
Je,unamtambua aliyepo pichani?
Dokezo:Ndiye msanii kutoka nchini Tanzania ambaye alijulikana na kusifika sana ulimwenguni kote ilhali nchini Tanzania,watu waliomfahamu,kuthamini kazi zake ni wachache sana ukilinganisha na mataifa ya nje hususani yale ya Ulaya.

Pichani ni Dr.Willbroad Peter Slaa akihutubia mamia ya wananchi waliokwenda kumsikiliza hivi karibuni mjini Arusha.
Hivi karibuni Dr.Slaa alitangazwa kuwa mgombea wa kiti cha Urais kwa kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) ambacho kwa muda sasa amekitumikia kama Katibu wake Mkuu.
Tangu ilipotangazwa kwamba Dr.Slaa sio tena candidate wa Ubunge bali Urais,kumekuwa na maoni tofauti tofauti.Kuna ambao wanasema Dr.Slaa asingethubutu kugombea Urais na badala yake angeendelea tu kugombea kiti chake cha Ubunge wa Karatu kwani nafasi ya kumshinda mgombea wa Chama Cha Mapinduzi-Jakaya Mrisho Kikwete ni ndogo sana.
Wanaounga mkono hoja hiyo wanasema,kwa sababu uwezekano wa Dr.Slaa kumshinda Kikwete ni mdogo,hiyo ina maana kule Bungeni kutakuwa kumepungukiwa na mbunge makini na ambaye kwa muda wa miaka mitano iliyopita,aliwapa tabu na challenge kubwa,wabunge na viongozi wa chama tawala cha CCM.
Kwa upande mwingine,wale wanaounga mkono uamuzi wa CHADEMA kumsimamisha Dr.Slaa katika kuwania Urais,wanasema ni kitu kizuri kwa ukuaji wa demokrasia na wanaamini kwamba Dr.Slaa atamshinda Jakaya Mrisho Kikwete na kwa maana hiyo he will become our next President.
Tungependa kupata maoni yako.Je,unakubaliana na wale wa kundi la kwanza au la pili? Will Dr.Slaa become our next President?
BC iliwahi kufanya naye mahojiano ya kina na Dr.Slaa.Unaweza kuyasoma mahojiano hayo kwa kubonyeza hapa.

Wanasema picha moja ni sawa sawa na maneno elfu moja(1,000).Unaona nini katika picha hii?Is there anything wrong with this picture?

Katika siku chache zijazo,nitafanya mahojiano na msanii wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul maarufu kama Diamond.
Je una swali au maswali ambayo ungependa niyajumuishe katika maswali yangu kwa msanii huyo ambaye mapema mwaka huu alibeba Tuzo 3 za Kilimanjaro (Kilimanjaro Music Awards).
Unaweza kutuma swali au maswali yako kupitia bongocelebrity at gmail dot com au info at bongocelebrity dot com. Asante.
Burudika kidogo na wimbo wake Kamwambie

Unaweza kusema alikuwa na mchango gani katika ukuzaji wa Muziki wa Dansi nchini Tanzania?

Bila shaka viongozi hao wawili katika picha hawahitaji utambulisho wa ziada. Kuna mtu kaniuliza swali lililopo katika kichwa cha habari hii. Je unaweza kunisaidia na kumsaidia aliyeuliza swali? Kama jibu lako ni Ndiyo,misimamo yao ilifanana kivipi?Kama jibu ni hapana,kivipi haikufanana?

Leo timu yetu ya taifa ya soka(Taifa Stars) ilikuwa inaumana na timu ya taifa ya Brazil katika mchezo ambao umeishia kwa Taifa Stars kufungwa 5-1.Nasikitika kwamba tumefungwa! Unacheka nini sasa? Lazima nisikitike hata kama nilitarajia.
Kufungwa ni kama kupoteza kitu au mtu.Hata kama ulijua, inauma.Sina uhakika kama vijana wetu wa Taifa Stars wamejifunza chochote au kama lengo la ‘kuitangaza nchi” limefanikiwa kwani uwanja ulifurika matangazo ambayo sikuyaelewa elewa hivi.Au yalikuwa ya Brazil yale?Pia sikuona juhudi za ziada za “kuitangaza nchi”.We can do better.Maoni yangu.
Eti ni kweli kwamba ujio wa Brazil ulikuwa na ncha za kisiasa? Nasikia kwamba hivi karibuni tutaanza kusikia majukwaa ya kisiasa yakizungumzia ujio huu sambamba na maendeleo ya kiuchumi. Mmmh…siamini.Ngoja nisubiri. Anyway,kutufungwa wametufunga lakini chenga na sisi tumewala.Kama kawaida,tunafungua ukurasa mwingine.
Kwa upande mwingine,vijana wanaokua hivi leo wanaweza kukata tamaa na “uanamichezo” wa nchi yetu.Wanaweza kuona kwamba alichowahi kukisema Rais mstaafu,Ally H.Mwinyi kwamba sie kama kichwa cha mwendawazimu vile,ni cha kweli tangu zama zile mpaka kesho. Kila kukicha wanaona tunafungwa.Tukitoka suluhu ni sawa na kushinda.Hawajawahi kumuona Mkuu wa nchi akinyanyua juu kikombe cha ubingwa!
Jibu ni kwamba,Hapana.Zipo zama ambazo Tanzania ilikuwa na wanamichezo hodari waliosifika na kufanikiwa kuitangaza nchi kwa mapana na marefu hapa ulimwenguni. Zipo enzi zile ambapo tuliwahi kucheza hata Fainali za Ubingwa wa Afrika.Enzi zile…
Mfano mzuri ni huyo aliyepo pichani. Je unamtambua? Yuko wapi hivi sasa na alitamba zaidi wakati gani katika mashindano yaliyofanyikia wapi? “Wazee” wenzangu mnaweza kuwakumbusha vijana?

Kuna mtu kaniuliza swali ambalo sikuweza kuwa na jibu lake.Sasa kama unavyojua,BC ina watu.Watu kama wewe.Ninapokuwa sina jibu la swali au maswali,naomba msaada kutoka kwako.Ndio raha ya kuzungukwa na jamii.Penye wengi hapaharibiki neno. Mwenzetu kauliza;
Eti ni kweli Irene Uwoya na Jacquiline Wolper wanafanana kiasi kwamba wengine kuthubutu kumuita Jacquline kuwa ni pacha wa Irene Uwoya?
Pichani aliyepo kushoto ni Irene Uwoya na kulia ni Jacquiline Wolper.Wewe unasemaje?Wamefanana?

Eti unamtambua huyu jamaa kwenye picha?Ni nani na anajishughulisha na nini?Kwanini umeweza kumtambua?Wewe ni mshabiki au mfuasi?Wa kitu gani?

Historia ya muziki wa kizazi kipya (bongoflava) haiwezi kukamilika pasipo kutaja matukio ya uhasama kati ya baadhi ya wasanii wakongwe wa muziki huo.Pengine neno ‘uhasama’ halileti ladha inayopendwa katika anga za muziki.Kwahiyo ni vema nikatumia neno ‘bifu’,linalotokana na ‘beef’ ambayo slang ya Kiingereza cha Wamarekani Weusi,na ina maana hiyohiyo ya uhasama.
Bila shaka wafuatiliaji wa bongoflava wanakumbuka bifu kati ya Juma Nature na Inspekta Haroun,na ile ya wasanii wa East Coast Team na wale wa maeneo ya Temeke.Japo sifahamu vizuri historia ya bifu hizo mbili lakini kwa hakika zilivuta hisia za wapenzi wengi wa bongoflava.
Mwandishi mmoja wa gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza aliwahi kuandika kuwa ‘vituko katika fani ya muziki wa hip-hop na rap ni miongoni mwa chembechembe muhimu kwa mafanikio ya msanii wa muziki huo’.Alitaja vituko hivyo kuwa ni pamoja na bifu.Iwapo bifu zinasaidia uhai wa hip-hop na rap au zinadidimiza, mie sina jibu bali kwa namna moja au nyingine zimewasaidia baadhi ya wasanii kufanya vizuri katika mauzo ya albamu zao.
Mfano wa hivi karibuni ni bifu kati ya msanii Rick Ross na 50 Cent.Inaaminika kuwa mauzo mazuri ya albamu ya Rick Ross inayofahamika kama ‘Deeper Than Rap‘ yalichangiwa zaidi na bifu lake na 50 Cent.Lakini kama hiyo ni kweli,kwanini basi mauzo ya albamu ya 50 Cent ya ‘Before I Self Destruct‘ hayakuwa mazuri sana?
Tukiangalia nyuma zaidi, kuna imani miongoni mwa baadhi ya wapenzi wa hip-hop na rap kwamba bifu kati ya wasanii marehemu Tupac Shakur na Notorious B.I.G ilisaidia sana umaarufu wa wasanii hao. Lakini sote tunajua hatma ya bifu hilo ambapo vifo vya wasanii hao vinahusishwa na bifu lao.
Hata hivyo,kama kweli bifu zinasaidia maendeleo ya wasanii,kwanini basi marapa kama Ja Rule na Fat Joe ‘wamepotea’ licha ya bifu lao na 50 Cent huku Benzino akibaki historia baada ya bifu lake na Eminem?Au ili bifu lizae matunda ‘yanayokusudiwa’ sharti wahusika ‘waimudu’(kama Rick Ross alivyoweza ‘kustahimili’ bifu lake na 50 Cent)?Lakini kama suala ni ‘kumudu bifu’ mbona Jadakiss ameweza ‘kusimama vizuri’ hata baada ya ‘kupatana’ na 50 Cent? (more…)

