MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Kwa wale ambao hawaupati mtandao wa www.globalpublisherstz.com; Wanashauriwa kubadilisha Browser na kutumia Mozilla Firefox.

Imeonekana kwa sasa website(tovuti) hiyo haifunguki kwa kutumia Browser ya Internet Explorer(IE).

Ni rahisi kubadilisha kutoka Internet Explorer kwenda Mozilla Firefox.Unachoweza kufanya ni ku-download Mozilla Firefox kwa kufungua link ifuatayo;

http://www.mozilla.com/en-US/products/download.html

Samahani kwa usumbufu wowote unaojitokeza kwa sasa.Tatizo linashughulikiwa.

GLOBAL PUBLISHERS


summit-logo

Je wewe ni mwanablogu (Blogger) au mdau wa habari na mawasiliano kwa umma kwa kutumia mtandao? Kama jibu ni ndio, tafadhali unaombwa kujiorodhesha kwa ajili ya maandalizi ya Kongamano Maalumu la Kitaifa kwa ajili Wanablogu (Bloggers) na wadau wa habari na mawasiliano wa Tanzania (Tanzanians Bloggers Summit) linalotarajiwa kufanyika Desemba mwaka huu jijini Dar-es-salaam,Tanzania.

Dhumuni la kongamano hili ni Kuelimishana, Kufahamiana, Kuamsha Utambuzi Rasmi Kuhusu Tekinolojia ya Blogu na Mawasiliano ya Umma kwa Kutumia Mitandao, Kusaidia Utambuzi Rasmi juu ya mchango wa blogu nchini Tanzania kama chombo muhimu cha habari na mawasiliano, Kuelimishana jinsi gani blogu zinaweza kutumika katika kuleta maendeleo katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi, kuburudisha, kukuza utamaduni nk.

Wataalamu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wataalikwa kutoa mada na mafunzo mbalimbali kuhusiana na tekinolojia ya kublogu, zana nyinginezo za mawasiliano mtandaoni kama vile mitandao jamii(social networking), online forums nk.Kutakuwa na vipindi vya maswali na majibu.

Ili kufanikisha maandalizi ya Kongamano hili la kihistoria, kujiorodhesha kwako ni muhimu sana. Muda wa kujiodhoresha ni kuanzia tarehe 12/8/2009 (Jumatano) mpaka 12/9/2009 (Jumamosi) tu.

Kinachohitajika ili kujiandikisha ni :

Jina Lako, Anuani yako ya barua pepe (E-mail), Mahali Ulipo au unapoishi (Nchi,mji nk),Namba ya Simu (sio lazima) na Anuani au URL(Universal Resource Locator) ya blogu yako (mfano www.kongamano.blogspot.com/wordpress.com/.com/typepad nk). Vyeti vya Ushiriki vitatolewa kulingana na habari utakazoziorodhesha hapa.

Unaweza kujiorodhesha kwa kutuma ombi lako kwa barua pepe kwenda; summit@bongocelebrity.com.

Zingatia tarehe za kujiandikisha.

Ni mwezi mmoja tu! Asante kwa ushirikiano. UMOJA NI NGUVU!

vinara-voting3-copybc

TUZO ZA
VINARA WA FILAMU 2009 KUWASHIRIKISHA WANANCHI

Mchakato wa kutafuta vinara wa filamu Tanzania kwa mwaka huu utawahusisha wananchi kupitia upigaji kura.

Wapenzi wa tasnia ya filamu nchini watapendekeza filamu ambazo wanaona zinastahili kuingia tuzo za vinara wa filamu. Mbali an wananchi pia kuna taasisi mbali mbali kama vile kampuni ya uhasibu inayotambulika kimataifa litasimamia zoezi la mapendekezo ya filamu. Filamu zenye kura nyingi ndizo zitakazoingia katika tuzo hizi. Pia filamu zitakubaliwa kutokana na mapendekezo ya waandaaji na majaji.

Kuteua filamu ni kwa njia ya ujumbe mfupi ambapo mpenzi atatakiwa kuandika neon vinara kasha jina la filamu anayoipenda na kutuma kwenda 15551 kwa gharama ya Tshs 300.

Vipengele vitakavyowaniwa mwaka huu katika tuzo za vinara ni Mwigizaji bora wa kiume na wa kike wa mwaka, Mwigizaji chipukizi wa kiume na wa kike, Filamu bora ya mwaka, Muongozaji bora wa Mwaka, Mwandishi bora wa filamu, Adui bora, Msanii bora msaidizi wa kiume na wa kike, Mhariri bora wa mwaka, Mtunza Sauti bora, Mtunza Mwanga bora, Mpiga picha bora wa mwaka, Mtayarishaji bora wa filamu, Mtunzi bora wa filamu, Mapambo na maleba bora, msanii maarufu wa kiume na kike na Tuzo ya heshima.

Vipengele vilivyoongezwa ni mtunza taa bora, mtayarishaji bora wa filamu (producer) na wasanii maarufu wa kike na wakiume (People’s choice Award).

Mwaka huu kampuni mbali mbali zimejitokeza kudhamini mashindano haya lakini yatatajwa baada ya upigaji kura

Filamu zinazostahili kupendekezwa ni zile zilizotengenezwa kuanzia januari 2009. Filamu zitakazo ingia moja kwa moja ni zile ambazo bado hazijaingia sokoni lakini yatawasilishwa na watengeza filamu wenyewe.

Zoezi la kupendekeza filamu litafanyika hadi septemba 30 kabla ya kupatikana wahusika kwenye kila kipengele kabla ya wananchi kupiga kura kuwapata washindi.

Khadija Khalili

Mratibu


zara-tours-logoLeo tunapenda kuwashukuru wadhamini wetu kampuni ya Zara Tours ambao wanaongoza kwa huduma zote zinazohusiana na utalii nchini Tanzania.Zara Tours ndio inayoongoza pia kwa kuandaa safari za kupanda Mlima Kilimanjaro.Shukrani nyingi kwa udhamini wenu.

Kwa habari zaidi kuhusu huduma za utalii zitolewazo na Zara Tours,bonyeza hapa ili kutembelea tovuti yao.

NB: Kama na wewe una biashara au kampuni na ungependa kuwa mmoja wa wadhamini wa BC,usisite kuwasiliana nasi kupitia bongocelebrity at gmail dot com au kupitia kwenye fomu inayopatikana katika ukurasa wa “Kuhusu BongoCelebrity” hapo juu.

party

Kazi kwenu wakazi wa Washington DC,maeneo ya jirani na wote wanaojua maana ya kujumuika na kustarehe!

Piga picha hii.Unanunua gazeti,unapata habari mbalimbali,unaburudika,kuelimika na kufahamu mengi yanayoendelea nchini Tanzania na hata sehemu zinginezo za ulimwengu.Kwa wengi hilo ni jambo muhimu na linalojitosheleza kabisa.Lakini je ungepewa pia nafasi ya kujishindia zawadi kama gari aina ya Mercedez Benz kwa ununuzi na usomaji wako huo huo wa gazeti/magazeti ungechangamkia tenda?

Basi hilo linawezekana kupitia promosheni kabambe inayoendeshwa na kampuni ya uchapishaji magazeti ya Global Publishers.GP ndio wachapishaji wa magazeti ya Uwazi,Championi,Ijumaa,Risasi,Amani,Ijumaa,Wikienda,Bongo Sun na Jarida la School & College.Kwa habari zaidi na jinsi ya kushiriki kwenye promosheni hii,bonyeza hapa.Kazi kwenu,Benz sio kwa ajili ya kina nani hii tu kumbe!

Kujua zaidi Bonyeza hapa.

Majira ya joto, maarufu kama “Summer”, huwa ni maarufu kwa mijumuiko na starehe za kila namna. Pia summer ni wakati mzuri wa kujumuika,kuchoma nyama(bbq),kusikiliza na kucheza muziki nk.

Kwa wakazi wa jiji maarufu la Chicago na majiji mengine ya jirani,wakati wenu umewadia.Tizama kwa makini tangazo hilo hapo chini.Usikose!

Ufuatao ni ujumbe kutoka kwa Michuzi.

Wadau kunradhi,

Kutokana na matatizo ya kiufundi aliyonayo host wa globu ya jamii, tutaendeleza libeneke kwa muda kama kawa kupitia michuziblog.blogspot.com hadi hapo mambo yatapokuwa mswano.

Wadau nawaomba msikonde wala nini haya ni mambo ya kawaida ikiwa ni katika kuboresha huduma maana sasa www.michuzi-blog.com ni website kamili na itafanya vitu maradufu ya awali.Asanteni kwa uvumilivu na kunradhi kwa usumbufu ulio nje ya uwezo wetu.

Tumepata e-mails na comments kadhaa zikihoji au kutaka kufahamishwa kwanini blog ya Michuzi haipatikani leo.Tumewasiliana na Michuzi ambaye ametufahamisha kwamba kuna matatizo ya kiufundi kwenye platform anayotumia kuhodhi blog yake yaani www.blogger.com ambayo ipo chini ya www.google.com. Kwa hiyo tatizo haliko upande wake bali kwa host.Tatizo hilo linashughulikiwa na matumaini ni kwamba hali itarejea kuwa kawaida muda si mrefu.

Pamoja na hayo,Michuzi ametufahamisha kwamba kutokana na ukweli kwamba bado anaendelea kuhamisha kazi zote(picha,maelezo na maoni) kutoka kwenye blog ya zamani kwenda kwenye uwanja wake mpya,rabsha za hapa na pale zinaweza kuwa zinatokea.

Hivyo anawaomba radhi kwa usumbufu wowote ambao umejitokeza au utakaojitokeza.Ahsanteni.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page