
Machupa ni mfungaji hodari. Usemi huo pekee unatosha kumuelezea Athuman Iddi Machupa (pichani) mshambuliaji kijana ambaye kwa upande wa Tanzania, aliwika zaidi alipokuwa akichezea timu ya soka ya Simba maarufu kama “Watoto wa Msimbazi”.
Hivi leo Machupa anasakata kabumbu nchini Sweden akiwa na timu ya Vasalund IF.
Niliwasiliana na Machupa hivi karibuni na kumuuliza maswali machache. Haya hapa mahojiano yetu;
BC: Mpaka sasa mambo yanakwendaje hapo Sweden?Unachezea timu gani na ipo daraja la ngapi?
Machupa: Kwa upande wangu hapa Sweden maisha yanakwenda poa kaka.Ninachezea timu inayoitwa Vasalund IF ilikuwa katika ligi ya Superettan (ligi ya pili kwa ukubwa hapa Sweden) lakini kwa bahati mbaya tumeshuka daraja hadi la kwanza..
BC: Umeshakaa Sweden kwa muda wa kutosha sasa.Unapaonaje na zaidi unaonaje nafasi za kuendeleza soka lako?
Machupa: Kwa sasa kaka napeleka mwaka hapa na kwa upande wangu mi naona maisha ni mazuri na hata nafasi ya kusonga mbele kwangu ni kubwa mno.Nazidisha bidii katika kila kitu na inshallah nitafanikiwa zaidi na zaidi.
BC: Kama mgeni katika nchi ya watu,ni mambo gani ambayo ilibidi ukabiliane nayo kwanza? Hapa nazungumzia mambo kama vile lugha,vyakula nk
Machupa: Of coz lugha kaka ni ngumu. Lakini nashukuru jamaa wamenishughulikia masuala yote ya muhimu ikiwa ni pamoja sehemu ya kujifunza lugha yao.Na kuhusu chakula; kwa kusema ukweli ni kizuri tu. Hakina tofauti sana na cha nyumbani Tanzania kwa sababu najipikia mwenyewe chakula ninachojisikia kula.Hali ya hewa nayo ilikuwa changamoto lakini taratibu ninazoea.
“Hebu ngoja nicheki kama vitu vishaiva”
BC: Una ujumbe gani kwa vijana wengine wanaosakata soka nyumbani Tanzania?
Machupa: Ujumbe wangu kwa vijana wanaosakata soka na hususani waliopo nyumbani ni kwamba waheshimu soka kwani soka ni kazi kama zilivyo kazi zingine zozote.Ukiheshimu soka hakika utafanikiwa.
BC: Mwakani ni mwaka wa kombe la dunia.Safari hii kipute kipo Africa.Nini matarajio yako kwa nchi za Afrika?
Machupa: Ni changamoto kubwa kwa timu za Africa ambazo zimefanikiwa kuingia katika finali hizo. Tusubiri tuone kwa sababu nina uhakika watajiandaa vizuri. Nina uhakika hatutosikia madai ya posho. Nina imani watatuwakilisha vyema kabisa,sina wasiwasi na hilo. Ila nahisi Ghana watafanya vizuri. Nawa-support.
Machupa akiwa mazoezini na timu yake.Anaonekana kulia katika picha akijaribu kutuliza mpira chini.
BC: Una lolote la kuongeza kwa mashabiki wako?
Machupa: Mashabiki ndio kila kitu.Nawapenda na ninawaheshimu sana na hakika bila wao hatuwezi songa kwa sababu wao ndio wanaotukosoa pale tunapokosea.I love all my fans popote walipo.

Kombe la Dunia lipo ziarani nchini Tanzania. Ziara hiyo imezinduliwa rasmi leo jioni nchini Tanzania na Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Ziara ya kombe hilo katika sehemu mbalimbali duniani, ni ishara ya kuwapa fursa mashabiki mbalimbali wa soka ulimwenguni,nafasi ya kuliona kombe hilo “live” na hata kupiga nalo picha kwa kumbukumbu nk. Hizo zote ni miongoni mwa shughuli mbalimbali kuelekea South Africa 2010.
Wakati nikimuangalia Rais Kikwete akiwa amejawa na tabasamu wakati akilinyanyua kombe hilo na kulibusu,nilijiuliza, hivi itakuja tokea kweli siku moja Rais wa Tanzania(yeyote yule atakayekuwa madarakani) kulinyanyua Kombe la Dunia baada ya kulipokea toka mikononi mwa nahodha wa Taifa Stars baada ya kulitwaa?
Well…naamini kila kitu kinawezekana. Sina tu uhakika kama tuna mipango madhubuti(ya mbali au karibu) ya kutimiza ndoto hizo.Tusiishie tu kuliona kombe kwa mbali au kulinyanyua pale tusipostahili.
Picha/Yahya Charahani

Hivi karibuni,tajiri bilionea mmiliki wa timu maarufu ya soka ya Chelsea FC ya nchini Uingereza, Roman Abramovich, alitinga nchini Tanzania na akiwa na nia ya kutalii na kuupanda mlima mrefu kupita yote barani Afrika yaani Mlima Kilimanjaro.
Safari ya Bilionea Abramovich kuja kupanda Mlima Kilimanjaro ilikuwa ni habari kubwa iliyoripotiwa na vyombo lukuki vya habari hususani nchini Tanzania na Uingereza.Kilichoifanya habari hiyo kuwa kubwa hakutokani tu na ukweli kwamba Abramovich ni miongoni mwa watu matajiri sana ulimwenguni bali pia ni ule uhusiano uliopo miongoni mwa mchezo wa soka ulimwenguni huku mashabiki wa timu ya Chelsea anayoimiliki Abramovich ya Chelsea ikiwa na mashabiki kibao ulimwenguni wakiwemo pia wale wanaoishi na kuitazama timu hiyo kutokea Tanzania.
Ingawa Roman Abramovich hakufika kileleni, ni wazi kwamba,kwa namna moja au nyingine,amesaidia kuinua soko la utalii la Tanzania na hususani upandaji wa Mlima Kilimanjaro.
Lakini ni nani aliyemuongoza njia Roman Abramovich? Kuna wadadisi wameuliza swali hili na tuna furahi kwamba jibu lake tumelipata. Aliyekuwa guide wa Roman na rafiki zake anaitwa Isaac Kitindi(pichani juu ndiye anayeonekana kushoto akiwa na Roman.
Isaac ni Mhitimu wa Advanced Diploma katika masuala ya Wildlife Management kutoka Chuo cha Elimu na Utawala wa Wanyamapori cha Mweka kilichopo Moshi,Kilimanjaro. Isaac alikuja Tanzania maalumu kwa shughuli ya kumsindikiza Roman Abramovich mlimani kwani hivi sasa anasomea masuala ya Huduma ya Kwanza (First Aid Training) katika chuo kikuu maarufu cha Havard nchini Marekani.
Isaac Kitindi ambaye wenzake hupenda kumuita Mountain Madness kutokana na umahiri wake wa kuupanda Mlima Kilimanjaro hivi sasa yupo njiani kurejea Havard huku kukiwa na habari kwamba atapitia nchini Uingereza ambapo ataonana tena na Roman Abramovich kwa mazungumzo ya kuileta Tanzania timu ya Chelsea FC hapo mwakani.
Ukitaka kujua ilikuwaje mpaka Roman Abramovich akashindwa kufika kileleni,bonyeza hapa.

Mshambuliaji hatari wa timu ya soka ya Yanga, Mrisho Ngassa hapo jana alijipatia “jiko”. Amemuoa Latifah Abdulhaman. Ndoa ilifungiwa huko Tabata Kisiwani.
Hivi karibuni Ngassa alikuwa nchini Uingereza kufanya majaribio ya kuchezea timu ya West Ham. Habari zinapasha kwamba sehemu ya kwanza ya majaribio hayo ilikwenda vizuri na kwamba kunako majaaliwa Ngassa atarejea tena nchini Uingereza kwa majaribio mengine.
BC inawatakia Mr.& Mrs Ngassa kila la kheri katika ndoa yao.
Photo/Michael Jamson via Charaz

Tuende mbele turudi nyuma,ukipata nafasi ya kuchezea Yanga au Simba basi suala la umaarufu au u-celebrity halina mjadala sana.Wapo watu lukuki ambao watalijua jina lako,wataitambua sura yako na ukiwa mitaani watapenda kupiga japo stori kidogo na wewe.Ndio maana zinapokuja habari kwamba ama Yanga au Simba wametwaa ubingwa nchini,basi hiyo huwa ni habari kubwa iwe mtaani au kwenye vyombo vya habari.Mpaka hivi leo mchezo wa Yanga na Simba huwa ni gumzo kubwa mtaani.
Kwa bahati nzuri au mbaya,safari hii ni Yanga tena.Yanga wameutwaa ubingwa wa ligi ya soka nchini Tanzania kabla hata ya ligi hiyo kumalizika.Kwa maana hiyo wanastahili pongezi.
Lakini ubingwa wa soka nchini Tanzania,umaarufu,pesa nk vinakuwa na raha yake kama angalau vitakumbuka walipolala na kuamkia mashabiki wao.Tumekuwa tukiona jinsi ambavyo wanamichezo katika nchi zilizoendelea wanajitolea kwa namna mbalimbali ili kuboresha jamii zilizowazunguka na pia mashabiki wao.Wengi wanajitolea kwa namna mbalimbali kama vile kujitolea muda wao,pesa zao,ujuzi wao .Kama sio hivyo, basi wamekuwa wakijitolea katika aidha kuhamasisha michango ya hiari,kujitegemea,kujiamini miongoni mwa vijana nk.
Nchini Marekani kuna kitu kinaitwa NBA Gives Back.Hawa ni wachezaji wa ligi ya mpira wa kikapu ya Marekani ya Kaskazini waki-toa chochote wanachoweza au walichopata kwa jamii zao,kwa mashabiki wao.Wachezaji wenye majina nchini Tanzania,wanaweza kuiga hili.Wadhamini wa ligi hiyo,Vodacom,wanaweza kuhamasisha hili kwa kuwatumia wachezaji wa ligi ya soka Tanzania.Shirikisho la Soka nchini linaweza kusimamia au kuongoza harakati kama hizo.
Tusiishie kwenye kufurahia tu Ubingwa bila kukumbuka walikolalia au kuamkia mamilioni ya mashabiki wa soka nchini.Lakini mbali ya yote,BC inatoa Hongera kwa Yanga!

Blog ya Yahya Charahani inaripoti kwamba timu ya Cameroon ikiongozana na nyota wake Samuel Eto’o(pichani) wametua jijini Dar tayari kuvaana na Taifa Stars jumamosi.Tuwatakie Kheri Taifa Stars maana bila hivyo inaweza kuwa balaa tupu.

Kwa wale wapenzi wa habari za michezo na burudani zikiwemo habari motomoto kuhusiana na ligi maarufu ulimwenguni kama vile Premier League, La Liga, Serie A na nyinginezo kijiji kipya kiitwacho Spoti na Starehe kimeanzishwa ili kukupa uhondo wa aina yake. Unaweza kukitembelea kwa kubonyeza hapa.Kazi kwenu.

Kwa mpenzi yeyote wa soka nchini Tanzania,jina Ismail Aden Rage (pichani) sio geni.Jina hili ni miongoni mwa yale majina ambayo yamekuwa yakisikika katika medani za ulimwengu wa soka nchini Tanzania kwa muda sasa hususani tangu enzi akiwa Katibu Mkuu wa wa kilichokuwa Chama Cha Soka Tanzania(FAT),sasa TFF na baadaye Makamu wa Pili wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Jina la Rage lilizidi kutawala vinywa vya wapenzi wa michezo nchini Tanzania, hususani soka, baada ya kushitakiwa kwa kosa la wizi wa mali na fedha za FAT kesi ambayo ilipelekea kupewa kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia za makosa hayo.Hata hivyo, alikata rufaa kupinga kifungo hicho na kabla ya rufaa hiyo kusikilizwa, Desemba 2005, alitoka kwa msamaha wa Rais.
Kufuatia hali hiyo Rage alibaki nje ya TFF kupigania rufaa yake na Alhamisi wiki iliyopita, jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa wakiongozwa na Damian Lubuva, walimfutia makosa yaliyokuwa yamemtia hatiani Rage.Hivi sasa Rage ni Mkurugenzi wa timu ya Moro United.
Sasa hivi majuzi klabu 12 kati ya 14 za Ligi Kuu Tanzania Bara zimetaka aliyekuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ismail Aden Rage, kurejea katika wadhifa wake.Unaweza kuisoma habari hiyo kwa kubonyeza hapa.Nini maoni yako?Je Rage arejee TFF?

Pichani ni kikosi cha kwanza cha Timu ya Soka ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars ambacho jioni hii kimetupwa nje ya Mashindano ya kugombea Kombe la Challenge kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati baada ya kufungwa magoli 2-1 na Timu ya Taifa ya Sudan. Kili Stars imetolewa katika hatua ya robo fainali katika mashindano hayo yanayoendelea katika vituo vya Dar-es-salaam na Arusha.
Majina ya wachezaji hao wa Kilimanjaro Stars ambo wote kwa pamoja ni “celebrities” wakubwa katika michezo (soka) ni kama ifuatavyo. Walio mstari wa mbele toka kushoto, Dani Mrwanda,Amir Mafta,Ali Mustafa ‘Bartez’,Uhuru Suleiman na Nizar Khalfan.
Mstari wa nyuma toka Kulia-Salum Swedi, Shaban Nditi,Michael Chuma,Erasto Nyoni,Meshack Abel na Castory Mumbara.
Safari ya soka la bongo bado inaelekea kuwa ndefu.
Picha kwa hisani ya Issa Michuzi.

Ingawa watanzania wengi wanaendelea kuwa washabiki wa kutupwa wa timu mbalimbali zilizoko kwenye ligi kuu ya Uingereza(Premier League), nchini Tanzania msisimko fulani kwenye medani ya soka unarejea kwa kasi.
Siku hizi “utaifa” unaanza kurudi.Ukisikia Timu ya Taifa inacheza,basi kila mtanzania husubiria matokeo kwa hamu.Wapo wanaoenda viwanjani kuiunga mkono timu ya taifa na wapo wanaoishia mitaani kule vijiweni kwenye ule ubishi wa kufa mtu.
Msisimko huo mpya ndio unaomfanya Kocha wa Timu ya Soka ya Taifa,Taifa Stars,Mbrazili Marcio Maximo Barcellos(pichani) kuwa mmojawapo kati ya watu mashuhuri nchini Tanzania hivi sasa. Maximo ambaye aliwahi kuwa mmoja wa wakufunzi wa timu ya taifa ya Brazili kwa vijana chini ya miaka 17 na pia chini ya miaka 20, aliwahi pia kufundisha timu ya Livingston Football Club ya nchini Scotland (daraja la kwanza) katika msimu wa 2003/2004. Akiwa na timu hizo za vijana za Brazili aliwahi kuwafundisha wachezaji nyota wa Brazili wanaotamba hivi sasa kama Ronaldo (AC Milan) na Ronaldinho(Barcelona). Aliwahi pia kuwa mkufunzi huko Cayman Islands.
Kuhusu wapi atalipeleka soka la bongo ni suala la kusubiri na kuona. Pamoja na hayo wapo wanaosema,dalili njema zimeanza kuonekana na hivyo wanawasihi watanzania wampe muda.Unaweza pia kuitembelea tovuti ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ili kujua mengi kuhusu soka la bongo kwa kubonyeza hapa.
Picha kwa hisani ya Mroki.

