Posti hii nilitakiwa kuipandisha jana lakini sikufanikiwa maana jana nilifunga kiroho na kifikra ili kumkumbuka Malcom X, mpigania haki za watu weusi kule Marikani. Malcom X alizaliwa na kupewa jina la Malcom Little kisha akaamua kubadili “Little” na kuweka “X” kwa kile alichodai kuwa jina la awali lilikuwa ni la kikoloni na lenye nia ya kuiba utu wake. “X” inasimama kama “Aliyepotea/Asiye na Jina” ikimaanisha Mwafrika aliyepoteza utambulisho wake baada ya kutekwa na kupelekwa utumwani kule Marikani.
Nimeona niweke posti hii ili tuelewe kwamba isingekuwa Malcom X na wengine waliotangulia kama Martin Luther King Jr., Mama Rosa Parks, au mapambano ya kuwakomboa watumwa ya Reli ya Ardhini” (Undeground Railroad) yaliyoongozwa na mwanamke mweusi Harieth Turbman, pengine Marekani ya leo isingekuwa na Rais Mweusi tunayemfahamu na kumshabikia, Barack Obama.
Malcom X alizaliwa katika familia yenye maisha duni na akiwa na umri wa miaka 13, baba yake ambaye alikuwa mpigania haki za watu weusi pia aliuawa na wazungu wabaguzi waliojulikana kama Ku Klux Klan (KKK), na mama yake alikuwa amefungiwa katika hospitali ya wagonjwa wa akili. Hivyo Malcom akaanza maisha ya kujitegemea akitumia wizi wa mifukoni kama njia ya kujipatia kipato.
Mwaka 1946 Malcom alifungwa jela kutokana na wizi. Akiwa Jela, Malcom ambaye hakuwahi kusoma vitabu akajikuta akiwa msomaji mkubwa wa vitabu ambavyo vilimwongezea maarifa aliyokuja kuyatumia baadae katika mapambano dhidi ya ubaguzi wa watu weupe kwa watu weusi. (more…)

Miezi saba baadaye,aliyekuwa daktari wa Mfalme wa Muziki wa Pop ulimwenguni,Michael Jackson, Dr.Conrad Murray ameshtakiwa rasmi kwa kifo cha mwanamuziki huyo maarufu ambaye katika maisha yake,aligusa wengi.Michael Jackson alifariki dunia tarehe 25 June mwaka jana akiwa na umri wa miaka 50.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, Dr.Murray ambaye alifikishwa mahakamani mchana huu huko Los Angeles,amekana shtaka lake na ameachiwa kwa dhamana ya dola 75,000. Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa tena tarehe 5 April.
Ndugu wa Michael Jackson,kaka zake Jermaine,Tito,Jackie na Randy ,dada yake LaToya na wazazi wake Joe na Katherine walikuwepo mahakamani kusikiliza kesi hiyo.
Hapo kabla Dr.Conrad Murray ambaye ni mzaliwa wa nchini Grenada,alikiri kwa polisi kwamba alimchoma Michael Jackson sindano ya dawa aina ya Anaesthetic Propofol kwa dhumuni la kumsaidia bingwa huyo wa Pop kulala.Alisema aliporudi tena chumbani alimkuta Michael akiwa hapumui.
Mchunguzi wa vifo wa Los Angeles alithibitisha baadaye kwamba dawa hizo ndizo zilizosababisha kifo cha Michael Jackson. Dr.Murray alikuwa ameajiriwa maalum kwa ajili ya kumuandaa Michael Jackson katika tour iliyokuwa ijulikane kama This Is It ambayo ilikuwa ianzie nchini Uingereza.
Unapoongelea sinema,hakuna ubishi kwamba majadiliano yako inabidi yaanzie Hollywood.Na unapokuwa Hollywood na kuamua kuanzisha mjadala wa Tuzo(awards) basi yakupasa uanzie kwenye tuzo maarufu za Academy au Oscars.
Muda mchache uliopita majina ya sinema,waigizaji,waongoza sinema na vipengele vingine walioteuliwa kuwania tuzo hizo kwa mwaka huu yametangazwa. Kama ambavyo ilitarajiwa, sinema ya Avatar iliyoongozwa na James Cameron pamoja na sinema ya The Hurt Locker ambayo imeongozwa na Kathryn Bigelow(mke wa zamani wa James Cameron) ndio zimepata teuzi nyingi zaidi katika kuwania tuzo hizo maarufu ambazo zinafanyika kwa mara ya 82 (miaka 82). Movie hizo zimeteuliwa mara 9 au katika vipengele 9.
Shughuli za mwaka huu za tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika tarehe 7 Mwezi Machi(takribani siku 33 zijazo).Zitaonyeshwa moja kwa moja(live) kupitia kituo cha televisheni cha ABC cha nchini Marekani.
Kwa orodha kamili ya Oscar Nominations kwa mwaka huu,bonyeza hapa. Je kuna movie,actor au actress ambaye ulitarajia angeteuliwa kuwania tuzo za mwaka huu ambaye hajatokea katika orodha?
Hatimaye Mfalme wa Pop,Michael Jackson,anatarajiwa kuzikwa leo huko Forest Lawn-Glendale,California katika makaburi yajulikanayo kama Holly Terrace.Mazishi yanatarajiwa kuanza saa moja usiku kwa saa za California.
Kwa mujibu wa taarifa kuhusu mazishi hayo,yatakuwa ni mazishi “private” na hivyo ni ndugu,jamaa na marafiki wa karibu pekee watakaoweza kuhudhuria.
Mazishi haya yanafuatia mlolongo wa matukio tangu alipofariki mwanamuziki huyo ikiwemo uchunguzi wa kipolisi kuhusiana na kifo chake na pia kupingana kwa ndugu na wanafamilia yake kuhusiana na swala la wapi azikwe. Mengine yaliyoibuka tangu afariki dunia ni pamoja na habari za matumizi mabaya ya madawa ya kutuliza maumivu na kulaza aliyokuwa nayo Michael Jackson.
Hivi karibuni Mchunguzi wa vifo wa California,alithibitisha kwamba Michael Jackson alifariki dunia kutokana na kuchomwa sindano ya kupunguza maumivu ambayo ilikuwa na dozi kubwa kuliko kawaida. Daktari aliyekuwa naye siku hiyo,Dr.Murray, ndiye anatupiwa lawama zote ingawa mpaka leo hakuna mashtaka rasmi kuhusiana na kifo cha mwanamuziki huyo.
Pumzika Salama Michael.
TAMKO LA MUUNGANO WA ASASI ZA KIRAIA (FemAct) NA MITANDAO YA WAFUGAJIKUHUSU KUKIUKWA KWA HAKI ZA BINADAMU NA HAKI ZA RAIA KATIKA WILAYA YA NGORONGORO KWA MASLAHI YA MWEKEZAJI; KAMPUNI YA ORTELLO BUSINESS CORPORATION (OBC)
Sisi Muungano wa Asasi za Kiraia zinazotetea Usawa wa jinsia, haki za binadamu na maendeleo na ukombozi wa wanawake kimapinduzi (FemAct) kwa pamoja na Mitandao ya Wafugaji mkoa wa Arusha tumeguswa na kusikitishwa na vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu, haki za raia na uvujaji wa sheria katika kutekeleza oparesheni ya kuhamisha wafugaji wakaazi wa jamii za Kimaasai unaoendelea katika wilaya ya Ngorongoro, Tarafa ya Loliondo inayofanywa na vyombo vya dola kwa maslahi ya mwekezaji kutoka Uarabuni, Kampuni ya Ortello Business Corporation (OBC).
Baada ya taarifa za kushitua za watendaji wa serikali kukiuka haki za binadamu dhidi ya jamii za kimasaai kutangazwa katika vyombo vya habari kadhaa ndani na nje ya nchini, FemAct na Mitandao ya Wafugaji, tuliamua kufuatilia kwa karibu ili kubaini usahihi wa taarifa hizo. Kati ya Agosti 19 na 23 2009, viongozi wa mashirika wanachama wa FemAct walifanya ziara maalum katika vijiji vya Ololosokwan, Soitsambu, Olorien – Magaiduru na Arash, pamoja na kutembelea kambi ya Oterloo Business Corporation (OBC) na uongozi wa wilaya ya Ngorongoro kwa lengo la kubaini na kuthibitisha kiwango na namna watendaji wa serikali wanavyoshirikiana na mwekezaji wa OBC kunyanyasa na kutesa raia wakaazi wa vijiji vilivyotajwa hapo juu. (more…)
Takribani mwezi mmoja sasa umetimia tangu Mfalme wa Pop,Michael Jackson, afariki dunia na kuwaacha mashabiki waliokuwa wakimsubiri awape burudani katika concerts zilizokuwa zimepewa jina la This is It. Mfululizo wa concerts hizo ulikuwa uanzie huko nchini Uingereza.
Mpaka ninavyoandika habari hii,Michael Jackson hajazikwa bado. Kulikuwa na taarifa kwamba angezikwa kesho( angekuwa hai angetimiza miaka 51) lakini mpango huo ukaahirishwa kutokana na kile ambacho kimeelezewa kuwa “kutoelewana au kukubaliana rasmi” miongoni mwa wanafamilia kuhusu wapi azikwe na kwanini azikwe siku fulani. Mpango uliopo hivi sasa ni kumzika tarehe 3 September huko Forest Lawn Memorial Park, Glendale, California.
Wakati hayo yote yakiendelea,jana imetolewa taarifa ya kushtusha. Inasemekana Michael alipewa dozi kubwa ya dawa za maumivu za Propofol(dawa hatari hizi).
Kwa maana hiyo polisi wa California wamekiita kifo chake kuwa homicide kwa maana ya kwamba alifariki dunia kufuatia kitendo cha mtu mwingine kilichosababisha mauti imfike. Anayelaumiwa au kunyooshewa kidole zaidi ni Daktari wake, Conrad Murray, ambaye ndie inasemekana alimpa hizo dawa na pia alikuwa naye mpaka dakika za mwisho.Uchunguzi bado unaendelea na polisi hawajasema rasmi ni nani wanaelekea kumfungulia mashtaka ya kuua bila kukusudia.
Je Michael Jackson aliuawa na Dr.Murray? Je hakujiua mwenyewe huyu kwa kutumia madawa ambayo bila shaka alikuwa anajua madhara yake?Nani alaumiwe?
Leo ni mwanzo wa mwezi mtukufu.Ni mwezi wa mfungo na toba hususani kwa wale wanaofuata dini ya kiislamu.
Ingawa mwezi mtukufu ni maalumu au mahsusi zaidi kwa waislamu,ni wakati mzuri pia kwa wengine wote kutafakari mambo mbalimbali ya kimaisha na ubinadamu.Ni wakati wa kusameheana,kutakiana kheri na kusaidiana.Ni wakati wa kutafakari na kufuata yale yote yaliyofundishwa na kusisitizwa na Mtume Mohamed ambayo kimsingi ni suala zima la ubinadamu,kupendana na kuvumiliana.
Napenda kuchukua nafasi hii kuwatakieni nyote mtakaokuwa kwenye mfungo na toba katika mwezi huu.Nawatakieni Ramadhan njema.

Jarida maarufu la Forbes limetoa orodha yake ya The Most Powerful Women in the World. Miongoni mwa wanawake hao,yumo Michelle Obama ambaye hii ndio mara yake ya kwanza kuingia katika orodha hiyo. Je unajua nani ameshika namba moja? Je unaweza kuhisi ni wanawake wangapi kutoka barani Afrika wamo katika orodha hiyo? Bonyeza hapa ujionee.
ALIYEKUWA mwanafunzi mzee kuliko wote duniani, Kimani Maruge amefariki Ijumaa wiki hii, katika hospitali ya Nairobi alipokuwa akipata matibabu ya kansa.
Maruge( 84), alifanya tukio la kihistoria pale alipoamua kujiunga na shule ya msingi Kapkenduiywo iliyopo Mashariki mwa Kenya, mwaka 2004 kufuatia kuanzishwa kwa utaratibu wa elimu bila malipo , ulianza rasmi mwaka 2003 chini ya chama cha Narc.
Katika enzi za uhai wake, Maruge alikuwa na malengo ya kuwa Daktari mwenye umri mkubwa. Mwaka 2008, alikuwa mmoja kati ya maelfu ya watu walioshindwa kurejea masomoni kutokana na vurugu za uchaguzi zilizotokea nchini humo,nyumba pamoja na mali zake ziliharibiwa vibaya na wapinzani.
Eneo la Langas Estate, ambapo ndipo alikuwa akiishi kuliathiriwa vibaya na vurugu hizo, iliripotiwa kuwa jumla ya watu 11 waliuawa nyumba ya pili kutoka kwake Disemba 30,2008. Maruge alifanikiwa kutoroka kutoka Eldoret hadi Nairobi kutokana na kutokuwepo na hali ya usalama huko nyumbani kwake.
Shirika la msalaba mwekundu nchini humo walimtafutia makazi katika nyumba ya wazee inayofahamika kama Chesire iliyopo jijini Nairobi. Muda mchache baada ya kuishi Nairobi aligunduliwa kuwa na kansa ya utumbo.
Maruge, ambaye ameweka rekodi katika kitabu cha Guinness ya kuwa mwanafunzi mwenye umri mkubwa zaidi kujiunga na elimu ya msingi.
Rekodi hiyo alichaguliwa kushika nafasi hiyo akiwa darasa la tano mwaka 2007, ambapo katika mtihani wake wa mwisho wa mwaka alishika nafasi ya 14 kati ya wanafunzi 58 waliofanya mtihani huo.
Akiwa shuleni hapo alisema taaluma aliyoipata imemsaidia sana kuongeza uelewa kwani hadi wakati huo aliweza kusoma vizuri biblia.Somo la Kiswahili ndio lilikuwa chaguo lake.
Jane Obinchu ambaye alikuwa ni mwalimu wake ni miongoni mwa watu waliotoa salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu Maruge.
Habari hii imeandikwa na Peter Ng’etch na imepatikana kupitia Mwananchi. Kwa habari zaidi kumhusu Mzee Marige unaweza kubonyeza hapa.

Leo ni Birthday ya Barack H.Obama. Obama alizaliwa tarehe 4 August 1961(mwaka wa Uhuru wa Tanganyika) huko Honolulu,Hawaii nchini Marekani.BC inaungana na wengine kumtakia Barack siku njema ya kumbukumbu ya kuzaliwa.Happy Birthday Mr.President.

