
Rais Jakaya Mrisho Kikwete,akila kiapo kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mbele ya Jaji Mkuu wa Tanzania,Augustino Ramadhan.Sherehe hizo zimefanyika mapema leo katika Uwanja wa Uhuru(Uwanja wa Taifa) jijini Dar-es-salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali barani Afrika bila kuwasahau wakazi wa jijini Dar-es-salaam na mikoa ya jirani.

Hatimaye Tume ya Uchaguzi Tanzania,imetangaza rasmi matokeo ya Kura za Uchaguzi wa nafasi ya Urais.Katika matokeo hayo,Rais Jakaya Mrisho Kikwete,ameshinda kwa kiwango cha asilimia 61.17%. Katika uchaguzi wa mwaka 2005, Rais Kikwete alipata ushindi wa asilimia 80.28%. Matokeo kamili ni kama yafuatayo;
1. KUGA PETER MZIRAY APPT – MAENDELEO 1.12%
2. KIKWETE JAKAYA MRISHO/CCM – 5,276,827 61.17%
3. SLAA WILLIBROD PETER/CHADEMA – 2,271,942 26.34%
4. LIPUMBA IBRAHIM HARUNA/CUF – 695,667 8%
5. RUNGWE HASHIM SPUNDA NCCR-MAGEUZI 26,388 0.31%
6. MGAYWA MUTTAMWEGA BHATT TLP 17,482 0.20%
7. DOVUTWA YAHMI NASSORO DOVUTWA UPDP 13,176 0.15%

Aliyekuwa Mgombea wa Kiti cha Urais kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA),Dr.Wilbrod Slaa, leo hii amejitokeza na kuongea na baadhi ya vyombo vya habari na kuelezea mapungufu,shaka za uchakachuaji wa kura na pia kutoa mapendekezo yake juu ya nini kifanyike au kifanywe na Tume ya Uchaguzi Tanzania(NEC).
Miongoni mwa vyombo vya habari alivyoongea navyo,ni pamoja na Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya America(VOA). Msikilize kwa kubonyeza player hapo chini akiongea na mtangazaji Sunday Shomari, wa Idhaa hiyo.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Kwa habari zaidi unaweza kutembelea Ukurasa wa Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika(VOA).

Gazeti la Mwananchi limefanya jambo moja muhimu sana.Limeorodhesha ahadi ambazo wagombea Urais wamekuwa wakizitoa kwa wapiga kura katika nyakati mbalimbali za kampeni.
BONYEZA HAPA KUZISOMA AHADI ZENYEWE. Kwa yeyote atakayeshinda kiti cha Urais(bado hatujajua mshindi wa kiti cha Urais mpaka jamaa wa Tume ya Uchaguzi watakapopenda kutoa matokeo!),ahadi hizi ndizo zitatumika kuona ni jinsi gani wanasiasa ni watu wa kuaminika au kutoaminika.
…ONE CAN SAY YES AND THE OTHER ONE CAN SAY NO…AND BOTH CAN BE RIGHT AND PEACEFUL…

Mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA,Dr.Wilbroad Slaa,akimnadi mgombea ubunge katika Jimbo la Ubungo kupitia chama hicho,John Mnyika.Wapiga kura wengi bila shaka walikubaliana na ombi la Dr.Slaa kwa kumchagua Mnyika kuwa mbunge wao mpya.

JK alipokuwa akimnadi Basil Mramba aliyekuwa mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Jimbo la Rombo mkoani Kilimanjaro.Kwa bahati nzuri au mbaya,wapiga kura walikuwa na mtazamo tofauti.

Mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA,Dr.Wilbroad Slaa,akimnadi mgombea Ubunge kupitia chama hicho katika Jimbo la Karatu,Mchungaji Israel Natse.Wapiga kura jimboni hapo waliafikiana na Dr.Slaa na kumchagua Mch.Natse kuwa Mbunge wao mpya.

Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM,Jakaya Kikwete,akimnadi Mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama hicho katika Jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza,Lawrence Masha.Huko nako wapiga kura walikuwa na mtazamo tofauti.Demokrasia ikaamua.

Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete,akimnadi mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama hicho katika Jimbo la Ilemela mkoani Mwanza,Anthony Diallo.Wapiga kura walikuwa na mrengo tofauti.

Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM,Jakaya Mrisho Kikwete,akimnadi mgombea Ubunge kupitia tiketi ya chama hicho katika Jimbo la Monduli,aliyewahi kuwa Waziri Mkuu,Edward Lowassa.Wapiga kura wa jimbo hilo walikubaliana na ombi la Jakaya Kikwete kwa kumrudisha bungeni Mh.Lowassa.

Halima James Mdee-Mshindi Jimbo la Kawe kwa tiketi ya CHADEMA.

January Makamba-Mshindi Jimbo la Bumbuli kwa tiketi ya CCM

John Mnyika- Mshindi Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya CHADEMA

Peter Serukamba-Mshindi Jimbo la Kigoma Mjini kwa tiketi ya CCM

Zitto Zuberi Kabwe-Mshindi Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya CHADEMA
More to come…stay tuned!

Wapo watu wengi,hususani vijana, ambao BC inawapongeza na kadiri siku zinavyokwenda,itazidi kuwapongeza kwa ushindi waliojinyakulia wakati wa kuwania nafasi za kuwawakilisha wananchi hao katika Bunge na pia kuwaongoza wananchi katika harakati za kujiletea maendeleo.
Kwa leo,tunadhani sio mbaya tukaanza kwa kumpongeza Mr.Joseph Mbilinyi a.k.a SUGU. Ukiwa huna hiana, unaweza kuanza kumuita Mheshimiwa Joseph Mbilinyi.Hongera sana.
Tunapompongeza,sio vibaya pia kukumbushana enzi zile(sina uhakika bado kama ataziacha kwa kuwa sasa ni mwendo wa tai na suti). Hapa chini ni wimbo wa “Mheshimiwa” uliokwenda kwa jina Sugu akiwa amemshirikisha Stara Thomas.Msikilize.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Umati uliojitokeza kumsikiliza Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM-Mh.Jakaya Mrisho Kikwete. Hapo ni Mwembeyanga-Temeke jijini Dar-es-salaam.

Umati uliojitokeza kumsikiliza Mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA.Hapo ni pale pale Mwembeyanga,Temeke jijini Dar-es-salaam.
Kama umekuwa ukifuatilia kwa makini kampeni za wagombea mbalimbali hususani wale wa kiti cha juu kabisa(Urais), bila shaka utakuwa pia umesikia tambo, majivuno na vijembe mbalimbali ambavyo vimekuwa vikitolewa na watu wanaoviunga mkono vyama au mgombea fulani.Wengine wamefikia hata hatua ya kutukanana,kupigana nk. Wengine wameenda hata jela. Sijui ni kwa ajili ya ushabiki tu au la?
Neno “nyomi” kwa maana ya wingi wa watu waliohudhuria mkutano wa kampeni,limetumika mara nyingi. Wingi wa watu waliojitokeza kuhudhuria umekuwa ni mwanya wa kuwashawishi wengine kwamba mgombea fulani au chama fulani kinakubalika zaidi!Bila shaka wingi huo huo ndio ulitumika na baadhi ya waendesha kura za maoni(polls) kupata matokeo yao! Uwanja umeshona vibaya sana leo.Ah mgombea wetu anakubalika sana.Anakubalika au inawezekana watu hao hawana ajira na wametumia muda huo kuja kusikiliza kama angalau una sera ya kuwakomboa kutoka walipo? Just thinking….
Utakuwa umesikia na kuona vichwa vya habari vilivyokwenda kwa staili ya “JK Funika Bovu Kilakala” au “Dr.Slaa Funika Bovu Manzese”.Sina uhakika sana na maana ya neno “funika bovu” lakini natumaini neno hilo lilikuwa linamaanisha kwamba mgombea fulani au chama fulani kupitia mgombea wake,kimeonyesha kuwa na sera zinazoeleweka na kutekelezeka.Kinyume na hivyo,neno hilo litakuwa limetumika visivyo.Limetumika kishabiki tu.
Ninaposema sera zinazoeleweka na kutekelezeka namaanisha sera zilizoundwa kutokana na mazingira halisi ya Tanzania na sio kukopi na kupesti kutoka katika vitabu vya nchi za nje kama ambavyo nimesikia wagombea wengi wakiwasukumia wananchi misemo na maneno ambayo kimsingi haina maana kwao. Eti kasema nini vile?…Info..mesheni.. teki nini? Hata mimi sijamsikia.Tusubiri labda atarudia tena.Imetoka hiyo.
Kumbuka kwamba kama mwananchi haelewi unachokiongelea, hatokuwa tayari kutoa ushirikiano wake katika kuleta maendeleo.Utamlaumu? Sidhani. Ulimfanya mbumbumbu,ukamweka mtu kati kwa mikogo na maneno ya kuazima. Lazima uweke mbwembwe.Watajuaje kwamba umesoma?Alah!
Nimesikia vijana wakibishana kwa misingi ya kwamba muziki uliofungwa kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea wake ulikuwa “sio wa kitoto”.Suala sio sera tena bali ukubwa wa sauti au burudani!Hawa ni vijana ambao wote hawana ajira,hawakusoma na ikitokea mmoja wao akaanguka kutokana na “mishipa ya ubishi” kumpasuka,hakuna gari wala njia ya kumwezesha kuwahishwa hospitalini!
Hapo ndipo ninaposema, nilichokiona mimi wakati wa kampeni ni Ushabiki Vs Utashi. Muda mwingi umetumika au umetumiwa katika kurushiana “makombora”. Sera zimekuwa sisi waungwana wao majangili.Muziki mnene, dhidi ya helikopta ile ya kisasa zaidi. Tumlaumu mwananchi? Kivipi.Mbona akifungua blog au kusoma gazeti,habari ndio hizo hizo?Maneno ndio yale yale?
Matumaini yangu ni kwamba Ushabiki utaishia siku ya Jumamosi.Jumapili ni siku ya Utashi.Ninaposema utashi namaanisha ile nguvu au ari ya kuona nchi yetu inasonga mbele,kuendelea kuwa na amani na utulivu. Siku ya kuweka kando matarumbeta,khanga,kofia,nk na kupiga kura inayofaa. GO VOTE.NENDA KAPIGE KURA.


sending...
