Kwa masikitiko makubwa tunawatangazia kifo cha Mzee wetu Robert Jaka wa Forest Hill- Morogoro, kilichotokea katika hospitali ya Regency mchana wa Jumapili ya tarehe 22/01/2012 Dar-es-salaam-Tanzania.
Marehemu katika uhai wake alifanya kazi katika vyuo vikuu vya Sokoine na baadae chuo kikuu cha Dar-es-salaam kabla ya kustaafu na kurejea Morogoro. Msiba upo Dar-es-salaam Mtoni-Kijichi (nyumba za maafisa wa Magereza)
Mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa kwenda Morogoro siku ya Jumanne na Mazishi yanatarajiwa kufanyika Morogoro siku ya Jumatano tarehe 25.01.2012.
Kwa taarifa zaidi za msiba unaweza kuwasiliana na Kizito Jaka (+255 762 583740) Paschal Kunambi (+255 713 233843) au Exupelius Kunambi (+255 767 201098)

Familia ya marehemu mwalimu Julius Banzi wa Mafiga Morogoro, inasikitika kuwatangazia msiba wa Mwalimu Innocentia Banzi kilichotokea alfajiri ya tarehe 12/01/2011 Dar-es-salaam-Tanzania.
Marehemu ni mama wa:
Dennis Londo wa Helsinki-Finland; Esther Londo na Walonzi Tatala wa Tampere-Finland;
Michael Gomela wa Reading-United Kingdom; Daniel Mtebe wa Stockholm-Sweden.
Habari za msiba huu ziwafikie wakuu wa shule zote za sekondari Tanzania, walimu na wanafunzi wa Kilakala sekondari, Morogoro sekondari na Masanze sekondari. Pia ziwafikie wanachama wote wa chama cha msalaba mwekundu Tanzania; wanachama wote wa chama cha maskauti Tanzania na wanamichezo wote wa Mkoa wa Morogoro.
Mazishi yanatarajiwa kufanyika Morogoro mara tu watoto wa marehemu watakapowasili.
Wale wote ambao mpo Finland msiba upo:
Lautamiehentie
2B 39 Vantaa (kwa maelezo zaidi piga simu 050 4863508, 040 5892123, 040 3750820)
Tanzania upo nyumbani kwa marehemu Mafiga-Morogoro, na Dar-es-salaam upo Mbezi Luis-njia panda ya kwenda Makabe (ulizia kwa Kunambi) Kwa maelezo zaidi piga simu namba: +255 732201098, +255 717365676, +255 713233843



We regret to announce the death of Mr. HUMPHREY NOEL MKONDYA, a Veteran Lawyer, husband to Edith Chisenga Mkondya, father to Eric, Kenneth, Lawrence and Dr. Ellen which occurred on Friday the 12th of November, 2010 at the Apollo Hospital in Chennai, India.
The funeral service will take place on Wednesday 17th November, 2010 at 1400hr, at his residence, House No. 23, Wakulima Road, Hannanasif Estate Kinondoni, Dares Salaam.
The body of the late Mr. Mkondya will be laid to rest on the very day at 1500hrs at Kinondoni cemetery
The Lord gave and the lord hath taken away;
Blessed be the name of Lord. Job 1: 2 1b
May his Soul Rest in Eternal Peace. Amen.

Bila shaka unatambua kwamba miongoni mwa mitandao maarufu zaidi ulimwenguni ni mtandao wa Facebook. Historia ya Facebook ni nzuri sana.Ukipata muda isome hapa.
BC ipo pia katika Facebook.Kule watu hukutana,kujadiliana mambo kadhaa na pia kupashana habari mbalimbali. Kama bado hujajiunga nasi katika Facebook Group yetu(shukrani kwa wale ambao mmeshajiunga) unaweza kufanya hivyo kwa kubonyeza hapa na kisha kuingia(login) kupitia akaunti yako ya Facebook


Familia ya Mzee Gembe wa Upanga Dar-es-salaam na Tabora,kwa moyo mkunjufu, tunapenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru ndugu,jamaa,majirani na marafiki wote waliofanikisha shughuli zote za msiba wa Marehemu mtoto wetu,mdogo wetu,dada yetu, Evaline Gembe ambaye alifariki huko Toronto nchini Canada katika hospitali ya Mtakatifu Michael tarehe 30/March/2010 na hatimaye kuzikwa tarehe 13/Aprili/2010 kijijini Inyonga Mkoa wa Tabora.
Shukrani za pekee tunaomba ziwafikie Jumuiya yote ya watanzania wanaoishi nchini Canada hususani katika Jiji la Toronto na vitongoji vyake. Asanteni sana kwa michango yenu ya hali na mali ambayo ilisaidia katika mipango na mikakati yote ya kuuhifadhi mwili hadi kuusafirisha kwa gharama kubwa kutoka Toronto hadi Dar-es-salaam mnamo tarehe 8/April/2010.Asanteni kwa sala,maombi na kujitokeza kwenu katika kutufariji na kututia nguvu.Shukrani za pekee ziwaendee kamati nzima iliyoratibu na kufanikisha shughuli nzima ya kuusafirisha mwili wa Marehemu Evaline kuja Tanzania.
Tunapenda pia kutoa shukrani nyingi kwa majirani,ndugu,jamaa na marafiki kwa misaada yenu ya hali na mali na pia kushiriki katika shughuli zote za mazishi. Shukrani kwa wote mliofika nyumbani Dar-es-salaam na Tabora katika kutufariji,mliotupigia simu au kutuma ujumbe kwa njia zingine kwa nia ya kutufariji na kututia nguvu.Asanteni sana.
Shukrani pia ziuendee Ubalozi wa Tanzania nchini Canada na Jumuiya mbalimbali za ki-Tanzania nchini Marekani na wanablogu wote waliolitoa tangazo la kifo kwenye Blogu zao.
Kwa kuwa ni vigumu kumshukuru kila mtu kipekee,tunaomba shukrani hizi mzipokee wote mliohusika kwa njia moja ama nyingine katika kufanikisha shughuli nzima ya msiba huu wa ndugu yetu Evaline.Hatuna cha kuwalipa bali tunamwomba Mwenyezi Mungu awajalie na kuwazidishia katika shughuli zenu za kila siku.
Sisi tulimpenda sana Evaline lakini
Mwenyezi Mungu amempenda zaidi,
Jina la Bwana lihimidiwe.
Amen

Familia ya Bwana na Bibi Gembe wa Upanga-Dar-es-salaam na Tabora, wanasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Evaline Gembe(pichani) kilichotokea hapo juzi tarehe 30.3.2010 huko Toronto,Canada.Evelyne amefikwa na mauti katika hospitali ya St.Michael’s ya Toronto alipokuwa amelazwa.
Taratibu na mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda nyumbani Tanzania kwa mazishi zinafanyika nyumbani kwa dada yake, Julie huko huko Toronto,Canada.
Ukiwa kama mtanzania,ndugu,jamaa au rafiki, unaombwa kuchangia fedha,hali na mali kwa ajili ya kuwezesha kuusafirisha mwili wa marehemu kurudi nyumbani kwa mazishi mapema kadri iwezekanavyo kwani kama wengi wenu mnavyofahamu, mwili unavyozidi kukaa Funeral-Home,gharama ndivyo zinavyozidi kuongezeka. Mwili utasafirishwa punde tu zitakapopatikana fedha za kutosha kwa ajili ya kulipia gharama husika.
Unaweza kutuma mchango wako kwenye Account maalumu ya wafiwa kama ifuatavyo:
BANK : CIBC (Canadian Imperial Bank of Commerce)
ACCOUNT NUMBER: 5681839
TRANSIT NUMBER: 00902
INSTITUTE NUMBER: 010
SWIFT CODE: CIBCCATT
Vilevile unaweza kutumia E-mail Money Transfer kwa Sania Esmail.Anuani yake ni saniae@yahoo. ca au kuwakilisha msaada wako kwa kutumia anuani hii:
1025 SCARLETT ROAD, APT 606, BUZZ # 178
TORONTO ON, M9P 3V3.
Kwa mawasiliano zaidi unaweza kuwasiliana na wafuatao:
Julie +1 416-247-8318
Esmail Manambi- +1 647- 299-2572
Victor Wambura- +1 647-428-4118
Prosper Luteganya- +1 905 626 3764
Tafadhali chukua muda kuwafariji na kuwaombea ndugu,jamaa na marafiki waliofikwa na msiba huu. Tunatanguliza shukrani kwa misaada yote iliyotolewa na itakayotolewa. Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Amen.

Kwa wale ambao hawaupati mtandao wa www.globalpublisherstz.com; Wanashauriwa kubadilisha Browser na kutumia Mozilla Firefox.
Imeonekana kwa sasa website(tovuti) hiyo haifunguki kwa kutumia Browser ya Internet Explorer(IE).
Ni rahisi kubadilisha kutoka Internet Explorer kwenda Mozilla Firefox.Unachoweza kufanya ni ku-download Mozilla Firefox kwa kufungua link ifuatayo;
http://www.mozilla.com/en-US/products/download.html
Samahani kwa usumbufu wowote unaojitokeza kwa sasa.Tatizo linashughulikiwa.
GLOBAL PUBLISHERS


sending...
