Mwishoni mwa wiki iliyopita alifanya uzinduzi rasmi wa nyimbo hii.Huyu sio mwingine bali ni Barnaba,msanii ambaye yupo ameketi na ametulia kabisa katika orodha ya waimbaji ambao naamini kabisa kwamba wanaweza kuimba katika steji yoyote duniani na kuamsha hisia za mashabiki.He can sing!

Wimbo aliozindua pale Club Billicanas unaitwa Gube Gube.Sijajua bado kwa hakika nini maana ya neno hili.Ntamtafuta Barnaba nizungumze naye kuhusu undani wa wimbo huu katika siku za usoni.Lakini kwa haraka haraka nilipochungulia Kamusi ya Kiswahili niliyonayo inasema Gube au aghalabu Magube ni Hila au Ujanja Ujanja…Unaweza kusema Fanya Magube ukamaanisha fanya ujanja ujanja.Anyway,usikilize wimbo huu hapa chini. Hii ni production ya Tudd Thomas na Mosse Kinanda.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Wakati huo huo tunayo furaha kumtambulisha Ally Nipeshe,huyu ni msanii mpya ambaye bila kwere anaonekana kuwa na kipaji kizuri cha kuimba.Hapa anakuja na wimbo wake unaokwenda kwa jina Ntalila.Hii pia ni production ya Tudd Thomas na Mosse Kinanda.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Mwezi wa kwanza wa mwaka 2012 ndio huo tumeshaanza kuuwashia indicator.Upo ukingoni.Wakati tukihesabu siku,kwenye tasnia ya Bongo Fleva,tayari wasanii kadhaa wameshaanza kuachia ngoma zao ambazo itakapofika Desemba mwaka huu,zitakamilisha orodha ya nyimbo zilizotoka mwaka huu.

Leo hapa tunao wimbo kutoka kwa Godzilla,msanii ambaye ana style inafanana kwa karibu na 50….(malizia mwenyewe kama unaafikiana nami).Hapa anakuja na wimbo Milele akiwa amemshirikisha Ally Kiba.Milele ni production nyingine kutoka pale MJ Records chini ya Marco Chali(wenyewe siku hizi wanapenda kumuita Dr.Chali). Usikilize hapo chini

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

 

Bila shaka jina la Ali Kiba hivi sasa lipo miongoni mwa top performing artists kutoka Tanzania. Mbali ya kutoa show kali kali,Kiba amekuwa akitoa vibao ambavyo vinatokea kupendwa na kukubalika sana.Unaweza kuiita ngekewa au bahati lakini ndivyo ilivyo.Inasemekana ndiye msanii ambaye ameshafanya tour za nje ya Tanzania kuliko msanii mwingine yeyote.Anaitwa Ali Kiba,yule tule wa Dushelele,Mac Muga,Cinderella,Nakshi Nakshi,Mapenzi yana-run dunia na zinginezo nyingi.

 

Sasa alipokuwa katika tour yake ya Europe mwaka jana alipita katika studio za See Records zilizopo nchini Italy katika jiji la Napoli ambapo alikutana na Producer anayekwenda kwa jina la Alasko(raia wa Benin anayeishi nchini Italy). Wakaketi studio na kutengeneza kitu ambacho utakisikia punde.Wimbo unaitwa Mi Nimo…kuna maneno yanasema “Mi Nimo Najikongoja taratibu ndani ya hili shimo”…

 

Studio ya See Records,ambayo inatarajiwa kufungua tawi lake jijini Dar-es-salaam kuanzia mwezi Machi mwaka huu, imeshawahi kufanya kazi na wasanii wengine wengi kama vile Diamond,Hussein Machozi na pia imeshatengeneza videos za wasanii kama vile Asley Ft Mh.Temba,Tip Top Connection,Miaka 50 Mkubwa na wanae,Ramso Ft Godzilla nk.

 

Usikilize wimbo Mi Nimo kwa kubonyeza player hapo chini

 

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

 


Wimbo huu nimeupokea siku kadhaa zilizopita.Muda wa kuusikiliza kwa makini nao ukawa haba.Mambo ya mwanzo wa mwaka,kurudi kazini,watoto kurudi shuleni(gharama zake sasa!).Duh,elimu imekuwa bidhaa ya ghali sana.Sijui nichague elimu mtaani?

Lakini kingine kilichonifanya “niskute” kidogo(niskute neno la zamani hili kiasi,enzi hizo) ni mabadiliko yaliyopo katika wimbo na msanii huyu.Ni kweli kwamba huyu ni Ferouz,yule yule alipitia enzi za kundi maarufu la Daz Nundaz.Ni kipaji au kujaribu soko.Ni kuingia au kutoka.Ni risk.Good or bad.Inategemea na maoni yako wewe msikilizaji.

Msikilize Ferouz katika wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina Majoto ukiwa katika style ya mchiriku,maarufu kutoka jijini Dar na pembezoni aka Pwani.Nini maoni yako?Kaelekea kuliko au kachemsha?

 

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

- Song – Majoto
- Artist – Ferouz
- Producer – Pancho Latino
- Studio – B Hit’z

Black Rhino au Black Chata,bila shaka bado walikumbuka na kulitambua jina hilo.Nimeanza kwa kusema kwamba bila shaka walikumbuka kwa sababu kwa muda kiasi Black Rhino au jina halisi Nicholaus Haule alikuwa kimya kidogo katika masuala ya muziki.Mwenyewe anasema maisha ilibidi ayaelekezee kwingine kidogo.Akaenda chuoni na kupata wakti wa kuvaa lile joho(la shule ya wakubwa na sio chekechea) na kisha baada ya hapo akaanza “mzigo” kama watu wengine. Kukaa kwake kimya kukatafsiriwa na watu wengine kwamba ndio amekacha muziki au muziki umemkacha.Hapana! He is back and doing what he knows best;good music. Na mara hii,pamoja na elimu aliyonayo,bila shaka hata soko la muziki atakuwa analiangalia tofauti. Juu ya yote,Black Rhino anathibitisha kwamba ukitoka kwenye familia ya muziki,basi muziki kamwe haukuachi na wewe huna jinsi bali kwenda nao sambasamba.Majina mengine kutoka katika familia yake ni kama vile The Heavy Weight MC,Professor Jay,Kolihombi,Simple X na Mr.Teacher.

Wimbo unaitwa Taking Ova.Umetengenezwa pale Dhahabu Records chini ya Producer anayekuja juu sana anayekwenda kwa jina Mbezi.Sikiliza Taking Ova hapa chini;

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

 

Jina la wimbo huu mpya kutoka kwa Diamond linaweza kukushtua kidogo hususani kama wewe ni mfuatiliaji wa habari za kwenye luninga,magazetini na bila shaka kwenye blogs na social networks zingine ambako mengi hujiri siku hizi! Ila kama hufuatilii basi ntakupa kiduchu…Diamond ni mpenzi wa Wema Sepetu.At least hivyo ndivyo inavyojulikana miongoni mwa wengi kupitia “live” screens za magazetini nk.Sasa wiki hii kumekuwepo na dodoso lukuki kwamba Diamond hayupo tena na Wema na kahamishia mahaba yake kwa Jokate Mwegelo,mlimbwende,mshehereshaji na pia fashion designer.Aliyetoa “siri” ni Wema Sepetu mwenyewe kupitia kipindi cha Zamaradi cha Take One pale Clouds TV.

Wakati yote hayo yanajiri,wimbo mpya wa Diamond unaingia sokoni.Unaitwa NIMPENDE NANI?Ni kutoka katika album aliyoiingiza sokoni hivi karibuni inayokwenda kwa jina Lala Salama. A coincidence? Kali zaidi ni maneno yaliyopo katika wimbo huu.In case unajiuliza ulitungwa lini,ninachoweza kukwambia ni kwamba ulitungwa muda mrefu.Sasa iweje uwe kama vile unaendana na matukio ya sasa,go figure out!Usikilize

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Mwanzoni alimsihi “Ridhiwani” aongee na mshua.Naamini wawili hao wahusika walishafanya mazungumzo na huenda matokeo tutayaona soon.Lakini wakati bado Ridhiwani akiwa anaongea na mshua,Izzo Bizness,anakuja tena na kitu Barua.Hii ni barua kwenda kwa wanasiasa na viongozi kwa ujumla.

Wimbo umetengenezwa pale Fishcrab Records chini ya Lamar.Usikilize

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Endapo tutasema Professor Jay amerudi tena au hata tuiweke kwa kimombo kwamba Professor Jay is back ili kuonyesha msisitizo,bila shaka tutakuwa tunakosea.Nasema hivyo kwa imani moja nyepesi kabisa; Professor Jay alikuwepo,yupo na hakuna ubishi kwamba ataendelea kuwepo.

Hii ni kutokana na jinsi ambavyo kwa muda mrefu Professor Jay(jina kamili Joseph Leonard Haule) amekuwa akifanya kama kupotea hivi  kabla hajaibuka upya kama sio kivingine kabisa kama ambavyo amefanya katika wimbo ambao nina furaha kuutambulisha kwako hivi leo.

Wimbo unaitwa Kamili Gado,ambalo ni neno la kimtaa kidogo lenye kumaanisha kitu au mtu aliyeko kamili katika mengi. Huu ni wimbo wa pili rasmi kutoka katika album yake mpya inayokwenda kwa jina Jaysco ambayo kwa mujibu wake,maandalizi  kabambe ya kuiweka uwanjani yanaendelea.

Katika wimbo huu ambao umetengenezwa pale MJ Records(Masaki jijini Dar-es-salaam),Professor Jay amemshirikisha Producer wa wimbo huo,Marco Chali.  Usikilize wimbo KamiliGado kwa kubonyeza player hapo chini na kisha tembelea tovuti maalumu ya wimbo huu,www.kamiligado.com kwa ajili ya kudownload wimbo wenyewe,Instrumental na Acapella.Kumbuka tu kwamba hiyo yote ni kwa ajili ya Promotions tu na sio matumizi mengineyo.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Kutoka pande za Temeke,Wanaume TMK wanaingiza karata yao.Wimbo unaitwa “Kichwa Kinauma“. Umetengenezwa pale Masaki kwa MJ Records chini ya Producer Marco Chali(Doctor Chali).

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Sina uhakika unaisomea wapi habari hii lakini nahisi unaisomea ukiwa katika mitkasi yako ya kila siku iwe ni kazini au katika sehemu zinginezo za kutafutia riziki.Kwa ufupi unafanya kitu! Lakini je,umeshawahi kuketi chini na kujiuliza kwa undani kabisa kwamba kwanini unafanya unachokifanya? Nini kinakusukuma kufanya hivyo?Unapohisi kukata tamaa na kitu unachokifanya,kwanini unaendelea?

Maudhui kama hayo hapo juu ndio yaliyomo katika wimbo mpya wa Mike Tee(Mnyalu) ambao amemshirikisha Fareed Kubanda au ukipenda Fid Q. Wimbo unazungumzia zaidi sanaa ya muziki.Ni wangapi wanafanya muziki kwa sababu wanapenda au wengi wanafanya kwa “Sababu Ya Njaa”?Msikilize kwa makini Mike Tee hapa.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Photo Courtesy:Get Mziki

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page