MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Kama mimi na wewe tunashabihiana kifikra, basi ulikuwa unatamani siku hii ifike.Siku ambayo angalau kwa muda mfupi,utapumzika kusikia kwamba kila production mpya ya Bongo Fleva, inakuwa imeelemea kwenye hadithi na visa kuhusu mapenzi.Sio kusema kwamba hadithi na visa vya mapenzi havina nafasi yake katika sanaa,La.Ni kuonyesha tu kwamba jamii ni pana na kuna mengi zaidi ambayo sanaa inaweza kuyagusia.

Aliyesikia kilio hicho ni Heavy-weight MC,Prof.Jay.Wimbo unaitwa Msilie akiwa amemshirikisha mkali mwingine wa hip hop nchini Tanzania,Chid Benz.Wimbo umetengenezwa na producer ambaye amekuja juu kwa sana.Ni Lamar kutoka Fish Crab Records.

Mambo kadhaa yamenifanya niusikilize wimbo huu siku nzima.Kikubwa ni ujumbe uliomo ndani yake.Kama ambavyo ungetarajia kutoka kwa Prof.kwa kina anaangalia yale yanayojiri katika jamii.Anatoa hoja,anafafanua,anaelekeza.Msikilize;

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Nimewahi kusema siku za nyuma kwamba mojawapo ya mambo ambayo nayapenda hapa BC ni kupata nafasi ya kumtambulisha msanii katika jamii ya watembeleaji,wachangiaji na washirika wa BC.

Leo ninayo furaha kumtambulisha Patrick Newman,mtanzania, msanii wa muziki wa Gospel ambaye makazi yake ni pale Seattle,Washington nchini Marekani.

Kimsingi Patrick sio mgeni katika anga za muziki.Kwa muda sasa amekuwa akifanya kazi zake nchini Marekani.Amewahi pia kufanya maonyesho kadhaa nchini Tanzania na hivi sasa anajiandaa kufyatua album yake.

Huu hapa ni wimbo wake unaoitwa Siku ya Kifo.Bila kujali dini yako wala kabila,ni wimbo wenye ujumbe mzuri sana.Je ukifa hivi leo marafiki zako watasemaje? Watasema mazuri yepi na mabaya yepi?Usikilize.Well done Patrick.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Zaidi unaweza kutembelea blog ya Patrick kwa kubonyeza hapa.

Siku chache zijazo,tarehe 25 mwezi huu kwa uhakika,Fareed Kubanda au maarufu kama Fid Q anatarajia kuiweka sokoni albamu yake mpya ambayo ameipa jina Propaganda.

Hivi karibuni ametoa single moja kama utambulisho wa kitachokuwepo katika album hiyo. Single inakwenda kwa jina la Danger akiwa amemshirikisha J-Bryant.Usikilize kwa kubonyeza player hapo chini.Usikilize kwa makini.Sikiliza midundo,hisia,ujumbe uliomo na kisha sema usikike.Kwa ufupi ninachoweza kusema ni kwamba kuna utofauti…

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Yapo majina ya wasanii wa kizazi kipya ambao ukisikia wameshirikiana(collaborate)kutengeneza kazi fulani, basi unakuwa na imani kubwa kwamba kazi hiyo ina nafasi kubwa ya kuwa nzuri. Hiyo inatokana na uzoefu na pia zingatio za kazi zao zilizopita,nafasi waliyonayo katika uwanja mpana wa sanaa ya muziki na mambo kama hayo.

Hivi karibuni nilipoletewa kazi mpya na kuambiwa kwamba wasanii waliomo katika kazi hiyo ni TID(Top in Dar) na Chid Benz, nilikuwa na uhakika kwamba kazi hiyo itakuwa imesimama.TID na Chid ni miongoni mwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao binafsi nawaheshimu na sioni noma kusema kwamba nazipenda nyingi kati ya kazi zao.Habari nzuri ni kwamba hawakuniangusha katika kazi hii ya hivi karibuni inayokwenda kwa jina Huyu.

Kama zilivyo kazi nyingi za wasanii wetu siku hizi,hii pia ni hadithi ya mapenzi (bado natamani wigo wa yaliyomo(content) za kazi za wasanii upanuke zaidi na kugusa maeneo mengine yanayoizunguka jamii).Kinachoufanya wimbo huu uwe tofauti ni uwezo binafsi wa wasanii husika na hadithi yenyewe.

Kazi hii imepikwa pale Tetemesha Records(kule kule alikoibukia Hussein Machozi) chini ya George Mpanda au maarufu kama Kid Bwoy. Bonyeza player hapo chini usikilize wimbo Huyu.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Nina imani kwamba hujawasahau Wagosi wa Kaya.Naam ni wale wale vijana kutoka Tanga ambao miaka ileee waliingia kwenye anga za muziki kwa kishindo  pale walipohoji “Tanga Kunani Pale”?

Tangu pale Wagosi wa Kaya wakawa wamejikita katika ile aina ya muziki wa kizazi kipya ambao mimi hupenda kuuita “conscious” kwa maana ya kwamba unalenga kwa undani kile kinachoendelea katika jamii.Ukipenda uite “muziki tambuzi”.

Baada ya kuwa kimya kwa miaka kadhaa(hata wao wanakiri katika wimbo huu kwamba walikuwa kimya kwa muda mrefu) wamerudi.Na mara hii wamerudi wakiwa na timing ya aina yake.Wanagusia uchaguzi,siasa na mambo kama hayo. Kama unavyojua,mwaka huu,watanzania watajipanga foleni ili kuchagua tena viongozi.Demokrasia.Wao wanasema ni Maumivu ya Miaka 10!

Wasikilize Wagosi wa Kaya kwa kubonyeza player hapo chini.Sikiliza kwa makini ujumbe kwani kwa maoni yangu,kidogo sauti ya beats ni ya juu kuliko za wanaoghani.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Picha kwa hisani ya outhere.de.

Mpoki ana single mpya.Single ya kwanza.Na yeye ameamua kujaribu “muziki”.Anasema anatest zali kwa sababu anasikia muziki unalipa.Anawaomba watanzania mu-mkaribishe.

Wimbo unaitwa Shangazi.Imetengenezwa ndani ya Fishcrab Studio na Producer Lamar. Kuna maneno ambayo nimeyasikia mtaani.Maneno yenyewe ni kwamba wimbo huu ni kama vile majibu ya wimbo wa Mjomba kutoka kwa Poet Mpoto Mrisho kwani Mjomba mara nyingi mwenzie ni Shangazi.Hebu usikilize hapa chini na kisha uniambie,je kuna uelekeo wowote kwa wimbo huu kuwa majibu kwa mjomba? Maudhui yake yanaonyesha hivyo? All in all, karibu Mpoki.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Ukitaka kusikiliza wimbo wa Mjomba kutoka kwa Mpoto Mrisho bonyeza hapa.

Kama unaijua vizuri historia ya “mapinduzi” ya muziki wa Tanzania ambao leo unabeba zaidi jina la “muziki wa kizazi kipya” au “bongo fleva”,bila shaka jina la Kolumba Mwingira unalijua fika. Huyu ni miongoni mwa wale wasanii wa mwanzo mwanzo kabisa kuamua kwamba inawezekana tukaimba nyimbo zetu wenyewe,kwa lugha yetu na tukakubalika.Vijana wakakusanyana na kuunda kundi la Mawingu ambalo mara moja lilianza kujipatia umaarufu.

Sasa baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu(binafsi nilidhani ameamua kuachana kabisa na muziki) Kolumba Mwingira ameamua kurudi tena. Hivi karibuni,chini ya Producer Akili Lusungu a.k.a Mtaalam,kutokea jijini Ohio nchini Marekani,amekuja na Single yake inayokwenda kwa jina Usiondoke.Ndio unayoisikia hapo chini.Yupo studio ili kukamilisha album inayotarajiwa kutoka mwaka huu.

Lakini je unakumbuka pia jinsi Kolumba alivyokuwa hodari katika mpira wa kikapu?Ilikuwaje akaachana na kikapu?Na anasemaje kuhusu kuamua kurudi tena katika muziki?Amekuwa wapi muda wote huu?Stay tuned kwa interview yangu na Kolumba ambayo itakujia hivi karibuni.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video


SAJNA-PIC-4BC

Mojawapo ya mambo ambayo huwa nayapenda katika uendeshaji mzima wa BC ni pamoja na kumtambulisha msanii mpya,nyimbo mpya,makundi ya wasanii nk.Binafsi naamini sana katika sanaa kama njia mojawapo muafaka kabisa katika kufikisha ujumbe kwa jamii na hivyo kuwa chachu katika kuleta maendeleo ya kijamii,kisiasa na hata kiuchumi.

Tizama kwa mfano elimu inayotolewa kwa njia ya maigizo,nyimbo au enzi zile kupitia ngonjera(nasikia siku hizi ngonjera hakuna tena mashuleni,ni ushamba eti!).Mpaka leo nikikumbuka kisa cha sungura kukatazwa kutumia maji ya kisimani,nakumbuka kuhusu wajibu wa kuwajibika na kushirikiana!Si unakumbuka enzi za kina Mahoka?Naam hiyo ndio kazi ya sanaa.

Lakini pamoja na kuwa kioo cha jamii,sio mara nyingi ukakuta msanii akifanya kazi zake kutokana na matukio ya kweli katika maisha yake na akawa wazi kwamba anachokifanya kinatokana na uzoefu binafsi wa maisha yake.Wengi tumeumbwa ili kuwanyooshea tu vidole wenzetu.Yule kafanya vile,huyu kasema vile na mambo kama hayo.

Msanii mpya kutoka jijini Mwanza anayekwenda kwa jina la Sajna(pichani)yeye ni miongoni mwa wachache.Anakuja kwa kishindo na kisa cha kweli. Sajna ambaye ana umri wa miaka 18 tu huku bado akiwa shuleni(form II),amekuja na wimbo unaoitwa NADHIFA. Wimbo huu ni true story ambayo imemtokea yeye mwenyewe. Kila alichokiimba katika wimbo huu ni cha kweli na kinamhusu yeye na familia yake. Kwa ufupi amemuimba dada yake wa damu ambaye alitoweka nyumbani kwao bila taarifa miaka kadhaa iliyopita.Wimbo umetengenezwa na producer Sam Timber.Msikilize na mkaribishe Sajna.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.



Jacquiline Ntuyabaliwe aka K-Lynn

Jacquiline Ntuyabaliwe aka K-Lynn

For many years music making in Tanzania has been “coin” oriented practice. A coin In a sense that it is only two sides that are involved to ensure the material reaches the audience. The artist has to compose, write and get in the booth and sing while correcting herself. The producer has to produce the instruments, record, mix and master. This being done for couple of tracks, one is bound to meet some terrible music along the way.  Because, no shoulder could handle such huge burden, without compromising its quality of deliverance.

K’Lynne in her comeback she decided to walk the most feared path by many Tanzanian artists, twice. She decided to use foreign language even though she is aware that she might lose her local fans, but she is up for that because she is now focused to represent our music out of our borders. She broke another rule by letting another person write her idea. Tanzanian artist usually consider singing someone else’s words is a sign of weak artistic skills, but she did not care for as long she makes a good music to bring massive impact.

This track has an urban context, a mixture of hip-hop and R n B, easy to penetrate Europe and America market.  All English, with little Swahili to identify her origin. It is about a very pretty woman with a massive sex appeal to the extent it makes every male she looks at, feel like she is flirting (giving sexual signals) with them and this makes his boyfriend very jealous, but it is not her fault it is just her looks.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

CREDITS:

Song: Not A Flirt

Artist: K-Lynne Ft. Hermy B

Created By K-Lynne

Written and Composed By Amani Joachim

Additional Background Vocals By: Amani Joachim

Produced, Recorded and Mix 1 By Pancho Latino at B’Hits Studios- Dar es Salaam

Mix 2 and Mastered By Hermy B at B’Hits Studios Dar es Salaam

Z

Tunapoelekea kuufunga mwaka 2009,yaelekea AY ameamua kwamba mwaka haushi bila kuonyesha kule anapojaribu kuelekea kisanii. Utakumbuka kwamba AY mwaka huu aliteuliwa kuwania tuzo za MTV Africa Music Awards na ndiye mwanamuziki ambaye amekuwa akipewa sifa na moyo zaidi kutoka kwa wasanii wengine wa kimataifa kama vile K9,Wyclef Jean,Akon na wengineo.

Safari hii anakuja na wimbo ambao ameuita Bed and Breakfast. Ni mchanganyiko kabambe wa Raga na Hip Hop. Wimbo umefanyika katika studio za B.Hitz Music Group chini ya Producer Hermy B huku mastering ikifanyika katika studio ya Ogopa Deejays ya nchini Kenya.

AY anasema video ya wimbo huu itafanyika mwezi huu ndani ya jiji la Johannesburg nchini South Africa chini ya kampuni ya Film Online ambayo ni miongoni mwa kampuni bora kabisa barani Africa katika utengenezaji wa videoz na mambo kama hayo.Miongoni mwa kazi walizowahi kuzifanya jamaa wa Film Online ni pamoja na Video Bora ya Mwaka ya MTV 2009 ya msanii S.A HHP.

Nilipoongea na AY hivi karibuni alinidokezea kwamba nia yake hivi sasa ni kuhakikisha kwamba Tanzania na wasanii wa kitanzania wanajikita na kuleta ushindani wa dhati katika soko la kimataifa la muziki na burudani kwa kwenda sambamba na wasanii wengine wanaofanya vizuri barani Africa kama vile kutoka nchi za South Africa,Nigeria etc.

Ukisikiliza wimbo wa Bed and Breakfast utagundua kwamba kuna kiitikio cha mwanadada fulani.Kwa bahati mbaya,mwanadada huyo hapendi kupewa credit zake kwa sababu zake binafsi.Kwa maana hiyo hatotajwa kwa sasa….labda baadaye. Pata burudani,sikiliza Bed and Breakfast.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.



Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page