Yanga wakifurahia mojawapo ya magoli kutoka katika mechi hiyo. Picha kwa hisani ya Bin Zubeiry Blog
Timu ya soka ya Yanga, jioni hii imewadhihirishia mashabiki wao ...
Takribani miaka 11 imepita tangu Eve alipotoa album yake ya mwisho. Habari njema ni kwamba sasa amerejea tena katika ulingo. Album yake ambayo imeshatoka inaitwa ...
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Mama Maria Nyerere, Naibu Waziri wa Afya Dr. Seif Rashid wakipozi na wakuu wa mikoa ...
Wapo wasanii ambao bado hawana majina makubwa.Hawa wanahitaji support yako hususani kwa wale ambao wana kipaji.Mfano mzuri ni huyu.Anaitwa Baridi.Single yake ambayo aliitoa mwaka jana ...
Bondia Floyd Mayweather Jr, ndiye mwanamichezo mwenye kipato kikubwa zaidi miongoni mwa wanamichezo katika aina mbalimbali za michezo nchini Marekani au Marekani ya Kaskazini kwa ...
Upo msemo wa Kiswahili unaosema "Mafahali wawili wapiganapo,ziumiazo ni nyasi". Kama kuna ukweli wowote kwenye msemo huo, basi ni dhahiri kwamba wanapombana Yanga na Simba, ...
Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo na Meneja Masoko wa Kampuni hiyo Furaha Samalu katika hatua za mwisho za maandalizi kabla ya kuwasili kwa ...
Sijui...lakini nadhani sijawahi kumsikia Diamond akiongelea mahusiano yake na wanawake mbalimbali ukiwemo uhusiano wake na Wema Sepetu ambao mara kwa mara umekuwa lulu ya magazeti ...
Ndani ya wiki mbili zijazo wapenzi wa vipindi au matukio mbalimbali yanajojiri kwenye luninga barani Africa watakuwa na kila sababu ya kuwa “busy” Msimu mpya ...
Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) limempongeza bondia maarufu wa kitanzania Francis Cheka kwa juhudi zake za kuwa bondia mzuri mwenye viwango vya kimataifa katika uzito wa Super Middleweight.
Francis Cheka aliweza kutetea mkanda wake wa IBF Africa uzito wa Super Middle baada ya kumshinda kwa KO bondia Thomas Mashali aka“Simba asiyefugika” tarehe 1 Mei, 2013 katika ukumbi wa PTA jijini Dar Es Salaam.
IBF inachukua fursa ya kumpongeza Francis Cheka baada ya ushindi huo ambao umedhihirisha kuwa yeye kweli ni bingwa wa bara la Afrika. Francis Cheka atarudiana na bondia wa Malawi Chimwemwe Chiotcha mwezi wa Agusti katika mpambano la kutetea mkanda wake.
Mpambano wao wa marudiano utafanyika katika jiji la Blantyre nchini Malawi na tayari majadiliano ya mpambano huo yanaendelea vizuri. Kampuni ya “Mawenzi Boxing Promotion” ya nchini Malawi chini ya bwana Stephen Mawezni ndiyoitakayoandaa mpambano huo.
Pambano hili linakuja baada ya wadau kadhaa wa ngumi kuomba mabondia hao warudiane walipoonyesha ujuzi mkubwa na ushindani katika mpambano wao Desemba 26 mwaka jana katika uwanja wa Sheikh Amri Abeidi jijini Arusha siku ya Boxing Day.
Baada ya mpambano huo, IBF itampatia Francis Cheka nafasi ya kugombea mkanda wa IBF wa Kimataifa (IBF International Super Middleweight) na mabondia wa Ulaya au Marekani. Hii ni kudhihirisha kuwa Francis Cheka hana tena mpinzanai nchini Tanzania na kumpambanisha na mabondia wa kitanzania ni kumpotezea muda na uwezekano wake wa kutengeneza jina na pesa.
Wakati huo huo bondia Thomas Mashali bado ni bingwa wa Afrika ya Mashariki na Kati (ECAPBF) katika uzito wa Middle kwani mkanda wake haukuwa kati ya mikanda iliyogombewa kwenye mpambano uliomalizika Mei mosi.
MABINGWA wa Afrika, Zambia ‘Chipolopolo’ wanatarajiwa kupimana nguvu na Timu ya Taifa Ya Soka Tanzania,Taifa Stars, katika mchezo wa kirafiki unaotarajiwa kufanyika Jumamosi hii tarehe 22 jijini Dar-es-salaam.
Timu hiyo ya Zambia, ikiwa chini ya nahodha Christopher Katongo ambaye hivi karibuni amepata Tuzo ya Shirika La Habari La Uingereza,BBC ya Mchezaji Bora wa Afrika, tayari wamewasili jijini Dar-es-salaam wakiwa na kikosi cha watu 32 wakiwemo wachezaji 24.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 7,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP C, sh. 20,000 kwa VIP B wakati VIP A itakuwa sh. 30,000.
Tiketi zinatarajiwa kuanza kuuzwa siku moja kabla ya mechi katika vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Uwanja wa Uhuru, Mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Sokoni Kariakoo, kituo cha mafuta cha Ubungo OilCom na Dar Live Mbagala.
Pia tiketi zitauzwa Ijumaa (Desemba 21 mwaka huu) kwenye tamasha la Kilimanjaro Premium Lager kuhamasisha washabiki wa Taifa Stars litakalofanyika kwenye viwanja vya Sigara, Chang’ombe.
Mashabiki wa Simba, leo wamemtembezea kichapo mama mmoja aliyekuwa amevalia jezi ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars yenye nembo ya Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), kosa kukaa kwenye jukwaa walilokuwa wamekaa wao.
Sasa haikuweza kufahamika mara moja, mashabiki wa Simba wana bifu na TFF au hawapendi timu ya taifa. Mama huyo alikimbizwa huku akipewa kichapo hadi kutokwa damu, kabla ya kuokolewa na Polisi waliomteremsha jukwaani. Aliporwa vitu vyake kama pochi na kadhalika.
Baadaye akiwa amekwishaokolewa na askari, ndipo msamaria mwema mmoja, albino akamuokotea baadhi ya vitu na kuwakabidhi askari. Huwezi kulipa jina lingine tukio lile, zaidi ya udhalilishaji wa kijinsia. Alikuwa anatia huruma mama huyo wakati anahangaika kujitoa kwenye kundi la mashabiki wa kiuma wa Simba, iliyofungwa 3-1 na Azam leo katika Robo Fainali ya Kombe la Kagame.
Picha na Habari Kwa Hisani ya Bin Zubery wa BongoStaz.Blog
Wachezaji wa Simba (Wabunge) wakishangilia ushindi baada ya kuwafunga watani wao wa Yanga (Wabunge) kwa penalti 3-2.
Yanga baada ya kipigo hicho.
Hivi ndivyo hali ilivyokuwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mtanange wa watani wa jadi Simba na Yanga (Wabunge) wakati wa TAMASHA LA MATUMAINI ambapo wabunge wapenzi wa timu ya Simba wameibuka kidedea kwa penalti 3-2. Simba wamefunga penalti 3 wakati Yanga wakifunga 2.
Inaeleweka kwamba mwaka jana Simba walisumbua sana vijana wa Jangwani kiasi hata cha kusababisha Jangwani kuelekea kuparang’anyika kabisa.Sasa mwaka huu Yanga inaaminika wamerudi kwa nia moja tu;kurudisha heshima yao.Je,watakuwa moto wa kuotea mbali au la?
Baada ya kuukosa mwaka jana kwa Dallas Mavericks,hatimaye ndoto ya Miami Heat wakiongozwa na “big three” wao hapo juu, LeBron James, Chris Bosh na Dwayne Wade, imetimia.Usiku huu(alfajiri ya tarehe 22 June kwa saa za Afrika Mashariki),imefanikiwa kunyakua ubingwa wa Ligi ya Mpira wa Kikapu(NBA) nchini Marekani,kwa kuwafunga timu ya Oklahoma City Thunders kwa jumla ya vikapu 121-106 na hivyo kuwatoa Thunders kwa jumla ya michezo 4-1 katika mzunguko wa mechi 7 ambao huwekwa ili kumpata mshindi katika NBA Finals.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen leo (Mei 14 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 25 kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia hatua ya makundi Kanda ya Afrika dhidi ya Ivory Coast.
Akitangaza kikosi hicho ambacho kitaingia kambini kesho kutwa (Mei 16 mwaka huu, Kim amesema uteuzi wake umezingatia uwezo wa mchezaji uwanjani, nafasi anayocheza na ubora wake.
Wachezaji walioitwa ni makipa; Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ally (Azam) na Deogratius Munishi (Mtibwa Sugar). Mabeki ni Nassor Masoud Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Simba), Waziri Salum (Azam), Shomari Kapombe (Simba) na Juma Nyoso (Simba).
Viungo ni Mwinyi Kazimoto (Simba), Salum Abubakar (Azam), Nurdin Bakari (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Edward Christopher (Simba- U20), Mrisho Ngasa (Azam) na Frank Domayo (JKT Ruvu- U20).
Washambuliaji ni Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Ramadhan Singano (Simba-U20), Simon Msuva (Moro United- U20), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Haruna Moshi (Simba) na John Bocco (Azam).
Stars inayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro itacheza mechi ya kirafiki nyumbani Mei 26 mwaka huu dhidi ya Malawi kabla kuivaa Ivory Coast ugenini Juni 2 mwaka huu jijini Abidjan.
Mchezaji wa timu ya Manchester City mwenye makeke na ukorofi unaokera mara nyingine,Mario Balotteli amefungiwa na Chama cha Soka Uingereza kucheza mechi nne baada ya kumpiga/kumchezea faulo mchezaji wa Tottenham, Scot Parker.
Uamuzi huo umefikiwa baada ya mwamuzi wa mchezo kurudia mkanda wa mchezo huo.. Mmoja wa viongozi wa Man City amesema bado hawajakutana ili kuzungumzia suala hlo na kuangalia namna ya kukata rufaa.
Hii ni kwa mujibu wa Gazeti la The Sun la Uingereza
Mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Cameroon,Samuel Eto’o ambaye hivi sasa anachezea timu ya Anzhi Makhachkala ya huko Urusi amesema hana tena mpango wa kuhamia kwingine na kwa maana hiyo atamalizia career yake katika medani ya soka akiwa na timu hiyo.
Samuel Eto’o ,kapteni wa Timu ya Taifa ya Cameroon,mchezaji anayelipwa mshahara mnono kushinda wote duniani na ambaye sasa ana umri wa miaka 30 anasema, ” Nina furaha kucheza hapa Anzhi na nimejipanga kushinda kitu kikubwa nikiwa na timu hii.Labda kwenye Ligi ya Mabingwa kama tukiwa na bahati ya kutosha.Natumaini kucheza kama miaka mitano au sita zaidi nikiwa hapa kabla sijatundika viatu vyangu”
Habari hii ni kwa mujibu wa shirika la habari la NFP