MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Mradi wa Zinduka.Nia ni kutokomeza malaria.Kila mtu analiunga mkono akiwemo Mheshimiwa Rais.Kumbe chini yake kuna mvutano.Mwanamuziki Sugu(Mr.II) ana kampuni yake.Inaitwa Deiwaka.Kwa upande mwingine kuna mfanyabiashara maarufu.Anaitwa Ruge Mutahaba.Anasaidia kuinua vipaji vya wasanii kupitia Tanzania House Of Talent(THT).Mpaka sasa wasanii kibao wameshainua vipaji vyao kupitia kwake. Kuna shirika la Malaria No More kutoka nchini Marekani.Mradi wa Zinduka ni wa nani?

Kama umechanganyikiwa na jinsi nilivyoandika hapo juu,pengine ni kwa sababu kitu chenyewe kinanichanganya hata mimi pia.Labda wasikilize wenyewe wahusika;

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Sugu akiongea na waandishi wa habari.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Ruge Mutahaba akijibu mashambulizi ya Sugu

Mimi sio mtaalamu wa Kiswahili.Ukweli huo ndio unanifanya niwe tayari kujifunza.Ndio sababu ya kuuliza swali lililopo katika kichwa cha habari hapo juu.Najaribu kujifunza.

Unapowaweka viongozi hao watatu pichani(wote,katika nyakati tofauti,waliwahi kushika wadhifa wa Waziri Mkuu wa Tanzania) ni sahihi kuwaita wote kuwa ni Waziri au Mawaziri wastaafu? Nauliza swali hili zaidi nikiwa nimemlenga Mheshimiwa Edward Lowassa (Mbunge wa Monduli) ambaye kwa mujibu wa kumbukumbu yangu,alijiuzulu wadhifa wa Uwaziri Mkuu mara baada ya sakata la Richmond kumkalia vibaya.Je kujiuzulu kule kunamaanisha kwamba ni sahihi hivi leo kumuita Waziri Mkuu Mstaafu,Edward Lowassa?

Hamis Ramadhan,maarufu kama H-Baba(pichani) yawezekana sio jina geni kwako.Huyu ni miongoni mwa wanamuzuki waliojikita katika mtindo ujulikanao kama TAKEU(Mr.Nice ndiye anasemekana kuwa mwanzilishi wake).

Ambacho unaweza kuwa hukijui ni kuhusu “imani” aliyonayo. Hivi karibuni H-Baba alinukuliwa na chombo kimoja cha habari akisema kwamba amelogwa na mmoja wa wasanii wenzake kitu ambacho anadai ndicho kilichosababisha mambo yake kwenda ‘kombo” katika siku za karibuni.

Kwa masikitiko na upole,H-Baba amenukuliwa akisema “Unajuwa mtu ataniona mimi kama naongopa lakini ukweli ni kuwa nilichezewa ila nilikuwa sijui nimekuja kugundua baada ya kupita pita kwenye tiba.Nilianza kujihisi hivyo mara baada ya kugombana na watu wengi sana nikiwa sijielewi”

H Baba anakiri kwamba hivi sasa ameshapona kutoka katika matatizo yaliyokuwa yakimsumbua baada ya kupata tiba toka kwa wataalamu wa miti shamba.

Bila kumtaja wazi huyo ‘mchawi” wake H-Baba alizidi kusema ” Unajuwa ni ukweli kabisa waswahili hawakukosea walivyosema kikulacho kinguoni mwako, kwani yote hayo yalikuwa yakifanywa na mtu wa karibu kabisa tena rafiki yangu mkubwa”.

Mfano mmojawapo wa matatizo yake,anasema “Matatizo mengi yalitokana na Irene(Uwoya), unajua watu wengi hawakupenda niwe na Irene, kwahiyo ili kunikomoa ikabidi waniroge, mimi na Irene tukawa hatuelewani, tunagombana mpaka tukaachana,”

Je,unaamini kwamba ni kweli yawezekana H-Baba amefanyiwa anachodai kufanyiwa au hii ni “publicity stunt”?

Kila siku huwa napokea hoja,mapendekezo,ushauri kutoka kwenu wasomaji wa BC.Pia huwa napokea maswali mbalimbali.Nikiwa na ufahamu mkubwa juu ya swali lililoulizwa huwa najibu.Ninapokuwa sina jibu,wajibu wangu ni kutafuta jibu ama kwa kuomba msaada kutoka kwenu wasomaji na wachangiaji wa BC au vinginevyo. Leo nimepokea swali ambalo sina jibu kwani swali hili limeelekezwa moja kwa moja kwa celebrities. Mwenzetu mmoja ameuliza swali lililopo hapo chini na mwisho ametoa ombi.

Ningefurahi sana kama angalau celebrity mmoja angejitolea kulijibu. Sio lazima ajibu kama mwakilishi wa celebrities wengine,bali yeye kama mtu binafsi. Asante Allen kwa swali zuri.

Napenda kuwapongeza sana kwa kazi nzuri mnayofanya. Nina swali dogo sana kwa hawa Bongo Celebrity kwamba mbona hatuwaoni wakiwa mstari wa mbele katika kuhakikisha nchi yetu inapunguza au kutokomeza kabisa vifo vya mama na mtoto vinavyotokana na uzazi.

Mwezi wa kumi na mbili mwaka jana tulishuhudia mwana Mitindo mashuhuri nchini Uingereza Naomi Campbel akifanya onyesho la mitindo pale Movenpick kwa ajili ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kupunguza vifo vya mama na mtoto dunia nzima. Wanamuziki wetu, wanamichezo , wanamitindo na hawa wengine tunaowaita Bongo Celebrity wako wapi katika kuhakikisha nchi yao inafikia malengo ya milenia namba 4 na tano ifikao 2015.

Hongera kwa Stara Thomas kwa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha nchi yetu inapunguza vifo vya mama na mtoto kwa kiasi kikubwa. Napenda kuwakumbusha kuwa Tanzania bila vifo vya mama na mtoto inawezekana.

Timu ya taifa ilipocheza na Ivory Cost fedha nyingi sana zilipatikana.
Wachezaji hawa ni matokeo ya kina mama hawa ambao leo wanakufa kutokana na matatizo ya ujauzito. Tunaweza kutumia timu yetu ya taifa kupunguza pia vifo hivi vya mama na mtoto.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni miongoni mwa viongozi wakubwa duniani wanaohakikisha nchi zao zinapunguza vifo vya mama na mtoto.

Nawaombatuungane pamoja kwa kutumia vipaji Mungu alivyotupatia kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa tanzania kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa vipaji vyetu na umaarufu tulio nao katika jamii yetu.

Sheikh Yahya

MTABIRI maarufu wa Afrika Mashariki, Shehe Yahya Hussein ametabiri kuwa Rais Jakaya Kikwete atashinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu ujao na atakayempinga ndani ya chama chake atakufa ghafla.

Sambamba na hilo, atakayeonekana kumshinda nje ya chama chake pia atapoteza maisha vivyo hivyo.

Akitoa utabiri wake jana Dar es Salaam, juu ya uchaguzi mkuu mwakani, Shehe Yahya alisema ushindi wa Rais Kikwete unatokana kurithishwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1995 ilipodaiwa kuwa Rais Kikwete alishinda kwenye kura za maoni lakini akamsihi amwachie Benjamin Mkapa.Kwa undani wa habari hii bonyeza hapa.

Je huu unaweza kuuita “utabiri” au ni…Unakubaliana naye ?Kwanini ?

Pichani juu ni Sheikh Yahya akiwa nyumbani kwake mapema mwaka huu.Ubavuni mwake ni mkewe Bi.Fetty

ngugi1

Bila shaka unaitambua sura yake na bila shaka umewahi kumsoma au kusoma vitabu vyake. Anaitwa Ngugi wa Thiong’o. Ni miongoni mwa wanazuoni na waandishi ambao bara la Africa linajivunia kuwa nao.Je nikikupa nafasi ya kumuuliza swali Ngugi ungependa kumuuliza nini? Tuma swali lako kupitia sehemu ya maoni(comments) au kwa kutumia barua-pepe info at bongocelebrity dot com

china

Viongozi wengi wa Africa wapo jijini Cairo nchini Misri kuhudhuria kongamano kuhusu ushirikiano baina ya nchi zao na China.Rais wetu,Jakaya Kikwete,ni miongoni mwa viongozi wanaohudhuria kongamano hilo.

Sasa kama unavyojua,uhusiano wa China na nchi za Africa ikiwemo yetu ya Tanzania una historia ndefu.Kuna ambao wanasema China ndio nchi pekee duniani ambayo imekuwa “true darling” wa bara la Africa.Wanaosema hivyo wanaangalia vitu kama misaada kutoka China,unafuu wa kufanya biashara na China,masharti nafuu ya misaada na mambo kama hayo.

Lakini katika siku za karibuni,uhusiano baina ya nchi za Africa na China umekuwa ukiongelewa katika namna tofauti.Masuala ya biashara,masoko,misaada nk ndio yameshika hatamu badala ya habari za udugu na ujamaa zilizokuwepo enzi zile kina Nyerere na Mao walipokuwa wakipanda mbegu za ushirikiano wa China na Tanzania.Hapo ndipo suala la kujadili au kufanya tathmini za uhusiano au ushirikiano huu linapokuwa na umuhimu wa aina yake.

Mijadala mbalimbali inazuka kila kukicha.Swali lililopo katika kichwa cha habari hapo juu ndilo linasumbua.Nani anafaidika zaidi na mahusiano haya? Je China wanafaidika zaidi au Africa ikiwemo nchi yetu ya Tanzania ndio inafaidika? Na bila kuficha wala kukwepesha macho,mtanzania wa kawaida ndiye anayefaidika au zaidi na uhusiano huo au ni viongozi wetu?Naomba kufungua mjadala.

Pichani ni Rais Jakaya Kikwete akiwa na Rais wa Misri,Hosni Mubarak huko Misri ambapo Rais Kikwete yupo kuhudhuria Kongamano la Ushirikiano baina ya China na Africa.Picha na Freddy Maro-Ikulu)

who

majinabc

mrishobcSwali lililopo kwenye kichwa cha habari hapo juu si langu.Ni swali kutoka kwa Mwandishi Saleh Ally wa gazeti la Mwanaspoti. Ni swali lililobeba makala nzito ambayo inahoji na hapo hapo kujaribu kupata majibu kutoka kwa wakongwe mbalimbali wa muziki wa hip hop nchini Tanzania.

Saleh anaungana na wote ambao wamekuwa wakihoji ulipopotelea miziki ya hip hop iliyokuwa imesheheni ujumbe ambao bila shaka ulipatikana baada ya msanii kuitazama jamii kwa umakini ule uliofanya akaitwa “kioo cha jamii”. Badala yake,leo hii nyimbo ni kuhusu suala moja pekee; mapenzi. Karibuni kila nyimbo inayotoka ni kuhusu mapenzi na starehe ambazo kimsingi hazisaidii sana katika kujenga jamii.Ujumbe wa leo ni nimemuona demu,kapendeza,anavutia,ana figure matata,nikamtongoza,tukaenda kwenye sita kwa sita…mtamu,kwisha kazi. Matatizo ya kijamii au hata mafanikio ya kijamii, hayamulikwi tena kupitia muziki.Kwa bahati mbaya,hata vyombo vingi vya habari navyo vinayapa kisogo mambo mazito mazito ya kijamii. Tunamuachia nani?

Pamoja hayo,Saleh Ally,anamtaja mwanamuziki/mshairi Mrisho Mpoto(pichani) kama miongoni mwa wachache waliobakia ambao wanaimba vitu vya “kueleweka”.Unakubaliana naye? Kama hukubaliani naye,nini maoni yako kuhusu muziki wa kizazi kipya?

Ili kusoma makala nzima ya Saleh,bonyeza hapa.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page