “maisha ya kutengenezewa” basi hiyo ndio dawa. Ndio maisha na ndio utu uzima.
Hii ni production kutoka Fishcrab na Mandugu Digital.Usikilize.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Unapodhani kwamba Diamond amepunguza kasi. Unapodhani kwamba sasa mzigo wa kupamba kurasa za mbele za magazeti ya udaku umemuelemea. Unapodhani kwamba huenda sasa sifa za kupendwa na mashabiki na kinadada zimempanda kichwani.Unapodhani kwamba sasa theme za mapenzi zimemwishia, anasema Hapana.
Huu hapa ni wimbo mpya kutoka kwa Diamond. Unaitwa Mapenzi Basi. Ni kutoka AM Records chini ya Maneke. Listen
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
The year 2012/2013 has been a tough one for Lord Eyez. He sat in a jail chamber. Got roughened up in the street. His image tarnished. Accused of stealing. It must have been a tough time.
But even with all hurdles and struggles he never forgot one thing. He is Lord Eyez because he is an artist. He belongs in the studios and on stages performing. So from his most anticipated Sanaa Album to drop later this year, here is the single Mapito. This track is a production of John Mahundi in collaboration with Bongo Records.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Katika maandiko matakatifu ya dini ya kikristo yaani Biblia, mke mwema ameongelewa vizuri katika Mithali 31. Pale “Mke Mwema” ameelezewa aweje na vitu gani vinaweza kumtambulisha.
Ukweli ni kwamba tunaishi katika dunia tofauti. Zama walizoishi babu zetu tumeshazipoteza. Tumepoteza mila na hata miiko. Bahati nzuri ni kwamba hatujafika. Bado tupo safarini. Yawezekana kumpata “Mke Mwema”.
Nimeikumbuka mistari ya Mithali 31 niliposikiliza wimbo mpya kutoka kwa Black Rhino akimshirikisha Soprano ambao umepewa jina Mke Mwema. Pengine haina uhusiano lakini kwa sababu moja au nyingine nimekumbuka Mke Mwema.
On a side note: Huu naamini ni mojawapo ya nyimbo nzuri zaidi kutoka kwa Black Rhino ambaye mwaka jana alifunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi, Beatrice. Well done Rhino. Usikilize hapa.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
This is a new joint from ABACUS EP, called “So Harder” featuring Albino Fulani, One Incredible & Godzilla. The Song was Produced by Duke Tachez of Mlab Records. This song features very diverse artists and it is a collaborative work that includes Tanzanian artists who live abroad (Wakazi, Albino Fulani) and those from right here in Bongo (One, Godzilla). The purpose was not competition but rather making the best music possible, and It will serve as a good way to integrate and bring different fanbases together, and also promote unity among artists.
ABACUS EP will be droppin at the end of the Month, and will feature songs like “Abacus”, “Taking over the Game” and “Tayari Kwa Yote”.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Folllow the artists on twitter @Wakazi @Albinofulani @King_Zilla @DukeTachez
Huu hapa ni mpya kutoka kwa Timbulo. Unakwenda kwa jina Sina Makosa. Sikiliza
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.




sending...





















